The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Gender Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Gender

2009-11-04

Central Asia & Caucasus

Mwanablogu wa Emotions on Air, Mind Mute anatafakari marajio ya jamii kwamba wanawake watabakia mabikira mpaka watakapofunga ndoa. Japokuwa ipo nchini Azerbaijan, blogu hiyo inabaini mfumo unaofanana wa maadili katika eneo lote la Caucasus na inaongelea kuhusu dhana na taratibu za namna hiyo za mfumo dume.

2009-11-02

Japan: Mkeo anapougua

Pale utamaduni wa "mifugo ya mashirika" au kwa maneno mengine “utamaduni wa ujumla wa wafanyakazi” (社蓄 shachiku) na maadili ya ndoa vinapogongana - zaidi ya watu 300 walitoa majibu kuhusiana na swali lililoulizwa kwenye jukwaa kubwa la mijadala lijulikanalo kama Hatsugen Komachi: Je, mwanaume aombe ruhusa kazini pale mkewe anapougua? Hali ...

2009-10-26

Americas

“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake kusikika”: Attillah Springer anajihusisha na kampeni ya hali ya hewa 350.

2009-04-14

Wanawake na Uchaguzi Nchini India

Demokrasi kubwa zaidi duniani, India, itafanya uchaguzi mkuu utakaoanza katika wiki chache zijazo kutoka sasa. Wanawake wa India, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakinyimwa nafasi yao ya haki majumbani, kazini na katika hatamu za uongozi wana dau kubwa katika uchaguzi ujao. Japokuwa wanawake wengi wanaanza kuwa na ufahamu wa haki zao za kupiga kura na wanashiriki katika siasa kwenye ngazi za chini, ripoti hii inaeleza kwamba inavyoelekea mwaka huu ni wanawake wachache zaidi watakaochaguliwa katika bunge la nchi.

2009-02-22

Indonesia: Talaka na Ndoa za Mitala

Najihisi nina hatia ninapoandika kuhusu talaka na ndoa za mitala wakati wa siku ya wapendanao ya Valentino. Lakini mada hizi zisizotamkika ni ukweli wa mapenzi na mahusiano. Katika Indonesia, wanawake wengi wanawataliki waume zao kwa sababu ya mitala.

2009-02-17

Jamaika: Miziki Yenye Maneno Machafu Yazuiwa

Utata wa muda mrefu juu ya usahihi wa kurushwa hewani kwa miziki fulani umezuka tena nchini Jamaika. Wanablogu wa Jamaika wanapaza sauti zao.

2008-10-26

Misri: Sisi sote ni Laila

Sisi sote ni Laila, ndivyo wanavyosikika kusema kwa sauti moja wanablogu wa kike wa Misri. Hivi, huyu Laila ni nani na kwa nini wasichana na wanawake wa kiMisri wanapenda kufananishwa naye? Hebu endelea kusoma ili uone ni kwa namna gani wanablogu wa Misri wanavyojihangaisha ili kuvunjilia mbali vikwazo vya jinsia na kufanya sauti zao zisikike.

2008-09-06

Saudi Arabia: Kina Mama Huru

WAKATI kukiwa hakuna shaka kwamba kuna vizuizi kwa wanawake waishio Saudi Arabia, havifanani na taswira iliyojengwa na wageni dhidi ya taifa hilo. Katika makala hii tunao ushauri kwa wakina mama wanaotaka kutembelea jiji la Jeddah wakiwa peke yao, kuna muhtasari wa hoteli za kina mama pekee jijini Riyadh, na wito kwa wageni wote wanajihisi kuzungumza kwa niana ya kina mama wanaokandamizwa wa Saudia.