· Disemba, 2009

Habari kuhusu Uhuru wa Kujieleza kutoka Disemba, 2009

Global Voices Yaingia Ubia na Google Katika Tuzo ya Uhuru wa Kujieleza

  30 Disemba 2009

Mapendekezo kwa ajili ya Tuzo ya Kuvunja Mipaka yatafunguliwa leo (Disemba 29, 2009), hii ni tuzo mpya aliyoundwa na Google pamoja na Global Voices ili kuienzi miradi ya kwenye mtandao wa intaneti iliyoanzishwa na watu au vikundi ambavyo vinaonyesha ujasiri, ari na uwezo katika kutumia intaneti ili kukuza uhuru wa kujieleza.

Morocco: Mwanablogu Mwingine Atupwa Gerezani

  20 Disemba 2009

Mnamo tarehe 14 Desemba, siku ya Jumatatu, mwanablogu Bashir Hazzam na mmiliki wa mgahawa wa Intaneti Abdullah Boukhou walihukumiwa kifungo cha miezi minne jela kwa huyo wa kwanza na mwaka mmoja kwa huyo wa pili pamoja na kulipa faini ya MAD 500 (sawa na dola za Marekani 63) kila mmoja katika mahakama ya Goulmim.

Misri: Makao Makuu ya Kuzimu Duniani

Wanablogu na wanaharakati wengi wa Kimisri wamekuwa wakikamatwa na Usalama wa Taifa katika nyakati tafauti kwa sababu mbalimbali –za kweli au za bandia –Wa7da Masreya aliwahoji wanablogu mbalimbali na kuweka makala ya kina kuhusu mbinu za utesaji na hila za kisaikolojia ambazo wanablogu wale wamekuwa wakikumbana nazo kwenye makao makuu ya Usalama wa Taifa katika wilaya ya Jiji la Nasr.

Brazil: Wito wa Kugomea Gazeti Linaloongoza Nchini

  14 Disemba 2009

Wanablogu wa Brazili wamekuwa wakihamasisha mgomo dhidi ya kile walichokiita Coupist Press Party, yaani Sherehe ya Chombo cha Habari ya Kutaka Kupindua Serikali, kwa hiyo wamekuwa wakiwataka watu kuacha kununua, kusoma au kutoa maoni na badala yake kufuta usajili wao kutoka kwenye gazeti la Folha de São Paulo na tovuti yake.

Indonesia: Sarafu za Kudai Haki

  8 Disemba 2009

Raia wa mtandaoni (Netizens) wamezindua kampeni ya kukusanya fedha zilizo katika muundo wa sarafu ili kumuunga mkono Prita Mulyasari, mama wa nyumbani raia wa Indonesia aliyeandika malalamiko yake mtandaoni dhidi ya hospitali iliyotoa huduma mbaya, na ambaye alipatikana na hatia na mahakama moja ya kosa la "kuchafua jina" la hospitali hiyo binafsi.