Habari kuhusu Uhuru wa Kujieleza kutoka Oktoba, 2009
Cambodia: Tuzo yamuenzi aliyenusurika na utumwa wa ngono
Sina Vann alikuwa na umri wa miaka 13 wakati alikupoja Cambodia kutoka Vietnam kwa kile kilichopaswa kuwa likizo. Badala yake, aliuzwa kama mtumwa kwa ajili ya ngono na alitumia miaka miwili iliyofuata ndani ya danguro. Alikombolewa wakati Somaly Mam, mwanaharakati wa kupinga utumwa na sura ya Taasisi ya Somaly Mam,...
Syria: Mwanaharakati wa Haki Za Binaadamu Mwenye Umri wa Miaka 80 Akamatwa
Omar Mushawah ameripoti [ar] kukamatwa kwa Haytham al-Maleh, mwanasheria wa Ki-Syria na mtetezi wa haki za binaadamu ambaye pia alitumia muda wa miaka 6 jela kati ya 1980 na 1986 kwa kudai mabadiliko ya kikatiba. Al-Maleh pia ni mwanzilishi mwenza wa Jumuiya ya Haki za Binaadamu ya Syria.
Marekani: Wanandoa wa rangi tofauti wanyimwa cheti cha ndoa
Juma lililopita huko Hammond, Louisiana, wapenzi wawili walituma maombi ya kibali cha kufunga ndoa na walikataliwa kwa misingi ya rangi zao tofauti. Afisa wa kutathmini na kuandikisha nyaraka (Muamuzi wa Amani) alidai kuwa “ndoa baina ya watu wa rangi hazidumu” na alisema kuwa anafanya hivyo “kwa ajili ya watoto.”