· Februari, 2009

Habari kuhusu Uhuru wa Kujieleza kutoka Februari, 2009

Kampuchea: Vikwazo Vya Intaneti Vyalenga Wasanii

  4 Februari 2009

Wizara ya Masuala ya Wanawake nchini Kampuchea imetishia kuizuia tovuti yenye michoro ya wacheza ngoma ya Apsara walio vifua wazi pamoja na mwanajeshi wa Khmer Rouge. Uchujwaji wa habari wa namna hii unawalenga wasanii wanaotambulika zaidi kwa uwepo wao katika mtandao wa intaneti.

Bahrain: Mabloga Waungana Kupinga Uamuzi wa Kufungwa Kwa Tovuti

  2 Februari 2009

Wanablogu wa Bahrain wameujia juu uamuzi wa Waziri wa Habari wa nchi hiyo wa kuzuia upatikanaji wa tovuti mbalimbali, kadhalika kuzuia matumizi ya tovuti vivuli [proxy sites] zinazoruhusu watumiaji kuperuzi tovuti nyingine zilizozuiwa na zana za kuchuja habari. Ayesha Saldanha anaangalia maoni kutoka Bahrain.