· Januari, 2010

Habari kuhusu Ubaguzi wa Rangi kutoka Januari, 2010

Marekani: Dkt. Martin Luther King, Jr. Akumbukwa

Martin Luther King Jr. alizaliwa tarehe 15 Januari, 1929 na akawa mmoja wa wasemaji na watetezi wakuu wa Harakati za Haki za Kiraia huko Marekani. Nchini Marekani, anaenziwa kwa sikukuu ya taifa, inayoadhimishwa kila mwaka siku ya Jumatatu ya tatu ya mwezi Januari. Leo, wanablogu wengi nchini Marekani wanaadhimisha kumbukumbu yake kwa kuandika makala za kumuenzi, huku wakiungalisha urithi wake wa masuala ya haki za jamii na masuala ya leo, wakionyesha wazi kuwa miaka 42 baada ya kuuwawa kwa King, maneno yake bado yana maana.

Australia: Mauaji ya Mhindi Yazua Mzozo

  9 Januari 2010

Mauaji ya mtu mwenye asili ya India mjini Melbourne yamewasha tena mjadala kuhusu ubaguzi wa rangi nchini Australia na usalama wa wanafunzi kutoka ng’ambo. Kadhalika yameathiri uhusiano kati ya Australia na India. Mwandishi wa GV Kevin Rennie anakusanya maoni ya wanablogu wa Australia.

Slovakia, Hungaria: Heri ya Mwaka Mpya!

  6 Januari 2010

Uhusiano kati ya nchi mbili jirani za Slovakia na Hungaria ulianza kutetereka katika mwaka uliopita - lakini baadhi ya wananchi wa Slovakia na Hungaria wanafanya juhudi kurekebisha hali hiyo kwa kuzindua kampeni ya mtandaoni inayojulikana kama "Štastný nový rok, Slovensko! / Boldog Új Évet Magyarország!" ("Heri ya Mwaka Mpya, Slovakia!/Heri ya Mwaka Mpya, Hungaria!).