mahojiano mafupi ya video kuhusu mashindano yaliyoandaliwa na timu ya mpira wa miguu ya Refugee VI soccer ynakusudia kuelimisha umma juu ya suala la ubaguzi dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini.
Habari Maalum Kuhusu Ethnicity & Race
-
Dondoo za Video: Maandamano, Chaguzi, Utamaduni na GV
31 Disemba 2011
-
Korea Kusini: Maombolezo ya Kitaifa ya Mwanamwali wa Kivietnam
8 Agosti 2010
-
South Africa: Mauaji ya kiongozi wa Afrikaner Resistance Movement 12 Aprili 2010
-
Haiti: Kwa Nini Habari Zote Hizi Kuhusu Yatima?
24 Februari 2010
-
Slovakia, Hungaria: Heri ya Mwaka Mpya! 6 Januari 2010
Habari mpya Kuhusu Ethnicity & Race
30 Aprili 2012
Ajentina: Dokumentari Kuhusu Wenyeji wa Mjini Yatafuta Tafsiri ya Maandishi
Dokumentari iitwayo Runa Kuti iliyoshirikishwa katika mradi wa Haki miliki wa “Creative Commons” kuhusu kutambuliwa kwa wananchi waliotokana na uzao wa wenyeji wa zamani walioishi mjini katika jiji la Buenos Aires, inatafuta watu wa kujitolea kusaidia kuiwekea video hiyo tafsiri ya maandishi kwenda katika lugha za asili za Ajentina kama ki-Quechua, ki-Aymara, -kiMapuche na ki-Guaraní pamoja na ki-Kiingereza.
Mali: Kimya cha Wanablogu wa Nchini Humo
Wakati mtandao wa intaneti umetawaliwa na blogu, ujumbe wa twita na video kutoka nchi mbalimbali, watumiaji wa intaneti wenyeji wa Mali wangali kimya. Mji mkuu, Bamako, umeathirika kwa kukatika kwa umeme kwa kile kinachodaiwa kuwa kuadimika kwa mafuta. Katika mazingira kama haya, kipaumbele si kutuma ujumbe, bali kutafuta kutafuta taarifa kuhusu viongozi wapya wa sehemu ya Kaskazini ya Nchi hiyo.
31 Julai 2010
Lebanoni: Utawala wa Dinosauri
Punde baada ya matukio ya unyanyasaji ya hivi karibuni nchini Lebanon, Msemo wa “Utawala wa Dinosauri” ulianza kutumika na wanaharakati wa mtandaoni kwenye kampeni dhidi ya uvamizi wa namna hii katika mitandao yao. Mwanablogu wa Lebanon Tony anaeleza maana ya msemo huo.
12 Julai 2010
3 Julai 2010

Ghana: Tangazo la Kibaguzi la Kombe la Dunia
Sokari anaandika kuhusu tangazo la biashara la Kombe la Dunia la kibaguzi lililotengenezwa na wakodishaji wa magari wa Kijerumani SIXT: “Tangazo hilo hapo juu lilitumwa kwangu na rafiki kutoka Ujerumani ambaye alifafanua hivi: Linacheza kauli mbiu kadhaa zenye mtazamo wa kiUlaya, mtazamo unaodharau Uafrika kuhusiana na mchezo wa mpira unaokuja kati ya Ghana/Ujerumani.”
21 Machi 2010

Lebanoni: Wafanyakazi wa Ndani Wanaotoroka
“Mfanyakazi wa ndani anapotoroka kutoka kwenye nyumba ya mwajiri wake, kituo cha polisi hakiwezi kufanya lolote kwa sababu hakuna sheria dhidi ya wafanyakazi wa ndani wanaotoroka. Kwa hiyo ofisa wa kituo cha polisi anamwambia mwajiri wa ki-Lebanoni aseme kuwa (mtoro huyo) aliiba pesa,” anaandika Ethiopian Suicides.
22 Februari 2010
Vazi la Burka Lauelemea Utaratibu wa Tamaduni Mbalimbali Kuishi Pamoja
Tangu mapendekezo ya kupiga marufuku uvaaji wa burqa au hijab huko Ufaransa, suala hilo limekuwa likitokota katika ulimwengu wa bloghu wa Australia. Mtangazaji wa redio katika mtindo wa kushtua umma, ambaye pia ni askari polisi wa zamani, alishutumiwa hivi karibuni juu ya kupinga kuvaliwa kwa hilo vazi la burqa.
22 Januari 2010
Marekani: Dkt. Martin Luther King, Jr. Akumbukwa
Martin Luther King Jr. alizaliwa tarehe 15 Januari, 1929 na akawa mmoja wa wasemaji na watetezi wakuu wa Harakati za Haki za Kiraia huko Marekani. Nchini Marekani, anaenziwa kwa sikukuu ya taifa, inayoadhimishwa kila mwaka siku ya Jumatatu ya tatu ya mwezi Januari. Leo, wanablogu wengi nchini Marekani wanaadhimisha kumbukumbu yake kwa kuandika makala za kumuenzi, huku wakiungalisha urithi wake wa masuala ya haki za jamii na masuala ya leo, wakionyesha wazi kuwa miaka 42 baada ya kuuwawa kwa King, maneno yake bado yana maana.
9 Januari 2010
Australia: Mauaji ya Mhindi Yazua Mzozo
Mauaji ya mtu mwenye asili ya India mjini Melbourne yamewasha tena mjadala kuhusu ubaguzi wa rangi nchini Australia na usalama wa wanafunzi kutoka ng’ambo. Kadhalika yameathiri uhusiano kati ya Australia na India. Mwandishi wa GV Kevin Rennie anakusanya maoni ya wanablogu wa Australia.
20 Disemba 2009
Wapiga picha wa Kiafrika, waandishi na wasanii wapata sauti zao kwenye blogu
Kadri Waafrika wengi wanavyozidi kugundua nguvu ya kublogu kama zana ya kutoa maoni kwa kiwango cha dunia nzima, tarakimu ya wanablogu imeongezeka na pia maudhui yanayopewa kipaumbele. Kwa tarakimu hiyo ya kukua kwa blogu, wasanii wengi wa Kiafrika wamejiunga, na ongezeko kubwa likionekana kwenye blogu za mashairi kama ilivyo kwa upigaji picha unaochipukia na blogu za sanaa za maonyesho. Tunazipitia baadhi.




























Kiungo cha RSS kwa Ethnicity & Race 









mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...