The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Environment Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Environment

2009-11-14

Philippines: Mti wa Dita Waokoa Maisha ya Watu 36 Wakati wa Mafuriko

Mti wa aina ya Dita huko Manila mjini uligeuka kuwa "Mti wa Uzima" wakati ulipotumika kama kimbilio na wakazi ambao walitegwa kwenye nyumba zao wakati wa janga la kimbunga na mafuriko ya hivi karibuni. Somo: Usikate miti.

2009-11-10

Sub-Saharan Africa

Chidi Opara anamkumbuka Ken Saro-Wiwa, Mwandishi wa Kinaijeria, mwanaharakati wa mazingira na haki za walio wachache ambaye aliuwawa na watawala wa kijeshi wa Naijeria tarehe 10 Novemba, 1995.

2009-11-08

Nepal: Mapinduzi Ya Gesi Inayotokana na SamadiVideo post

Nchini Nepal karibu asilimia 87 ya kaya zinategemea kuni kama chanzo cha nishati. Hata hivyo, vituo vya kuzalisha gesi inayotokana na samadi vinajitokeza kwa idadi kubwa nchini Nepal na kuanzisha mapinduzi ya kijani.

2009-11-07

Bolivia: Uhaba wa Maji Kwa Sababu ya Theluji Inayoyeyuka

Conversations for a Better World
Safu ya milima ya Chacaltaya ina baadhi ya vilele ambavyo ni alama zenye maana katika safu ya milima Andes iliyopo Bolivia. Kwa kuwa ilikuwa ni sehemu moja pekee ambapo mchezo wa kuteleza barafuni uliweza kufanyika katika nchi hii ya milimamilima, milima hii ni maarufu sana kwa wale walio kwenye Idara ...

2009-11-03

Middle East & North Africa

Katika Th!nk About It, Adela anaandika kuhusu Siku ya Kimataifa ya Bahari Nyeusi.

2009-10-28

Americas

Repeating Islands anaripoti kuhusu mauaji ya Wahaiti wanne katika Jamhuri ya Dominica

2009-10-26

Americas

“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake kusikika”: Attillah Springer anajihusisha na kampeni ya hali ya hewa 350.

2009-10-23

Ghana: Siku ya Kublogu mwaka 2009

Kwenye siku ya Kublogu Kwa Vitendo Duniani, Waghana waliwahoji viongozi wa dunia, walichachafya karatasi za Benki ya Dunia, walitambulisha tovuti mpya na walijiuliza ni kwa nini kulikuwa na majadiliano machache sana yanayohusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa nchini – na pia walitambua kwamba kuna mambo fulani nchi kama Ghana zinayafanya vyema.