Habari kuhusu Uchaguzi kutoka Aprili, 2011
Misri: Basboussa kwa Urais!
Mtangazaji habari wa zamani wa televisheni ya Misri na mwanaharakati Bothaina Kamel alitangaza kwenye twita kwamba ana mipango ya kugombea urais. Yafuatayo ni maoni ya kumuunga mkono na kupinga hiyo mipango yake .
Naijeria: Wafuatiliaji wa twita unaoweza kuwafuatilia wakati wa Uchaguzi wa Naijeria mwaka 2011
Ni wakati wa uchaguzi nchini Naijeria. Uchaguzi wa Wabunge umeahirishwa mpaka Jumatatu kutokana na hitilafu za kiuratibu. Uchaguzi wa Rais utafanyika tarehe 9 Aprili 2011. Hii ni orodha yetu ya kwanza ya watumiaji wa twita waliopendekezwa kama utapenda kufuatilia uchaguzi wa Naijeria 2011.
Naijeria: Wanablogu wa Ki-Naijeria wanasema nini kuhusu uchaguzi wa mwaka 2011?
Kadiri uchaguzi wa mwaka 2011 nchini Naijeria unavyozidi kukaribia, Wanablogu wa Naijeria wanatumia muda wao mwingi kuzungumza juu ya uchaguzi huo lakini je kuna mtu anayesikiliza?
Naijeria Yapiga Kura 2011: Maoni kutoka kwenye Uchaguzi
Wanaijeria walipiga kura jana katika uchaguzi wa tatu wa rais tangu taifa hilo lilipoingia kwenye utawala wa kiraia mwaka 1999. Mpaka sasa, uchaguzi huo umeelezwa na wengi kuwa ulikuwa wa mafanikio, huku kukiwa na taarifa za ghasia za hapa na pale pamoja na hitilafu za upigaji kura. Vyanzo vya habari vimeripoti kuwa watu wengi walijitokeza, foleni zenye kufuata utaratibu, na wapiga kura kusubiri hadi uchaguzi utakapomalizika ili kuhakikisha kwamba kura zao zimehesabiwa. Wanablogu wanajadili.
Attahiru Jega: Kiongozi wa Tume ya Uchaguzi ya Naijeria au Mtekaji?
Watumiaji wa mtandao wa Intaneti wa Naijeria wanadai kwamba utando usio na mwangaza wa siasa za Naijeria unahitaji mwamuzi mwenye uwezo wakati wa Uchaguzi wa 2011. Attahiru Jega, bosi wa tume ya uchaguzi itabidi adhihirishe katika majuma yajayo kuwa uchaguzi utakuwa mwepesi kama A, B, C.
Naijeria: Je, Teknolojia itaathiri uchaguzi wa mwaka 2011?
Wanaijeria wanaingia kwenye uchaguzi tarehe 16 Aprili 2011 kumchagua rais wao mpya. Uchaguzi uliahirishwa kutoka siku iliyokuwa imepangwa awali ya Aprili 9 kwa sababu ya kasoro za kimuundo. Katika makala hii tunatazama namna Wanaijeria wanavyotumia teknolojia kuwezesha uwazi katika uchaguzi, ushirikishwaji wa kisiasa na utawala bora.
Naijeria: Maonesho ya Picha za Kampeni ya Urais
George Esiri alifuatilia kampeni za kugombea urais za chama cha PDP huko Naijeria. Maonesho ya picha alizopiga yalizinduliwa jana katika Kituo cha Yar'Adua.