· Septemba, 2008

Habari kuhusu Uchaguzi kutoka Septemba, 2008

Angola: Uchaguzi Katika Picha

  22 Septemba 2008

Waangola wako katika uchaguzi kwa mara ya kwanza katika miaka 16 - uchaguzi bado unaendelea Jumamosi hii katika vituo 320 jijini Luanda. Mpaka sasa, hakuna matukio yoyote yaliyoripotiwa, na moyo wa utu umedumu, kama ilivyoangaliwa na mpiga picha Jose Manuel da Silva.

Msumbiji: Mgogoro wa Kisiasa Katika Jimbo la Kati la Beira

Waunga mkono wa Renamo wenye hasira walimwagika katika mitaa ya Beira ili kupinga uamuzi wa chama wa kumbadilisha Meya aliyeko madarakani Bwana Davis Simango na kumuweka Manuel Pereira kama mgombea wa kiti cha serikali ya manispaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Mwezi Novemba 2009. Mwanahistoria Egidio Vaz anaandika barua ya wazi kwa Rais wa Renamo, Bwana Alphonso Dhlakama katika blogu yake.

Paraguai: Kuapishwa Kwa Lugo Kwenye Flickr

  12 Septemba 2008

Rais wa paraguai alianza kutumia Flickr mnamo januari 2008 kama njia ya kuorodhesha nyendo zake wakati wa kampeni. Baada ya kuapishwa kama rais wa nchi siku ya tarehe 15 Agosti, anaendelea kutumia chombo hiki cha uandishi wa kijamii. Karibia picha 2,500 baadaye na zote chini ya haki miliki huria, Lugo anategemea kuwajumuisha WaParaguai nyumbani na ughaibuni katika urais wake.