The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Elections Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Elections

2009-11-04

Misri: Watu 10 Wenye Ushawishi Zaidi Nchini

Mtoto wa Rais wa Misri, Hosni Mubarak, anayitwa Gamal Mubarak, -- na ambaye anatarajiwa kumrithi baba yake nafasi hiyo -- aliibuka kama mmoja wa washindi 100 wa TIME. Wanablogu wa Ki-Misri wana ya kueleza kuhusu jambo hili.

2009-10-27

Uchaguzi Tunisia: haki Bila Ya Upendeleo!!?

Rais wa Tunisia Zine Al Abidine Ben Ali ameshinda uchaguzi kwa kipindi cha tano kwa asilimia 89.62 ya kura zote. Chama chake cha Democratic Constitutional Rally kilishinda viti vya bunge 161 katika viti 214. Wanablogu wa Tunisia wanatoa maoni katika makala hii.

2009-10-17

Sub-Saharan Africa

Mradi Wa Uchaguzi Afrika (AEP) www.africanelections.org utakuwa unafuatilia uchaguzi mkuu wa wa 10 wa Botswana, unaofanyika Oktoba 16, 2009.

2009-10-12

Gabon: Upinzani waendelea kupinga matokeo ya Uchaguzi

Wapinzani wa kisiasa wa Gabon wanaonyesha muungano wa vyama vya siasa kupinga matokeo ya uchaguzi wa mwezi Agosti, ambayo yalimkabidhi urais mwana wa mtawala wa kiimla aliyepita, Omar Bongo. Wanasiasa na raia wanaikemea Ufaransa kwa kuingilia siasa za nchi hiyo.

2009-07-27

Mauritania: Uchaguzi wenye udanganyifu?

Tarehe 18-07-2009, miezi 11 baada ya mapinduzi ya kijeshi yakiongozwa na Jenerali Mohamed Ould Abdel Aziz, Mauritania imemchagua Jenerali huyu kwa Urais, na kusababisha wapinzani wakuu wa Abdel Aziz kuukataa uchaguzi kwamba ni “kiini macho,” kwa mujibu wa Habari za BBC. Pitio la haraka haraka kwenye blogu za nchi za Saheli linaonyesha kwamba wapinzani wako katika ushirika mzuri.

2009-06-16

Irani: Maandamano na UkandamizajiVideo post

Mamia ya maelfu ya Wairani mjini Tehran na katika miji mingine kadhaa wameandamana kumuunga mkono mgombea urais Mir Husein Mousavi huku wakiipuuza amri ya serikali inayokataza maandamano. Japokuwa huduma za Twita, FaceBook pamoja na YouTube zimezuiliwa kwa kuzimwa nchini Iran, Wairani wengi wamekuwa wakitumia tovuti-vivuli ili kuvizunguka vichujio vilivyowekwa na wanaripoti habari kadiri zinavyotokea. Utawala wa Irani pia umezuia huduma za jumbe za maandishi kwa kutumia simu za mkononi (SMS), kadhalika utawala huo unachuja tovuti kadhaa zinazoakisi maoni ya wanamageuzi.

2009-06-14

Irani: Kimbunga cha Maandamano Baada Ya UchaguziVideo post

Maelfu ya watu waliandamana mjini Tehran, Mashdad na kwenye miji mingine mikubwa ya Irani ili kupinga ushindi wa Rais Mahmoud Ahmadinejad katika uchaguzi mkuu uliofanyika Ijumaa. Washindani wawili wanamageuzi pamoja na mashabiki wao wanasisitiza kwamba palitokea udanganyifu.

2009-06-13

Ramani ya Ulimwengu wa Blogu za Irani Siku ya Mkesha wa Uchaguzi

John Kelly na Bruce Etling wanaelezea utafiti wao unaohusu ulimwengu wa blogu za Irani na uchaguzi katika blogu ya Intaneti na Demokrasi. Intaneti na Demokrasi ni blogu ya timu ya mradi wa Intaneti na Demokrasi wa Kituo cha Berkman cha Intaneti & Jamii kilichoko Harvard. Kufuatana na ufuatiliaji wetu wa ...