GlobalVoices katika

Education

Hifadhi ya mada · 27 jumbe


Habari mpya Kuhusu Education

22 Januari 2013

Jukwaa la Kiafrika Lenye Makala za Bure za Kitaaluma

Video inayoonesha namna www.hadithi.org inavyofanya kazi kuboresha upatikanaji wa zana za utafiti kwa Afrika

Januari 24, ni siku ambayo inategemewa kuwa ya kuzindua rasmi Hadithi, ambalo ni jukwaa la kuhifadhia zana za bure za kitaaluma mjini Nairobi, Kenya. Wasomi mbalimbali na wadau wa mitandao watakusanyika pamoja kujadili upatikanaji wa zana huru za kitaaluma katika elimu ya juu nchini Kenya. Hadithi itasaidia kutafuta, kuona na kushusha makala kutoka katika taasisi za kitafiti duniani kote. Kujiandikisha kwa tukio hili, itafute Hadithi mtandaoni kupitia Facebook na tovuti ya Eventbrite.

23 Disemba 2012

Utambulisho wa Jamii ndogo ya Balkan

Face the Balkans subjects of stories

Picha ya mwonekano wa tovuti ya Balkans.

Waandishi vijana kumi na watano kutoka katika nchi zipatazo sita tofauti wametengeneza mfululizo wa masimulizi binafsi kuhusu masuala ya namna jamii zenye watu wachache (kwa mapana yake) zinavyoweza kuwakilishwa kutoka Bosnia na Herzegovina, Kosovo, Serbia, na Macedonia. Habari zinapatikana katika lugha za Kiingereza, Kijerumani, na Kifaransa katika mwonekano wa tovuti ya Balkans.

12 Novemba 2012

Maelfu Watia Saini Pendekezo la Zawadi ya Nobel na Kusherehekea Siku ya Malala

Soma makala hii.

Mwanaharakati wa elimu mwenye umri wa miaka 15 -- Malala Yousufzai -- aliyepigwa risasi mnamo tarehe 9 Oktoba 2012 na wanamgambo wa TTP, anaendelea kupata nafuu japo polepole. Mnamo tarehe 10 Novemba, watu kote ulimwenguni walimpongeza Malala kama kielelezo kwa ajili ya wasichana wapatao milioni 32 ambao hawapati fursa ya kwenda shulen.

30 Agosti 2012

Brazil: Mtoto wa Miaka 13 Aonyesha Matatizo ya Shule Kupitia Facebook

Diário de Classe [pt], ukurasa wa Facebook uliofunguliwa na Isadora Faber, aliye na miaka 13 na anayetokea Santa Catarina, Brazil, tayari umeonyesha kupendwa zaidi ya mara 176,000. Huku lengo lake likiwa ni “kuonyesha ukweli kuhusu shule za umma”, Isadora anaweka picha zinazoonyesha maeneo yanayohitaji kufanyiwa ukarabati katika shule yake pamoja na kutoa taarifa kuhusu matatizo mengine mengi ya jumla.

18 Agosti 2012

Photos jumbe
Morocco: Wanafunzi Wadai Marekebisho kwenye Mfumo wa Elimu

Soma makala hii.

Mwezi Julai, kikundi cha wanafunzi wa nchini Morocco kilizindua ukurasa wa Facebook ulioitwa "Umoja wa Wanafunzi wa Morocco kwa ajili ya Mabadiliko ya Mfumo wa Elimu". Pungufu ya mwezi mmoja, kikundi hiki kilivuta uungwaji mkono mkubwa hasa kupitia mitandao ya kijamii.

15 Julai 2012

Afrika: Ujuzi wa Matumizi ya Zana za Habari za Kijamii kwa Vijana Wanaoishi na Ulemavu.

Soma makala hii.

Warsha ya vijana walemavu kutoka kote barani Afrika lafanyika Dakar, Senegali. Warsha hii ilipangwa na DRI na YI. Imeandikiwa na Haute Haiku.

3 Aprili 2011

Saudi Arabia: Mfalme Awaahidi Wananchi wa Saudia Fedha Zaidi

Fedha zaidi zimeahidiwa kutolewa kwa wananchi wa Saudia, ahadi ambayo Mfalme Abdulla ameitoa kupitia hotuba yake kwa taifa leo. Katika hotuba hiyo iliyokuwa fupi, Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu aliwashukuru viongozi wa dini, waandishi na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa juhudi walizofanya kutetea ufalme. Matamko na Amri vilifuata ya kwamba mabilioni yatagawanywa kwa watu wa Saudia.

17 Agosti 2010

China: Pato la Taifa Linaongezeka, Matumizi Katika Huduma za Jamii je?

Soma makala hii.

Tunaendelea kusikia kuwa uchumi wa China unaendelea kukua; je matumizi ya huduma za jamii yameongezeka? Akiba binafsi zinabaki kwenye benki, anaandika mwanablogu mmoja: kutokea hospitali mpaka shuleni mpaka malipo ya uzeeni, China haiwezi kujilinganisha.

16 Agosti 2010

Moroko: Mtoto Mwanablogu Asalimia Ulimwengu

Soma makala hii.

Salma alianza kublogu akiwa na umri wa miaka sita ili kuwasiliana na ndugu na marafiki. Chii ya usimamizi wa wazazi wake, mwanablogu huyu mdogo wa Moroko anapendelea kuandika hadithi fupi fupi na kuielezea dunia matukio anayokumbana nayo kila siku shuleni.

16 Julai 2010

China: Kashfa ya Wizi wa Kitaaluma Uliofanywa na Wang Hui, Mtazamo wa Kimataifa

Kuna kashfa ya wizi wa kitaaluma iliyoibuka mwezi Machi katika duru za kitaaluma za Kichina pale Profesa wa Fasihi wa Chuo Kikuu cha Nanjing, Wang Binbin, alipotuhumu kwamba kazi ya...

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha