· Januari, 2010

Habari kuhusu Uchumi na Biashara kutoka Januari, 2010

China: Kwa Heri Google

  13 Januari 2010

Kufuatia tangazo la Google leo kuwa ikiwa serikali ya China haitaruhusu tawi lake la China kusitisha uzuiaji wa matokeo ya kutafuta tawi la Google nchini China litafungwa, wanamtandao walitembea mpaka kwenye ofisi za Google mjini Beijing ili kuweka maua. HABARI MPYA: picha zaidi hapa, uwekaji rasmi wa maua (ya rambirambi)...

Msumbiji: Kifo Cha Mradi Mkubwa wa Mazao Nishati

Mwishoni mwa mwezi Disemba, Baraza la Mawaziri la Msumbiji lilitoa tamko muhimu. Kibali cha kutumia Hekta 30,000 za ardhi kwa kampuni ya mazao nishati (biofuels) Procana, kimebatilishwa. Shauri la Mradi wa Procana, ulipo kwenye eneo kubwa linalopakana na Mbuga ya Taifa ya Limpopo ambayo imetanda mpaka nje mpaka wa nchi, lilikuwa na utata pamoja na mvutano mkubwa tangu (shauri hilo) lilipoanza mwanzoni mwa mwaka 2007.