GlobalVoices katika

Economics & Business

Hifadhi ya mada · 49 jumbe


Habari mpya Kuhusu Economics & Business

27 Februari 2013

Bulgaria: Gharama Kubwa za Nishati Zasababisha Maandamano

Soma makala hii.

Ruslan Trad anataarifu kuwa, siku ya Jumapili tarehe 17 Februari, makumi ya maelfu ya watu katika mji mkuu wa Bulgaria, Sofia pamoja na majiji mengine waliendelea na maandamano kupinga bei kubwa za nishati ya umeme pamoja na gharama za kupasha joto.

29 Disemba 2012

China Inaelekea Wapi kwa Mwaka 2013?

Kadri mwaka wa 2012 unavyosogea karibu, jarida la CHINA DIGITAL TIMES limetoa muhtasari wa mabadiliko na changamoto zinazoikabili China mwaka 2013 kwa kutumia taarifa na bashiri mbalimbali za vyombo vya habari.

15 Oktoba 2012

Video jumbe
Zambia: Filamu yaYouTube Kuhusu Athari za Machimbo ya Madini

Soma makala hii.

Filamu ya Uchunguzi yenye jina "Zambia: Shaba Nzuri, Shaba Mbaya" inayohusu machimbo ya shaba nchini Zambia na athari zake kwa jamii imewekwa kwenye mtandao wa YouTube na mpaka sasa imevuta watazamaji zaidi ya 6,000. Baada ya kuitazama filamu hiyo, mtumiaji mmoja wa mtandao wa YouTube aliandika, "Jililie eeh nchi yangu nzuriKwa nini tubaki masikini katikati ya utajiri huu wa madini yanayochimbwa kwa gharama ya afya za wenyeji?"

10 Oktoba 2012

Côte d'Ivoire: Wafanyakazi wa Afya Wagoma baada Miezi Minne Bila Mshahara

S.B anatoa maoni juu ya kuanza kwa mgomo usio na ukomo unaoratibiwa na wafanyakazi wa taasisi za afya mjini Abidjan. Katika mtandao wa Connection Ivorienne, anabainisha [fr] kwamba:

Kufuatia mabadiliko ya utolewaji wa huduma za afya ambazo zilitolewa bure kabisa baada tu ya kumalizika kwa mgogoro wa baada ya uchaguzi, sera iliyoanzishwa na serikali ya Côte d'Ivoire, ambayo sasa imeelekeza baadhi ya huduma tu ndizo zitakuwa bure, wafanyakazi wa taasisi kadhaa za afya hawajapata mishahara yao kwa wakati. Kibaya zaidi ni kwamba wakubwa wao hawakupata fungu lolote kwa ajili hiyo kwa zaidi ya miezi kumi na sita.

30 Septemba 2012

Video jumbe
Mbinu za Kugundua Dawa Bandia katika Nchi Zinazoendelea

Soma makala hii.

Watu 700,000 hufa kila mwaka kwa kutumia dawa bandia za malaria na saratani pekee. Shirika la Afya Duniani, WHO linasema katika ripoti yake kuwa, mapato kutoka kwa dawa hizi kila mwaka hukaribia dola bilioni 200.

12 Juni 2012

Video jumbe
Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella

Soma makala hii.

Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.

Kenya: Intani walipwe au wasilipwe?

Soma makala hii.

Mada hapa ni kuhusu kama inafaaa au haifai kwa intani kulipwa,mjadala ulioanzishwa na @RobertAlai.

14 Disemba 2011

Madagaska: Wajadili Uhalali wa Uwekezaji wa Kigeni wa Moja kwa Moja

Soma makala hii.

Wakati Madagaska ikijaribu kutafuta suluhisho la matatizo ya muda mrefu ya kiasa, Wanablogu wa ki-Malagasi wanajadili thamani ya Uwekezaji unaofanywa Moja kwa Moja na raia wa Kigeni. Wa-Malagarasi wanaamini kwamba Madagaska, kama nchi nyingine za Kiafrika inao utajiri mkubwa wa rasili mali lakini tatizo likiwa ardhi yenyewe kupokonywa kwa sababu ya utawala mbovu na biashara zisizoangalia maslahi ya wananchi.

13 Disemba 2011

Zambia: Rais Sata Aituhumu Benki Kuu Kuchapisha Noti Bandia

Soma makala hii.

Rais Michael Sata ameweka wazi kwamba Benki Kuu ya Zambia kwa maelekezo ya kilichokuwa chama cha Upinzani nchini humo MMD, ilichapisha “noti bandia” ambazo inasemekana ziko kwenye mzunguko wa fedha. Hata hivyo, Chama cha MMD kwa kupitia Waziri wake wa zamani wa Fedha Situmbeko Musokotwane, kimekana tuhuma hizo kikisema Benki Kuu inayo uhuru wa kuchapisha noti mpya za ziada bila kuwasiliana na Waziri wa Fedha ama Rais kwa sababu ina mamlaka kamili ya kufanya hivyo.

3 Aprili 2011

Saudi Arabia: Mfalme Awaahidi Wananchi wa Saudia Fedha Zaidi

Fedha zaidi zimeahidiwa kutolewa kwa wananchi wa Saudia, ahadi ambayo Mfalme Abdulla ameitoa kupitia hotuba yake kwa taifa leo. Katika hotuba hiyo iliyokuwa fupi, Mlinzi wa Misikiti Miwili Mitukufu aliwashukuru viongozi wa dini, waandishi na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa juhudi walizofanya kutetea ufalme. Matamko na Amri vilifuata ya kwamba mabilioni yatagawanywa kwa watu wa Saudia.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha