The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Disaster Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Disaster

2009-11-14

Philippines: Mti wa Dita Waokoa Maisha ya Watu 36 Wakati wa Mafuriko

Mti wa aina ya Dita huko Manila mjini uligeuka kuwa "Mti wa Uzima" wakati ulipotumika kama kimbilio na wakazi ambao walitegwa kwenye nyumba zao wakati wa janga la kimbunga na mafuriko ya hivi karibuni. Somo: Usikate miti.

2009-05-19

Sri Lanka: Wanablogu Watathmini Kifo cha Kiongozi wa LTTE

Serikali ya Sri Lanka imetangaza kwa kupitia vyombo vya habari vya taifa pamoja na ujumbe wa simu za mkononi mchana leo (Jumatatu, 18 Mei, 2009) kwamba kiongozi wa Kundi linalotaka kujitenga la Wa-Tamil, the Liberation Tigers of Tamil Eelam (LTTE), Vellupillai Prabhakaran, amefariki. Salamu za rambirambi zinaashiria kwamba alikuwa shujaa kwa baadhi ya watu kadhalika wengine walimchukulia kama muuaji katili. Wanablogu wa Ki-Sri Lanka wanatathmini urithi wa kiongozi huyu wa vita na maana ya kifo chake kwa mustakabali wa Watamil na watu wa Sri Lanka.

2009-02-26

Misri: Wanablogu Wafuatilia Milipuko ya Mabomu Mjini Kairo

Mtalii wa Kifaransa ameuwawa na watu wapatao 20 wamejeruhiwa wakati bomu lilipolipuka nje ya msikiti wa Al Hussein uliopo katika eneo la utalii la Khan Al Khalili mjini Kairo. Na wakati dunia ilipokuwa inaanza kufahamu ni kipi kilichokuwa kinatokea, wanablogu wa Misri waliingia kazini haraka, wakipashana habari za yanayotukia, taarifa, uchambuzi na hofu zao.

2009-01-27

Madagaska: Kimbunga Chasababisha Kimbunga Cha KisiasaPhotos post

Baada ya siku chache kupita nchini Madagaska, idadi rasmi ya madhara yaliyosababishwa na kimbunga kilichopewa jina la Fanele zimewasilishwa. Rais Ravalomanana alikwenda kwenye moja ya maeneo yaliathirika na kimbunga ili kutathmini madhara yaliyotokea. Uandishi wa kiraia wakati wa kimbunga Wakati idara inayoangalia athari na majanga, BGNRC bado haina tovuti, taarifa zinahusu ...

2009-01-21

Malaysia: Mafunzo Yanayotokana na Mafuriko

Wiki iliyopita, mafuriko yaliyakumba maeneo mbalimbali katika jimbo la Sarawak nchini Malaysia. Wanablogu wanaandika yaliyotukia na mafunzo yaliyotokana na janga hilo la mafuriko. Mafuriko hayo ni mabaya zaidi kutokea katika miaka mingi nchini Malaysia.