Habari kuhusu Harakati za Mtandaoni kutoka Machi, 2012
Korea Kusini: Wahudumu wa ndege wapigania haki ya kuvaa suruali
Katika Siku ya Wanawake Duniani, wahudumu wa moja ya mashirika makubwa ya ndege nchini Korea Kusini, waliitisha mkutano na waandishi wa habari mbele ya makao makuu ya shirika lao la ndege kudai haki ya kuvaa suruali. Madai hayo yamepata uungwaji mkono mkubwa sana na watumiaji wa mtandao wa nchini humo.
Amerika Kusini: Waathirika wa ‘biashara’ ya kukuza matiti waingia mtandaoni
Wanawake wengi wameungana kwenye tovuti za kijamii kusema wanachofikiri na kubadilishana taarifa kuhusu matatizo yanayosababishwa na viini vya kukuzia matiti. Wakati huohuo wanapanga hatua gani za kisheria wachukue. Kumekuwa na ongezeko kubwa la ugonjwa wa saratani huko Amerika ya Kusini. Je, ni kina nani hawa wanaopaaza sauti zao barani humo? Fuatilia ...
Baada ya Kony 2012, “What I Love About Africa” Yanyakua Mazungumzo
Kampeni katika mtandao kuhusu mhalifu wa kivita Joseph Kony umesababisha utata mkubwa barani Afrika. Kampeni nyingine ya kupinga utata huo na kuonyesha upande bora wa bara la Afrika, unaojulikana kama #WhatILoveAboutAfrica (Nini Ninachopenda Kuhusu Afrika) sasa unaenea katika tovuti la Twitter.