Habari kuhusu Harakati za Mtandaoni kutoka Agosti, 2010
Tunisia: Picha ‘Zilizochakachuliwa’ ni Dalili ya Hali Halisi katika Vyombo vya Habari vya Kitaifa
Utumiaji vyombo vya habari vya kitaifa nchini Tunisia kama chombo vya kupigia propaganda ni jambo ambalo limeripotiwa vya kutosha. Ushahidi wa hivi karibuni kabisa wa utumiaji mbaya wa vyombo vya habari umewekwa bayana na wanablogu wa nchi hiyo mnamo tarehe 20 Agosti baada ya magazeti ya Le Temps na Assabah kuchapisha ripoti kuhusu taasisi ya hisani ya Zeitouna kutuma msaada wa kibinadamu wa chakula kwa waathirika wa mafuriko nchini Pakistani.
Irani: Kampeni ya Kutaka Mwanablogu-Mpiga Picha Hamed Saber Kuachiwa Huru
Zaidi ya wanafunzi 70 waliohitimu elimu ya chuo kikuu na wasomi wa nchini Irani wametoa wito wa kuachiwa kwa Hamed Saber, ambaye ni mwanablogu-mpiga picha na mwanasayansi wa kompyuta wa nchini humo aliyekamatwa pasipo sababu za kuelewekea mnamo tarehe 21 Juni 2010 jijini Tehran.
Italia: HAPANA kwa Vikwazo Dhidi ya Uhuru wa Kujieleza wa Mtandaoni
Muswada mpya wa habari na Unasaji wa siri wa Mawasiliano ambao umewasilishwa kwenye bunge la Italia unaweza kuanzisha "hatari ya malipo ya fidia" kwa wanablogu wote na vyombo vya habari vya mtandaoni.