The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Development Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Development

2009-11-10

Angola: Gharama za Juu za Maisha Mjini Luanda

Gharama kubwa ya maisha nchini haieleweki: viashiria vya maendeleo vya hali ya juu havishabihiani na hali ya kifedha ya Waangola wengi na havitafsiriki katika viwango vya maisha vya wasio na hali nzuri kiuchumi.

2009-11-04

Sub-Saharan Africa

Mradi wenye lengo la kutengeneza ramani mpya ya wazi ya kitongoji cha Kibera mjini Nairobi, Kenya: “Na jana tulimaliza siku nzima pale MS Action Aid kenya, ambako wanafunzi wa ki-Denmark pamoja na wengine waliotokea kwenye mashirika mbalimbali kama vile Ushahidi, UNICEF, Umande Trust na World Bike, walipoonyeshwa mbinu za kutengeneza ramani.”

2009-10-23

Ghana: Siku ya Kublogu mwaka 2009

Kwenye siku ya Kublogu Kwa Vitendo Duniani, Waghana waliwahoji viongozi wa dunia, walichachafya karatasi za Benki ya Dunia, walitambulisha tovuti mpya na walijiuliza ni kwa nini kulikuwa na majadiliano machache sana yanayohusu Mabadiliko ya Hali ya Hewa nchini – na pia walitambua kwamba kuna mambo fulani nchi kama Ghana zinayafanya vyema.

2009-06-09

Uganda: Mradi wa Katine Wawafikisha Wanakijiji Kwenye Ulimwengu wa Blogu

Inakadiriwa kuwa matumizi na uenezi wa intaneti nchini Uganda ni kwa kiwango cha asilimia sita tu, idadi ambayo inazuia sehemu kubwa ya watu kujiunga na ulimwengu wa blogu nchini Uganda au kuweza kuwasiliana na ulimwengu wa blogu duniani. Mradi wa Katine unaoendeshwa na Guardian and Observer unafanya kazi kubadilisha hali hiyo katika kijiji kimoja.

2009-03-24

Papa Nchini Kameruni (1): Utata wa Safisha-safisha Jijini Yaounde

Papa Benedikti wa XVI anazuru Kameruni kuanzia tarehe 17 mpaka tarehe 20 Machi 2009. Ziara hii imepelekea serikali kuchukua hatua kali za usafi, ambazo zimezua utata mkubwa katika ulimwengu wa blogu nchini Kameruni.

2009-03-06

Gumzo la moja kwa moja kuhusu Virusi vya ukimwi na Ukimwi mtandaoni Tarehe 6 machi

Rising Voices
Mradi wa Rising Voices na Global Voices wanaandaa gumzo la moja kwa moja mtandaoni kwa wanablogu na wanaharakati siku ya Ijumaa mwezi wa tatu mwaka huu(saa 11 jioni kwa saa za Nairobi) mada kuu ikiwa jinsi ya kublogu na kuongeza uelewa na habari kuhusu virusi vya ukimwi na Ukimwi.

2008-09-21

Msumbiji: Mgogoro wa Kisiasa Katika Jimbo la Kati la Beira

Waunga mkono wa Renamo wenye hasira walimwagika katika mitaa ya Beira ili kupinga uamuzi wa chama wa kumbadilisha Meya aliyeko madarakani Bwana Davis Simango na kumuweka Manuel Pereira kama mgombea wa kiti cha serikali ya manispaa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Mwezi Novemba 2009. Mwanahistoria Egidio Vaz anaandika barua ya wazi kwa Rais wa Renamo, Bwana Alphonso Dhlakama katika blogu yake.

2008-09-06

Venezuela: Wahindi wa Yukpa, Chavez na Mgogoro wa ArdhiVideo post

Picha za video zinazotumwa kwenye mtandao wa internet na vyombo vya habari vya kiraia zinaonyesha yale yanayojiri kuhusu mgogoro unaoibuka nchini Venezuela kati ya Wahindi wa jamii ya Yukpa wanaoishi katika milima ya Perijá, wamiliki wa ardhi na Rais Chávez. Mgogoro huu kuhusu mipaka ya ardhi umekuwapo kwa takribani miaka 30, yaani tangu pale vikosi vya jeshi vilipowandoa kwa nguvu wanajamii wenyeji ya Ki-Yukpa na kuwapa ardhi hiyo wamiliki wapya walioanzisha mashamba makubwa ya mifugo, hasa ng'ombe, ambao wameendelea kuitumia ardhi hiyo tangu wakati huo.