GlobalVoices katika

Development

Hifadhi ya mada · 36 jumbe


Habari mpya Kuhusu Development

12 Februari 2013

Udhaifu wa Watawala wa Afrika unajionesha Mali?

Ousmane Gueye katika tovuti ya Mondoblog anaandika [fr] kuhusu kuchelewa kupeleka vikosi vya kijeshi kasikazini mwa Mali:

Kama tungekuwa tunasaiili matokeo ya watu wenye amani na huru kuingilia kati hali ya mambo nchini Mali, basi ni wazi kuwa kwa kuchelewa kupeleka vikosi vya ulinzi, nchi za Afrika zimewakosea wananchi wa Mali kwa mara nyingi…kelele zote za wakuu wa nchi lakini bado hawajaweza kutimiza lengo lolote waliloliweka wao kama hatua ya kupunguza nguvu ya Waslamu wenye msimamo mkali nchini Mali.

1 Januari 2013

Kuhusiana na Vuguvugu la Mabadiliko ya Umma

Gaurav Mishra anachambua nguvu ya vuguvugu la mabadiliko linaloanzia kwa watu wa kawaida na namna inavyofanya kazi kuleta mabadiliko chanya katika utendaji wa vyombo vikuu vya habari kwa kutumia vyombo vya habari vya kiraia.

30 Disemba 2012

Video ya Kuomba Ujenzi wa Vyoo vya Umma huko Jharkhand, India

Amit Topno, mwakilishi wa jumuiya ya hiari “inayopiga picha za video” aliripoti kwamba wakati wa kijiji cha Nichitpur katika Jimbo la Jharkhand hawana choo chochote cha umma kinachotumika. Wanavijiji wanaziomba mamlaka za serikali za mitaa kupitia video hii kuhakikisha kuwa vyoo vinavyostahili matumizi ya binadamu vinajengwa.

22 Oktoba 2012

India: Mgogoro wa Mtambo wa Nyuklia wa Kudankulam Waendelea.

Soma makala hii.

Mradi wa Nguvu za Nyuklia mjini Koodankulam katika wilaya ya Tirunelveli iliyo katika Jimbo la kusini la Tamil Nadu nchini India umeanza kufanya kazi mwezi uliopita lakini maandamano ya kuupinga mradi huo umeendelea na kamata kamata inasababisha waandamanaji kuishia jela. Juma hili limeshuhudia maandamano yakienea India yote kwa ushirikiano na watu wanaopinga matumizi ya Mtambo wa Nyuklia.

15 Oktoba 2012

Video jumbe
Zambia: Filamu yaYouTube Kuhusu Athari za Machimbo ya Madini

Soma makala hii.

Filamu ya Uchunguzi yenye jina "Zambia: Shaba Nzuri, Shaba Mbaya" inayohusu machimbo ya shaba nchini Zambia na athari zake kwa jamii imewekwa kwenye mtandao wa YouTube na mpaka sasa imevuta watazamaji zaidi ya 6,000. Baada ya kuitazama filamu hiyo, mtumiaji mmoja wa mtandao wa YouTube aliandika, "Jililie eeh nchi yangu nzuriKwa nini tubaki masikini katikati ya utajiri huu wa madini yanayochimbwa kwa gharama ya afya za wenyeji?"

30 Septemba 2012

Video jumbe
Mbinu za Kugundua Dawa Bandia katika Nchi Zinazoendelea

Soma makala hii.

Watu 700,000 hufa kila mwaka kwa kutumia dawa bandia za malaria na saratani pekee. Shirika la Afya Duniani, WHO linasema katika ripoti yake kuwa, mapato kutoka kwa dawa hizi kila mwaka hukaribia dola bilioni 200.

12 Juni 2012

Video jumbe
Ethiopia: Ardhi, Historia na Haki katika Eneo la Gambella

Soma makala hii.

Wanaharakati wa masuala ya ardhi wanatumia hati ya malalamiko ya mtandao, mtandao wa facebook na twita kufanya kampeni dhidi ya unyang’anyi wa ardhi nchini Ethiopia. Inaarifiwa kwamba wanakijiji kwenye jimbo msikini zaidi nchini humo, Gambella, wanalazimishwa kuhamia kwenye vijiji vilivyobuniwa na serikali ili kuwapisha wanaoitwa 'wawekezaji' wakubwa.

7 Juni 2012

Kenya: Wanaharakati wapigana vita dhidi ya ufisadi kwa intaneti

Soma makala hii.

I Paid a Bribe ni njia mojawapo inayotumiwa na wanaharakati dhidi ya ufisadi nchini, kwa kutumia teknolojia mpya ili kuwawezesha kupata ripoti za utoaji wa hongo.' I paid a Bribe' imefuatia muundo wa ‘India Anti-Corruption Portal (IPAB)' na ni ushirkiano kati ya IPAB na Wamani Trust ya Kenya ili kuleta IPAB katika Afrika Mashariki na Kati.

15 Aprili 2012

Photos jumbe
Zambia: Rais Awakera Raia Waishio Nje

Soma makala hii.

Rais wa Zambia, Michael Sata, amewakasirisha raia wa nchi hiyo wanaoishi ng'ambo baada ya kuwakejeli wakati wa ziara yake ya siku tatu nchini Botswana na kufifisha matumaini yao ya kuanzishwa kwa uraia wa nchi mbili katika Katiba ya nchi ya hiyo.

14 Disemba 2011

Madagaska: Wajadili Uhalali wa Uwekezaji wa Kigeni wa Moja kwa Moja

Soma makala hii.

Wakati Madagaska ikijaribu kutafuta suluhisho la matatizo ya muda mrefu ya kiasa, Wanablogu wa ki-Malagasi wanajadili thamani ya Uwekezaji unaofanywa Moja kwa Moja na raia wa Kigeni. Wa-Malagarasi wanaamini kwamba Madagaska, kama nchi nyingine za Kiafrika inao utajiri mkubwa wa rasili mali lakini tatizo likiwa ardhi yenyewe kupokonywa kwa sababu ya utawala mbovu na biashara zisizoangalia maslahi ya wananchi.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha