Kutokuwepo uwazi na weledi katika mchakato wa kumchagua mgombea, mbali na kufahamika nani hasa watachukua nafasi zinazogombewa kabla hata ya uchaguzi katika taasisi hiyo. Hizo zilikuwa baadhi ya sababu zilizotolewa na mwanaharakati wa haki za binadamu, Benilde Nhalivilo, wakati akijitoa rasmi kugombea nafasi kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Msumbiji[pt], chombo kinachohusika na kuandaa na kusimamia chaguzi nchini humo. Taarifa zaidi zinapatikana kwenye gazeti la A Verdade [pt].
Habari Maalum Kuhusu Citizen Media
-
China Yadhibiti Habari za Maandamano Yakupinga Kujenga Kiwanda cha Kemikali
6 Mei 2013
-
Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia
4 Mei 2013
-
Urusi: Wapinzani Wapumbazwa na Uchaguzi wa Awali, Wapoteza Uchaguzi Halisi
30 Aprili 2013
-
Irani: Je, Dola Inamwogopa Msichana wa Miaka 13?
30 Aprili 2013
-
Bangladesh: Jengo Laporomoka, Mamia Wauawa kwenye Vifusi
29 Aprili 2013
Habari mpya Kuhusu Citizen Media
7 Mei 2013

Mfululizo wa Tamthilia ya Runinga ya Nchini Tanzania
The Team Tanzania (Timu Tanzania) ni mfululizo wa Tamthilia ya Runinga yenye kuzungumzia:
[...] Bi. Wito, mwalimu mahiri wa somo la uraia, anaigeuza kabisa mitazamo ya vijana makinda watatu anapowauliza maswali mazito mfano “Wewe ni nani”? vijana wale wenye umri wa miaka 16, waliofahamiana vyema tangu wakikua. Katika kuingia katika umri wa utu uzima, vijana hao wanatafuta kujitambua huku wakikabiliwa na misongo mingi ya kifamilia na kiutamaduni.

Michoro ya Dar: Sanaa kwa Maendeleo Endelevu
Dar Sketches (Michoro ya Dar) ni sehemu ya mradi unaoanzia ngazi ya Mtaa jijini Dar Es Salaam, Tanzania ulioanzishwa na msanii na mchoraji Sarah Markes:
Ni katika kuenzi urithi wa kitamaduni na wa sanaa ya ubunifu wa majengo kwa jiji la Dar Es Salaam sambamba na juhudi za kukuza uelewa kwa wananchi juu ua tishio la urithi huu linalotokana na kasi kubwa ya kupanuka holela kwa jiji hilo.
6 Mei 2013

TEDXSão Tomé: Mkutano Wanukia São Tomé na Príncipe

TEDXSão Tomé
Uandikishaji wa awali kwa ajili ya mkutano wa TEDXSão Tomé umezinduliwa rasmi. Mkutano huo una kaulimbiu inayosema “Visiwa Vimeunganishwa : São Tomé + Príncipe = Áfrika Vimeunganishwa na Ulimwengu” na utafanyika tarehe 20 Juni. Wasemaji katika mkutano huo waliothibitishwa ni pamoja: Dynka Amorim, Ismael Sequeira, Profesa Robert Drewes na Aoaní d'Alva. Tiketi linapatikana kwa Euro 20. Zaidi kuhusu mkutano huo tembelea ukurasa wa Facebook na tovuti [viungo vyote katika lugha ya Kireno].
5 Mei 2013

Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska
Habari Mpya: Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito.
Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana wasiotarajiwa wamejitokea kuwania kiti hicho. Wakati wagombea wa awali walikuwa wapya kabisa wasiofahamika sana, wanasiasa wachache machachari wanaofahamika wanatarajiwa kugombea akiwemo rais wa zamani Didier Ratsiraka, rais wa sasa wa mpito Andry Rajoelina [fr] na mke wa rais wa zamani Ravalomanana, anayeitwa Lalao Ravalomanana.
4 Mei 2013
Ethiopia: Mwanablogu Ahukumiwa Miaka 18 Jela kwa “Kuvunja Katiba”

Mnamo Mei 1, Mahakama Kuu ya Ethiopia ilitoa hukumu kali kwa mwandishi aliyeshinda tuzo Eskinder Nega, ambaye sasa atatumikia kifungo cha miaka 18 jela. Mohamed Keita wa Kamati ya Kuwalinda Waandishi anasema, “Kushitakiwa na hatimaye kutiwa hatiani kwa Eskinder na waandishi wengine ni dalili za utawala unaoogopa maoni ya raia wake.”
Wabunge wa Ukraine Wataka Utoaji Mimba Upigwe Marufuku Kisheria
Mapema mwezi Aprili, Wabunge watatu kutoka kambi ya Upinzani iitwayo“Svoboda” walipeleka mswada bungeni wenye lengo la kupiga marufuku utoaji mimba nchini Ukraine. Tetyana Bohdanova anataarifu mwitikio wa watumiaji wa mtandao kufuatia hatua hii ya Bunge la Ukraine.
29 Aprili 2013
Ujasiriamali,Utamaduni na Mshikamano katika Afrika
Pamoja na ukuaji mkubwa wa kiuchumi, bara la Afrika bado linahangaika kukuza kada ya wajasiriamali wazawa watakaoweza kudhibiti viwanda vya kimkakati. Wasomi na watafiti wengi wa ki-Afrika wanajaribu kuelewa atahri za tabia za kimila katika ujasiriamali barani humo.
28 Aprili 2013
Serikali ya Bangladeshi Yawafuatilia Wanablogu, Yawatuhumu Kuukashfu Uislam.
Kadri mapambano makali kati ya wanaharakati wa Kiislamu na serikali yanavyoendelea kusababisha migongano ya kidini nchini Bangladesh, Mamlaka ya Mawasiliano ya nchi hiyo imechukua hatua ya kuwanyamazisha wanablogu wanaoonekana wapinzani wa Uislamu na serikali. Asif mshindi wa tuzo ya mwanablogu bora amekuwa akilengwa na hatua hizo kwa siku za hivi karibuni.
Uganda: Kukumbuka milipuko ya mabomu ya 2010
Wananchi wa Uganda wameutumia mtandao wa Twita na Facebook kuwakumbuka wahanga 2010 wa milipuko yha mabomu iliyotokea kwenye klabu ya Rugby huko Kyaddondo na katika baa ya Kijiji cha Kiethiopia jijini Kampala Uganda.Mashambulizi hayo yalitokea wakati ambao wapenzi wa kandanda walikuwa wakitazama mpambano wa fainali kati ya Uhispania na Uholanzi uliofanyika nchini Afrika Kusini.




























Kiungo cha RSS kwa Citizen Media 











mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...