<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Breaking News</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/topics/breaking-news/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Urusi: Jinsi Abiria wa &#8220;Nevsky Express&#8221; Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 01 Dec 2009 11:11:27 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Russian]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=738</guid>
		<description><![CDATA[Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/gregory-asmolov/">Gregory Asmolov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/29/russia-how-passengers-of-nevsky-express-tell-their-stories-through-social-media/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mamlaka nchini Urusi yanaendelea <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/28/russia-at-least-25-people-killed-in-the-neva-express-train-crash/">kuchunguza ajali ya treni la &#8220;Nevsky Express&#8221; </a>[ENG] ambayo ilitokea kati ya Moscow na St Petersburg usiku wa Ijumaa. Kwa mujibu wa maofisa, dhahama hiyo iliyochukua maisha ya angalau abiria 25 ilikuwa ni shambulio la kigaidi. Ajali hiyo imezua maswali mengi. Watu wengi wanauliza ni nini kilichotokea katika masaa ya mwanzo baada ya ajali na ni kwa nini ilichukua muda mrefu kuanza kutoa taarifa za ajali hiyo.</p>
<p>Kwa kuwa dhahama hiyo ilitokea mbali na maeneo yenye makazi ya watu, ilichukua muda mrefu kwa wanahabari kuwasili kwenye eneo la ajali. Na ndipo picha za kwanza na video zilipoanza kuonekana kila mahali. Je nini kilichoyatokea majukwaa ya uanahabari wa kijamii ambayo yalitaarifu vilivyo kuhusu <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/europe/7614951.stm">ajali ya ndege mjini Perm</a> [ENG] mwezi Septemba 2008.</p>
<p>Abira pekee ambaye alitoa taarifa mara moja kuhusu ajali ya “Nevsky Express” alikuwa mtumiaji wa Twita <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog</a>. Aliandika mara 12 kuhusu ajali hiyo kabla ya kuwasili nyumbani. Haya ndio aliyoandika: </p>
<blockquote><p>Nipo hai. Lakini nitaeleza kuhusu (ajali) baadaye. Kama mtu ataeleza chochote kwenye habari, tafadhali niandikie. Hawatuambii kila kitu hapa.</p></blockquote>
<p>Baadaye, abiria wengi kutoka mabehewa ya kwanza – ni mabehewa ya mwisho ambayo yaliteguliwa kutoka kwenye reli –walisema kuwa kwa saa zima baada ya ajali hawakufahamu chochote. <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy frog</a> alituma habari mpya za nyongeza: </p>
<blockquote><p>Tumepanda treni jingine. Nilifanya kila nilichoweza.</p>
<p>Hivi sasa tupo SAPSAN (treni mpya ambyo iliwachukua abiria kwenda St. Petersburg – G.A). Natamani ingekuwa inakwenda polepole.</p>
<p>Wametangaza sasa hivi kuwa watu walitayarishwa rasmi wangetulaki kwenye kituo cha treni.</p></blockquote>
<p>Siku iliyofuata baada ya dhahama, <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog </a>aliandika muhtasari wa uzoefu wake:</p>
<blockquote><p>Nilizihisi hisia za kwanza kuhusu kilichotokea wakati tulipofika karibu na Piter (St. Petersburg G.A). Sikuwa na wasiwasi nilipokuwa katika eneo la ajali. Nilikuwa na hofu kidogo na viatu vyangu – kulikuwa na tope kila mahali na mawe yenye ncha.</p></blockquote>
<p>Jumamosi habari nyingi zilijitokeza wakati abiria walipoanza kublogu kuhusu yaliyowakuta. Makala ya blogu maarufu zaidi inayohusiana na mada hii iliandikwa na mtumiaji wa LJ <em>paltus_mk</em> [RUS] ambaye alikuwemo ndani ya mabehewa ya mwisho yaliharibiwa vibaya na mlipuko. <a href="http://paltus-nk.livejournal.com/23747.html">Aliandika </a>[RUS]:</p>
<blockquote><p>Yote yanatokea ndani ya sekunde 10 wakati unapofahamu ni nini kitakachotokea. Nilikuwa na muda wa kutosha kuutayarisha mwili wangu. Lakini hakuna linaloweza kusaidia dhidi ya kanuni za Newton wakati dazeni za tani za vyuma zinaposimama mara moja wakati zikiwa katika mwendo wa kasi – ni bahati tu… kwa hiyo nilikuwa na bahati tu. Kaka yangu alikuwa na bahati, pia, ukiachilia mbali ukweli kuwa majeraha yake yalikuwa yanatisha kuliko yangu.<br />
[…]</p></blockquote>
<blockquote><p>Kila kitu ambacho kilikwenda mrama hadi kusimama kabisa kulichukua kama sekunde 30 hivi. Ilikuwa giza na kimya. Watu walioumia walianza kulia. Nilikuwa sakafuni, nimekandamizwa na miili mingine. Niliisogeza ile miili. Niliona kuwa nimelowana na damu lakini damu ile haikuwa yangu. Niliona kuwa ni mzima na miguu yangu na mikono vuinafanya kazi. Kichwani nilikuwa na jeraha linalovuja damu. Ilinibidi ninyanyuke na kusubiri kwa muda kiasi kabla ya watu wenye majeraha mado waliposafisha njia ya kutoka.<br />
[…]<br />
Mateso yalikuwepo kila mahali. Tulikuwa tumeketi mwishoni mwa behewa na mikoba yote ilipaa ikituelekea. Watu wengi waliojeruhiwa. Katika dakika chahce baada ya ajali, behewa lilikuwa ni kama fungu la miili, viti na sehemu za treni ambazo zilikuwa zimesambaa sawia kila mahali.</p></blockquote>
<p><em>Paltus_mk </em>anasimulia habari za uokoaji zenye maelezo ya kina kuanzia dakika za mwanzo baada ya ajali, lakini wakati huo huo anaepuka ufafanuzi ambao ungeweza kuwastua wasomaji. Anaandika kuwa abiria walianza kupeana huduma ya kwanza kwa ushujaa bila kuogopa. Anasema haikuwezekana kuhesabu ni wagtu wangapi waliofariki. Waokoaji waliwasili saa moja na nusu baada ya ajali. <em>Paltus_mk</em> na kaka yake hatimaye waliokolewa na kupelekwa kwenye hospitali jirani na baadaye aliwasili mjini St. Petersburg. </p>
<p>Hadithi nyingine ya kunusurika ilichapishwa na mwanablogu pancakyes katika huduma nyingine ya kublogu ya Kirusi Ya.Ru. behewa lake halikuharibiwa na mlipuko. Alichapisha makala yake ya kwanza saa 4:11 za usiku – nusu saa baada ya ajali – pale pale kwenye eneo la ajali.  Aliandika kuwa treni ilisimama kutokana na ajali ya namna fulani, mabehewa machache yaliteguliwa na kwamba angewasili nyumbani kwa uchelevu kuliko ilivyotarajiwa. Karibu saa zima baadaye, aliongeza kuwa kulikuwa na waathirika katika mabehewa mawili ya mwisho. Jumamosi,  <em>pancakyes</em> <a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442">alichapisha habari nzima kuhusu ajali</a> [RUS] kama alivyoshudia mwenyewe:</p>
<blockquote><p>Tulihisi mitetemo michache ambayo ilikuwa ikiongezeka nguvu. Vitu vilianza kuanguka kutoka mezani. Haikuwa wazi ni nini kilichotokea. Hapakuwa na matangazo. Kwanza tulidhani kuwa halikuwa jambo lenye uzito. Pengine kuna mtu aliyesimamisha treni kwa makosa. Lakini makondakta wenye sura zenye hofu walianza kukimbia kila mahali wakikusanya magodoro, vitambaa vya mezani na maji. Walitutaka tusiondoke kwenye viti vyetu isipokuwa kama ni madaktari. Tulisikia mambo mabaya kutoka kwenye redio zao. Uvumi ulianza kusambaa. Hatukuamini kuwa mabehewa mawili yalikuwa yametengana na yalikuwa mbali sana. Baadaye tuligundua kuwa ilikuwa kweli.</p>
<p>Tulitoka nje na tulitaka kusaidia. Tulikwenda mpaka behewa la tatu. […] hatukutaka kuwa waduwazi ambao wanaongeza wingi wa watu bila fursa yoyote ya kusaidia. Pia hatukutaka kuona yale ambayo watu waliotoka huko walikwishatueleza.</p></blockquote>
<p>Mara baada ya ajali, majukwaa ya uanahabari wa kijamii yalikuwa sehemu ya kwanza ambayo wanahabari wa Kirusi  walikuwa wakitafuta habari. Mwandishi kutoka Shirika la Habari la RIA-Novosty aliacha maoni kwenye blogu ya <em>pancakyes</em> na kumtaka mwanablogu huyo ampigie simu mara moja. Tatyana Landa (mtumiaji wa LJ mwenye jina la Elada) <a href="http://elada.livejournal.com/220534.html">aliandika kwenye blogu yake</a> [RUS] kuhusu rafiki aliyenusurika ambaye alikuwemo kwenye treni. Mara moja wanahabari wawili waliacha maoni ya kumtaka awasiliane nao. Baadaye Tatyana <a href="http://elada.livejournal.com/220866.html">alichapisha makala ya hasira</a> [RUS] ambamo alisema kuwa mwanahabari kutoka “Komsomolskaya pravda” (gazeti la udaku la Kirusi) alikuwa akijaribu kumpata kwa simu mara kadhaa usiku huo. Makala hiyo iligeukia mahali ambapo watu walianza kujadili kama wanahabari wanaweza kuwatumia wanablogu kama chanzo cha taarifa zinazohusu hii ajali ya treni. Wanahabari pia walijaribu kuwasiliana na mwanablogu ambaye <a href="http://naechst-naechst.livejournal.com/105582.html#comments">aliandika</a> [RUS] kuwa aliamua kutopanda treni la “Nevsky Express” katika dakika ya mwisho.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu <a href="http://tema.livejournal.com/509436.html">walieza kughafirika kwao </a>[RUS] na ukweli kuwa ni watu wachache mno kutoka kwenye treni walitumia vyombo vya habari vya kijamii kutoa taarifa za kile kilichokuwa kinatokea., Na, inavyoonekana, kuna fafanuzi kadhaa zinazoelea ni kwa nini  uanahabari wa kijamii haukuchukua nafasi kubwa katika upashaji wa habari za ajali ya “Nevsky express”.</p>
<p>Twita, jukwaa zuri la kublogu moja kwa moja, si maarufu nchini Urusi. Kwa mujibu wa <a href="http://twitter.com/twitRU">twitRU </a>[RUS], kuna watumiaji wa Twita 2,700 tu ambao wanaandika kwa lugha ya Kirusi. Wakati huo huo, majukwaa maarufu ya kublogu nchini Urusi kama vile Livejournal.com au ya.ru yangeweza kutumika ili kublogu moja kwa moja lakini, kama ilivyojadiliwa hapo juu, kuna mifano michache tu ya matumizi hayo.</p>
<p>Ufafanuzi wa pili unahusiana na nafasi ya zana za mkononi na uunganishaji. Zana za mkononi zinaongezeka nchini. Warusi zaidi na zaidi wanaweza kutumia mtandao wa intaneti na zana nyingine za mtandaoni. Tabia hii ina nguvu katika maeneo ya Moscow na St. Petersburg. Lakini ajali ilitokea mbali na maeneo ya mjini ambako, kama mashihidi walivyotaarifu, uwezo wa kupatikana kwa mawasiliano ya simu za mkononi ulikuwa mdogo. Mwanablogu  <em>pancakyes </em><a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442&#038;ncrnd=2805">anasimulia</a> tatizo la mawasiliano:</p>
<blockquote><p>
Mawasilian ya simu yalikuwa mabaya sana. Inawezekana kuwa kila mtu alijaribu kupiga simu kwa wakati mmoja na mtandao ulielemewa. Nilianza kupata jumba za maandishi pale tu nilipokuwa kwenye treni la pili (treni ambalo liliwachukua abiria kwenda Saint- Petersburg G.A.). Ningeliweza kutumia mtandao wa intaneti, lakini ilikuwa ni vigumu mno.</p></blockquote>
<p>Hii ni tofauti, ajali ya ndege kule Perm mwaka jana ambayo ilitoa fursa nyingi kwa uanahabari wa kiraia:</p>
<p>1. Ndege ilianguka ndani ya mipaka ya mji ambako watu wengi waliweza kuona ni nini kilichokuwa kinatokea kutokea madirishani. Ajali ya “Nevsky express”, kama ilivyoelezwa awali, ilitokea sehemu za vijijini.</p>
<p>2.Habari zilizoandikwa kwa uanahabari wa kijamii kule Perm zilitokana na maelezo ya walioishuhudia ajali ambao hawakuwamo katika ajali (kwa bahati mbaya, hapakuwa na walionusurika kutoka katika ile ndege). Mashahidi wote wa tukio la “Nevsky Express”  walikuwa ni abiria katika treni. </p>
<p>3. Watu wengi walituma habari mpya juu ya ajali ya ndege kule Perm kwa kutumia tarakilishi za nyumbani. Walionusurika kwenye “Nevsky Express” walitegemea zana za mikononi.</p>
<p>Tofauti hizi zinabainisha kwa nini vyombo vya habari vya kiraia vilikuwa mbele katika ajali ya  ndege na vilikaribia kutokuwepo kwenye tukio la “Nevsky Express.” </p>
<p>Pia inawezekana kudai kuwa urusi bado haijaendeleza utamaduni wa utoaji taarifa kupitia uanahabari wa kiraia. Na ndiyo sababu abiria wawili tu walikuwa na msukumo wakutosha kwenda kwenye mtandao na kujipa kazi ya uanahabari wa kijamii. Na pia inaweza kufafanua upinzani wa abiria na wanablogu kwa wanahabari ambao walikuwa wanatafuta taarifa za ajali kwenye vyombo vya habari vya kijamii. </p>
<p>Inaonekana kana kwamba ulimwengu wa blogu wa Kirusi bado uko mbali na kuwa chanzo kikuuu cha kutangaza habari mpya. Bado unabaki kuwa sehemu ya usambazaji wa habari na mijadala mipana inayohusu nini kilichotokea. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-haki-ya-kijerumani-kwa-marwa-el-sherbini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-haki-ya-kijerumani-kwa-marwa-el-sherbini/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 11:06:45 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[Germany]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Racism]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=669</guid>
		<description><![CDATA[Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens,  ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/tarek-amr/">Tarek Amr</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/egypt-german-justice-for-marwa-el-sherbini/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Hatimaye, haki imetolewa katika <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/07/06/egyptian-woman-killed-in-german-court-for-being-veiled/">shauri la Marwa El-Sherbini</a>, mwanamke wa Kimisri aliyeuwawa kwa kuchomwa visu na muhamiaji mwenye asili ya Urusi-na-Ujerumani ndani ya mahakama huko Ujerumani. Baada ya karibu miezi mine na nusu, Alex Wiens amehukumiwa kifungo cha maisha, bila ya matarajio ya kuachiwa mapema kabla ya kifungo kumalizika.</p>
<p><em>Bikya Misr</em> <a href="http://bikyamasr.com/?p=5678">ameandika kuhusu kesi hiyo</a>:</p>
<blockquote><p>Baada ya karibu miezi mine na nusu, mkasa wa Marwa el-Sherbini umefikia hitimisho la namna Fulani baada ya mahakama ya Ujerumani kumhukumu kifungo cha maisha bila uwezekano wa kuachiwa mapema mtu aliyemchoma visu “shahidi aliyevaa shela” mara 17 ndani ya mahakama mnamo mwezi Julai. Wamisri, Waarabu na kadhalika Wajerumani wameikaribisha hukumu hiyo na wanatumaini kuwa Ulaya na Mashariki ya Kati zitaanza kupona majeraha ya mauaji hayo na kusonga mbele “kuelekea mustakabali bora zaidi.”</p></blockquote>
<p><em>Hicham Maged </em><a href="http://blog.hichamaged.net/justice-and-stereotype/">ameandika jinsi alivyoridhika na hukumu, na kuwa ana imani na mfumo wa sheria wa Ujerumani</a>:</p>
<blockquote><p>Hakimu alikuwa anazitambua mbinu kadhaa za timu ya utetezi ya muuaji na hapa ninanukuu maneno kwa mujibu wa makala hii: “Aliua… si kutokana na hofu bali kutokana na kisasi. Kwa makusudi alitumia nia njema na udhaifu wake (marehemu). “Ninakubaliana na hili na usisahau kuwa alijaribu pia kumuua mume wake.<br />
Ninafarijika kuwa chumba cha mahakama ambamo usaliti huo ulitokea kimeoshwa kwa mikono na kimaadili kwa kutumia haki. Baada ya hayo, imani yangu kwa mfumo wa sheria wa Ujerumani haupaswi kuelezwa kwani kosa hili lilikuwa ni la kustusha kwetu sote na si kwa Wajerumani pekee. Kwa hivyo basi, ni leo hii Marwa na mwanawe ambaye alikuwa hajazaliwa wanaweza kupumzika kwa amani baada ya malipo kwa muuaji. </p></blockquote>
<p><em>Zeinobia</em> aliifurahia hukumu, naye pia <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/11/this-is-fair-rule-not-political-rule.html">aliandika kuwajibu wale ambao waliamini kuwa hukumu ile ilikuwa ni ya kisiasa, na kuwa mahakama ya Ujerumani ilitoa hukumu inayomnufaisha Marwa ili kuwaridhisha Wamisri na Waarabu</a>:</p>
<blockquote><p>Sasa nataka kusema jambo, baadhi ya wabaguzi “na si wachache duniani hivi sasa”, watasema kwamba uamuzi huu ni wa kisiasa; ambao mahakama ilibidi iuchukue ili kushinda mioyo na fikra za Waislamu duniani na kuokoa maslahi ya Ujerumani katika ulimwengu wa Kiislamu.<br />
Naam, kwa heshima yangu yote nilikwishasema hapo awali na nitasema tena; usimfikirie Marwa kama mwanamke wa Kiislamu; mfikirie kama mwanamke mjamzito na mama ambaye kwa yakini alichomwa visu mara 18 mbele ya mwanawe mdogo wa kiume. Aliua roho mbili, roho zisizo na hatia kwa sababu ya chuki isiyoona pamoja na ubaguzi. Anastahili kuwa jela kwa maisha yake yote yaliyobaki kwa kutoa maisha ya roho zisizo na hatia na kuota uhai wa mama kutoka kwa mwanawe.</p></blockquote>
<p><em>Aam Mina</em> kwa upande mwingine aliandika makala, ya <a href="http://voice-of-egypt.blogspot.com/2009/11/blog-post_12.html">kuwakebehi wale wanaoamini katika nadharia za njama na waliokuwa wakitarajia Wajerumani kufanya uamuzi utakaompendelea muuaji</a>:</p>
<blockquote><p>
مش عارف ليه من ساعة الجكم مش سامعين صوت الناس اللي فلقتنا وقت الحادث عن عنصرية الألمان و كرههم للعرب و المسلمين و عن إن القضية هتتظبط و الراجل هياخدله سنة أو سنتين و خلاص و انه الحل الوحيد هو الجهاد و محاربة الغرب الصهيوني الفاسد العلماني الكافر </p></blockquote>
<div class="translation">Sijui kwa nini, tangu kutangazwa kwa uamuzi, sijamsikia yeyote kati ya wale waliokuwa wakiongelea juu Wajerumani na jinsi walivyo wabaguzi, na kuwa wanawachukia Waarabu na Waislamu. Pia walidai kuwa mahakama ingetoa uamuzi uanompendelea muuaji na kuwa atafungwa kwa mwaka mmoja au miwili tu, na kuwa tumaini letu pekee ni kutangaza vita takatifu dhidi ya utawala usio na dini, uliooza, Wakizayonisti, na Wamagharibi makafiri.</div>
<p>Kisha aliandika kuhusu mafundisho mengi ambayo tunapaswa kujifunza kutokana na tukio hili:</p>
<blockquote><p>
دي بعض الدروس المستفادة من الغرب الكافر<br />
١- سرعة العدالة.. جريمة القتل تمت في يوليو ٢٠٠٩ يعني من حوالي ٤ شهور.. ماحتاجناش ٢٠ سنة دراسة للقضية زي ما بيحصل عندنا<br />
٢- عدالة الحكم.. تم تطبيق أقصي عقوبة علي المتهم و هي المؤبد (عقوبة الإعدام غير معمول بيها في القانون الألماني) من دون التمييز ما بين مسلم و مسيحي أو عربي و ألماني.. الكل سواسية أمام القانون </p></blockquote>
<div class="translation">Haya ni baadhi ya mafundisho tunayotakiwa kujifunza kutoka kwa makafiri wa Magharibi:<br />
1.	Toeni haki haraka: Mauaji yalitokea mwezi Julai 2009, yaani, takriban miezi 4 iliyopita, na haikuwachukua miaka 20 kulichambua shauri, kama ambavyo hufanyika hapa.<br />
2.	Haki yenyewe: Muuaji amepokea adhabu ya juu – adhabu ya kifo haimo kwenye sheria ya ujerumani – bila ya kubagua kati ya Muislamu, Mkiristu, Mwarabu au Mjerumani. Wote wako sawa mbele ya sheria. </div>
<p>Na mwisho, <em><a href="http://blog.hichamaged.net/justice-and-stereotype/">Hicham Maged</a></em> aliandika:</p>
<blockquote><p>Kilichotokea kwa Marwa kiwe ni mbiu ya ‘kuamsha’ ambayo itawafanya watu wafanye kazi ili kufanikisha, kwa kukosoa vitendo vilivyozidi mipaka ambavyo vinafanywa dhidi ya watu kutokana na imani zao au rangi na kuelewa tofauti zetu na hii inamaanisha kuzizima imani potofu kutoka kwa yeyote dhidi ya yeyote.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-haki-ya-kijerumani-kwa-marwa-el-sherbini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ofisa Aweka Wazi Ufisadi wa Polisi kupitia Mtandao</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 10 Nov 2009 11:10:26 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=595</guid>
		<description><![CDATA[Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko Novorossiysk alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/vadim-isakov/">Vadim Isakov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/09/officer-exposes-police-corruption-using-the-web/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/YouTube-%D0%92%D0%B8%D0%B4%D0%B5%D0%BE%D0%BE%D0%B1%D1%80%D0%B0%D1%89%D0%B5%D0%BD%D0%B8%D0%B5-%D0%BC%D0%B0%D0%B9%D0%BE%D1%80%D0%B0-%D0%BC%D0%B8%D0%BB%D0%B8%D1%86%D0%B8%D0%B8-%D0%BA-%D0%9F%D1%83%D1%82%D0%B8%D0%BD%D1%83-1_1257748652019-75x75.jpg" title="YouTube - Видеообращение майора милиции к Путину (#1)_1257748652019" class="alignleft" width="75" height="75" /> Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko <a href="http://maps.google.com/maps?q=Novorossiysk&#038;oe=utf-8&#038;rls=org.mozilla:en-US:official&#038;client=firefox-a&#038;um=1&#038;ie=UTF-8&#038;hq=&#038;hnear=Russian+Federation,+Region+of+Krasnodar,+Novorossiysk&#038;gl=us&#038;ei=aa73SouZJZDR8QbxpNDzCQ&#038;sa=X&#038;oi=geocode_result&#038;ct=title&#038;resnum=1&#038;ved=0CAoQ8gEwAA">Novorossiysk</a> alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi. </p>
<p>Kwenye ujumbe wake wa video unaopotakina katika anwani hii ya mtandaoni <a href="http://www.dymovskiy.ru/">www.dymovskiy.ru</a> na YouTube (<a href="http://www.youtube.com/watch?v=2G3KbBfpg24&#038;feature=related">sehemu ya I</a> na <a href="http://www.youtube.com/watch?v=2dJkMLxvulw">sehemu ya II</a> [RUS]), Aleksey Dymovskiy anaonekana kuwa mtulivu na anayejieleza kwa usahihi mkubwa. Anazungumzia juu ya kushuka kwa hadhi ya polisi, rushwa, ufisadi na jinsi gani malipo duni yanavyokuwa kama sumu inayowala maafisa wengi wa polisi nchini Urusi.</p>
<blockquote><p>Nafikiri watu wengi watanielewa. Nataka kuchapa kazi, lakini nimechoshwa na mipango ya kingano ambapo tunalazimishwa kupeleleza jinai ambazo hazipo.  Nimechoshwa na mipango ya kutunga ambapo tunaambiwa tuwafunge watu fulani. Nimechoshwa na jinai za kutunga zinazoandaliwa ili kuwatupa watu fulani gerezani. </p></blockquote>
<p>Akiendelea kuweka wazi mambo mbalimbali, Dymovskiy anakiri kumtupa mtu asiye na hatia gerezani kwa sababu ya kulazimishwa na mkubwa wake kazini:</p>
<blockquote><p>Mkurugenzi wa Idara ya mambo ya Ndani alinitunukia cheo cha Meja, ambacho nilikipata mwezi Mei, kwa sababu tu nilimwahidi kutumpa mtu asiye na hatia gerezani. Siogopi kueleza jambo hili. Naelewa kuwa naweza kuadhibiwa kwa sababu hii. Lakini ni ukweli nami ninaukiri.</p></blockquote>
<p>Dymovsky pia anamwomba Waziri Mkuu Vladimir Putin kupeleleza matatizo hayo na kumalizia mbali tatizo la ufisadi katika jeshi la polisi.<br />
Video yake hiyo ilipata watembeleaji wengi sana muda mfupi tu tangu ichapishwe na vilevile maelfu waliibofya kwenye YouTube. Ilichukuliwa pia sana na kuchapishwa na vyombo vikuu vya habari za Urusi na kujadiliwa sana katika blogu nyingi. Ni mfano mmoja kati ya kadhaa ya kwanza ambapo raia wa Urusi wanafaulu vema kabisa kutumia miundo mipya ya majukwa ya habari ili kuwasiliana na serikali hasa kuhusu masuala nyeti yanayoikabili nchi. </p>
<p>Upekee wa &#8220;hotuba za kiraia kwa njia ya video&#8221; nchini Urusi inaelezwa vema zaidi kwa maoni yenye tahadhari kutoka katika moja ya blogu maarufu zaidi nchini inayoitwa <a href="http://dolboeb.livejournal.com/1696532.html">dolboeb</a>:</p>
<blockquote><p>Risala yenye nguvu ya pekee. Sitashangaa kama itageuka kuwa mbinu ambukizi ya utafutaji masoko. Mhusika mkuu anaonekana kama mtu wa kutoka sayari nyingine.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu mwingine <a href="http://marchenk.livejournal.com/191686.html">marchenk</a> anaandika:</p>
<blockquote><p>Hakuna hata mmoja wetu aliye malaika&#8230; simhusudu [Dymovskiy] kama askari mwaminifu na mpenda ukweli (mwenyewe amekiri kwamba alitunukiwa cheo cha Meja kwa kumfunga mtu asiye na hatia gerezani).  […] Hata hivyo, nampa heshima kwa ajili ya ujasiri wake wa kuwa mkweli. Kwa hiyo, kumbe kuna maafisa wengine wa polisi walio waaminifu. Kwa sababu yao, ni muhimu kuhakikisha kunakuwepo na mabadiliko katika jeshi la polisi. </p>
<p>Ninamwombea Mungu ili kwamba uwekaji wake wazi huu wa mambo umpe kinga na atendewe haki katika hali yake. </p></blockquote>
<p>Siku ya Jumapili, tarehe 8 Novemba, Rashid Nurgaliev, Waziri wa Urusi wa Mambo ya Ndani, alitangaza ukaguzi wa jeshi la polisi huko Novorossiysk. Wakati huohuo, Dymovskiy amefukuzwa kazi kwa sababu ya “uzushi na vitendo ambavyo vinaharibu sifa” ya polisi.</p>
<p>Katika mahojiano yake na kituo cha redio cha Urusi, “<a href="http://www.echo.msk.ru/">Ekho Moskvy</a>,” Dymovskiy alisema kwamba amekuwa akifuatiliwa na kwa hiyo alikuwa akifikiria kuhamishia familia yake jijini Moscow kwa sababu za kiusalama. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cuba-ukweli-wa-sanchez-kutiwa-mbaroni-waibuka/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cuba-ukweli-wa-sanchez-kutiwa-mbaroni-waibuka/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 08 Nov 2009 11:22:03 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Cuba]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[LANGUAGES]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=584</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naGeorgia Popplewell  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari na katika ulimwwengu wa blogu [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/georgia-popplewell/">Georgia Popplewell</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/07/cuba-details-of-the-sanchez-detention-emerge/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika <a href="http://www.reuters.com/article/mediaNews/idUSN0620636520091107">vyombo vikubwa vya habari</a> na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani <a href="http://www.desdecuba.com/generaciony/?p=2468">ameandika</a> (es) kuhusu tukio hilo kwenye blogu yake, Generación Y, na blogu za Kiingereza kama vile <a href="http://babalublog.com/2009/11/breaking-news-yoani-sanchez-arrested-in-cuba/">Babalú Blog</a>, <a href="http://repeatingislands.com/2009/11/07/yoani-sanchez-detained-briefly/">Repeating Islands</a> pamoja na <a href="http://marcmasferrer.typepad.com/uncommon_sense/2009/11/cuban-bloggers-arrested.html">Uncommon Sense</a> zinafuatilia habari hiyo. <a href="http://www.youtube.com/watch?v=gKx0KJhiNL4">Mahojiano ya sauti</a> (es) na Sanches kuhusu tukio hilo yamepandishwa kwenye YouTube.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cuba-ukweli-wa-sanchez-kutiwa-mbaroni-waibuka/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Yoani Sanchez Pamoja na Wanablogu Wengine wa Cuba Wakamatwa na Kupigwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/yoani-sanchez-pampja-na-wanablogu-wengine-wa-cuba-wakamatwa-na-kupigwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/yoani-sanchez-pampja-na-wanablogu-wengine-wa-cuba-wakamatwa-na-kupigwa/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 08 Nov 2009 11:15:24 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Cuba]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[LANGUAGES]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=579</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naGeorgia Popplewell  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú iliweka kiungo kuelekea makala iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/georgia-popplewell/">Georgia Popplewell</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/07/yoani-sanchez-other-cuban-bloggers-detained-beaten/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú <a href="http://babalublog.com/2009/11/breaking-news-yoani-sanchez-arrested-in-cuba/">iliweka kiungo</a> kuelekea <a href="http://www.penultimosdias.com/2009/11/06/la-seguridad-de-estado-detiene-a-yoani-sanchez-y-otros-blogueros-cuando-iban-a-participar-en-una-manifestacion-performance-en-la-calle-23/">makala</a> iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na majeshi ya usalama. Habari mpya kutoka kwa Penultimos Días zinataarifu kuwa Sanchez na Orlando Luis Pardo “walipigwa vibaya na kutukanwa”.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/yoani-sanchez-pampja-na-wanablogu-wengine-wa-cuba-wakamatwa-na-kupigwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Uchaguzi Tunisia: haki Bila Ya Upendeleo!!?</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/uchaguzi-tunisia-haki-bila-ya-upendeleo/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/uchaguzi-tunisia-haki-bila-ya-upendeleo/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 27 Oct 2009 12:04:47 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Elections]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Tunisia]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=480</guid>
		<description><![CDATA[Rais wa Tunisia Zine Al Abidine Ben Ali ameshinda uchaguzi kwa kipindi cha tano kwa asilimia 89.62 ya kura zote. Chama chake cha Democratic Constitutional Rally kilishinda viti vya bunge 161 katika viti 214. Wanablogu wa Tunisia wanatoa maoni katika makala hii.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/lina-ben-mhenni/">Lina Ben Mhenni</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/26/tunisia-elections-fairness-and-impartiality/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kama ilivyotabiriwa, rais Zine Al Abidine Ben Ali ameshinda uchaguzi kwa mara ya tano. Ambalo halikutarajiwa ni kuwa angeshinda kwa asilimia 89.62 ya kura zote. Utabiri ulikuwa kwamba angepata kura zaidi.</p>
<p>Chama kinachotawala cha Ben Ali, Democratic Constitutional Rally nacho pia kilifanya vizuri. Kilishinda viti vya bunge 161 katika viti 214. Viti 53 vilivyobaki vilinyakuliwa na vyama sita tofauti: Movement for Democratic Socialists, viti 16; Party of People&#39;s Unity, kinachoongozwa na Mohamed Bouchiha, viti 12; chama cha Union of Democratic Unionists  cha Ahmed Inoubli, viti 9; Social Liberal Party, viti 8; Party of Greens for Progress, viti 6 na chama cha  Ettajdid  cha and Ahmed Brahim, viti 2.</p>
<p>Chama tawala kilitangaza haki na usawa katika uchaguzi wa 2009. Lakini viongozi wa upinzani na wanablogu wana maoni mengine: wanafikiri kuwa vitendo vya ukandamizaji na udhibiti mkali kwenye taratibu za uchaguzi vilitawala uchaguzi wa rais na wabunge nchini Tunisia mnamo tarehe 25, Oktoba 2009.</p>
<p><em><a href="http://arabasta1.blogspot.com/2009/10/blog-post_26.html">Arabasta</a></em> anasema kwa kejeli:</p>
<blockquote><p>مبروك عليكم ما عملتو<br />
نتوجه بالشكر أولا إلى الشعب التونسي اللي قام بواجبو الإنتخابي في كنف الديموقراطية و الشفافية و الروح الرياضية البارح و إنتخب رئيس جديد للبلاد و مجلس نواب أخر لمدة خمسة سنين. الإختيار هذا كان محكم و مدروس و حتى واحد ما حاول يأثر على العباد و حتى من التلفزة و الصحافة كانو في المستوى و عطاو وقت متساوي لكل المترشحين و الأنصار متاعهم بقطع النظر عن<br />
قربهم أو بعدهم عن السلطة<br />
نتوجه بالشكر زادة لسيادة رئيس الجمهورية (لمدة 5 سنوات أخرى) و نعتذر عن عدم الدعوة و التصويت ليه و نستنكر و نشجب<br />
التصرفات المشينة هذي أما نذكر أنو عمري ما شككت في نزاهة الإنتخابات و حريتها، فمن المعروف أنو في حالة تزوير الإنتخابات النتائج تكون من نوع 99،98% لكن الملاحظ النزيه يعرف أنو نتيجة 2009 ما تبعدش برشة على النسبة اللي ربح بيها شيراك في 2002 في فرنسا و لذا فالإنتخابات هذي إرتقت بينا إلى مصاف الدول العظمى و المتقدمة </p></blockquote>
<div class="translation">Hongera kwa ulichofanya!<br />
Shukrani nyingi ziwafikie kwanza raia wa Tunisia ambao walitimiza wajibu wao jana katika uchaguzi ndani ya muundo wa demokrasia na usawa. Walimchagua rais mpya wa nchi na bunge jipya kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Chaguo lilikuwa la busara na lililotafakariwa vyema. Hakuna aliyejaribu kuwashawishi watu na hata idhaa za televisheni na vyombo vya habari vya maandishi havikufungamana na upande wowote na vilihakikisha kuwa wagombea na wafuasi wao wanapata nafasi sawa bila kujali uhusiano wao na serikali.<br />
Shukrani zangu pia zimfikie rais (kwa miaka mingine mitano) na naomba radhi kwa kutomuunga mkono na kutokumpigia kura. Ninailaani tabia hii ya aibu japokuwa ninakumbuka ukweli kuwa sijawahi kutilia shaka kutofungamana kwenu na upande wowote wakati wa uchaguzi. Kama inavyoeleweka kuwa kama pangetokea udanganyifu basi matokeo yangekuwa asilimia 98.99. Lakini msimamizi asiyefungamana na upande wowote anafahamu kwamba matokeo ya 2009 hayana tofauti sana na yale ya 2002 nchini Ufaransa wakati Chirac aliposhinda uchaguzi. Na hiyo ndio sababu inayotufanya tuweze kusema kuwa uchaguzi huu umetupandisha na kufikia daraja la nchi zilizoendelea na mataifa makubwa.</div>
<p><em><a href="http://nakhlat.blogspot.com/2009/10/blog-post_26.html">Nakhlet Wed El Bey</a> </em>(Mtende wa mto Bey) anaandika katika lugha ya Kitunisia:</p>
<blockquote><p>
أنا لا أشكك في نزاهة التمثيلية الإنتخابية<br />
…<br />
آش كان عليه لو كان حلّينا اللعب شويّة<br />
و نزعنا الأكمام من أفوه المعارضة الحقيقية<br />
لإنتصر الرئيس بسبعة و سبعين في المية<br />
و انتزعنا من قلوب الرعايا النفاق و السكيزوفرينية </p></blockquote>
<div class="translation">Sihoji haki na kutopendelea kwenye maigizo ya uchaguzi wa Tunisia.<br />
Je ingekuwaje kama tungelikuwa na <em>uwezo</em> zaidi<br />
Na kuondoa viziba midomo kutoka kwenye mdomo wa upinzani wa kweli<br />
Hapo rais angelishinda kwa asilimia 77.7<br />
Na tungeondoa unafiki na wehu kutoka kwenye mioyo ya watu</div>
<p>Mwanablogu <em><a href="http://a-free-tn.blogspot.com/2009/10/blog-post.html">Some Thoughts from Tunisia</a>,</em> kwa upande wake, alielezea kilichomtokea wakati alipokwenda kupiga kura katika masaa ya mwisho wa siku hiyo:</p>
<blockquote><p>
كيما قلت سبقني مرافقي للقاعة متاع الانتخاب وكيف دخلت انا نلقا الدنيا داخلة بعضها والجماعة يتغامزو عليه ويتلفوا في الجرّة (ما فاقوش اللي احنا مع بعضنا). اكهو فهمت آش صار: ضهر السيّد مازال في دارو وهوما ريڨلولو اموروا وانتخبوا في بلاصتوا وصححوا في الدفتر في بلاصتوا… آيا قالولو ما صار شيء برّا للخلوة اختار وموش لازم تصحح (الورقة كلها مصححة وماعادش فمة بلايص)… هاذا كلّو صاير وانا واقف نتفرّج!! السيّد مشى للخلوة وانا نسمع فيهم يْوَشْوْشُو ويحكيو بالسرقة بالحرف الواحد:<br />
“هذا العمدة انتخب في بلاصتوا…!!!!”</p></blockquote>
<div class="translation">Kama nilivyosema, mwenzangu alikwenda kwenye kituo cha kupigia kura kabla yangu. Wakati nilipoingia chumbani, niliwaona wale waliokuwepo wamechanganyikiwa na wangine walikuwa wakipepeseana macho wakijidai kana kwamba hakuna lolote lililotokea (hawakugundua kwamba tulikuwa pamoja). Haraka nikaelewa kila kitu: wakati bado yule bwana akiwa nyumbani kwake, walikwishapiga kura na kusaini badala yake.<br />
Halafu wakamwambia: “hakuna kilichotokea Unaweza kuchagua wagombea wako na hauhitajiki kusaini. (Karatasi lote lilikuwa limesainiwa na hapakuwa na nafasi kwa saini nyingine).<br />
Haya yote yalitokea wakati nikiwa nimesimama pale. Mwenzangu alikwenda kupiga kura na nikawasikia wananong’ona:<br />
“Omda” (chifu wa jamii) alipiga kura badala yake.</div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/uchaguzi-tunisia-haki-bila-ya-upendeleo/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title></title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/373/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/373/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 12 Oct 2009 12:43:35 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Guinea]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=373</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naAbdoulaye Bah  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Ripoti ya MISNA (Shirika La Kimataifa la Habari La Wamisionari) iliyochapishwa tarehe 25 Septemba inaeleza kuwa maandamano makubwa ya upinzani yalifanyika mjini Labe, jiji la pili kwa ukubwa nchini Guinea, dhidi ya Mkuu wa Nchi Mwanajeshi, Kapteni Moussa Dadis [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/abdoulaye-bah/">Abdoulaye Bah</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/09/26/massive-protests-in-guinea/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Ripoti ya MISNA <a href="http://www.misna.org/default.asp?IDLingua=3">(Shirika La Kimataifa la Habari La Wamisionari)</a> iliyochapishwa tarehe 25 Septemba inaeleza kuwa maandamano makubwa ya upinzani yalifanyika mjini Labe, jiji la pili kwa ukubwa nchini Guinea, dhidi ya Mkuu wa Nchi Mwanajeshi, Kapteni Moussa Dadis Camara.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/373/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Wanablogu Wa Asia Kusini Na Tuzo Ya Nobeli Ya Amani Aliyopewa Obama</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/wanablogu-wa-asia-kusini-na-tuzo-ya-nobeli-ya-amani-aliyopewa-obama/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/wanablogu-wa-asia-kusini-na-tuzo-ya-nobeli-ya-amani-aliyopewa-obama/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 12 Oct 2009 12:31:53 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bangladesh]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[India]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Pakistan]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Sri Lanka]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=368</guid>
		<description><![CDATA[Rais wa Marekani Barack Obama amepokea tuzo mashuhuri ya Amani ya Nobeli leo. Wanablogu na wanaoblogu habari fupi fupi huko Asia kusini wanaelezea maoni yao kuhusu habari hiyo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/rezwan/">Rezwan</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/09/south-asian-bloggers-on-obama%E2%80%99s-nobel-peace-prize/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption aligncenter" style="width: 430px"><img alt="Picha kwa hisani ya http://www.flickr.com/photos/marcn/2174935053/ na imetumika chini ya hati miliki huria " src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/barack-Obama-640x480.jpg" title="Barack Obama" width="420" height="282" /><p class="wp-caption-text">Picha kwa hisani ya http://www.flickr.com/photos/marcn/2174935053/ na imetumika chini ya hati miliki huria </p></div><br />
Rais wa Marekani Barack Obama amepokea tuzo mashuhuri ya Nobeli ya Amani leo. <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/europe/8298580.stm">Kwa mujibu wa kamati ya Nobeli</a> (Obama) amestahili kupokea tuzo hiyo kutokana na “juhudi zake za kuimarisha diplomasia ya kimataifa na ushirikiano baina ya watu”.</p>
<p>Hili limekuwa ni jambo la kushangaza kwa watu wengi duniani. Kwa nadharia tuzo hii inapaswa kutolewa kwa mtu au shirika lililojihusisha katika kupata ufumbuzi wa mgogoro mrefu wa kijeshi. Lakini kumeshawahi kuwepo na utofauti huko nyuma na Obama ni mmoja wa hali hizo tofauti kwani alianza kazi ya urais baada ya kupendekezwa mwezi Februari.</p>
<p>Gazeti la The New york Times <a href="http://thelede.blogs.nytimes.com/2009/10/09/world-reaction-to-a-nobel-surprise/">limetoa muhtasari</a> wa baadhi ya marejeo ya maoni kutoka duniani kote. Sasa hebu na tuangalie jinsi wanablogu na wale wanaoblogu makala fupi fupi kutokea Asia Kusini wanavyoelezea maoni yao kuhusu habari hii.</p>
<p>Kutokea Bangladeshi, <em><a href="http://bdoza.wordpress.com/2009/10/09/obama-own-nobel-peace-prize-2009-is-it-premature/">An Ordinary Citizen</a></em> haamini na anasema kuwa tuzo hiyo imetolewa kabla ya wakati wake.</p>
<blockquote><p>
Tunazienzi juhudi zake za kuleta amani ambazo huwa anazianzisha tu na bado tunasubiri matokeo.<br />
Je si kweli kwamba muda bado haujafika kwake kuipokea tuzo hiyo? Hatuna hakika ni kwa jinsi gani (tuzo hii) itaathiri mtazamo wake.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa India <a href="http://churumuri.wordpress.com/2009/10/09/churumuri-poll-does-obama-deserve-nobel/">Churumuri</a> anayo maswali kadhaa rahisi:</p>
<blockquote><p>Je Obama anastahili tuzo hii? Je amefanya jambo lolote linaloihalalisha? Je kwa kumpa kijana mbichi kama huyu, wakati wa uchanga wa urais wake, kunawashusha hadhi wale wote waliofanya kazi ngumu na kwa muda mrefu ili kuipokea? Au haidhuru chochote, kwani tuzo ya Nobeli ni tuzo ya kisiasa aliyopewa Yasser Arafat na Menanchem Begin? (kama vile ambavyo yeyote aliyewahi kusoma The Prize kilichoandikwa na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Irving_Wallace">Irvin Wallace</a> anaweza kufahamu)</p></blockquote>
<p>Na bado kutokea India, <a href="http://zoooni.blogspot.com/2009/10/obama-n-his-nobel-win.html">Zooni </a>ni mshabiki wa Obama, lakini ameshangazwa pia:</p>
<blockquote><p>Ok kabla haujafikiria vibaya mimi si kati ya wale wanaomchukia Obama… ninampenda vilivyo, nimeandika makala ya kumpongeza kwa ushindi wake wa urais, je ameshinda nini na kwa sababu ipi, alikuwa kazini kwa wiki 2 tu wakati alipopendekezwa (mapendekezo yalikoma tarehe 1 Februari). Nadhani Obama alishinda tuzo kutokana na kampeni yake kabambe!</p></blockquote>
<p>Kutokea Pakistan, <em>Temporal</em> wa blogu ya <em>Baithak</em> <a href="http://baithak.blogspot.com/2009/10/nobel-peace-prize-2009-obama-gets-what.html">amekuwa mkali kidogo katika maoni yake</a>:</p>
<blockquote><p>Mwaka huu unaweza ukawa ndio mwaka ambao utaashiria kuanza kushuka kwa tuzo ya Nobeli. Wanakamati walikuwa wanakula au kuvuta kitu gani?</p>
<p>Rais Obama anaweza kustahili tuzo hii katika miaka ijayo. Lakini sio katika wakati huu. Ndio kwanza  ameanza jitihada na  ado hajaacha alama yake kwenye amani ya dunia.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa Ki-Sri Lanka <em>Indi.ca</em> <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/10/09/south-asian-bloggers-on-obama%E2%80%99s-nobel-peace-prize/Indi.ca%20http://indi.ca/2009/10/obamas-nobel-peace-prize/">anafikiri kuwa</a> tuzo hii itamuumiza Obama nyumbani (Marekani):</p>
<blockquote><p>Nafikiri kuwa Obama ni mtu muungwana zaidi anayetembea katika uso wa dunia hii leo. Hata hivyo, sidhani kama ameshafanya kile ambacho anataka kukifanya. Nobeli inaweza kumsaidia kinadharia, lakini inaweza kumuumiza nyumbani (Marekani). </p></blockquote>
<p>Wanaondika blogu fupi fupi duniani kote walikuwa wametingwa leo kwa kuelezea mshangao na kutoamini baada ya kuzisikia habari. Yafuatayo ni baadhi ya maoni kutoka kwa watumiaji wa Twita wa Asia Kusini:</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/vijaysankaran">@vijaysankaran</a>: Tuzo ya nobeli sasa imekuwa kama <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Bharat_ratna">Bharat Ratna</a>… inahusu wewe ni nani, na siyo ulichokifanya-)</p>
<p><a href="http://twitter.com/tantanoo">@tantanoo</a>: kwa hiyo Bush alitangaza vita, Obama anaomba amani na kushinda tuzo ya Nobeli. Mahesabu mazuri.</p>
<p><a href="http://twitter.com/santhemant">santhemant</a>: “rais wa Marekani Obama apokea tuzo ya Amani kwa kuendesha VITA sehemu nyingi.. kwa kuiunga mkono Pakistani na kupuuza nchi za kidemokrasia kama vile India.</p>
<p><a href="http://twitter.com/saniakhan">saniakhan</a>: sijui kama naweza kuunga mkono ushindi wa Rais Obama wa Tuzo ya Nobeli huku kukiwa na ndege za kivita za drones huko Pakistan bado zikiendelea kupiga.</p>
<p><a href="http://twitter.com/YusufKhan">YusufKhan:</a> Guantanamo bado iko wazi, ndege za drone bado zinaangusha mabomu huko Pakistani, vita bado vinaendelea huko Iraq/Afghanistan, na bado Obama anashinda tuzo ya Amani ya Nobeli. Yay.</p>
<p><a href="http://twitter.com/TinyToots">@TinyToots</a>: mimi pia ninahitaji Tuzo ya Amani ya Nobeli. Kila siku ninajiepusha na kuwafanyia fujo watu wengi. Kwa nini hakuna mtu anayenipendekeza?</p>
<p><a href="http://twitter.com/OldmonkMGM">@OldmonkMGM</a>: mchague mtu asiyefanana na wengine: Dalai Lama, Mother Teresa, Martin Luther King, Barack Obama.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/wanablogu-wa-asia-kusini-na-tuzo-ya-nobeli-ya-amani-aliyopewa-obama/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Indonesia: Tetemeko Kubwa Laikumba Sumatra</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/indonesia-tetemeko-kubwa-laikumba-sumatra/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/indonesia-tetemeko-kubwa-laikumba-sumatra/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 04 Oct 2009 04:45:41 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bahasa]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Disaster]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Indonesia]]></category>
		<category><![CDATA[Refugees]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=332</guid>
		<description><![CDATA[Mji wa mwambao wa Padang, Sumatra Magharibi umeharibiwa tena na tetemeko la ardhi.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/carolina-rumuat/">Carolina Rumuat</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/09/30/indonesia-strong-earthquake-hit-west-sumatra/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Tetemeko kubwa la ardhi limeikumba <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Padang,_Indonesia">Padang</a>, Sumatra Magharibi mnamo majira ya saa 11 jioni siku ya Jumatano.</p>
<p>Filamu ya video iliyotumwa na <a href="http://www.youtube.com/watch?v=0b_8aBBO6Wc">mtumiaji wa Youtube</a> aliyeko Padang:<br />
<object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/0b_8aBBO6Wc&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/0b_8aBBO6Wc&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
Tetemeko la ardhi lililotokea chini ya bahari lenye ukubwa wa vipimo vya Rikta 7.6 limesababisha madhara makubwa kwa majengo na kujeruhi watu, hasa katika maeneo ya <a href="http://regional.kompas.com/read/xml/2009/09/30/2120107/Guncangan.Gempa.Paling.Terasa.di.Pariaman.">Pariaman</a>, sehemu ya pwani ya Padang.</p>
<p><div class="wp-caption aligncenter" style="width: 330px"><img alt="Picha iliyowekwa kwenye Twitpic na marcellodecaran" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/09/gempa-padang.jpg" title="gempa padang" width="320" height="240" /><p class="wp-caption-text">Picha iliyowekwa kwenye Twitpic na marcellodecaran</p></div><br />
<a href="http://www.detiknews.com/read/2009/09/30/174704/1212114/10/peringatan-tsunami-dikeluarkan-untuk-indonesia-malaysia-thailand-india?991101605">Tahadhari ya kimataifa ya Tsunami</a> [id] ilitolewa nchini Indonesia, Thailand, Malaysia pamoja na India, lakini iliondelewa baada ya kama saa moja hivi baadaye.</p>
<p>Shirika la Habari la Indonesia Antara <a href="http://www.antaranews.com/berita/1254326936/bnpb-75-orang-meninggal-akibat-gempa-sumbar">liliripoti</a> kuwa idadi ya waliofariki imefikia 75, lakini inaweza kuongezeka kwani bado kuna watu waliofunikwa chini ya kifusi, na wengine wengi bado <a href="http://www.tempointeraktif.com/hg/nusa/2009/09/30/brk,20090930-200134,id.html">wameamua kukaa nje</a> [id] ya nyumba zao kwa kuogopa mitetemo mingine inayoweza kutokea.</p>
<p>Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Mamlaka ya Taifa ya Kudhibiti Majanga (BNPB) Purnomo Sidik huko Antara, makao makuu ya BNPB mjini Jakarta hayajapokea taarifa ya kina kutoka maeneo yaliyoathirika kutokana na mawasiliano mabaya huko Sumatra ya Magharibi.</p>
<p>Asilimia hamsini ya mji imeharibiwa na <a href="http://www.thejakartapost.com/news/2009/09/30/flights-padang-canceled-after-quake.html">safari za ndege ziingiazo Padang zilisitishwa</a> kufuatia uharibifu uliotokea kwenye barabara za kiwanja cha ndege cha Minangkabau.</p>
<p>Ulimwengu wa Twita wa Indonesia umejaa salamu za masikitiko, habari mpya kutoka kwa ndugu na ripoti za misaada.</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/henzter">henzter</a>: ndiyo kwanza nimepokea majibu ya ujumbe wa simu ya mkononi kutoka kwa jamaa yangu @ sumbar: bado ninamtafuta kaka. *Ninaomba dua*</p>
<p><a href="http://twitter.com/martinmanurung">martimanurung</a>: Majimbo ya Kusini na Kaskazini Sumatra yatalisaidia jimbo la Sumatra Magharibi katika misaada ya tetemeko.</p>
<p><a href="http://twitter.com/veraalexandra">veraalexandra</a>: Mungu tafadhali wasaidie kaka na dada zetu walioko <strong>Padang</strong>&#8230;  wape nguvu na uvumilivu.. amen.</p>
<p><a href="http://twitter.com/aditdmid">aditdmid</a>: bru lht dmpak <strong>gempa Padang</strong> td sore. evakuasi mlm ni trhmbt hjn deras &#038; mati lstrk,75% kota lumpuh. smg para krbn dbri kkuatn&#038;ktabahn. amin.</p></blockquote>
<div class="translation"><a href="http://twitter.com/aditdmid">aditdmit</a>: nimeshuhudia matokeo ya tetemeko la Padang, jioni hii uokoaji umeahirishwa kutokana na mvua kubwa pamoja na kukatika kwa umeme, asilimia 75 ya mji umepooza. Tunatumaini waathirika watapata nguvu na uvumilivu. Amen.</div>
<p>Makamu wa Rais, Jusuf Kalla, alifupisha ghafla ya kuwaapisha wabunge wa bunge jipya na aliwatuma mawaziri sita kwenye eneo la tukio kutathmini madhara yaliyotokea.</p>
<blockquote><p>
<a href="http://twitter.com/aulia">Aulia</a>: Tuliwapigia kura. Ombi letu rasmi la kwanza ni kuwataka kutoa michango kutoka mifukoni mwenu kwa ajili ya waathirika wa tetemeko. Wanahitaji (michango) kuliko nyinyi mnavyohitaji.</p></blockquote>
<p>Majira ya saa 5:45 usiku <a href="http://twitter.com/darlingalih">darlingalih</a> anasema:</p>
<blockquote><p>darlingalih: RT @isatbb: Jaringan data GPRS ISAT aman terkendali di <strong>Padang</strong>, anjuran komunikasi ke <strong>Padang</strong> via fitur BB: Email, BBM, YM, FB. Please RT</p></blockquote>
<div class="translation"><a href="http://twitter.com/darlingalih">darlingalih</a>: RT <a href="http://twitter.com/isatbb">@isatbb</a>: GPRS Indosat’s [kwa mujibu wa mwandishi: huduma ya pili kwa ukubwa ya simu za viganjani nchini Indonesia] imerudi tena huko Padang, tunawashauri kuwasiliana na padang kwa kutumia nyenzo za Blackberry: barua pepe, BBM, YM, FB.</div>
<p>Waziri wa Ustawi wa Jamii <a href="http://www.detiknews.com/read/2009/10/01/015308/1212329/10/korban-tewas-diperkirakan-akan-terus-bertambah">Abu Rizal Bakrie</a> amesema kuwa uharibifu wa miundombine uliosababishwa na tetemeko la hivi karibuni unaweza kulingana na ule uliosababishwa na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/May_2006_Java_earthquake">tetemeko la mwaka 2006 huko Yogakarta</a>.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/indonesia-tetemeko-kubwa-laikumba-sumatra/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Philippines:Mafuriko Mabaya Zaidi Katika Kipindi cha Miaka 40</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/philippinesmafuriko-mabaya-zaidi-katika-kipindi-cha-miaka-40/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/philippinesmafuriko-mabaya-zaidi-katika-kipindi-cha-miaka-40/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 30 Sep 2009 12:07:32 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Disaster]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Philippines]]></category>
		<category><![CDATA[Refugees]]></category>
		<category><![CDATA[Relief & Rescue]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=329</guid>
		<description><![CDATA[Kimbunga kilichopewa jina la 'Ondoy" kimeikumba Philippines jumamosi iliyopita na kusababisha mafuriko mabaya zaidi katika kipindi cha miaka 40 ambayo yamesababisha vifo vya watu 50 na kusababisha wakazi 280, 000 kupoteza makazi. Tovuti za kijamii zilipashana habari za kimbunga hicho na jinsi ya kuwasaidia walioathirika. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/mong/">Mong Palatino</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/09/27/philippines-worst-flooding-in-40-years/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Zaidi ya watu 50 wamefariki baada ya kimbunga kilichopewa jina la &#8220;Ondoy&#8221; (Jina la Kimataifa: Ketsana) kilipolipiga jiji la Manila na majimbo jirani. Kimbunga hicho kilisababisha <a href="http://ph.politicalarena.com/presidential-elections/news/51-dead-280-000-displaced-by-ondoy">mafuriko mabaya zaidi nchin</a>i katika kipindi cha miaka 40 na kuwapotezea makazi watu 280,000 jijini Manila na katika majimbo mengine , kuna watu zaidi ya 41,000 kwenye vituo vya dharura. Wakati makala hii inaandikwa, <a href="http://newsinfo.inquirer.net/breakingnews/nation/view/20090927-227141/12M-still-without-power">wakazi milioni 1.2 </a>bado hawana umeme katika mji mkuu wa Philippines.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/09/ondoy.jpg" title="ondoy" class="aligncenter" width="500" height="333" /><br />
Tovuti za kijamii zilitumika vyema siyo tu kwa kupashana habari zinazohusu mvua hiyo kubwa bali pia kuripoti jitihada na kesi za dharura kwenye sehemu zilizoathika na janga hilo. Joey Alarilla <a href="http://joeyalarilla.com/filipinos-turn-to-twitter-as-storm-ondoy-floods-metro-manila/">anaangalia</a> jinsi intaneti ilivyotumiwa na wanamtandao wa Kifilipino wakati kumbunga kilipoikumba Manila.</p>
<blockquote><p>Ninablogu kwa kutumia modemu ya HSDPA USB kwa sababu makazi yetu bado hayana umeme baada ya masaa kadhaa, na bado nina bahati zaidi kuliko wengi wa wananchi wenzangu, ambao baadhi bado wamekwama njiani au bado wako kwenye mapaa ya nyumba zao</p>
<p>Twita na mitandao mingine ya kijamii kama vile Facebook ndiyo njia pekee ambazo watumiaji wa intaneti wa Kifilipino wamekuwa wakizitumia kwenda sambamba na maendeleo pamoja na habari nyingine kama vile kutuma namba za mashirika ya misaada ya dharura na mashirika ya kujitolea hasa hivi sasa wakati mitandao ya simu imefurika.</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/09/ondoy2.jpg" title="ondoy2" class="aligncenter" width="500" height="333" /><br />
Kituo cha Taarifa za Uokoaji kina <a href="http://spreadsheets.google.com/lv?key=tohu9kthNU6anlf21Low08g&#038;toomany=true">lahajedwali</a> ambayo ina orodha ya watu walioathirika na mafuriko ambao wanahitaji kuokolewa. Ramani ya google pia ilitengenezwa ili kufuatilia maeneo yaliyofurika katikati ya jiji la Manila na kuongoza mamlaka kwenye vijiji ambako waathirika na mafuriko wanahitaji msaada.</p>
<p><small>Angalia <a style="color: rgb(0, 0, 255); text-align: left;" href="http://maps.google.com/maps/ms?ie=UTF8&amp;hl=en&amp;msa=0&amp;msid=110868206150348750692.00047479b6400ee29bd89&amp;source=embed&amp;ll=14.645791,121.107874&amp;spn=0.107954,0.154324">ramani kubwa ya hali ilivyo katika Kimbunga cha Ondoy</a> katikati ya jiji la Manila</small></p>
<p>Wafilipino pia walitumia Twita na Plurk kufuatilia habari za kimbunga kadiri zilivyokuwa zinatokea, kwa kweli, &#8220;<a href="http://twitter.com/#search?q=Ondoy%20OR%20%23ondoy">Ondoy</a>&#8221; na &#8220;<a href="http://twitter.com/#search?q=NDCC">NDCC</a>&#8221; (Baraza la Taifa la Kuratibu Majanga) viliondokea kuwa mada maarufu zaidi kwenye Twitter Jumamosi iliyopita. Hii ni mifano ya jumbe za Twita:</p>
<blockquote><p><em><a href="http://twitter.com/pretzelgurl/statuses/4409254925">pretzelgurl</a></em>: baba yangu bado amekwama kazini kwake huko manggahan, mjini pasig. tafadhalini tumeni msaada<br />
<em><a href="http://twitter.com/angeliesa/statuses/4409294878">angeliesa</a></em>: Aliruhusiwa na profesa majira ya mchana. Alitembea na kuhangaika kwenye mafuriko. Alifika nyumbani majira ya saa 2 usiku. Hivi sasa mwili wangu wote u dhaifu<br />
<em><a href="http://twitter.com/janblando/status/4409121638">janblando</a></em>: Bibi yangu bado amekwama kwenye kibanda chake cha kienyeji, huko Cainta. Mafuriko mtaani kwake ni kima cha kiuno na mkondo wake una nguvu.<br />
<em><a href="http://twitter.com/ValfrieClaisse/statuses/4409062388">ValfrieClaisse</a></em>: Oh mie! Hakuna umeme hapa tangu jana. Mafuriko makubwa na machafu yameivamia jamii yote.<br />
<em><a href="http://twitter.com/dementia/statuses/4409040490">dementia</a></em>: kuna misaada mingi inayoingia lakini kinachotakiwa ni njia ya kusafirisha vifaa kwa waathirika<br />
<em><a href="http://twitter.com/teeemeee/statuses/4408293620">teeemeee</a></em>: mafuriko yameshuka chini katika eneo letu la kuegesha magari lakini bado bado ni kima cha magoti au kiuno. Kina kilifikia Karibu na kifua jana usiku<br />
<em><a href="http://twitter.com/ArmelEspiritu/statuses/4406963044">ArmelEspiritu</a></em>: Ndio kwanza nimefika nyumbani baada ya kukesha kwenye gari langu. Ilinibidi nilipeleke sehemu ambyo hakuna mafuriko ili kulinusuru</p></blockquote>
<p>Kuna filamu kadhaa za video zilizopandishwa kwenye Youtube ambazo zinaonyesha madhara ya mafuriko katikati ya jiji la Manila. Video ya kwanza: mafurikokatika mji wa Makati, kitovu cha biashara nchini. Video hii ilipakiwa na yugaabe<br />
<object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/RYrSYTIT3k0&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/RYrSYTIT3k0&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Video hii inaonyesha mafuriko katika mto Marikina. Video ilipakiwa na Initiate360</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/dqAdaiCZBQ4&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/dqAdaiCZBQ4&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Katika mtaa wa Katipunan, basi dogo lilizama kwenye barabara iliyofunikwa na maji.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/XfWpVe7w3DA&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/XfWpVe7w3DA&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Waendao kwa miguu wakijaribu kuvuka barabara iliyofurika</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/f4iX0i1Z8eo&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/f4iX0i1Z8eo&#038;color1=0x3a3a3a&#038;color2=0x999999&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Michango bado inahitajika. Kuna vikundi kadhaa ambavyo <a href="http://burymeinthisdress.com/blog/2009/09/where-to-send-donations-for-victims-of-typhoon-ondoy/">bado vinapokea michango</a> kwa ajili ya walioathirika na mafuriko.</p>
<p>Picha kutoka kwenye Ukurasa wa Flickr wa <a href="http://www.flickr.com/photos/rembcc/sets/72157622458559722/">rembcc</a></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/09/philippinesmafuriko-mabaya-zaidi-katika-kipindi-cha-miaka-40/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
