· Januari, 2011

Habari kuhusu Habari za Hivi Punde kutoka Januari, 2011

Dunia ya Uarabu: “Acheni Kulia Juu Sudani”

  31 Januari 2011

Kura ya maoni kwa ajili ya uhuru wa Sudani ya Kusini leo imeiweka nchi hiyo kwenye uangalizi wa karibu miongoni mwa watumiaji wa twita wa Kiarabu. Kuanzia Saudi Arabia mpaka Palestina, watumiaji Twita wa Kiarabu wanajadiliana kuhusu mshikamano, kugawanyika na rasili mali za Sudani.

Urusi: Mlipuko Katika Kiwanja cha Ndege cha Domodedovo

RuNet Echo  25 Januari 2011

Bomu lililipuka katika kiwanja cha ndege cha Domodedovo mjini Moscow, kwa uchache vifo vya kadri ya watu kumi vimeripotiwa. Mmiminiko wa Twita unapatikana hapa (RUS) na hapa (RUS, ENG). @ann_mint, ambaye anafanya kazi Domodedovo, alikuwa ni mmoja wa watumiaji wa kwanza wa Twita kuripoti juu ya mlipuko huo; “Kuna wahanga...

Tunisia: Anonymous Dhidi ya Ammar – Nani Atashinda Vita ya Kuchuja Habari?

Kichuja habari cha Tunisia, kinachojulikana kama Ammar, kinaeendelea kutishia kuziharibu na kuzifunga anuani za wanaharakati wa mtandaoni, katika nchi hiyo ambayo imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano tangu katikati ya mwezi Desemba. Ni leo tu, wanaharakati wamedai kwamba serikali imeingilia anuani zao za barua pepe,na kuziingilia blogu na mitandao yao ya kijamii, na kuzizuia zisifanye kazi. Hatua hii inaonekana kuja kama kulipiza kisasi kwa shambulio lililofanywa na kikundi cha wanaharakati wa mtanda0ni wanaojulikana kama Anonymous, ambalo lililenga njia na mitandao ya muhimu ya Serikali ya Tunisia.