Habari kuhusu Habari za Hivi Punde kutoka Juni, 2009
Honduras: Zelaya Akamatwa na Kuondolewa Madarakani
Nchini Honduras siku ilianza na habari zinazosema kwamba Rais Mel Zelaya amekamatwa akiwa nyumbani kwake na wanajeshi wenye silaha mnamo siku ya kupigwa kura tata ya maoni. Siku chache kabla, Zelaya alimuondoa madarakani mkuu wa majeshi. Maoni yanatofautiana kutokea yale yanayosema kwamba hali iliyopo ni sawa na mapinduzi ya kijeshi mpaka yale yanayosema kuwa hii ilikuwa ndio njia pekee ya kukomesha jitihada za Zelaya za kutaka kugombea urais kwa awamu nyingine tena.
Msumbiji: Shambulio Dhidi Ya Mgombea Urais
Wanablogu wa Msumbiji wanaandika kuhusu shambulio dhidi ya mwanasiasa Daviz Simango, kwenye mji wa kaskazini wa bandari ya Nacala. Pamoja na maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu, chama cha Simango pia kilitumia huduma ya Twita kuandika kuhusu shambulio hilo.