The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Breaking News Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Breaking News

2009-10-27

Uchaguzi Tunisia: haki Bila Ya Upendeleo!!?

Rais wa Tunisia Zine Al Abidine Ben Ali ameshinda uchaguzi kwa kipindi cha tano kwa asilimia 89.62 ya kura zote. Chama chake cha Democratic Constitutional Rally kilishinda viti vya bunge 161 katika viti 214. Wanablogu wa Tunisia wanatoa maoni katika makala hii.

2009-10-12

Sub-Saharan Africa

Ripoti ya MISNA (Shirika La Kimataifa la Habari La Wamisionari) iliyochapishwa tarehe 25 Septemba inaeleza kuwa maandamano makubwa ya upinzani yalifanyika mjini Labe, jiji la pili kwa ukubwa nchini Guinea, dhidi ya Mkuu wa Nchi Mwanajeshi, Kapteni Moussa Dadis Camara.

Wanablogu Wa Asia Kusini Na Tuzo Ya Nobeli Ya Amani Aliyopewa Obama

Rais wa Marekani Barack Obama amepokea tuzo mashuhuri ya Amani ya Nobeli leo. Wanablogu na wanaoblogu habari fupi fupi huko Asia kusini wanaelezea maoni yao kuhusu habari hiyo.

2009-08-16

Palestina: Maoni Juu ya Kuzinduliwa Kwa Huduma ya Google.ps

Google imeongeza anwani ya google.ps (google palestina) kwenye orodha yake zana inayotoa huduma za utafutaji zinazolenga sehemu mbali mbali. Anwani hiyo mpya inakusudiwa kufanya kazi katika ukanda wea Magharibi na Gaza, ambako watoaji huduma za intaneti hufanyia kazi zao.

2009-08-12

Korea: Ziara ya Clinton Korea Kaskazini

Habari ya kushangaza. Kwa ghafla, Clinton alizuru Korea ya Kaskazini na kama vile 007 aliwarudisha nyumbani wanahabari wawili wa kike ambao walikuwa wameshikiliwa nchini Korea Kaskazini. Kuhusiana na habari hii ya ghafla, hakuna habari zilizowekwa kwenye vyombo vya habari vya umma vya Korea na hata kwenye maoni ya wanablogu. Zifuatazo ...

2009-07-27

Mauritania: Uchaguzi wenye udanganyifu?

Tarehe 18-07-2009, miezi 11 baada ya mapinduzi ya kijeshi yakiongozwa na Jenerali Mohamed Ould Abdel Aziz, Mauritania imemchagua Jenerali huyu kwa Urais, na kusababisha wapinzani wakuu wa Abdel Aziz kuukataa uchaguzi kwamba ni “kiini macho,” kwa mujibu wa Habari za BBC. Pitio la haraka haraka kwenye blogu za nchi za Saheli linaonyesha kwamba wapinzani wako katika ushirika mzuri.

2009-06-29

Honduras: Zelaya Akamatwa na Kuondolewa Madarakani

Nchini Honduras siku ilianza na habari zinazosema kwamba Rais Mel Zelaya amekamatwa akiwa nyumbani kwake na wanajeshi wenye silaha mnamo siku ya kupigwa kura tata ya maoni. Siku chache kabla, Zelaya alimuondoa madarakani mkuu wa majeshi. Maoni yanatofautiana kutokea yale yanayosema kwamba hali iliyopo ni sawa na mapinduzi ya kijeshi mpaka yale yanayosema kuwa hii ilikuwa ndio njia pekee ya kukomesha jitihada za Zelaya za kutaka kugombea urais kwa awamu nyingine tena.

2009-06-13

Msumbiji: Shambulio Dhidi Ya Mgombea Urais

Wanablogu wa Msumbiji wanaandika kuhusu shambulio dhidi ya mwanasiasa Daviz Simango, kwenye mji wa kaskazini wa bandari ya Nacala. Pamoja na maoni kutoka kwenye ulimwengu wa blogu, chama cha Simango pia kilitumia huduma ya Twita kuandika kuhusu shambulio hilo.