The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Breaking News Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Breaking News

2009-11-16

Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini

Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens, ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.

2009-11-08

Americas

Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani ameandika (es) kuhusu tukio hilo kwenye blogu yake, Generación Y, na blogu za Kiingereza kama vile Babalú Blog, Repeating Islands pamoja na Uncommon Sense zinafuatilia habari hiyo. Mahojiano ya sauti (es) na Sanches kuhusu tukio hilo yamepandishwa kwenye YouTube.

Americas

Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú iliweka kiungo kuelekea makala iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na majeshi ya usalama. Habari mpya kutoka kwa Penultimos Días zinataarifu kuwa Sanchez na Orlando Luis Pardo “walipigwa vibaya na kutukanwa”.

2009-10-27

Uchaguzi Tunisia: haki Bila Ya Upendeleo!!?

Rais wa Tunisia Zine Al Abidine Ben Ali ameshinda uchaguzi kwa kipindi cha tano kwa asilimia 89.62 ya kura zote. Chama chake cha Democratic Constitutional Rally kilishinda viti vya bunge 161 katika viti 214. Wanablogu wa Tunisia wanatoa maoni katika makala hii.

2009-10-12

Sub-Saharan Africa

Ripoti ya MISNA (Shirika La Kimataifa la Habari La Wamisionari) iliyochapishwa tarehe 25 Septemba inaeleza kuwa maandamano makubwa ya upinzani yalifanyika mjini Labe, jiji la pili kwa ukubwa nchini Guinea, dhidi ya Mkuu wa Nchi Mwanajeshi, Kapteni Moussa Dadis Camara.

Wanablogu Wa Asia Kusini Na Tuzo Ya Nobeli Ya Amani Aliyopewa Obama

Rais wa Marekani Barack Obama amepokea tuzo mashuhuri ya Amani ya Nobeli leo. Wanablogu na wanaoblogu habari fupi fupi huko Asia kusini wanaelezea maoni yao kuhusu habari hiyo.

2009-09-30

Philippines:Mafuriko Mabaya Zaidi Katika Kipindi cha Miaka 40Video post

Kimbunga kilichopewa jina la 'Ondoy" kimeikumba Philippines jumamosi iliyopita na kusababisha mafuriko mabaya zaidi katika kipindi cha miaka 40 ambayo yamesababisha vifo vya watu 50 na kusababisha wakazi 280, 000 kupoteza makazi. Tovuti za kijamii zilipashana habari za kimbunga hicho na jinsi ya kuwasaidia walioathirika.

2009-08-16

Palestina: Maoni Juu ya Kuzinduliwa Kwa Huduma ya Google.ps

Google imeongeza anwani ya google.ps (google palestina) kwenye orodha yake zana inayotoa huduma za utafutaji zinazolenga sehemu mbali mbali. Anwani hiyo mpya inakusudiwa kufanya kazi katika ukanda wea Magharibi na Gaza, ambako watoaji huduma za intaneti hufanyia kazi zao.