The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Arts & Culture Hifadhi ya mada

Kiungo cha RSS kwa Arts & Culture

2009-11-16

Sub-Saharan Africa ,
Americas

Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, katika makala hii kutoka Haiti, na hii kutoka Guadeloupe na hii kutoka Martinique [Fr].

Western Europe

Nordic Voices anaandika kuhusu 'suala la lugha” huko Finland.

2009-11-13

Venezuela: Kukutana na kazi za msanii Jesus Soto

Kazi za msanii wa Kivenezuela Marehemu Jesus Soto zinapaswa kuguswa na kujizamisha ndani yake ili kuzielewa. Wachache waliwahi kutembelea kazi zake kwenye makumbusho wameandika uzoefu wao.

2009-11-07

Sub-Saharan Africa

Sehemu ya kwanza ya vionjo vya Ghana iliyotayarishwa na Gayle: Nchini Ghana, kila kanda ina kitu cha kutoa. Utamaduni, historia, pwani, wanyama na mimea, unaweza ukavivinjari nchini kote, kutokea kwenye mitisitu ya kitropiki kule kusini mpaka mbuga za savana za kaskazini. kama ni mpenzi wa pwani au historia, utaburudika na ziara hii ya sehemu za pwani.

2009-10-28

Caribbean: Tafakari Mpya Kuhusu Uchapishaji wa Mtandaoni

Wanablogu wa ukanda wa Karibea wanawaza kuanzisha jumuiya ya uandishi na uchapishaji ya mtandaoni ikitumia njia za mawasiliano zilizo shirikishi ili kukabiliana na ugumu wa uchapishaji vitabu unaoukabili ukanda wao.

2009-08-25

Mexico: Simulizi za Siri Kwenye Twita

Rafa Saavedra ni mtaalamu wa utamaduni wa chini chini kutoka mji wa Tijuana, Maxico. Katika mahojiano, anaelezea kila kitu kinachohusu mradi wake mmoja wa hivi karibuni unaojumuisha Twita na utoboaji wa siri.

2009-07-20

Afrika: Wanablogu wamwombolezea Michael Jackson

Barani Afrika, wanablogu wanatoa heshima zao za mwisho kwa Michael Jackson baada ya kifo chake hivi karibuni kwa kutuma picha, video za muziki, mashairi pamoja na tafakari. “Pumzika Kwa Amani” anaandika Mwanablogu wa Kenya WildeYearnings. “Sasa unalo anga zima kucheza kwa madaha kwa staili ya kutembea mwezini…”

2009-07-19

Afrika Kusini: Kuvuvuzela au Kutovuvuzela?

Mjadala kuhusu kifaa maarufu kinachoitwa vuvuzela kinachopigwa na mashabiki wa mpira wa miguu Afrika Kusini umetawala katika blogu mbalimbali duniani tangu kuanza kwa Kombe la Mabara la mwaka huu nchini Afrika Kusini, lililohitimika wiki iliyopita. Waandishi wa habari, watazamaji wa televisheni, makocha na baadhi ya wachezaji wa kigeni walitoa wito wa kusitisha matumizi ya kifaa hiki katika Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini. Mabishano haya yana sauti kubwa kama chombo chenyewe.