Mradi wa Lingua wa Global Voices katika lugha ya ki-Malagasi umechapisha mtandaoni posti yake ya 5,000. Mradi huo ulianza mwezi Septemba 12, 2007 ukiwa kati ya miradi ya mwanzo kabisa ya Mradi mkubwa wa Lugha za Kiafrika. Kwa sasa mradi huo unaendeshwa na watafsiri wa ki-Malagasi wapatao 16 miongoni mwao akiwamo mmoja wa watafsiri wadogo kabisa wa Global Voices , mwenye umri wa miaka 16 aitwaye Radifera Felana Candy.
Habari Maalum Kuhusu Announcements
Angalia Moja kwa Moja Yanayojiri Sasa Hivi Katika Mkutano wa Global Voices

Mkutano wa Global Voices wa 2012 umeshafunguliwa muda mfupi uliopita katika jiji la Nairobi, nchini Kenya. Tungetamani sana kama ungeweza kujumuika nasi mkutanoni, lakini kama hilo haliwezekani, waweza pia ukatutazama moja kwa moja kupitia mtandao wa intaneti na pia tunaweza kujadiliana moja kwa moja.
Wanablogu wa Kenya: Je, ungependa kushiriki kwenye Mkutano wa Global Voices kuhusu Vyombo vya Habari vya Kiraia pasipo kulipia?

Mtandao wa Global Voices unawapa wanablogu sita (6) fursa ya kushiriki pasipo kulipia kwenye Mkutano wake unaohusu Vyombo vya Habari vya Kiraia utakaofanyika jijini Nairobi. Ili uweze kushinda moja ya nafasi hizo, andika makala ya walau maneno 500 au pungufu kidogo kuhusu mada hii: "Jinsi gani vyombo vya habari vya kiraia vinaweza kusaidia kufanya uchaguzi mkuu wa Kenya wa mwaka 2013 uwe wa amani".
Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011

Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011
-
Global Voices: Changia Leo
28 Disemba 2011
-
Tangazo la Mkutano Mkuu wa Uanahabari wa Kiraia wa Global Voices 2010
9 Februari 2010
-
Sisi ni Sauti za Dunia: Miaka Mitano Baadaye
2 Januari 2010
-
Global Voices Yaingia Ubia na Google Katika Tuzo ya Uhuru wa Kujieleza 30 Disemba 2009
-
Kutambulisha Sauti Zinazotishwa
6 Novemba 2009
Habari mpya Kuhusu Announcements
2 Januari 2013
Kusherehekea Mwaka 2012 na Sauti za Dunia
Kadiri mwaka 2012 unavyofikia tamati, tungependa kutoa shukrani zetu kwa kazi nzuri, ubunifu pamoja na kuonesha kujali mambo mengi katika jumuia ya Sauti za Dunia. Mwaka 2012 umekuwa ni mwaka wa ukuaji wa kasi kabisa na wa mafanikio kwa Sauti za Dunia ( Global Voices). Yafuatayo ni baadhi tu ya mafanikio:
16 Septemba 2012

Global Voices Yashinda Tuzo Ya Highway Africa

Washindi: Dorothee Danedjo kutoka Kameruni akiwa na Ndesanjo Macha wa Global Voices. Picha ya Ettione Ferreira (imetumiwa kwa ruhusa)
Timu ya Global Voices inayoandika habari za Nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara imeshinda Tuzo ya Telekom Highway Africa katika kundi la “Blogu bora ya TEHAMA ya Kiafrika”. Mhariri wa Eneo hilo Ndesanjo Macha alikuwepo Afrika Kusini kuipokea tuzo hiyo (na kikombe cha ushindi!) tarehe 11 Sepetemba, 2012 kwa niaba ya timu nzima. Mwanablogu na mwandishi wa habari Dorothy Dandejo kutoka Kameruni alikuwa mshindani wa karibu aliyeibuka mshindi wa pili katika kundi hilo hilo.
27 Agosti 2012
Mgogoro wa Umoja wa Ulaya: Kitabu cha Kwanza cha Global Voices cha Kieletroni
"Umoja wa Ulaya katika Mgogoro" (EU in Crisis) ni chapisho letu la kwanza katika Mradi wa Vitabu wa Global Voices na ambao unahusisha makala bora zaidi kuhusu mazungumzo ya kijamii, ushiriki na uhamasishaji unaopewa nguvu na raia wanaopitia nyakati ngumu za kubana matumizi katika bara la kale zaidi na kwingineko.
21 Julai 2012
Matangazo ya Mkutano wa Sauti za Dunia (Sehemu ya 1)
Sauti za waliowakilisha GV katika warsha mjini Nairobi, Kenya.
6 Machi 2009
Gumzo la moja kwa moja kuhusu Virusi vya ukimwi na Ukimwi mtandaoni Tarehe 6 machi

Mradi wa Rising Voices na Global Voices wanaandaa gumzo la moja kwa moja mtandaoni kwa wanablogu na wanaharakati siku ya Ijumaa mwezi wa tatu mwaka huu(saa 11 jioni kwa saa za Nairobi) mada kuu ikiwa jinsi ya kublogu na kuongeza uelewa na habari kuhusu virusi vya ukimwi na Ukimwi.




























Kiungo cha RSS kwa Announcements 












mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...