<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Swahili</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/languages/swahili/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Afrika: Ujio wa Mkonga wa Seacom Wazua Mjadala</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 27 Jul 2009 14:18:29 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[Mozambique]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[Tanzania]]></category>
		<category><![CDATA[Uganda]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=276</guid>
		<description><![CDATA[Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. Seacom, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, ilianza kutumika moja kwa moja Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/rebekah-heacock/">Rebekah Heacock</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/07/24/africa-the-arrival-of-seacom-cable-sparks-debate/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. <a href="http://www.seacom.mu/index2.asp">Seacom</a>, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, <a href="http://www.guardian.co.uk/technology/2009/jul/23/east-africa-broadband-revolution">ilianza kutumika moja kwa moja</a> Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana.<br />
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 310px"><img alt="Seacom inaunganisha mwambao wa Afrika ya mashariki na Ulaya pamoja na Asia" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/07/picture-1-300x271.png" title="Seacom" width="300" height="271" /><p class="wp-caption-text">Seacom inaunganisha mwambao wa Afrika ya mashariki na Ulaya pamoja na Asia</p></div></p>
<p>Miji ya Johannesburg, Nairobi na Kampala <a href="http://www.google.com/hostednews/afp/article/ALeqM5iHrESmY6eTaALo3tbsjwGSPkPP1Q">iliunganishwa </a>Alhamisi, na Addis Ababa pamoja na Kigali inatarijia kufuata. Ujio wa mkonga huo ulipangwa kufikav mnamo mwanzoni mwa mwezi wa saba, lakini <a href="http://allafrica.com/stories/200906290065.html">mashumbulizi ya maharamia</a> nje kidogo ya pwani ya Somalia yalichelewesha utekelezaji.</p>
<p>Kiunganishi hiki cha chini ya bahari kinatarajiwa kupunguza gharama za upana wa masafa kwa asilimia 90 na kuongeza uwezo wa makongamano yanayotumia video, urushaji wa matangazo ya televisheni yenye picha za hali juu pamoja na huduma za intaneti zenye mwendo wa kasi kwenye mwambao wa Afrika ya mashariki.</p>
<p>“Mmmh… nasuburi kwa hamu kuanza upakuzi,” anaandika <a href="http://itblogkenya.blogspot.com/2009/07/seacom_22.html">IT blog Kenya</a>.</p>
<p>Huko Uganda, Josh kutoka blogu ya <a href="http://inanafricanminute.blogspot.com/2009/07/kung-fu-baby-and-seacom-cable-launch.html">In African Minute</a> ameshaanza kubaini tofauti:</p>
<blockquote><p>Mbinu inayojulikana ili kuangalia video za YouTube barani Afrika ni kwa kubonyeza alama ya kugandisha video wakati inapoanza, subiri kwa dakika 20 (au zaidi) mpaka hapo video itakapopakuliwa yote, halafu angalia. Leo nipo kwenye sherehe ya kuzindua SEACOM… kwenye kona ya chumba cha kongamano, Peter Mereton Meneja wa ununuzi wa SEACOM, alinipa ishara niionyeshe tarakilishi yenye ukurasa wa YouTube uliokuwa tayari. Tuliizindua <a href="http://www.youtube.com/watch?v=bxAirY-5QCQ">Kung Fu Baby</a> na kwa mara ya kwanza katika Afrika, niliona video ya YouTube ikipakuliwa yote na kuchezwa katika sekunde 6.</p></blockquote>
<p>Munashe wa <a href="http://www.techmasai.com/2009/07/24/seacom-the-under-sea-cable-has-arrived/">TechMasai</a> naye anafurahia:</p>
<blockquote><p>Mkonga wa chini ya bahari wa Seacom tuliouandika <a href="http://www.techmasai.com/2008/04/02/eassy-east-african-submarine-cable/">kitambo kidogo nyuma</a> umetimia na umeanza kufanya kazi leo. Ni mchakato wa kimapinduzi kutokana na ukweli kwamba nchi ambazo zitautumia hivi sasa, ambazo zinajumuisha kenye, Uganda, Msumbiji, Afrika Kusini na Uganda.</p>
<p>… Ni wakati mzuri kwa Afrika, Ninaweza kudhibitisha hilo kwa Kenya ambayo mpaka hivi sasa ilitegemea setilaiti kwa ajili ya mahitaji yake ya intaneti.</p></blockquote>
<p>Jeremy, mwanablogu wa Kinaijeria anayeandika katika <a href="http://naijablog.blogspot.com/2009/07/east-africa-goes-broadband.html">NaijaBlog</a>, analinganisha Seacom na mikongo mbalimbali ya Afrika magharibi. Afrika Magharibi bado ipo chini:</p>
<blockquote><p>Afrika ya Mashariki imekwenda na huduma ya masafa mapana ya intaneti… wakati Afrika ya Magharibi bado ipo kwenye sehemu ya kuanzia mbio (kwa kweli, bado ipo kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ikijiuliza ni nini cha kuvaa) wakiwa na SAT3 isiyo na manufaa ambayo hukatika-katika, pamoja na Glo1 9je wakandarasi wa Alcatel wamekwama chini ya mabiwi ya mchanga?) na wakandarasi wengine wawili wapya, WACS na Main1 bado wakiwa mbali zaidi ya upeo (mwaka kesho kama tukiwa na bahati). Afrika ya mashariki imekumbatia huduma ya masafa mapana ya intaneti na kushika mbio wakati Afrika ya Magharibi  inasuasua na kukodoa macho.</p></blockquote>
<p>Twita nayo inanguruma na habari za Seacom. Baadhi ya watumniaji wana shauku, wakati wengine wana mashaka:</p>
<p>“Bado sijaweza kuamini kuwa unaweza kupakua mtandao wote wa Intaneti kupitia mkongo mmoja mdogo wa manjano <a href="http://twitter.com/search?q=%23seacom">#seacom</a>&#8220;<br />
— <a href="http://twitter.com/ncallegari/statuses/2815733071">ncallegari</a></p>
<blockquote><p>“Seacom ilizinduliwa_kwa hakika_leo. Na tuangalie itachukua muda gani kwa mawakala wa intaneti kuongeza kasi na kupunguza gharama…”<br />
— <a href="http://twitter.com/dnyaga/status/2808617797">dnyaga</a></p>
<p>‘je ni mimi au ni huduma za intaneti katika Nairobi ambazo zimezorota leo tangu <a href="http://twitter.com/search?q=%23seacom">#seacom</a> ilipozinduliwa? Pengine uwezo wa mkubwa wa inteneti unaburudika na mandhari ya bahari kabla ya kutufikia”<br />
— <a href="http://twitter.com/mentalacrobatic/statuses/2804058608">mentalacrobatic</a>
</p></blockquote>
<p>Mengi ya mashaka juu ya Seacom yapo kwenye suala la bei: japokuwa baadhi ya wataalamu wa mambo wanadai kuwa gharama za upana wa masafa zitashuka kwa asilimia 90, wengine wanaamini kwamba makato ya gharama yanaweza yakawa madogo zaidi. <a href="http://www.kachwanya.com/?p=428">Kachwanya</a> anaandika:</p>
<blockquote><p>Katika dunia sawa gharama zinapaswa zishuke kwa zaidi ya asilimia 90, hivi sasa inawagharimu mawakala wa kutoa intaneti dola 6500  za Kimarekani (takriban Shilingi 487500 za Kenya) kwa kila kipimo cha Megabiti za upana wa masafa, lakini shika pumzi yako, usitarajie miujiza katika hili. Hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa UUnet Tom Omariba alidai kuwa mikonga itashusha gharama kwa asilimia 20-30.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu <a href="http://www.truekenyan.com/2009/07/23/oh-kenyans-we-have-been-duped-again/">TrueKenyan</a> guswa na suala la uwazi:</p>
<blockquote><p>
Seacom wamekataa katu kutuwekea wazi, sisi walaji wa intaneti, ni mawakala gani wa kusambaza intaneti walionunua upana wa masafa kutoka kwao. Hivyo bado tupo kizani na hatufahamu ni wapi tunapoweza kununua huduma ya intaneti yenye uhakika na kwa bei nafuu… kwa hiyo jambo pekee ninaloweza kufanya ni kuendelea na wakala wangu wa intaneti huku nikiitazama mashine wakati ikipakua kurasa kwa kasi inayoamua yenyewe huku nikiwaza kuwa siku moja ndoto yetu itatimia. </p></blockquote>
<p>Akitoa maoni katika blogu ya Mtanania <a href="http://issamichuzi.blogspot.com/2009/07/jk-azindua-kituo-cha-mkongo-wa-fibre.html">Issa Michuzi </a>[SW}, mdau pia anahofu juu ya gharama, japokuwa ana matumaini makubwa ya baadaye: </p>
<blockquote><p>Asanteni sana kwa huo mkonga. Sasa kutandaza fibre-optic cables kwenye miji mbalimbali tunaanza lini? Manake kuwa na inter-country connection wakati within the country hatuna connection nzuri bado gharama zitakuwa juu na kwa maoni yangu tutakuwa tuna-under utilise capacity ya hiyo under sea cable. For the moment, well done! For the future, we have to work had!</p></blockquote>
<p>Kwa <a href="http://jellyfishcoolman.wordpress.com/2009/07/24/seacom-goes-live/">Jellyfish</a>, ambaye anayatupilia mbali masuala ya gharama kwa kusema kuwa ongezeko la kasi la kiasi hicho na kiwango cha huduma mkwa kawaida huenda sambamba na ongezeko la bei, ujio wa Seacom ni jambo zuri:</p>
<blockquote><p>
Katika tukio lililoratibiwa na kutangzwa sana SEACOM iliwasha funguo ambayo mara moja ilieneza Terabiti za upana wa masafa katika kasi ya mwanga kupitia nyuzi za vioo zilizotengenezwa na kupigwa msasa katika kiwango cha hali juu. </p></blockquote>
<p>Na kwa mwanablogu wa Afrika Kusini <a href="http://twitter.com/akianastasiou/status/2797795511">Aki Anastasiou</a>, “Hii ni MB ndogo kwa talakilishi yangu ya mapajani, TB moja kubwa kwa Afrika.”</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Saudi Arabia: Kina Mama Huru</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/09/saudi-arabia-kina-mama-huru/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/09/saudi-arabia-kina-mama-huru/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 06 Sep 2008 01:57:04 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Humor]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[TOPICS]]></category>
		<category><![CDATA[TYPE]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=16</guid>
		<description><![CDATA[WAKATI kukiwa hakuna shaka kwamba kuna vizuizi kwa wanawake waishio Saudi Arabia, havifanani na taswira iliyojengwa na wageni dhidi ya taifa hilo. Katika makala hii tunao ushauri kwa wakina mama wanaotaka kutembelea jiji la Jeddah wakiwa peke yao, kuna muhtasari wa hoteli za kina mama pekee jijini Riyadh, na wito kwa wageni wote wanajihisi kuzungumza kwa niana ya kina mama wanaokandamizwa wa Saudia.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ayesha-saldanha/">Ayesha Saldanha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/29/saudi-arabia-independent-women/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>WAKATI kukiwa hakuna shaka kwamba kuna vizuizi kwa wanawake waishio Saudi Arabia, havifanani na taswira iliyojengwa na wageni dhidi ya taifa hilo. Katika makala hii tunao ushauri kwa wakina mama wanaotaka kutembelea jiji la Jeddah wakiwa peke yao, kuna muhtasari wa hoteli za kina mama pekee jijini Riyadh, na wito kwa wageni wote wanajihisi kuzungumza kwa niana ya kina mama wanaokandamizwa wa Saudia.</p>
<p>Tunaanza na Hala, ambaye anaishi Marekani hivi sasa na anablogu katika blogu yake HALA_IN_USA, anayetoa ushauri kwa marafiki zake akinamama wasio na waume watakaotaka kutembelea jiji la <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jeddah">Jeddah</a> kwa mara yao ya <a href="http://hala1.wordpress.com/2008/08/27/visiting-jeddah-a-single-woman-perspective/">kwanza</a>:</p>
<blockquote><p>Wanawake katika jiji la Jeddah huvaa gauni lijulikanalo kama &#8220;<a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Abaya">Abaya</a>&#8220;, gauni hili hupaswa kuvaliwa juu ya mavazi mengine hivyo vaa nguo nyepesi za ndani haswa wakati wa majira ya kiangazi. Ushungi si lazima kwa akina mama wageni lakini ni vazi linalopendekezwa kuvaliwa (kwa ajili ya usalama na kuepuka usumbufu usiokuwa wa lazima) katika maeneo ya kiutamaduni.</p>
<p>Kuna maeneo mbalimbali ya kuyaona jijini Jeddah, ninapendekeza Balad, jiji la kale la Jeddah, likiwa na majengo yaliyosanifiwa kizamani, Jengo la Naseef ni mfano mmojawapo wa majengo ya kale. Unaweza kununua bidhaa za kitamaduni za kale kutoka katika maduka ya kizamani na ukafurahia marashi ya Kiarabu kama vile Udi Bukhour, vilevile kuna bidhaa za kazi za mikono za kitamaduni kama balbu, [fanusi], tende, pipi na vitambaa vya rangi mbalimbali.</p>
<p>Pia kuna <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jeddah_Corniche">barabara maarufu jijini Jeddah iliyokatiza ufukweni mwa bahari </a>. Napendekeza upite katika barabara hiyo mapema alfajiri au jioni saa 12 ili uweze kujionea maumbile ya kupendeza baharini, pia kuna chemchem ya baharini, moja ya chemchem zilizoko juu zaidi kuliko nyingine yoyote duniani. Kuna machaguo mbalimbali ya vyakula katika barabara ya kupendeza ufukweni mwa bahari, kuanzia migahawa ya ya anasa mpaka maduka ya vyakula vya haraka au hata vijiduka vidogo vya biskuti na chipsi. Wenyeji hukuketi katika ufukweni kwa masaa na watoto wao wakicheza karibu yao huku wakiwaangalia wapita njia.</p></blockquote>
<p>Kwa ushauri zaidi wa Hala kuhusiana na unachotaka kukiona jijini Jeddah, angalia <a href="http://hala1.wordpress.com/2008/08/27/visiting-jeddah-a-single-woman-perspective/">hapa</a>.</p>
<p>Wakati huo huo bloga <em>American Bedu</em>, ambaye ni Mmarekani anayeishi Saudi Arabia, anatueleza kile anachokifikiri kuhusiana na hoteli za kina mama pekee jijini <a href="http://americanbedu.com/2008/08/28/so-what-if-riyadh-has-a-women-only-hotel/">Riyadh</a>.</p>
<blockquote><p>Hoteli ya <a href="http://www.luthanspa.com/default.htm">Al Luthan</a> na bafu lake ni hoteli ya kwanza kabisa ya wanawake pekee ya aina yake jijini Riyadh. Ni hoteli ya kifahari na ina bafu la chemchem maalumu kwa wanawake pekee. Ni hoteli ya huduma zote yenye kutoa huduma za uhakika na yenye kutoa malazi salama. Al Luthan inapokea wageni wa kike kutoka Saudia na wasio Wasudia. Hivi sasa baadhi ya wanawake wamezungumza na vyombo vya abari wakisema kuwa kuzinduliwa Al Luthan ni mojawapo ya upigani hatua nyuma.  Kwa mujibu wa wanawake hawa, wanaona kama ni kupiga hatua kuelekea nyuma kwa ufalme wa taifa hilo kutokana na ukweli kwamba tayari kuna ubaguzi na siyo tu kwamba wanawake wana haki kidogo lakini kwa kushabikia na kuafiki uanzishwaji wa hoteli ya wanawake peke yao yenye eneo la kuogea inarudisha nyuma harakati za kina mama kudai haki. Pengine nimo kwenye kundi dogo katika jamii, lakini nachukua mtazamo mbadala. Al Luthan siyo hoteli ya kipekee ikilinganishwa na hoteli nyingine duniani. Hoteli za wanawake au hoteli zinazotenga safu nzima ya ghorofa kwaa jili ya wanawake zipo karibu katika kila jiji kubwa (na hata kwenye miji isiyo mikubwa) duniani. Siku za nyuma wakati nilipokuwa nikisafiri safari nyingi za kimataifa, nilikuwa nikifurahia kupanga katika hoteli zenye safu maalumu kwa ajili ya wanawake pekee. Haswa katika  majiji ya kigeni ambayo hayakuzoea kuwa na wafanyabiashara wanawake wanaosafiri peke yao. Kwa hiyo mimi sioni kama kuanzishwa kwa hoteli hii maalumu kwa wanawake kuwa ni hatua ya kurudi nyuma asilani bali chaguo jema kwa wanawake kuwa nalo ndani ya falme.</p></blockquote>
<p>Bloga kutoka Riyadh, <em>Sweet Anger</em> amechoshwa na wageni wanaodhani kuwa wanawake wa Kisaudia wanakandamizwa, wakati hawajui lolote kuhusu maisha yao au <a href="http://sweetangerksa.blogspot.com/2008/08/saudi-arabia.html">jamii</a>: </p>
<blockquote><p>Basi, nilikuwa nikitafiti mtandaoni kitu kimoja au kingine nikakutana na ujumbe kuhusu ripota aliyekuwa Saudia ambaye ni mwanamke na hivyo hakuruhusiwa kukaa kwenye sehemu ya wanaume ndani ya mgahawa wa Starbucks.umm boo hoo hoo. Kitu kilichonishika zaidi siyo ile makala yenyewe, lakini maoni. […] Nataka ieleweke kwamba Saudi siyo mahema machache yanayounganishwa na ngamia wanaorandaranda, na wanaume wenye vilemba waimbao &#8220;Allah o akbar&#8221; huku wakiwabaka wanawake kwa sababu ni haki yao na wanamiliki nyumba ya harimu yenye vigoli si  chini ya 20. Oh, na pia  hatutahiri wanawake wetu, hilo ni jambo la hovyo na ni kosa katika ngazi nyingi.  Wanawake hawafungiwi nyumbani na yeyote yule ambaye kwamba hilo ni jambo la  utamaduni wa familia na siyo nchi, upo? Vyema. Hatuko nyuma nyie mafidhuli, sisi ni wahafidhina, yaani, kama unapotaka kwenda kujichanganya na mtu wa jinsia tofauti kuna maeneo maalumu. […] Sasa hoja yangu ya msingi hapa ni kwamba hivi tangu lini mmeanza kuhukumu watu: &#8220;Fungeni Starbucks!! Zisiwe na sehemu zinazokaribisha familia&#8221; – umm, hapana samahani? Silalamiki na ninahitaji kahawa yangu, tuache utani, POTEENI MBALI, sikukodi mtu yeyote awe msemaji wangu.</p>
<p>Kwa wale ambao bado mnashawishika kwamba sisi ni taifa kandamizi na kwamba sisi wanawake masikini tunahitaji kufunzwa namna ya kupambana na kama sivyo vyema vyema endeleeni kutupigania, ngojeni niwape maelezo mafupi namna siku ya kawaida inavyokuwa jijini Riyadh. Jana niliamka nikatengeneza kahawa yangu… nikatinga vazi langu la abaya (kama unaona hili linatisha kufikirika, lifikirie kama jaketi), nikamchukua malaika wangu mdogo, nikaingia ndani ya gari yangu iendeshwayo na dereva ndani yake, nikamshusha binti yangu, halafu nikaenda kazini. Mida ya saa 7:30 napata chakula cha mchana na marafiki zangu wa kike kutoka mgahawa wa Subway, halafu nikarejea kazini na kutoka saa 10:30 jioni, narejea nyumbani, napumzika, naoga natinga mavazi yangu, namsubiri dereva anipeleke mgahawa wa Wachina kwani nilikuwa nimewakaribisha marafiki zangu wa kike. Nafika pale mida ya saa 3:45 hivi halafu naondoka kama saa 6, nafika nyumbani, naingia mtandaoni, naangalia facebook na hotmail, halafu naingia kitandani saa 8. MUNGU WANGU, JINAMIZI GANI HILI, NINAWEZAJE KUISHI MAISHA YA KIKANDAMIZWA NAMNA HII, AAAAHHHHHH!!!! […] Hoja yangu ni kwamba baadhi ya watu hawana welewa kuhusu nini kinaendelea ndani ya maisha yetu na bado wanafikiri wana haki ya kuamua na kuwa wakuu. Tuko tofauti, naam, na kwa kuwa tuko tofauti na vile ambavyo unafikiri ni sawa haitufanyi sisi kuwa wabaya au wenye makosa inatufanya sisi kuwa sisi. Kabiliana na ukweli huo au jitoe.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/09/saudi-arabia-kina-mama-huru/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Pakistani: Musharraf Aondoka Jengoni</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/pakistani-musharraf-aondoka-jengoni/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/pakistani-musharraf-aondoka-jengoni/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 22 Aug 2008 14:29:29 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Pakistan]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=12</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naAwab Alvi  &#183; Imetafsiriwa na Deogratias Simba &#183;  Angalia ujumbe mama 
Imepita miaka nane, siku mia tatu na ushee tangu mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu yaliyoongozwa na Jenerali wa Jeshi la Pakistani yalipofanyika na hivyo kumpokonya madaraka kiongozi fisadi Nawaz Sharif. Wakati huo kulikuwa na matumaini ya kesho mpya, ilikuwa ni [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/awab-alvi/">Awab Alvi</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/19/pakistan-musharraf-has-left-the-building/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Imepita miaka nane, siku mia tatu na ushee tangu <a href="http://kadnan.com/blog/2008/08/18/17th-august-1988-18th-august-2008/">mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu</a> yaliyoongozwa na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Pervez_Musharraf">Jenerali wa Jeshi la Pakistani</a> yalipofanyika na hivyo kumpokonya madaraka kiongozi fisadi Nawaz Sharif. Wakati huo kulikuwa na matumaini ya kesho mpya, ilikuwa ni mwendo wa madaha kuelekea kwenye dira iliyofifia iliyopachikwa jina la ‘mwamko wa wastani wenye kuongozwa na fikra pevu’ na ama kwa hakika hatua muhimu katika kuiondolea jamii gonjwa lililogeuka kuwa janga, yaani, rushwa. Wakati huo raia wa Pakistani walisherehekea, lakini haikupita muda mrefu kabla watu hawajang’amua kuwa walikuwa tena kwenye janga wasilotaka, na kwa bahati mbaya ujaji huo polepole uligeuka kuwa utawala wa kidikteta usiotakikana. Baada ya miezi mingi ya utawala wa mabavu, hivi majuzi kulitokea tukio la kumaliza utawala uliodumu muda wa miaka tisa kasoro siku sitini, na hapa Pakistani inafungua ukurasa mpya. </p>
<p>Ilionekana kama siku nyingine nchini Pakistani lakini mara iligeuka kuwa inayojijaza munkari na mara minong’ono ilianza kusambaa miongoni mwa raia wakati habari zilipoanza kusambaa. Watu hao waligubikwa na <a href="http://www.teeth.com.pk/blog/2008/08/18/safe-exit-today-safe-entry-for-future-dictators-tomorrow">mnong’ono mmoja baada ya mwingine</a> kutoka katika taarifa zilizorushwa na vituo vya televisheni kwenda kwenye ujumbe mfupi wa maneno na hata barua pepe; ilikuwa kana kwamba majaaliwa ilikuwa yaamuliwe na kila mmoja wao. Gazeti tando moja linalokwenda kwa jina la linatupa muhtasari makini kuhusu msukumo wa minong’ono hiyo katika sentenso moja: &#8216;<a href="http://www.deadpanthoughts.com/?p=509">Simu inaita – Mushy anaondolewa madarakani kwa manufaa ya umma … tazama GEO (kituo kimoja cha televisheni) … SASA hivi&#39; </a>Wapo waliotuaminisha kwamba huyu jamaa anayekwenda zake angejaribu kujitetea ili abaki madarakani, wapo waliotabiri kwamba huenda angerejesha mfumo wa mahakama kama njia yake pekee ya kujinusuru na kulipiza kisasi; kinyume chake hali imegeuka kuwa hotuba ya kuagia, akiachia mambo mbele ya watu wake wa karibu waliokuwa wakilengwalengwa na machozi, hali ambayo tunahabarishwa kupitia kwamba ‘<a href="http://saim-baig.blogspot.com/2008/08/no-last-punch-musharraf-resigns.html">akiwa amevaa uso usio na tabasamu Musharraf, huku akipepewa na bendera za Pakistani nyuma yake na picha ya ‘mwanzilishi’ wa taifa hili</a> aliishia kusema “<strong>Naweka hatma yangu mikononi mwa umma</strong>.”</p>
<p><img src='http://farm1.static.flickr.com/153/345600341_bf03e54162.jpg?v=0' alt='' class='alignnone' /></p>
<p><strong>Pervez Musharraf</strong> - Picha kwa hisani ya: <a href="http://www.flickr.com/photos/worldeconomicforum/345600341/">Mtiririko wa picha za Flickr wa Mkutano wa Uchumi Duniani</a> zilizo chini ya <a href="http://creativecommons.org/licenses/by-sa/2.0/deed.en">haki miliki huria kwa umma</a>.</p>
<p>Kuaga huku kulikotawaliwa na machozi kulikofanya na Musharraf mnamo tarehe 18 Agosti mwaka huu kulikuja zikiwa zimepita siku nne tu tangu Taifa liadhimishe sherehe za miaka 61 ya Uhuru. Ni katika hali ya tahadhari kubwa kwamba Pakistani inaadhimisha mwisho huu wa miaka tisa ya utawala wa familia hii. Hotuba yake ya mwisho ilijaa hasa <a href="http://www.pakspectator.com/look-back-at-musharrafs-era/">kurejelea historia</a> na hii ni kama ilivyonukuliwa na <em>The Pakistani Spectator</em>, yaani hasa kuelezea ni kwa namna gani <a href="http://changinguppakistan.wordpress.com/2008/08/18/its-official-musharraf-resigns/">alitumikia nchi na watu wake</a>.  </p>
<p>Wanablogu wa KiPakistani walipokea taarifa hizi kwa hisia tofauti, wapo waliomshabikia kwa miluzi yenye kuashiria kwamba alikuwa ‘<a href="http://pitafi.com/2008/08/18/for-he-is-a-jolly-good-fellow/">a Jolly Good Fellow’ </a>(mtu mwema na mchangamfu), wakati huohuo washabiki wake waaminifu hawakukawia <a href="http://pak1stanfirst.com/2008/08/18/support-for-president-musharraf/">kumpigia mbija za kumpongeza</a>, hata hivyo wapo waliochukua hali hii kwa tahadhari huku wakisherehekea kumalizika kwa utawala wa kidikteta. Katika namna ya kukejeli, <em>Yeah That Too</em> alishirikisha <a href="http://think-islam.blogspot.com/2008/08/he-came-he-saw-poof.html">maneno machache</a>, <em>Ammar</em> kwa upande wake aliandika kuhusu namna ‘<a href="http://ammar360.com/2008/08/18/the-cat-fight-now-begins/">Mpambano mpya wa manyau’ unavyokaribia kuanza</a>, <em>Chowrangi</em> anazungumizia <a href="http://www.chowrangi.com/pervez-musharrafs-resignation-and-the-way-forward.html">mustakabali wa nchi ya Pakistani baada ya Musharraf</a>, <em>Psychotic Discourses </em>anatupatia mwanga juu ya <a href="http://blog.anasimtiaz.com/2008/08/18/welcome-to-demon-cracy/">muundo mpya wa ‘Utawala wa Kishetani’ </a>(Demon-cracy), wakati ambapo <em>MB</em> anatuchanganya zaidi kwa kuzungumizia hali hii kama moja ya <a href="http://publicmb.wordpress.com/2008/08/18/the-circle-in-the-circus-completes-again/">mizunguko ya kisarakasi</a>. </p>
<p>Swali kubwa kwa sasa linabaki kuwa endapo Musharraf anaruhusiwa kutafuta ukimbizi nje ya Pakistani au endapo <a href="http://kadnan.com/blog/2008/08/18/17th-august-1988-18th-august-2008/">atafikishwa mbele ya sheria</a> ili kujibu <a href="http://www.teeth.com.pk/blog/2008/08/11/reference-against-pervaiz-draft">tuhuma mbalimbali zinazomkabili</a>. Ama kwa hakika ni changamoto kubwa kwa Taifa la Pakistani na ambayo inaweza kuwa na matokeo mengi.</p>
<p>Mtu anabaki kujiuliza, <a href="http://pakistanpolicy.com/2008/08/18/after-musharraf-the-next-president/">hivi nini kinafuata</a>, hasa katika kipindi hiki ambapo kuna wanasiasa wenye matumaini ya kunyakua cheo hicho cha juu zaidi katika taifa hili, ambapo hata hivyo jukumu la kuiondoa nchi katika mkanganyiko huu mkubwa liko zaidi mabegani mwa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Asif_Ali_Zardari">Asif Zardari</a> na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Nawaz_Sharif">Nawaz Sharif</a>, ambapo wote wawili ni wanasiasa ambao hawakuchaguliwa lakini ambao wengi wanawawekea matumaini makubwa ya kuiondoa nchi hii kutoka katika lindi la vurugu ambamo imo kwa sasa. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/pakistani-musharraf-aondoka-jengoni/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
