<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Spanish</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/languages/spanish/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Paraguay: Wenyeji Wanyunyiziwa Dawa za Kuua Wadudu kwa Ndege</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/paraguay-wenyeji-wanyunyiziwa-dawa-za-kuua-wadudu-kwa-ndege/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/paraguay-wenyeji-wanyunyiziwa-dawa-za-kuua-wadudu-kwa-ndege/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 17 Nov 2009 09:56:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Agriculture]]></category>
		<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Indigenous]]></category>
		<category><![CDATA[Paraguay]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=685</guid>
		<description><![CDATA[Huko Mashariki mwa Paraguay, jumla ya watu 217 wa jumuiya ya wenyeji ya Ava Guaraní walianza kusumbuliwa wakionyesha dalili mbalimbali za kiafya zinazoaminika zilisababishwa na unyunyiziaji wa makusudi wa dawa za kuua wadudu hasa baada ya wao kuwa wamegoma kuhama kutoka katika ardhi waliyoirithi kutoka kwa mababu zao.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/eduardo-avila/">Eduardo Avila</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/12/paraguay-indigenous-group-sprayed-aerially-with-pesticides/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Huko Mashariki mwa Paraguay, jumla ya watu 217 wa jumuiya ya wenyeji ya Ava Guaraní walianza kusumbuliwa wakionyesha dalili mbalimbali za kiafya zinazoaminika zilisababishwa na unyunyiziaji wa makusudi wa dawa za kuua wadudu hasa baada ya wao kuwa wamegoma kuhama kutoka katika ardhi waliyoirithi kutoka kwa mababu zao.</p>
<p>Watendaji wa serikali wamethibitisha kwamba baadhi ya sehemu za ardhi ya wenyeji iliyo katika Wilaya ya Itakyry katika <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Alto_Paran%C3%A1_Department">Idara ya Alto Paraná</a> ilinyunyiziwa wakati ambapo <a href="http://www.ultimahora.com/notas/272060-Ministra-confirma-que-fumigaron-tierras-sin-cultivo-en-Itakyry">hakukuwa na mazao yoyote </a>[es]. Ishara nyingi zinaelekezwa kwa walima maharage ya soya wa KiBrazili kwamba ndiyo wanaohusika na unyunyiziaji huo, kwani kwa kiasi kikubwa ardhi iliyo mikononi mwa jamii za wenyeji ingefaa sana kwa zao hilo na kwamba hawa wamekuwa katika mgogoro na Ava Guaraní kuhusu <a href="http://interparaguay.blogspot.com/2009/11/ministros-comprobaron-la-fumigacion.html">umiliki wa takribani hekta 3,000</a>, kwa mujibu wa blogu ijulikanayo <em>Interparaguay [es]</em>.</p>
<blockquote><p>José Ángel López Barrios wa Bienvenidos! [es] akielezea eneo la jamii lililo mbali na mengine ambapo tukio hilo lilitokea:<br />
Itakyry es uno de los distritos del Departamento de Alto Paraná, distante a unos 450 kilómetros de Asunción, capital de la Republica, se llega a el por caminos no pavimentados, su época de esplendor se dio en la época de las explotaciones yerbateras. Que termino al cabo de 100 años abriendo paso a la explotación de la soja en estos últimos tiempos……</p></blockquote>
<div class="translation">
Itakyry ni moja ya wilaya za Idara (Mkoa wa) Alto Paraná, iliyo umbali wa kilomita 450 kutoka katika mji mkuu wa Asunción. Kufika huko mtu huna budi kutumia barabara za vumbi, katika kilele cha mafanikio yake ilikuwa ni wakati wa ulimaji wa yerba maté. Jambo hilo lilikoma baada ya miaka 100, na kupisha ulimaji soya katika miaka ya hivi karibuni……</div>
<p>Ni mahitaji ya maharage ya soya na bei yake inayozidi kupanda ambayo inaifanya ardhi hiyo kuwa inayofaa kwa zao hili lenye kipato kikubwa sasa. Sehemu ya ardhi hii iko kwenye ardhi ya kurithi ya mababu wa jamii za wenyeji, kama vile <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Guaran%C3%AD">Guaraní</a>. Mwanablogu Carlos Rodríguez wa <em>Rescatar [es]</em> <a href="http://rescatar.blogspot.com/2009/11/soja-y-genocidio-fumigan-indigenes.html">hafikiri kwamba tukio la unyunyiziaji dawa dhidi ya makundi ya wenyeji ni tukio dogo, analiita tendo hilo kama &#8220;mauaji ya halaiki</a>&#8220;: </p>
<blockquote><p>Hubo un tiempo en que en Paraguay los aborígenes no eran considerados seres humanos. Eran cazados como animales y sus crías rescatadas como trofeos.<br />
(…)<br />
Otros fueron apropiándose a bala y sangre de sus tierras y como los indígenas no hacían gestiones ante las instituciones encargadas de titular las tierras que siempre les pertenecieron, el hombre blanco si lo hizo y se plantea el contrasentido de que los legítimos dueños de estas tierras, hoy son “los invasores”.<br />
Y siguen siendo tratados como animales. Sólo así se puede entender que los productores de soja les envíen aviones fumigadores para lanzarles venenos encima, tal como lo ha comprobado el Ministerio de Salud que socorre en estos momentos a los indígenas intoxicados por plaguicidas para soja.</p></blockquote>
<div class="translation">Kuna kipindi hapa Paraguay ambapo WaAborigino hawakudhaniwa kuwa ni binadamu. Waliwindwa kama wanyama na watoto wao walichukuliwa kama mapambo fulani hivi.<br />
(…)<br />
Sehemu ya ardhi yao iliporwa kwa risasi na damu, na hasa kwa kuwa wenyeji hawa hawakwenda kwenye mamlaka zinazohusika na utoaji hati miliki za ardhi kuhusu ardhi ambayo daima wameimiliki, Wazungu hawakwenda kwenye taasisi hizo, na katika jambo ambalo ni la kushangaza, hawa wanaochukuliwa kwamba wao ndiyo wamiliki wa ardhi hiyo ni hawa &#8220;wavamizi&#8221;.<br />
Wanaendelea kutendewa kama wanyama. Ni kwa njia hii tu ambapo mtu anaweza kuelewa kwa namna gani wazalishaji wa soya wanaweza kutuma ndege za kunyunyiza dawa ya sumu dhidi ya wenyeji, jambo ambalo limethibitishwa na Wizara ya Afya, ambayo sasa inajaribu kuwasaidia wenyeje walioathiriwa na sumu hiyo. </div>
<p>López Barrios <a href="http://lopezbarrios.blogspot.com/2009/11/matte-larangeira-la-industrial.html">pia anaona aibu kwa hitoria ya vitendo vibaya vinavyofanywa na jamii za wenyeji huko Paraguay [es]. </a>Kama mtoto wa wahamiaji kwenye nchi hii, anaandakika kwamba matukio hayo &#8220;yanamfanya atamani kurejea Ulaya&#8230; lakini kwa kweli &#8230;angependa wanyonyaji hao waondoke zao.&#8221;</p>
<blockquote><p>
Ensañarse con un pueblo indígena que tiene más de 38 siglos de existencia en sus propios y verdaderos territorios, no me parece apropiado…. Si no respetamos a nuestros mayores nuestros días se acortaran sobre la tierra y si anteponemos la avaricia a cualquier otra virtud caeremos sin remedio…..</p></blockquote>
<div class="translation">Kuwachukia wenyeji ambao wameishi hapo kwa zaidi ya karne 38 kwenye ardhi yao wenyewe, si jambo la kukubalika kwangu &#8230;. Kama hatuwaheshimu wakubwa zetu, basi siku zetu duniani zitafupishwa, na kama choyo (tamaa) ikiwekwa mbele ya kitu chochote, ipo siku tutaangamia &#8230;. </div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/paraguay-wenyeji-wanyunyiziwa-dawa-za-kuua-wadudu-kwa-ndege/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Venezuela: Kukutana na kazi za msanii Jesus Soto</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/venezuela-kukutana-na-kazi-za-msanii-jesus-soto/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/venezuela-kukutana-na-kazi-za-msanii-jesus-soto/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 13 Nov 2009 13:14:48 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Venezuela]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=617</guid>
		<description><![CDATA[Kazi za msanii wa Kivenezuela Marehemu Jesus Soto zinapaswa kuguswa na kujizamisha ndani yake ili kuzielewa. Wachache waliwahi kutembelea kazi zake kwenye makumbusho wameandika uzoefu wao. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/laura-vidal/">Laura Vidal</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/venezuela-interacting-with-the-works-of-artist-jesus-soto/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kazi za msanii wa Kivenezuela <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jesus_Soto">Jesús Soto (1923 - 2005)</a> ni kati ya kazi maarufu zaidi zinazoonyesha sura ya sanaa ya kisasa ya Amerika ya Kati (Latin), anafahamika zaidi kwa kazi za kutumia mikono yake mwenyewe.  Soto alizaliwa huko Ciudad Bolivar, Venezuela, ambako alianza kufanya kazi kama mchoraji wa mabango ya sinema. Alipata elimu yake katika miji ya Caracas na Maracaibo, lakini ilikuwa ni huko Paris ambako kazi yake ilipata mwelekeo wenye nguvu zaidi. Kazi zake maarufu ni zile “zinazoingiliana” ambazo ni vinyago vyenye muonekano wa mistari ya miraba, mirija miembamba inayoning’inia, yenye rangi zinazong’aa zilizotengenezwa na plastiki na ambayo watu huweza kupita katikati yake. </p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha ya mtoto kwenye maonyesho ya Soto iliyopigwa na Ale na imetumiwa chini ya  leseni ya Cretive Commons" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/kids.jpg" title="kids" width="400" height="268" /><p class="wp-caption-text">Picha ya mtoto kwenye maonyesho ya Soto iliyopigwa na Ale na imetumiwa chini ya  leseni ya Cretive Commons</p></div>
<p>Kwa mujibu wa wataalamu wa sanaa, sanaa ya Sato haijitengi na mtazamaji, ambaye ni mshiriki hai wa kazi ya msanii. Mauzauza na hisia vinakamilishwa na mtazamo wa akili kama matokeo ya kuona, kugusa na kuwa sehemu ya kazi yenyewe. Wanablogu wa Venezuela na jamii ya mtandaoni kwa ujumla, wanasherehekea sanaa yake kwa kupitia makala, mapitio, na video zilizochukuliwa kwenye  makumbusho na ndani ya kazi zenyewe, wakati wakieleza maana ya kazi za Sato katika utamaduni wao, sura ya nchi na maisha yao ya kila  siku. </p>
<p>Katika blogu yake, <em><a href="http://literanova.eduardocasanova.com/index.php/2009/09/24/jesus-soto-y-el-cinetismo-conceptos-e-hi">Literanova[es]</a></em>, Eduardo Casanova anaingia ndani zaidi kidogo kuhusu maisha ya Sato na kutupa mwanga wa histroia ya mji alikozaliwa: </p>
<blockquote><p>Jesús Rafael Soto nació en Venezuela, en 1923, en una población cargada de historia: Ciudad Bolívar, donde se instituyó la prensa escrita y se fraguó la creación de la llamada Gran Colombia (…) Era una población aislada, sin museos ni actividades del arte. El mismo ha dicho que aprendió solo el arte de la pintura. Deja su ciudad natal y viaja a Maracaibo, en el occidente del país, para encargarse de la dirección de una escuela de artes plásticas. En 1950 se va a París y allí comienza su carrera de artista creador de nuevas formas.</p></blockquote>
<div class="translation">Jesus Soto alizaliwa mwaka 1923 katika mji wenye historia kubwa; Ciudad Bolivar, ambako vyombo vya habari vilitoa taarifa rasmi kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi na ndipo  wazo la kuundwa kwa kwa Colombia Kuu lilipoanzishwa. Ilikuwa ni eneo la watu waliotengwa, wasio na makumbusho ya kihistoria wala shughuli za kisanii. Alizoea kusema kwamba alijifunza namna ya kuchora yeye mwenyewe. Aliondoka kwenye mji huo alikozaliwa na kwenda Maracaibo, magharibi ya nchi kuwa Mkurugenzi wa shule ya sanaa. Mwaka 1950, Soto alienda Paris na huko ndiko alikoanza ubunifu wa mtindo mpya (wa sanaa).</div>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha ya tufe la Soto katika Cracas ya Gillermo Ramos Flamerich chini ya leseni huru ya GNU. " src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/sotosphere.jpg" title="sotosphere" width="400" height="379" /><p class="wp-caption-text">Picha ya tufe la Soto katika Cracas ya Gillermo Ramos Flamerich chini ya leseni huru ya GNU. </p></div>
<p>Chaneli ya YouTube ya  <a href="http://www.youtube.com/watch?v=kqetiW8MClE&#038;feature=fvw">VenezuelaTuya</a> inatoa mfano wa uzoefu wa kutembea kwenye mchoro wa maonyesho kwenye Makumbusho ya  Jesús Soto, mjini Ciudad Bolívar:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/kqetiW8MClE&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/kqetiW8MClE&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Blogu ya <em><a href="http://talentovenezolano.blogspot.com/2007/01/jess-soto-venezolano-universal.html">Talento Venezolano [es]</a></em> pia inatoa nafasi maalumu kwa ajili ya kuzungumzia yanayohusu wasaniii na ubunifu wao maarufu: </p>
<blockquote><p>En 1967 creó la primera obra de la serie Penetrables, la cual consiste en instalaciones de tubos de plástico a través de los cuales el espectador se siente en un espacio mágico. Ambas obras que pudieron admirarse en el Museo de Arte Moderno, en el Grand Palais y el Centro Pompidou de París.</p></blockquote>
<div class="translation">
Mwaka 1967 (Soto) alitengeneza moja ya kazi zake za kwanza “zinazoingiliana” ambazo ni mirija ya plastiki ambapo mtazamaji anaweza kujisikia kwenye eneo  la kimazingaombwe. Kazi zote zilizonyeshwa kwenye Makumbusho ya sanaa ya Kisasa, huko Paris kwenye Grand Palais na Kituo cha Pompidou. </div>
<p>You Tube vilevile imekuwa njia ya watu kuonyesha mawasiliano na hisia zao wakati wanashiriki kazi za Soto kwa vitendo. Hasa watoto, wamekuwa na muelekeo maalum wa uzoefu ndani ya kazi za msanii, ambao umeonyeshwa na kushirikishwa kwenye viideo hizi: </p>
<p>Mtumiaji wa YouTube elizaul1:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/kWZd2DQ1ASc&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/kWZd2DQ1ASc&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Na mtumiaji wa YouTube skaracas:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/OlacQOCh0H4&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/OlacQOCh0H4&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kwenye <a href="http://www.jr-soto.com/fset_menuprincipal_fr.html">tovuti</a> ya msanii kuna kurasa za picha na habari zaidi.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/venezuela-kukutana-na-kazi-za-msanii-jesus-soto/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cuba-ukweli-wa-sanchez-kutiwa-mbaroni-waibuka/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cuba-ukweli-wa-sanchez-kutiwa-mbaroni-waibuka/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 08 Nov 2009 11:22:03 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Cuba]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[LANGUAGES]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=584</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naGeorgia Popplewell  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari na katika ulimwwengu wa blogu [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/georgia-popplewell/">Georgia Popplewell</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/07/cuba-details-of-the-sanchez-detention-emerge/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika <a href="http://www.reuters.com/article/mediaNews/idUSN0620636520091107">vyombo vikubwa vya habari</a> na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani <a href="http://www.desdecuba.com/generaciony/?p=2468">ameandika</a> (es) kuhusu tukio hilo kwenye blogu yake, Generación Y, na blogu za Kiingereza kama vile <a href="http://babalublog.com/2009/11/breaking-news-yoani-sanchez-arrested-in-cuba/">Babalú Blog</a>, <a href="http://repeatingislands.com/2009/11/07/yoani-sanchez-detained-briefly/">Repeating Islands</a> pamoja na <a href="http://marcmasferrer.typepad.com/uncommon_sense/2009/11/cuban-bloggers-arrested.html">Uncommon Sense</a> zinafuatilia habari hiyo. <a href="http://www.youtube.com/watch?v=gKx0KJhiNL4">Mahojiano ya sauti</a> (es) na Sanches kuhusu tukio hilo yamepandishwa kwenye YouTube.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cuba-ukweli-wa-sanchez-kutiwa-mbaroni-waibuka/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Yoani Sanchez Pamoja na Wanablogu Wengine wa Cuba Wakamatwa na Kupigwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/yoani-sanchez-pampja-na-wanablogu-wengine-wa-cuba-wakamatwa-na-kupigwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/yoani-sanchez-pampja-na-wanablogu-wengine-wa-cuba-wakamatwa-na-kupigwa/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 08 Nov 2009 11:15:24 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Cuba]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[LANGUAGES]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=579</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naGeorgia Popplewell  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú iliweka kiungo kuelekea makala iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/georgia-popplewell/">Georgia Popplewell</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/07/yoani-sanchez-other-cuban-bloggers-detained-beaten/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Jioni ya tarehe 6 Novemba, blogu ya Babalú <a href="http://babalublog.com/2009/11/breaking-news-yoani-sanchez-arrested-in-cuba/">iliweka kiungo</a> kuelekea <a href="http://www.penultimosdias.com/2009/11/06/la-seguridad-de-estado-detiene-a-yoani-sanchez-y-otros-blogueros-cuando-iban-a-participar-en-una-manifestacion-performance-en-la-calle-23/">makala</a> iliyoandikwa na Penultimos Dias (es) ilitoa taarifa kuwa baadhi ya wanablogu mashuhuri wa Cuba, wakiwemo Yoaní Sánchez na mchangiaji wa Global Voices Claudia Cadelo, walitiwa mbaroni na majeshi ya usalama. Habari mpya kutoka kwa Penultimos Días zinataarifu kuwa Sanchez na Orlando Luis Pardo “walipigwa vibaya na kutukanwa”.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/yoani-sanchez-pampja-na-wanablogu-wengine-wa-cuba-wakamatwa-na-kupigwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Bolivia: Uhaba wa Maji Kwa Sababu ya Theluji Inayoyeyuka</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/bolivia-uhaba-wa-maji-kwa-sababu-ya-theluji-inayoyeyuka/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/bolivia-uhaba-wa-maji-kwa-sababu-ya-theluji-inayoyeyuka/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 07 Nov 2009 12:55:48 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Bolivia]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=572</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naEduardo Avila  &#183; Imetafsiriwa na Deogratias Simba &#183;  Angalia ujumbe mama 
Safu ya milima ya Chacaltaya ina baadhi ya vilele ambavyo ni alama zenye maana katika safu ya milima Andes iliyopo Bolivia. Kwa kuwa ilikuwa ni sehemu moja pekee ambapo mchezo wa kuteleza barafuni uliweza kufanyika katika nchi hii ya milimamilima, [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/eduardo-avila/">Eduardo Avila</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/02/bolivia-water-shortages-due-to-melting-glaciers/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Chacaltaya">Safu ya milima ya Chacaltaya</a> ina baadhi ya vilele ambavyo ni alama zenye maana katika safu ya milima Andes iliyopo Bolivia. Kwa kuwa ilikuwa ni sehemu moja pekee ambapo mchezo wa kuteleza barafuni uliweza kufanyika katika nchi hii ya milimamilima, milima hii ni maarufu sana kwa wale walio kwenye Idara ya La Paz, na pia kwa wageni wapenda kuvumbua mambo mapya. Ni katika milima hiyohiyo ambapo zilifanyika mechi za soka za hisani ambazo kwazo Rais Evo Morales alishiriki ili kuthibitisha kwamba michezo inaweza kuchezwa katika maeneo ya ukanda wa juu.</p>
<p>Hata hivyo, theluji ya Chacaltaya imeanza kupungua kwa kasi inayotisha na kali sana. Athari ya mabadiliko ya hali ya hewa kwa barafu iliyoko kwenye mlima huu na mingine iliyo katika eneo hili zimekuwa zikichunguzwa na Profesa wa Chuo Kikuu cha San Andrés, Edson Ramírez, <a href="http://revistavirtual.redesma.org/vol5/articulo6.php?id=c1">ambaye anahitimisha kwa kusema kwamba kuna uhusiano wa moja kwa moja</a> kati ya kuongezeka kwa kiwango cha joto na kutokweka kwa theluji au barafu hiyo.</p>
<p>Ramírez na timu yake wamekuwa pia wakitafiti barafu iliyoko kwenye  mlima mwingine ambao nao umekuwa ukipatwa na athari zinazofanana na huo mwingine na madhara ya mwenendo huo kwa jamii inayoishi maeneo ya jirani. barafu iliyoko kwenye  mlima unaoitwa Tuni Condoriri glacier unayeyuka katika kasi kubwa, hivyo kuwaathiri wapenzi wa alpine, lakini pia hali hiyo inaathiri jamii za wahamiaji walio katika hatari ambao huitegemea ili kujipatia maji ya kunywa na kwa ajili ya shughuli za kilimo. </p>
<p>Tenki la kuhifadhia maji yanayotoka <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/americas/6496429.stm">kwenye barafu iliyoko kwenye  mlima huo hutoa kiasi cha 80% cha maji ya kunywa kwa jiji la El Alto na vitongoji vyake vya La Paz</a>. Kwa mujibu wa sensa ya hivi karibuni, <a href="http://es.wikipedia.org/wiki/El_Alto">El Alto ina jumla ya watu wapatao 827,000 [es]</a>,ambapo idadi hiyo inakua kwa 5.1% kila mwaka. Kwa mujibu wa mwandishi wa habari na mwanablogu Mónica Oblitas, <a href="http://monioblitas.blogspot.com/2008/06/glaciar-nuestro-tesoro-se-derrite.html">kiwango hiki ni zaidi ya mara mbili ya wastani wa taifa [es]</a>. Wataalamu wanabashiri uhaba wa maji na kulipia maji, ambapo <a href="http://observadorglobal.com/bolivia-un-futuro-sin-agua-informe-especial-n45.html">watu wengine wanabashiri kwamba suala la mgao wa maji limekaribia [es]</a>. <em>Timu kutoka Observador Global [es]</em> (Wafuatiliaji wa Ulimwengu) <a href="http://observadorglobal.com/bolivia-un-futuro-sin-agua-informe-especial-n45.html">waliandaa makala ya video yenye sehemu sita kuonyesha madhara ya upungufu wa maji katika eneo hilo</a>.</p>
<p>Jiji hilo ni <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/El_Alto">makazi ya wahamiaji kutoka jamii za wenyeji wa Aymara  katika Altiplano ya Bolivia</a>, ambao huhamia katika jiji la El Alto, mara nyingi wakiwa katika hali ya umaskini uliokithiri. Mwanablogu wa Ki-Bolivia, Cristina Quisbert anayeandika katika blogu ya <em>Indigenous Bolivia</em> <a href="http://boliviaon.blogspot.com/2009/09/our-mountains-melt.html">anaelezea hali inayowakabili wakaazi wengi hususani kuhusu maji salama ya kunywa</a>:</p>
<blockquote><p>Kuna mambo mengine yanayochangia katika ugumu wa kupata maji. Watu wengi wanafika kutoka vijijini kuingia katika jiji la El Alto na kuanzisha makazi pale wanapoweza kufanya hivyo. Kwa sababu ya ukosefu wa fedha, wanaishi popote pale mara nyingi ambapo hapana maji ya kunywa wala hakuna mfumo wa maji taka. Baadhi yao huchimba visima vifupi vya hadi mita tatu hivi hadi wapate maji. Kwenye mwezi Novemba hivi, mvua za mwanzo huanza kunyesha, hivyo kufanya uwezekano wa kupata maji kwa majirani hawa. Mwishowe, uhaba wa maji huchangia katika kuongeza umaskini na vyote hivyo husababisha maradhi.</p>
<p>Kuna hali fulani ya mambo mbalimbali na tofauti kuwa pamoja . Mimi napata maji nyumbani lakini jirani zangu hawapati. Hili ni jambo zito kwa familia. Kwa upande wangu, ninawagawia maji familia nyingine. Basilio naJuana wana watoto wanne. Wanaishi katika nyumba ya kupanga. Nyumba wanamoishi haina maji yanayofaa kunywa. Kila wanapoyahitaji, basi hawana budi kutumia mpira ili kupata maji kutoka nyumbani kwangu na mwisho wa mwezi basi tunagawana gharama kadiri ya ankra. </p></blockquote>
<p>Hata hivyo, siyo tu kwamba Tuni Condoriri hutoa maji ya kunywa kwa ajili ya jiji hilo tu, lakini pia hutoa maji kwa ajili ya shughuli za kilimo kwenye safu za Altiplano. Endapo uendelezaji wa shughuli za kilimo utapungua kwa sababu ya uhaba wa maji, watu wengi zaidi kutoka maeneo ya vijijini watatiririka kwenda El Alto kujitafutia maisha, ambapo watakumbana na tatizo lile lile la uhaba wa maji na papo hapo wakiongeza mahitaji ya maji. </p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Wanaharakati wa 350.org wakikwea kwenye mlima barafu Chacaltaya huko Bolivia kufanya maandalizi ya tukio kubwa mnamo tarehe 24 Oktoba. Picha imetumika chini ya leseni ya haki miliki huru." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/chacaltaya.jpg" title="chacaltaya" width="400" height="268" /><p class="wp-caption-text">Wanaharakati wa 350.org wakikwea kwenye &#39;mlima&#39; barafu Chacaltaya huko Bolivia kufanya maandalizi ya tukio kubwa mnamo tarehe 24 Oktoba. Picha imetumika chini ya leseni ya haki miliki huru.</p></div>
<p>Ni sura inayopewa kipa umbele ya barafu iliyoko kwenye mlima wa Chacaltaya ndiyo inayovuta usikivu wa ofisa wa serikali za mitaa na vikundi vingine vya wanaharakati ili kutazama tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa katika ukanda wa Bolivia. <a href="http://www.facebook.com/event.php?eid=173999981920&#038;ref=nf">Tukio lililotokea mahali hapo siku za hivi karibuni lililohusiana na kampeni ya 350.org lilitangazwa katika Facebook [es]</a>, likiwaalika raia wa Bolivia kutembelea &#8216;mlima&#39; barafu wa Chacaltaya kujionea wenyewe madhara yanayofanyika. </p>
<p>Hatimaye, Oblitas <a href="http://monioblitas.blogspot.com/2008/06/glaciar-nuestro-tesoro-se-derrite.html">anahitimisha kwa swali hili lifuatalo [es]</a>:</p>
<blockquote><p>Chacaltaya ya no está y pronto dejarán de existir otros glaciares, ¿está el país preparado para esas pérdidas?, ¿somos conscientes de la importancia de tomar un rol activo e inmediato contra el calentamiento? Para muchos, el cambio climático no es un fenómeno global y no creen sentirse afectados, pero lo cierto es que absolutamente todos estamos en riesgo y no todos podemos enfrentarlo en las mismas condiciones. La lucha continúa, aunque ya sea tarde para lugares como Chacaltaya.</p></blockquote>
<div class="translation">&#8216;Mlima&#39; barafu wa Chacaltaya haupo tena, vilevile hivi karibuni &#8216;milima&#39; barafu mingine nayo itatoweka. Je, nchi iko tayari kupata hasara hii? Je, tunatambua umuhimu wa kuchukua wajibu wa haraka wa kushiriki kukabili kuongezeka kwa joto duniani? Kwa walio wengi, mabadiliko ya hali ya hewa si tatizo la kiulimwengu na hawajihisi kuathiriwa, kila mmoja yuko kwenye hatari ingawa si kila mmoja anaweza kukabiliana na hatari hiyo kwa namna moja. Mapambano yanaendelea, hata kama tayari tumechelewa katika maeneo kama Chacaltaya.</div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/bolivia-uhaba-wa-maji-kwa-sababu-ya-theluji-inayoyeyuka/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Amerika ya Kati: Kasi Kubwa ya Ueneaji wa Jangwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:24:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Chile]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=556</guid>
		<description><![CDATA[Ueneaji wa jangwa unasambaa kimyakimya lakini kwa kasi kubwa mahali pengi duniani na Amerika ya Kati haijaweza kukwepa hali hii iliyo na athari mbaya za kutisha. Wakati ambapo majangwa ni maumbo ya asili, ueneaji wa jangwa ni mchakato wa kuharibika kwa nyanda za ardhi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu unaofanywa na binadamu. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/belen-bogado/">Belen Bogado</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/  '>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Pengine maneno ueneaji jangwa yanaweza kusikika sawa na jangwa, lakini kuna tofauti kubwa ya msingi kati ya maneno hayo: wakati ambapo majangwa ni moja kati ya maumbo mazuri ya kipekee ya asili, ueneaji jangwa ni mchakato wa kuharibika ambako kanda za ardhi hupitia baada ya kuathiriwa vibaya na mabadiliko ya hali ya hewa, shughuli za binadamu na majanga ya asili mpaka hatimaye zinageuka na kuwa majangwa.</p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/desertification.jpg" title="desertification" width="400" height="258" /><p class="wp-caption-text">Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons.</p></div>
<p>Ingawa athari ya mabadiliko ya hali ya hewa katika ueneaji jangwa bado haijaeleweka vema, yaani kwa mujibu wa GreenFacts, inafahamika kwamba <a href="http://www.greenfacts.org/en/desertification/index.htm">viwango vya juu vya joto vinavyotokana na kuongezeka kwa viwango vya dioksidii ya kaboni kunaweza kuwa na athari mbaya kutokana na kuongezeka kwa upotevu wa maji kutoka ardhini na kupungua kwa viwango vya mvua katika maeneo yenye ukame</a>. Wakati huohuo ueneaji jangwa nao huchangia katika mabadiliko ya hali ya hewa kwa kuruhusu kaboni iliyohifadhiwa kwenye mimea ya maeneo yenye ukame na udongo kurushwa kwenye anga.</p>
<p>Ueneaji jangwa unazidi kuwa na athari mahali pote duniani. Kwa sasa hivi ueneaji huo unaathiri mavuno, unasababisha kupanda kwa bei za vyakula vilivyopo, na katika baadhi ya maeneo, hata wanyama wanakufa. Watu wanalazimika kuhamia maeneo mengine ya mbali na nyumbani kwao, kama anavyoeleza mwanablogu Miguel Angel Alvarado anayetokea El Salvador <a href="http://www.ecoportal.net/content/view/full/61308/">kuhusu mpango wa kuhamisha makazi ya rais kwa sababu ya ueneaji jangwa[es]</a>:</p>
<blockquote><p>El traslado de casa presidencial, del Barrio san Jacinto al local en donde estaba el Ministerio de Relaciones exteriores, según informes extrajudiciales, obedece a la prevención del ejecutivo ante un posible hundimiento del suelo generado por cárcavas en este sector.</p></blockquote>
<div class="translation">Kwa mujibu wa nyaraka zisizo rasmi kisheria, kuhamishwa kwa makazi ya rais kutoka maeneo ya San Jacinto kwenda ilipokuwa Wizara ya Mambo ya Nje hapo awali, ilikuwa ni hatua ya kujihami iliyofanywa na mhimili wa dola ili kuepuka kutitia kwa ardhi kutokana na makorongo yaliyotokea pale.</div>
<p>Bara lililoathiriwa zaidi ni Afrika, na jambo hili linaweza kuonekana zaidi nchini Kenya, ambapo moja ya sekta zinazoweza kupata athari kubwa za ueneaji jangwa na ukame ni wasichana. Pale maji yaliyohifadhiwa kwenye matenki yalipokuwa yametumika yote katika Nyumba ya Watoto Yatima ya Dago Dala Hera huko Magharibi mwa Kenya, akina mama wanaojitolea na watoto wanalazimika kuteka maji yasiyo salama kutoka katika mto ulio karibu kwa ajili ya kupikia na kunywa. <a href="http://us.oneworld.net/article/367320-africa-famine-deepens-drought-worst-decades">“Kwenda mtoni kuteka maji peke yao nyakati za jioni kunawaweka wasichana katika hatari ya kukumbana na wanaume wanaoweza kuwanyanyasa kingono,”</a> alisema Edwin Odoyo, ambaye mama yake anayeitwa Pamela ndiye aliyeanzisha makazi hayo ya watoto yatima.</p>
<p>Ingawa ueneaji jangwa una athari kubwa zaidi barani Afrika, hali ya mazingira ya Amerika ya Kati nayo inapitia mabadiliko makubwa, kama ilivyojadiliwa siku za karibuni katika Mkutano wa Tisa wa Kongamano kuelekea Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Kukabili Ueneaji Jangwa uliofanyika jijini Buenos Aires, Ajentina. Mtaalamu wa Kiitaliano, Massimo Candelori, aliyekuwa mwakilishi wa Mkataba wa Kukabili Uenejaji Jangwa, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=esp&#038;idnews=3422">alisema katika mahojiano na  Tierramerica</a> kwamba hali ilivyo Amerika ya Kati inatisha kwa kuzingatia kwamba hakuna taarifa za kutosha kuhusu kiwango cha ueneaji jangwa katika eneo hilo. “Hatuna takwimu za sasa hivi. Moja ya lengo lililojadiliwa katika Mkutano wa Tisa lilikuwa ni kupata viashirio vinavyoturuhusu kuelewa vizuri zaidi hali halisi &#8230; takwimu tulizonazo mpaka sasa ni zile za miaka kumi iliyopita,” alisema Candelori.</p>
<p>Katika nchi za Amerika ya Kati ambapo kilimo na ufugaji ni moja ya sekta kuu za uchumi, ueneaji jangwa unaweza kuwa wa kimyakimya, lakini wenye madhara makubwa kama mnyama hatari mwindaji. Walau <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">asilimia 25 ya sehemu ya eneo zima</a> tayari imeharibiwa na wakati huohuo watu wanazidi kuwa na wasiwasi juu ya suala hili, kama inavyojionyesha katika blogu mbalimbali. </p>
<p><em>Eco Briefings [pt]</em>, blogu ya KiBrazili, inaonyesha kwamba <a href="http://ecobriefings.com/2009/10/05/desertificao/">WaBrazili waishio Kaskazini Mashariki mwa nchi wanashuhudia ueneaji wa kasi sana wa jangwa[pt]</a>:</p>
<blockquote><p>Mais um alerta está ligado. Temos pouco tempo para corrigir as coisas. (…)</p>
<p>No Brasil a desertificação tem avançado na caatinga, e zonas do polígono da seca no Nordeste e Norte de Minas Gerais, e também em Estados que antes não tinham áreas secas ou desertificadas como o Rio Grande do Sul. O Rio Amazonas viveu já uma grande seca a pouco tempo, grande com mortandade de peixes.</p></blockquote>
<div class="translation">Kiitia hatari kingine kinanguruma. Tuna muda mfupi sana wa kurekebisha mambo (…)</p>
<p>Nchini Brazili, ueneaji jangwa umeongezeka sana katika Caatinga, katika ukanda wa maeneo kame Kaskazini Mashariki na Kaskazini mwa jimbo la Minas Gerais, na vilevile katika majimbo ambayo hayakukumbwa na ukame wala ueneaji jangwa hapo kabla kama vile Rio Grande do Sul. Mto Amazon umepitia ukame mkubwa kabisa katika kipindi kifupi kilichopita, jambo lililosababisha samaki kufa kwa idadi kubwa.</p></div>
<p>Ajentina nayo ina maeneo kadhaa yaliyoathiriwa. Katika mkoa wa Valles Aridos, Kaskazini Mashariki, ambapo shughuli kuu ya kiuchumi ni ufugaji kondoo, inakadiriwa kwamba <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/www.inta.gov.ar/salta/info/documentos/Desertificaci%C3%B3n.pdf">katika miaka 100 iliyopita, walau watu 180,000 walilazimika kuhama. [es] (katika mfumo wa .pdf)</a>. Kusini mwa nchi ya Ajentina nako hakujapona na ueneaji jangwa. Mwanablogu Ailen Romero, anaandika maoni katika blogu inayoitwa <em>Geoperspectivas [es]</em> <a href="http://geoperspectivas.blogspot.com/2009/06/dia-mundial-de-la-desertificacion-2009.html">kwamba katika mkoa wa Patagonia, juhudi za serikali za kukabili ueneaji jangwa bado hazitoshi</a>:</p>
<blockquote><p>En la Patagonia, la amplitud del problema es de tal magnitud que ha comenzado a adquirir estado público. Pocos ignoran el tema, pero pocos tienen la posibilidad de actuar de alguna forma o con el conocimiento para hacerlo. El problema de la desertificación en el caso de la Patagonia supera a los planes que se han elaborado para combatirlo. Es por eso que no deben ahorrarse esfuerzos, ni limitar la imaginación de soluciones alternativas.”Si la geografía es la manifestación de la sociedad en el espacio físico, un espacio físico deteriorado refleja una sociedad deteriorada” afirman del Valle y Coronato(investigadores del Centro Nacional Patagónico)</p></blockquote>
<div class="translation">Katika Patagonia, ukali wa tatizo ni mkubwa kiasi kwamba umma wote umetambua tatizo hilo. Ni watu wachache tu ndiyo wanaolipuuza na ni wachache tu walio na nafasi au maarifa ya kufanya juhudi kulikabili. Tatizo la ueneaji jangwa huko Patagonia unazidi mipango iliyokwishaainishwa kulikabili. Ndiyo sababu kila juhudi haina budi kufanywa, wala kusiwe na mipaka katika kufikiria ufumbuzi mwingine wowote. ‘Kama Jiografia ni kielelezo cha jamii katika nafasi halisia, kuharibika kwa nafasi halisia huko kunaakisi kuharibika kwa jamii, wanasema  Valle na Coronato (watafiti kutoka katika Kituo cha Taifa cha Patagonia).</div>
<p>Huko Chile, ambapo <a href="http://www.conaf.cl/?seccion_id=8ad00d8dd61d22aa152575a1e5c08e58&#038;unidad=0&#038;PHPSESSID=db19e79870c9e01418e62b8576a26daf">takribani asilimia 62 ya eneo la taifa tayari imeathiriwa na ueneaji jangwa [es]</a>, mwanablogu Alfredo Erlwein alieleza wasiwasi kupitia katika blogu inayoitwa <em>El Ciudadano [es]</em>(Raia) kuhusu jinsi gani watu <a href="http://www.elciudadano.cl/2009/03/26/desertificacion-y-sequia-el-gran-problema-ambiental-de-chile-y-el-mundo/">wasiyo na maarifa ya kutosha kuhusu ueneaji jangwa</a>.</p>
<blockquote><p>
Efectivamente la desertificación es el problema ambiental más grave de Chile y muy poco conocido. Existen grandes zonas, como en la costa de la octava región, donde la erosión severa supera el 50% de la superficie: esto es que literalmente más de la mitad de los suelos se ha perdido por completo. En esas zonas se encuentran cárcavas de más de 50 metros de profundidad. Una tasa normal de formación de suelo puede ser de 0.2 cm por año, lo que evidencia la gravedad del asunto.</p></blockquote>
<div class="translation">Ueneaji jangwa kwa hakika ni tatizo kubwa kabisa lakini lisilofahamika miongoni mwa matatizo ya kimazingira nchini Chile. Kuna maeneo makubwa, kama vile pwani ya Nane ya Mkoa, ambapo mmomonyoko mkali wa udongo unazidi asilimia 50 ya ardhi: hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya ardhi imepotea, huo ndiyo ukweli. Katika maeneo hayo kuna makorongo yenye kina cha mpaka mita 50. Kiwango cha kawaida cha utengenezekaji ardhi ni kama sm 0.2 kwa mwaka, huo ndiyo uthibitisho wa ukali wa tatizo lililopo.</div>
<p>Kwa mujibu wa mtaalamu Mwitaliano Candelori, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">kutumia udongo katika soko la Kaboni kutasaidia kupambana na ueneaji jangwa</a>; jambo hili pengine litaamuliwa katika Kongamano litakalofanyika jijini Copenhagen. Tayari kongamano hilo limeanza kuhesabiwa siku na ulimwengu unalisubiri kwa hamu.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ujauzito na Magereza: Afya na Haki za Wanawake Magerezani</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 05 Nov 2009 13:24:11 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[Ecuador]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Laos]]></category>
		<category><![CDATA[Peru]]></category>
		<category><![CDATA[Photography]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Spain]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=493</guid>
		<description><![CDATA[Mapambano bado yanaendelea kuhakikisha haki za binadamu kwa wanawake wajawazito duniani pote, ni inaelekea kwamba katika mchakato huo, wanawake waliopo magerezani wanasahauliwa. Je ni hatua zipi zilizochukuliwa kuhakikisha kuwa nao wanaangaliwa kwa utu, kwa kuzingatia uhai wanaoubeba.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/24/pregnancy-and-prisons-womens-health-and-rights-behind-bars/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/2044749780_4ade9e2e3f-300x225.jpg" title="2044749780_4ade9e2e3f" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><strong>Je, wanawake wote wajawazito wanastahili haki sawa za binadamu, au wanawake wajawazito walio jela huziacha haki hizo? </strong></p>
<p>Kuna maswali machache yanayokuja akilini kuhusu haki ya mwanamke mjamzito kuishi na kumlea mwanae anapokuwa kapatikana na hatia kwa kosa la jinai la namna fulani:<br />
•	Inakuwaje kwao wanapokuwa wajawazito na kupata mtoto wakiwa gerezani?<br />
•	Je, wanapaswa kuwa kipaumbele wakati kuna wanawake wengine nje ya vyuo vya mafunzo bila msaada wa kitabibu?<br />
•	Je, ujauzito unapaswa kuwa juu ya hali nyinginezo za kisheria kumhakikishia mwanamke mjamzito haki zake za kibinadamu? </p>
<p><strong>Marekani: wanawake walio kwenye uchungu wa kuzaa hawatafungwa tena minyororo.  </strong></p>
<p>Je unaweza kufikira mwanamke akijifungua huku mikono yake ikiwa kwenye pingu na miguu yake ikiwa imefungwa na minyororo kwenye kitanda? <a href="http://www.rhrealitycheck.org/user/malika-sadaa-saar">Malika Saada Saar</a>, mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa <a href="http://www.rebeccaproject.org/">Mradi wa Rabecca kwa Haki za Binadamu</a>, <a href="http://www.rhrealitycheck.org/blog/2009/10/06/in-labor-and-in-chains">anatuelezea</a> kuhusu kitendo hiki ambacho bado kinatokea nchini Marekani, ambapo wanawake wajazito wanaotumikia kifungo wamekuwa wakifungwa minyororo wakati wa uchungu na kujifungua na kuwa hiki ni kitendo kilichozoeleka katika baadhi ya magereza (ya kurekebishia tabia), ingawa ni hatari kwa afya ya mama na mtoto. Ifuatayo ni video ya mahojiano yaliyoambatanishwa kwenye makala iliyoandikwa kwa ajili ya mradi wa <em>RH Reality Check</em>, jamii ya mtandaoni kuhusu afya na haki ya uzazi na jinsia inatupa taarifa na uchambuzi kwa afya ya uzazi:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
<strong><br />
Kitu gani hutokea kwa mtoto mchanga wa wa mfungwa baada ya kuzaliwa?</strong></p>
<p>Nchi mbalimbali zina kanuni tofauti kuhusiana na watoto magerezani. Kwa mfano, nchini Argentina, kwa mujibu wa <em>Ajintem</em>, chombo cha mawasiliano cha taarifa za uhamamiaji,  <a href="http://portal.ajintem.com/archivo/80-argentina-prision-domiciliaria-para-embarazadas-y-madres.html">sheria ilipitishwa</a> mwaka uliopita ikifafanua kwamba wanawake wajawazito, wanawake wenye watoto wadogo chini ya miaka mitano na wale wenye watoto walemavu wangenufaika na mpango wa kutumikia kifungo chao makwao chini ya ulinzi wa nyumbani. Sheria hii ingewanufaisha si tu akina mama, ambao kwa kuwa gerezani wasingepata huduma za afya wakati wa ujauzito, lakini pia (ingemnufaisha) mtoto, ambaye angelelewa ama katika mazingira yasiyo salama yanayokosa uhuru na upungufu wa udhibiti wa afya na chakula, au wangelelewa mbali na mama, na hivyo kusababisha mlolongo wa matatizo mengine. Hata hivyo, ujumbe ni kwa ajili ya mahakimu kufuatilia kiini cha sheria na kutoa ruhusa hii kwa wanawake wale ambao hawahusishwi na mashitaka ya jinai ya matumizi ya nguvu, kuhakikisha kwamba idadi kubwa ya raia iliyobaki haiuchukulii ujauzito kama kadi ya kumtoa mtu jela bure.</p>
<p>Katika visiwa vya Canary, kwa mujibu wa blogu ya <em>Prisiones y penas</em>, ambayo huandika kuhusu habari zinazohusu jela na magereza, wanawake wanaruhusiwa <a href="http://prisionesypenas.blogspot.com/2009/09/detenidas-con-hijos-en-carceles.html">kuishi na watoto wao hadi umri wa miaka mitatu</a> ndani ya selo zao, lakini wakiwa pamoja na wafungwa wenzao, kitu ambacho sio mazingira mazuri sana kwako. Kwa hiyo, wanawake wajawazito au wanawake wenye watoto wenye umri wa chini ya miaka 3 huambiwa kuhusiana na kuingia kwenye magereza kuwa si vizuri kwa mtoto kukualia gerezani, na hupewa uchaguzi wa kumpeleka mtoto kwa wanafamilia wengine. Hali ni hii hii huko <a href="http://www.reuters.com/article/worldNews/idUSTRE5085ZV20090109">Peru</a> na <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">Urusi</a>. Nchini Marekani, kuna magereza mawili tu yenye kuruhusu jambo hili, huko New York na Nebraska, <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/e_moms.html">kama ilivyoonyeshwa na mpiga picha maarufu Jane Evelyn Atwood</a> kwenye insha ya picha zake tatu kwa ajili ya <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/"><em>Shirika la kimataifa la Amnesty International</em>, inayoitwa <em>Too Much Time</em></a>, ambapo alitembelea dazani nyingi za magereza kote duniani kurekodi na kuweka kumbukumbu za maisha ya wafungwa.</p>
<p>Kwa nini mfumo wa magereza nchini Marekani hauruhusu, kwa ujumla, wanawake wenye watoto kubaki nao? Atwood anaeleza kwamba kwa sababu ya mazingira ufungwa, hairuhusiwi. Kwenye <a href="http://prisonphotography.wordpress.com/2009/10/07/women-behind-bars-jane-evelyn-atwoods-too-much-time/"><em>blogu ya Prison Photography</em> wanaelezea madai haya</a>: </p>
<blockquote><p>Watoto hawahusishwi kwenye magereza yote isipokuwa mawili tu nchini Marekani. Tishio la usalama linatajwa kama sababu: mtoto ndani ya gereza ni dhaifu na atakuwa shabaha ya malengo maovu siku zote. Madai yanaonekana kuwa hayana maana kwa kiasi fulani kwa unapofananisha na mifumo ya adhabu kwa nchi nyinginezo.</p></blockquote>
<p>Insha ya Atwood kwenye wavuti ya <em>Amnesty International</em> inaonyesha mambo mawili, sehemu inayohusu taratibu za kujifungua huku umefungwa minyororo kama yalivyoelezwa kwenye <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/f_vanbab.html">Mtoto wa Vanessa</a> na pia inaonyesha jambo jingine kuhusu mfumo wa magereza na umama, kwa kutumia picha za wanawake wakati mpigapicha akisoma insha kuhusu uzoefu wake wa kutembelea magereza huku akipiga picha. </p>
<p><strong>Ujauzito kama zana ya mapatano? </strong></p>
<p>Kwa nini haki za wanawake wajawazito gerezani zinatatanisha? Katika  <em>Russia Today</em>, idhaa ya matangazo ya Kirusi, <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">mada hii inatajwa</a> panapojadiliwa suala la watoto kuzaliwa na kulelewa katika mfumo wa magereza wa Kirusi:</p>
<blockquote><p>Wenye kutilia mashaka (suala hili) wanadhani akina mama wengine hupata ujauzito kwa makusudi ili tu kurahisisha maisha huko gerezani. Ruhusa ya kwenda hospitali, halafu kuwa na ratiba iliyojaa muda mwingi na mwanao –ni afadhali kuliko kukaa kwenye seli ya magereza, wanadai. </p></blockquote>
<p>Na kuna wanawake ambao wanaona kwamba kuwa na mimba ni njia pekee ya kukwepa hukumu, kama ilivyotokea mwezi Juni, pale mwanamama wa Kiingereza aliwekwa ndani na kuhukumiwa kifo huko Laos kwa sababu ya kusafirisha madawa ya kulevya akapata ujauzito gerezani na akanusurika kunyongwa, kwa sababu serikali ya Laos isingemnyonga mwanamama mjamzito. <a href="http://www.dailyexpress.co.uk/posts/view/105278/No-firing-squad-for-girl-who-fell-pregnant-in-jail">Madai yaliyotolewa </a>kwa mujibu wa jarida la Kiingereza la <em>Daily Express</em>, ni kwamba alipata ujauzito kwa kupandikiziwa mbegu za kiume ‘ili kupata hukumu nyepesi zaidi” </p>
<p><strong>Kwa maneno yao: Wanawake wanaeleza kuhusu watoto wao na maisha ya gerezani</strong></p>
<p>Geraldin Rodríguez, Mwajentina aliye kwenye jela za Ecuador kwa sababu ya biashara ya madawa ya kulevya anamueleza <a href="http://marcosbrugiati.blogspot.com/2009/07/carcel-de-mujeres.html">Marcos Brugiati</a>, mwandishi mshiriki katika chapisho la mtandaoni linalohusiana na masuala ya sanaa liitwalo <em><a href="http://www.indexarte.com.ar/noticias/562/las-rejas-de-la-carcel-el-arte-de-la-espera.htm">Plastica-Argentina</a></em>, masimulizi kuhusu kuigiza na kufanya maonyesho ndani ya jela, kupata ujauzito gerezani na kumpata mwanae. Aliruhusiwa kuwa na mwanae, lakini akaamua kwamba mwanae anahitaji kukua akiwa mtu huru:</p>
<blockquote><p> “Decidí que salga para vivir, tenía miedo que sufra de grande los traumas que hoy tengo. Se lo llevó al año mi hermano quien se hice cargo con su esposa”.</p></blockquote>
<div class="translation">Niliamua aondoke ili aishi, nilikuwa na wasiwasi angeteswa na msongo wa mawazo nilionao leo. Baada ya mwaka kaka yangu alimchukua na anamtunza kwa kushirikiana wa mke wake. </div>
<p>Juvinete yuko kwenye <a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">gereza la Kihispania</a>, na alikuwa mjamzito wakati alipofungwa kwa kusafirisha madawa ya kulevya. Anasimulia habari zake kwenye gazeti la kanda huko Uhispania linaloitwa <em><a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">NorteCastilla</a></em>. Miaka mitatu baada ya kujifungua mwanae akiwa gerezani, mwanae ilibidi aondoke, na alipelekwa kwa familia ya kufikia. Juvinete humuona mwanae huyo wa kike kila baada ya siku 15 na kila miezi miwili hupata ruhusa ya wiki mbili kukaa na mwanae. Hata hivyo, mambo hayaonekani kuwa mazuri sana: kuna uwezekano kwamba Juvinete atapelekwa Brazil alikozaliwa, na anahofia matokeo ya mabadiliko haya kwa mwanae. Anao ushauri kwa mwanamke yeyote anayeamua kupata ujauzito akiwa jela:</p>
<blockquote><p>-Intento convencerlas para que no se queden en estado dentro porque ver a un niño privado de libertad es muy duro, es irresponsable. Ellos no tienen que pagar nuestros errores.</p></blockquote>
<div class="translation">
Ninajaribu kuwashawishi wasipate ujauzito wakiwa bado ndani kwa sababu kumuona mtoto akikosa uhuru wake ni vigumu sana, ni kutokuwajibika. (Watoto wanaozaliwa jela) wasilipie gharama ya makosa yetu</div>
<p>.  </p>
<p>Kwenye wavuti ya <em><a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">Woman and Prison</a></em>, iliyojikita katika kuyatazama maisha ya wanawake wakiwa kwenye mifumo ya magereza , <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">mfungwa Kebby Warner anaongelea ujauzito wake</a> mwenyewe alipokuwa akitumikia kifungo kwenye gereza la Kimarekani, na jinsi alivyotendewa wakati wa ujauzito wake, utungu na baadae, wakati alipokuja kunyang’anywa mwanae. Hapa ni muhtasari anapoandika kuhusu hatua za kujifungua: </p>
<blockquote><p>Wakati wa utungu, hakuna mtu anaruhusiwa kuwa kwenye chumba cha kujifungulia. Familia yangu wala haikujua kwamba nilikuwa ninajifungua au nimempata (mwanagu) mpaka nilipokuwa nimetoka hospitali. Wakati huo wa siku tatu baadhi ya walinzi walikuwa ndani ya chumba, lakini muda mwingi, wakati wauguzi walipowaomba kukaa nje ya mlango, walitii. Nimesikia simulizi za kutisha za wanawake wakifungwa kwa mnyororo kwenye kitanda cha uzazi. Ninashukuru kwa kutokukumbana na hali hiyo. Wauguzi wengi walinitendea kama binadamu badala ya mfungwa.</p></blockquote>
<p>Unaweza kusoma shuhuda zaidi kuhusu kukua na mzazi gerezani na madhara mbalimbali ambayo kufunga wanawake kunaweza kuyawasababisha kwa watoto wao <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/index.html">kwenye Wanawake na Magereza</a>.</p>
<p>Kwa hiyo unafikiriaje? Kwa wanawake wajawazito duniani kote kutokupata huduma za afya za namna yoyote, je jitihada zaidi zinahitajika kuwanufaisha wanawake walio gerezani? Je, kuna tofauti kati ya wanawake wanaotumikia kifungo kwenye magereza (ya mafunzo) na wale wanaoishi nje? Je, ni lazima kuwatendea tofauti?<br />
<em><br />
Picha iliyotumika kwenye makala hii ni “17 de noviembre” ya <a href="http://www.flickr.com/photos/daquellamanera/2044749780/">daquella manera</a>.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Mexico: Simulizi za Siri Kwenye Twita</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/mexico-simulizi-za-siri-kwenye-twita/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/mexico-simulizi-za-siri-kwenye-twita/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 25 Aug 2009 12:59:31 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Literature]]></category>
		<category><![CDATA[Mexico]]></category>
		<category><![CDATA[Software & Tools]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[TYPE]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=306</guid>
		<description><![CDATA[Rafa Saavedra ni mtaalamu wa utamaduni wa chini chini kutoka mji wa Tijuana, Maxico. Katika mahojiano, anaelezea kila kitu kinachohusu mradi wake mmoja wa hivi karibuni unaojumuisha Twita na utoboaji wa siri.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/issa-villarreal/">Issa Villarreal</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/08/11/mexico-telling-secrets-on-twitter/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/08/rafa-262x300.jpg" title="rafa saavedra" class="alignright" width="262" height="300" /><br />
Rafa Saavedra, muandishi na <em>mtaalamu</em> wa utamaduni wa chini chini kutoka mji wa mpakani wa Tijuana, nchini Maxico, amegeuza kila moja ya zana zake ya uanahabari wa umeme. Kwa upande upande mmoja, anachapisha hadithi fupi fupi na miradi katika blogu yake <em><a href="http://crossfadernetwork.wordpress.com/">Crossfader Network [es]</a></em> (pamoja na vibadiliko vyake); na kwa upande mwingine, ni mtumiaji wa twita anayeshindwa kujizuia <a href="http://www.twitter.com/rafadro">@rafadro</a>, ameichukulia twita kama chanzo cha ubunifu. Mradi wake wa kiuandishi, “soweird”, unachanganya utunzi mfupi-mfupi, siri na jumbe za twita.</p>
<p>“<em>Mtandao wa Crossfader</em> ndio nyumbani kwangu, sehemu ambayo ninakusanya mawazo yangu, na kufikiria dunia njema zaidi na kuyagawa yale ninayoyafanya”, anaeleza Rafa kwenye mahojiano ya barua pepe, “Twit ani nyumba yangu ya ukapera: sherehe isiyo na mwisho na marafiki pamoja na wafuasi, chanzo cha (karibu) habari zote za mwanzo, maabara ya ubunifu iliyojaa makorokoro, kejeli pamoja na dhati kwa alama 140”.</p>
<p>Mwezi Julai mwaka huu a<a href="http://twitter.com/rafadro/status/2212608608">liwataka wafuasi zaidi ya 200 wa twita</a> kuchangia siri zao kubwa (au hata siri ndogo, kama alivyokiri muda mchache baadaye) ili kutengeneza utunzi unaosimuliwa na sauti mbalimbali. Baada ya kupokea siri 40 kwa kupitia Twita alikuja na kazi ya <a href="http://crossfadernetwork.wordpress.com/2009/07/26/nuevo-relato-soweird/">&#8220;Soweird&#8221;</a>, ambamo utunzi na ukweli ulieleza matukio 22 ya ngono, aibu na jinai. <a href="http://crossfadernetwork.wordpress.com/2009/07/26/nuevo-relato-soweird/">Hadithi iliyotokana (na maradi huu) inapatikana kupitia blogu yake katika lugha za Kihispania na Kiingereza</a>, imepangwa kuchapishwa katika jarida la kiuandishi huko Mexico <a href="http://elperro.com.mx/">El Perro [es]</a>.</p>
<p>Katika sehemu moja ya “Soweird” inayotilia maanani masuala ya familia, tumekutana na siri hii:</p>
<blockquote><p>11. Mauritz alimuhujumu mpenzi wake wa kike na kutembea na mpenzi wa kike wa rafiki yake mkuu. Baada ya msichana huyo kutengana na rafiki yake mkuu, aliolewa na kaka yake Mauritz. Na hivi sasa (Mauritz) anashindwa kumfafanulia mpezni wake wa kike ni kwa nini hawawezi kuhudhuria shughuli za kifamilia bila ya kujawa na hofu ya kuzua zahama ya kiwango cha kibiblia.</p></blockquote>
<p>Katika sehemu ya jinai, tunakutana na siri hii nyingine:</p>
<blockquote><p>17. Elwin alianza kutumia hundi ambazo baba yake alimtumia ili kulipia gharama za masomo kwenye chuo kikuu binafsi ambacho alikuwa ahudhurii kununulia vitabu vya vikatuni. Kisha, alichukua na kutumia kiasi kikubwa cha fedha kazini kwake; na kudai kuwa aliporwa. Kuna wakati alihitaji kufanya shughuli ya haraka katika ofisi ya manispaa na aliiomba kampuni yake kiwango kikubwa zaidi ili kumuhonga afisa aliyekuwa zamu (na kutumia nusu ya kiwango kile kwenye pombe).</p></blockquote>
<p>Mtazamo wa Saadvera kuhusu huduma hii ya kuandika blogu fupi-fupi unafika mbali zaidi ya kuandika vitu visivyo na maana: Katika twita mara nyingi watu hukiri vitu vya ajabu, visivyoaminika na vya aibu. Kuna hata anwani ya kukiri <a href="http://twitter.com/search?q=%23yoconfieso">#yoconfieso</a> (ninakiri). Kwa hivyo badala ya kunakili siri kutoka kwenye mafaili, niliamua kwamba ingekuwa ni jambo la kuvutia kufanya na siri za mtu mwingine. Nilitaka kuona ni kwa kiwango gani wanaweza kuthubutu, na ni kwa kiwango gani wanatofautiana na sura ambayo wanawaonyesha wafuasi wao kwenye twita. Kuchungulia kwa mwandishi 2.0.”</p>
<p>Japokuwa hawezi kufichua majina halisi ya wafuasi wake, Saadvera aliwaweka katika makundi watumiaji waliojiunga naye katika mradi: “Kuna watu wachache wan chi za nje, kundi la umri wao ni kati ya miaka 19-40. kama inavyosomeka kwenye maandishi, kuna sehemu nane ambazo zinazigawa siri (Ngono, Aibu, Wapenzi wa zamani, Familia, Jinai, starehe, vishawishi na marafiki wa zamani). Siri za watumiaji wa twita zinahusiana zaidi na familia, ngono, aibu na vishawishi. Kuna siri chache za kustusha.”</p>
<p>“Soweird” siyo mradi wa kwanza unaunganisha twita na fasihi ambao Saadvera ameufanya. Mwaka 2007, alikuwa kiongozi wa mradi wa ushirikiano Microtxt, ambao ulikusanya hadithi fupi-fupi 238 kwa kutumia jina la <a href="http://twitter.com/microtxts">@microtxt</a>, ambao ulichapiswa (kama fasihi teule) kwenye majarida ya Ki-Mexico <a href="http://www.revistareplicante.com/">Replicante [es]</a> na Balbuceo. ”Niliwaalika marafiki ambao ni waandishi, wanahabari, wanafunzi wa mawasiliano na watu ambao nilifikiri wangevutiwa katika utengenezaji wa maandiko mafupi-mafupi na ule uandishi wa watu wanaoficha majina yao. Kanuni ya msingi katika warsha hii ilikuwa ‘uandishi ni ushirika.’ Mwanzoni hawakuelewa matumizi ya twita aidha utaratibu wa uandishi na namna ya kuandika bila kutaja jina. Baadaye tulifikia washiriki 100”, alisema katika mahojiano. </p>
<p>“Hivi sasa siwezi kuyaelewa maisha yangu bila intaneti, bila ya mitandao ya kijamii, bila ya kila kitu kinachotokana na hayo mawili”, alieleza, “lakini katika wakati huo huo, ninaweza kuizima tarakilishi yang una kuishi maisha yangu bila hofu yoyote. Maisha ya kwenye mtandao wa intaneti, uanahabari wa umeme na matumizi pia ni mipaka ambayo tunaweza kuivuka kukiwa au pasipokuwa na vizuizi. Kitu kama hicho hutokea katika maisha yangu hapa Tijuana&#8221;.</p>
<p>Saadvera alieleza ‘ukweli” anaomuhusu yeye kwa herufi 140 (au pungufu):</p>
<blockquote><p>“Sijawahi kutaka kuwa mtu ambaye si mimi; hata hivyo, huwa ninabadilika kila wakati kiasi kwamba wakati mwingine huwa nashindwa kujitambua: naam, ninajipinga”. </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/mexico-simulizi-za-siri-kwenye-twita/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Honduras: Zelaya Akamatwa na Kuondolewa Madarakani</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/06/honduras-zelaya-akamatwa-na-kuondolewa-madarakani/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/06/honduras-zelaya-akamatwa-na-kuondolewa-madarakani/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 29 Jun 2009 14:43:57 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Honduras]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=227</guid>
		<description><![CDATA[Nchini Honduras siku ilianza na habari zinazosema kwamba Rais Mel Zelaya amekamatwa akiwa nyumbani kwake na wanajeshi wenye silaha mnamo siku ya kupigwa kura tata ya maoni. Siku chache kabla, Zelaya alimuondoa madarakani mkuu wa majeshi. Maoni yanatofautiana kutokea yale yanayosema kwamba hali iliyopo ni sawa na mapinduzi ya kijeshi mpaka yale yanayosema kuwa hii ilikuwa ndio njia pekee ya kukomesha jitihada za Zelaya za kutaka kugombea urais kwa awamu nyingine tena.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/eduardo-avila/">Eduardo Avila</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/06/29/honduras-zelaya-arrested-and-removed-as-president/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Nchini Honduras siku ilianza na habari zinazosema kwamba Rais Mel Zelaya amekamatwa akiwa nyumbani kwake na wanajeshi wenye silaha. Kura ya maoni ilikuwa imepangwa kupigwa siku hiyo, kura hiyo ilikuwa inapingwa na mahakama ya juu, na majeshi ya nchi pamoja na baraza la wawakilishi. Siku chache kabla, Zelaya <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/06/27/honduras-political-crisis-over-controversial-referendum/">alimuondoa madarakani mkuu wa majeshi, Jenerali Romeo Vasquez Velasquez, jambo ambalo lilifuatiwa na kujiuzulu kwa wanajeshi wengine wa vyeo vya juu kwa sababu hawakukubaliana na kura hiyo ya maoni.</a></p>
<p>Mara baada ya hapo ilifahamika kuwa Zelaya amepelekwa nchini Costa Rica, ambako aliendelea kujiita kuwa yeye ndiye mkuu halali wa nchi. Kadhalika palikuwa na uvumi kuwa Zelaya amejiuzulu. Hata hivyo, barua inayodaiwa kueleza hivyo <a href="http://miradadehalconhn.blogspot.com/2009/06/la-renuncia-es-un-papel-falso.html">iligundulika kuwa ni ya uongo</a> kama anavyobaini <em>Juan Carlos Rivera wa Miradas de Halcón [es]</em>. Maoni ya mwanzo katika ulimwengu wa blogu na ule wa Twita yalitofautiana kutokea yale yanayosema kwamba hali iliyopo ni sawa na mapinduzi ya kijeshi mpaka yale yanayosema kuwa ile ilikuwa ndio njia pekee ya kukomesha jitihada za Zelaya za kutaka kugombea urais kwa awamu nyingine tena.</p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha na Roberto Brevé na inatumika hapa chini ya hati miliki huria http://www.flickr.com/photos/breve/3668996322/" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/06/honduras1.jpg" title="honduras1" width="400" height="266" /><p class="wp-caption-text">Picha na Roberto Brevé na inatumika hapa chini ya hati miliki huria http://www.flickr.com/photos/breve/3668996322/</p></div>
<p>Umeme umekuwa ukikatika-katika katika mji mkuu wa nchi, kama inavyoripotiwa na gazeti la Honduras Daily News ambalo linahisi kuwa kukatika huko kwa umeme <a href="http://hondurasnews.com/2009/06/28/power-out-in-tegucigalpa">ni moja ya “jitihada za kuzuia upashanaji habari.”</a> Hata hivyo habari zimekuwa zikitoka kwa kutumia mitandao ya kijamii kama vile Twita na Blipea ambayo ilikuwa hai kutwa nzima.</p>
<p><em>Hibueras[es]</em>, mmoja wa wanaomuunga mkono Zelaya <a href="http://hibueras.blogspot.com/2009/06/exigimos-que-se-libere-el-presidente.html">aliandika</a> :</p>
<blockquote><p>Manuel Zelaya fue detenido y sometido por la furza bruta de la jauria criminal de nuestra historia esclavista para evitar que el pueblo hondureño posea el poder de inclusion y de construccion de su patria, los responsables de tan ignomioso acto son todos conocidos y pagaran caro su abuso.<br />
Llegó la hora de buscar por otros medios, lo que se nos niega por la paz, y los responsables seran jusgados por sus actos de traicion a la patria.</p></blockquote>
<div class="translation">Manuel Zelaya alikamatwa na kudhuriwa na nguvu katili za waovu ambazo zimewatia utumwani watu wa Honduras, ili kuwazuia watu wasijichukulie nguvu ambazo zingepelekea ushirikishwaji na ujenzi wa nchi yao, wale ambao wanawajibika na tendo hili chafu wanajulikana vizuri na wataulipia uonevu wao.<br />
Huu ni wakati wa kutafuta kwa njia nyingine yale mambo ambayo tunanyimwa (tunapoyatafuta) kwa njia halali, na wale wanaowajibika kwa vitendo vya uhaini watahukumiwa.</div>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Wanaomuunga mkono rais Mel Zelaya, picha na Roberto Brevé na inatumika hapa chini ya hati miliki huria. http://www.flickr.com/photos/breve/3668437385/" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/06/honduras3.jpg" title="honduras3" width="400" height="266" /><p class="wp-caption-text">Wanaomuunga mkono rais Mel Zelaya, picha na Roberto Brevé na inatumika hapa chini ya hati miliki huria. http://www.flickr.com/photos/breve/3668437385/</p></div>
<p>Baadaye siku hiyo, Bunge lilipiga kura ya kumuondoa madarakani Zelaya kama rais na kumuweka <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Roberto_Micheletti">Roberto Micheletti</a> ambaye alikuwa ni mkuu wa baraza la wawakilishi. Mara tu baada ya kupewa madaraka, alitangaza kuwa uchaguzi utafanyika kama ilivyopangwa mwezi Novemba. Kuwekwa madarakani kwa Micheletti kama kaimu rais kumezua kauli za ukosoaji kutoka kwa maswahiba wa karibu wa Honduras, hasa Venezuela, ambayo imetishia kutumia nguvu za kijeshi ikiwa mfanyakazi yeyote wa ubalozi wake aliyepo nchini Honduras atatekwa au kuuwawa. Zaidi ya hilo, <a href="http://www.reuters.com/article/topNews/idUSTRE55R1S820090628">Rais Hugo Chavez ametamka kwamba serikali mpya inayoongozwa na Micheletti itashindwa</a>.</p>
<p>Watumiaji wa huduma ya Twita kama vile Hugo Chinchilla wanahofu matamko yalitolewa na Chavez na wanayachukulia kama ishara kuwa maswahiba kama hawa wanahusika. Aliambiwa ‘kiholela’ kuwa jeshi <a href="http://twitter.com/hugochinchilla/status/2377758400">linajiandaa kukabili uvamizi wa majeshi ya Venezuela na Nicaragua [es]</a>. </p>
<p>Na kuna wengine kama  Jorge Garcia ambaye anaiunga mkono  serikali mpya na <a href="http://twitter.com/jagbolanos/status/2378901954">anatoa rai kwa watumiaji wenzie wa Twita kutoa msaada maji na chakula kwa wanajeshi [es]</a>. Kadhalika <a href="http://twitter.com/jagbolanos/status/2376327568">anaeleza</a>:</p>
<blockquote><p>
En #honduras no hubo golpe de estado, el estado de derecho continúa, la constitución sigue vigente.</p></blockquote>
<div class="translation">Nchini  #honduras hapajatokea mapinduzi ya kijeshi, utawala wa sheria bado unaendelea, katiba bado inatumika.</div>
<p>Kwa kuwa hivi sasa macho ya dunia yako nchini Honduras, Wilmer Murillo anahofia kutengwa na jamii ya kimataifa. <a href="http://blipea.com/blip/91425">Anaomba</a>:</p>
<blockquote><p>que devuelvan a Mel! estamos quedando como retrogradas ante los ojos del mundo. </p></blockquote>
<div class="translation">Turejesheeni Mel! Tunaonekana kama nchi duni katika macho ya dunia.</div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/06/honduras-zelaya-akamatwa-na-kuondolewa-madarakani/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Paraguai: Rais Lugo Akiri Kuzaa Mtoto Wakati Bado Akiwa Askofu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/paraguai-rais-lugo-akiri-kuzaa-mtoto-wakati-bado-akiwa-askofu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/paraguai-rais-lugo-akiri-kuzaa-mtoto-wakati-bado-akiwa-askofu/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 19 Apr 2009 09:00:14 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Paraguay]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=118</guid>
		<description><![CDATA[Hivi karibuni Rais wa Paraguai Fernando Lugo alikiri kuwa alizaa mtoto wakati alipokuwa askofu wa kanisa la Katoliki la Roma. Habari hii imesababisha utata kati ya wanasiasa, vyombo vya habari, na wanablogu ambao wanaandika kuhusu kusikitishwa kwao na kiongozi huyo, na kadhalika jinsi ambavyo kuna matatizo mengine makubwa zaidi yanayotisha ambayo yanapaswa kutiliwa mkazo ikilinganishwa na vitendo vinavyofanywa na wanasiasa wengine. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/muna-annahas/">Muna Annahas</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/04/17/paraguay-president-lugo-admits-fathering-a-child-as-bishop/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Hivi karibuni <a href="http://globalvoicesonline.org/2008/04/21/paraguay-ex-bishop-becomes-next-president/">rais wa Paraguai Fernando Lugo</a> alikiri kuwa yeye ni baba mzazi wa mtoto wa Viviana Carillo, mtoto ambaye alitungwa wakati Lugo akiwa bado ni askofu wa Kanisa Katoliki la Roma. Pia alikiri uhusiano wa muda mrefu na Carillo. Habari hii inazua utata hivi sasa baina ya wanasiasa, vyombo vya habari, na wanablogu ambao wanaandika kusikitishwa kwao na kiongozi huyo, na ukweli kwamba kuna matatizo mengine makubwa yanayopaswa kuangaliwa ikilinganishwa na vitendo vinavyofanywa na wanasiasa.</p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><a href="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/04/lugo1-300x201.jpg"><img alt="Picha kwa hisani ya akaunti ya APC Flickr ya Fernando Lugo. Chini ya Hati Miliki Huria." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/04/lugo1.jpg" title="lugo1-300x201.jpg" width="400" height="268" /></a><p class="wp-caption-text">Picha kwa hisani ya akaunti ya APC Flickr ya Fernando Lugo. Chini ya Hati Miliki Huria.</p></div>
<p>Carlos Rodríguez wa <em>Rescatar [es]</em> analinganisha (mkasa huu) na yale yaliyotokea miaka iliyopita nchini Marekani, wakati aliyekuwa rais wakati huo - rais Bill Clinton alipokuwa na mahusiano yasiyofaa, nje ya ndoa na Monica Lewinski. Kuna wale wanaosema kuwa mahusiano hayo yalikuwa ni ya faragha na ya kibinafsi na kwamba hayakuathiri maslahi ya nchi aidha hayakuwa na athari yoyote kwa maisha ya wananchi wa Wamarekani. Na sasa Lugo amejitokeza na amekubali wajibu, <a href="http://rescatar.blogspot.com/2009/04/hijo-de-lugo-no-puede-generar-mas.html">anaandika kwamba suala hilo limefikia tamati kwa wananchi wa Paraguai [es]. </a>Anaongeza kwamba kuna vitendo nyeti ambavyo vinatendwa na wanasiasa wengine ambavyo vinapaswa kusakamwa na wananchi wa Paraguai, na kwamba vyombo vya habari virejee na kumakinikia yaliyomo kwenye &#8220;ajenda ya taifa&#8221;</p>
<p>Hata hivyo, kwa kuwa Paraguai ni nchi ya Kikatoliki (Wnanchi wake wengi ni Wakatoliki) , wengi wamesikitishwa na ukweli kwamba Lugo alikiuka ahadi ya kanisa ya kujitenga na ngono, lakini kwa baadhi ya wanojiita wasiokuwa na dini kama vile Liam wa <em>Políticamente Incorrecto</em> [es], hilo si suala. Pia <a href="http://liamdro.blogspot.com/2009/04/el-hijo-de-la-bestia.html">anaangalia maoni ya sekta tofauti kuhusiana na habari hii [es] ndani ya nchi na pia kimataifa</a>: </p>
<blockquote><p>Kuna shutuma zisizothibitishwa kutoka pande na sekta tofauti, wanawake waliokerwa, wanaume waliofurahi, wanachama wa chama cha Colorado wanaovuja furaha na wanachama wa chama cha Liberal wanaotamani mashitaka ya kisiasa, kuna wanahabari wanaolipwa kumlinda na wengine wanaomuandama kwa kadiri wanavyoweza. Watu wanaongelea mahusiano ya kimapenzi ya Lugo na nini kinachotokea katika wakati uliopo? Hakuna chochote, kama kawaida, nchi inasambaratika vipande vipande.</p></blockquote>
<p>Jorge Torres Romero anaandika kwenye blogu yake <em>Detrás del Papel [es], </em><a href="http://www.abc.com.py/blogs/post/855/el-pastor-mentiroso">kwamba Lugo aliuhadaa umma</a>:</p>
<blockquote><p>Lugo aliuhadaa umma. Alijikweza kana kwamba ni mgombea tofauti, mgombea wa mabadiliko, wa maadili na ukweli. Lakini mwishowe, hana lolote bali ni muongo mkubwa. Alituuzia (aliwauzia, kwa sababu sikumpigia kura) sura ya utakatifu na hivi leo amepoteza mtaji huo pekee ambao alitegemeza ugombea wake: ukweli.</p></blockquote>
<p>Ukweli ni kwamba japokuwa habari hizi zilitikisa na kuwashtua watu wote, wengi wanandhani kuwa suala hili halipaswi kuyaondoa macho kutoka kwenye yale yanayowagusa watu wa Paraguai.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/paraguai-rais-lugo-akiri-kuzaa-mtoto-wakati-bado-akiwa-askofu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
