GlobalVoices katika

Portuguese

Hifadhi ya lugha Katika Makundi · 27 jumbe


Below are posts about citizen media in Portuguese. Don't miss Global Voices em Português, where Global Voices posts are translated into Portuguese! Read about our Lingua project to learn more about how Global Voices content is being translated into other languages.

Habari mpya Kuhusu Portuguese

11 Mei 2013

Uchaguzi Tume ya Uchaguzi Msumbiji: Mwanaharakati Ajitoa Kugombea

Kutokuwepo uwazi na weledi katika mchakato wa kumchagua mgombea, mbali na kufahamika nani hasa watachukua nafasi zinazogombewa kabla hata ya uchaguzi katika taasisi hiyo. Hizo zilikuwa baadhi ya sababu zilizotolewa na mwanaharakati wa haki za binadamu, Benilde Nhalivilo, wakati akijitoa rasmi kugombea nafasi kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Msumbiji[pt], chombo kinachohusika na kuandaa na kusimamia chaguzi nchini humo. Taarifa zaidi zinapatikana kwenye gazeti la A Verdade [pt].

6 Mei 2013

TEDXSão Tomé: Mkutano Wanukia São Tomé na Príncipe

TEDXSão Tomé

TEDXSão Tomé

Uandikishaji wa awali kwa ajili ya mkutano wa TEDXSão Tomé umezinduliwa rasmi. Mkutano huo una kaulimbiu inayosema “Visiwa Vimeunganishwa : São Tomé + Príncipe = Áfrika Vimeunganishwa na Ulimwengu” na utafanyika tarehe 20 Juni. Wasemaji katika mkutano huo waliothibitishwa ni pamoja: Dynka Amorim, Ismael Sequeira, Profesa Robert Drewes na Aoaní d'Alva. Tiketi linapatikana kwa Euro 20. Zaidi kuhusu mkutano huo tembelea ukurasa wa Facebook na tovuti [viungo vyote katika lugha ya Kireno].

10 Aprili 2013

Vyama vya Siasa Msumbiji na Matumizi ya Intaneti

(…) kuna nafasi ambayo mpaka sasa haijatumiwa ipasavyo na vyama vya siasa nchini Msumbiji, iwe ni kwa ajili ya kueneza propaganda za kisiasa au kufanya kampeni za uchaguzi: nalo ni mtandao wa intaneti.

Jukwaa la Msumbiji liitwalo Olho Cidadão (Jicho la Wananchi) lilizindua blogu mpya tarhe 2 Aprili, 2013, kwa uchambuzi wa uwepo wa vyama vya siasa mtandaoni [pt]. Msumbiji itafanya uchaguzi wa manispaa tarehe 20 Novemba mwaka huu.

29 Januari 2013

Msumbiji: Uhamasishaji wa Kiraia Kuwasaidia Waathirika wa Mafuriko

sos chokwe

Baada ya mvua kubwa iliyosababisha mafuriko kusini mwa Msumbiji yaliyowaacha maelfu ya raia bila makazi na wengi kupoteza maisha, kikundi cha kiraia cha Msumbiji Makobo kimeanza kampeni ya mshikamano inayoitwa “S.O.S. Chókwè” kukusanya misaada ya hisani kwa ajili ya waathirika.

30 Agosti 2012

Brazil: Mtoto wa Miaka 13 Aonyesha Matatizo ya Shule Kupitia Facebook

Diário de Classe [pt], ukurasa wa Facebook uliofunguliwa na Isadora Faber, aliye na miaka 13 na anayetokea Santa Catarina, Brazil, tayari umeonyesha kupendwa zaidi ya mara 176,000. Huku lengo lake likiwa ni “kuonyesha ukweli kuhusu shule za umma”, Isadora anaweka picha zinazoonyesha maeneo yanayohitaji kufanyiwa ukarabati katika shule yake pamoja na kutoa taarifa kuhusu matatizo mengine mengi ya jumla.

31 Julai 2012

Angola: Raia Wadai Kampeni za Uchaguzi za Wazi

Asasi za kiraia nchini Angola zinatoa wito wa uwazi zaidi [pt] katika maandalizi ya uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 31 agosti, 2012. Moja wapo ya miradi iliyozinduliwa hivi karibuni kwa lengo hilo ni maombi ya mtandaoni [pt] ikiwataka viongozi wa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo kushiriki midahalo ya moja kwa moja kupitia televisheni za nchi hiyo.

12 Julai 2012

Msumbiji: Je, Zana za Uandishi wa Kiraia Zimeua Blogu?

Katika mfululizo mfupi wa makala zake, Profesa Carlos Serra anabainisha baadhi ya sababu zinazoeleza kwa nini blogu za Msumbiji zinaendelea kupungua siku hadi siku. Msomaji mmoja anatoa maoni akidhani kwamba kublogu kunahitaji kazi kubwa katika kuhakikisha kuwa habari mpya zinaendelea kuwepo sambamba na kiwango cha habari hizo. Wakati Serra anasema kwamba zana za uandishi wa kiraia (kama vile twita na facebook) zinaweza kulaumiwa kusababisha hali hii, pamoja na faida za matumizi ya zana hizo.

12 Juni 2012

Video jumbe
Brazili: Jarida Lawapa Nafasi Wasio na Makazi

Soma makala hii.

Jarida la Ocas linalosambazwa katika mitaa ya mjini São Paulo pamoja na Rio de Janeiro tangu 2002, ni jarida ambalo husheheni habari ambazo hulitofautisha na vyombo vikuu vya habari nchini Brazil. Na linakwenda zaidi ya hapo. Aidha huwapa mwanzo mpya na fursa za kazi watu ambao hawana makazi na ambao wamo katika hatari ya kuangamia kijamii.

23 Agosti 2010

Cape Verde: Midahalo Kuhusu Vijana na Siasa Inayoendelea Huko Ureno

Kuna kundi la raia wa Cape Verde ambalo huandaa mikutano mjini Lisbon ili kujadili uhusiano kati ya vijana na siasa, kama anavyoeleza Suzano Costa katika video [pt] kama ilivyowekwa tena na Amilcar Tavares. Katika blogu yao – Tertúlia Crioula [pt] - unaweza kusoma maelezo yaliyochukuliwa kutoka “Cape Verde katika Mdahalo” kadhalika unaweza kusoma majadiliano mengine kuhusu masuala muhimu.

31 Julai 2010

Brazil: Ukatili Dhidi ya Wanawake Kila Siku

Soma makala hii.

Nchini Brazil, wanawake 10 huuwawa kila siku. Mauaji ya hivi karibuni na anasadikiwa kuwa mzazi wa mtoto wake, mlinda mlango nyota aneyetarajiwa, yamewasha cheche za majadiliano katika uwanja wa blogu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha