Habari kuhusu Kifaransa kutoka Aprili, 2009
Rwanda: Miaka kumi na tano baada ya mauaji ya Kimbari
Hivi karibuni zilifanyika sherehe za kitaifa nchini Rwanda kuadhimisha kumbukumbu ya kutimiza miaka 15 tangu mauaji ya Kimbari. Mauaji hayo yaliangamiza maisha ya watu wapatao 800,000. Mnamo tarehe 7 Aprili, maadhimisho yalifanyika katika mji mkuu wa Kigali, na pia katika mji wa Nyanza, ambapo watu wapatao 5000 waliuawa kinyama. Katika Uwanja wa Mpira wa Kigali, maelfu ya mishumaa iliwashwa na kupangiliwa katika namna ambayo iliunda neno "Matumaini" katika lugha tatu.
Jamhuri Ya Kidemokrasi ya Kongo: Mahojiano na Kabila Yaamsha Gadhabu
Wanablogu wa Kikongo wakosoa mahojiano ya hivi karibuni ya rais Joseph Kabila aliyoyafanya kwenye gazeti la New York times, wanauchambua msimamo wa Kabila juu ya Rwanda, ni nani wa kulaumiwa kuhusu rushwa, na jinsi wanahabari wa Magharibi wanavyoripoti kuhusu Afrika.