GlobalVoices katika

French

Hifadhi ya lugha Katika Makundi · 65 jumbe


Below are posts about citizen media in French. Don't miss Global Voices en Français, where Global Voices posts are translated into French! Read about our Lingua project to learn more about how Global Voices content is being translated into other languages.

Habari mpya Kuhusu French

5 Mei 2013

Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska

Habari Mpya:  Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito.

Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana wasiotarajiwa wamejitokea kuwania kiti hicho. Wakati wagombea wa awali walikuwa wapya kabisa wasiofahamika sana, wanasiasa wachache machachari wanaofahamika wanatarajiwa kugombea akiwemo rais wa zamani Didier Ratsiraka, rais wa sasa wa mpito Andry Rajoelina [fr] na mke wa rais wa zamani Ravalomanana, anayeitwa Lalao Ravalomanana.

24 Aprili 2013

Jaribio la Mapinduzi katika Visiwa vya Comoro

Jeshi la Pilisi nchini Comoro limesema linawashikilia watu wanaosemekana kuwa wahaini raia wa Kongo na Chadi kwa tuhuma za jaribio la kuiangusha serikali lililofanyika mwisho wa wiki. Linfo.re anaongeza kwamba [fr]:

Makamanda wa Jeshi hawakutaka kupambana waziwazi na wahaini hao. Waliamini kwamba ” Kujeruhi raia wa Comoro kwa lengo la kuwalinda wakubwa inaleta picha ya usaliti kwa nchi hiyo ya Comoro”.

12 Februari 2013

Udhaifu wa Watawala wa Afrika unajionesha Mali?

Ousmane Gueye katika tovuti ya Mondoblog anaandika [fr] kuhusu kuchelewa kupeleka vikosi vya kijeshi kasikazini mwa Mali:

Kama tungekuwa tunasaiili matokeo ya watu wenye amani na huru kuingilia kati hali ya mambo nchini Mali, basi ni wazi kuwa kwa kuchelewa kupeleka vikosi vya ulinzi, nchi za Afrika zimewakosea wananchi wa Mali kwa mara nyingi…kelele zote za wakuu wa nchi lakini bado hawajaweza kutimiza lengo lolote waliloliweka wao kama hatua ya kupunguza nguvu ya Waslamu wenye msimamo mkali nchini Mali.

22 Januari 2013

Jukwaa la Kiafrika Lenye Makala za Bure za Kitaaluma

Video inayoonesha namna www.hadithi.org inavyofanya kazi kuboresha upatikanaji wa zana za utafiti kwa Afrika

Januari 24, ni siku ambayo inategemewa kuwa ya kuzindua rasmi Hadithi, ambalo ni jukwaa la kuhifadhia zana za bure za kitaaluma mjini Nairobi, Kenya. Wasomi mbalimbali na wadau wa mitandao watakusanyika pamoja kujadili upatikanaji wa zana huru za kitaaluma katika elimu ya juu nchini Kenya. Hadithi itasaidia kutafuta, kuona na kushusha makala kutoka katika taasisi za kitafiti duniani kote. Kujiandikisha kwa tukio hili, itafute Hadithi mtandaoni kupitia Facebook na tovuti ya Eventbrite.

“Wanasemaje Bamako?” Mazungumzo na Awa anayeishi Mali

Mazungumzo ya kila siku kwa njia ya skype(kwa Kifaransa)  kati ya Awa Traoré aliyeko Bamako na Anne Morin akiwa Ufaransa (kupitia anuani ya @annagueye)

Anne Morin na Awa Traoré wanabadilishana mawazo kuhusiana na maisha ya kila siku mjini Bamako, ujira usiokidhi mahitaji, gharama za maisha na hali ya kisiasa isiyotabirika wakati huu ambapo vita vinanukia nchini humo.

11 Januari 2013

Mashoga Washambuliwa Kaskazini mwa Kameruni

Oscarine Mbozo’a anaripoti [fr] katika blogu ya L'Actu kuwa shoga mmoja akiwa ameambatana na mwenzi wake walizomewa karibu na soko mnamo tarehe 6, Januari 2013, mjini Maroua, Kaskazini mwa Kameruni:

Goche Lamine, mfanyabiashara wa madawa, alikamatwa na mwanafunzi wa shule ya sekondari aitwaye Sanda, mwenye umri wa miaka 17. Umati wa watu uliokuwepo sehemu hiyo baada ya kugutushwa na mtoto aliyekuwa akipiga kelele “samaroka! Samaroka (yaani mashoga katika lugha ya ki-Fulfulde), uliwakimbilia watu hao na kuanza kuwarushia mawe.

Rais wa Chadi Awateua Wanawe Kushika Nafasi Nyeti

Djamil Ahmat anaripoti kuwa rais Déby wa Chadi amemteua mwanae wa kiume Mahamat Idriss Déby, 24, kuwa brigedia jenerali  [fr] pamoja na maafisa wengine wanne. Tchadanthopus anaongeza kuwa mwanae mwingine Zackaria Idriss Deby alisemekana kukabidhiwa umakamu wa rais [fr]  nafasi ambayo inampa madaraka yote wakati baba yake anapokuwa nje ya nchi.

2 Januari 2013

Watu 60 Wauawa kwa Msongamano nchini Abidjan

Magogo ya miti yaliyokuwa yameanguka barabarani yanaonekana kusababisha msongamano mkubwa na ulioua watu 60 na kujeruhi wengine 49 wakati wa sherehe za kuukaribisha mwaka mpya mjini Abidjan, Côte d'Ivoire. Kutokana na ukweli kuwa eneo hilo halikuwa na mwanga wa kutosha inawezekana ndio sababu iliyochangia tukio hilo la msongamano ulisababisha mkanyagano wa watu.

Israel Yoroba jijini Abidjan anaripoti kuhusu msongamano huo wa kutisha [fr] wakati watu wengi wakiwa wamekusanyika kusubiri kushuhudia milipuko ya fataki kuashirika mwaka mpya katika wilaya ya Plateau. Alama habari #drameplateau ilianzishwa kutoa nafasi ya kupatikana kwa habari za wakati huo huo kuhusu tukio hilo la kusikitisha na namna ya kuwasaidia waathirika. Hili nijanga la tatu la namna hii tangu mwaka 2009 [fr] nchini Côte d'Ivoire.

23 Disemba 2012

Utambulisho wa Jamii ndogo ya Balkan

Face the Balkans subjects of stories

Picha ya mwonekano wa tovuti ya Balkans.

Waandishi vijana kumi na watano kutoka katika nchi zipatazo sita tofauti wametengeneza mfululizo wa masimulizi binafsi kuhusu masuala ya namna jamii zenye watu wachache (kwa mapana yake) zinavyoweza kuwakilishwa kutoka Bosnia na Herzegovina, Kosovo, Serbia, na Macedonia. Habari zinapatikana katika lugha za Kiingereza, Kijerumani, na Kifaransa katika mwonekano wa tovuti ya Balkans.

16 Oktoba 2012

Ghana: Vikwazo Vinavyowakabili Wanawake Kimaendeleo

Betty Mould Iddrisu, Jaji na Waziri wa Sheria wa Ghana, anaandika [fr] kwenye blogu ya pambazuka.org:

Kufikia ngazi za juu kabisa za utawala si rahisi, na hata unapopanda mpaka juu kabisa, bado unajikuta unakabiliwa na hisia za watu zenye uadui na watu wanakuwa na mashaka na uwezo wako, kwa sababu tu wewe ni mwanamke. Mwanamke akikamata madaraka ya juu humbidi kufanya kazi kwa bidii zidi kuliko mwanaume ili kuthibitisha uwezo wake, lakini bado hata akifanya hivyo anakumbana na uadui pamoja na mfumo unaomwona kuwa duni, iwe katika majukumu yake kama meneja na kiongozi, na hata katika mazingira yoyote ya kazi ambayo yanatawaliwa kwa kiasi kikubwa na wanaume.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha