<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; English</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/languages/english/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Video: Vijana duniani kote wajieleza kwa sekunde 60</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/video-vijana-duniani-kote-wajieleza-kwa-sekunde-60/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/video-vijana-duniani-kote-wajieleza-kwa-sekunde-60/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Antigua and Barbuda]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Bangla]]></category>
		<category><![CDATA[Bangladesh]]></category>
		<category><![CDATA[Central Asia & Caucasus]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Film]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Mongolia]]></category>
		<category><![CDATA[Niger]]></category>
		<category><![CDATA[Poland]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=743</guid>
		<description><![CDATA[mradi wa OneMinuteJr unawapa vijana......]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/30/video-worldwide-youth-express-themselves-in-60-seconds/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption alignleft" style="width: 85px"><img alt="Nembo ya OneMinutesJr" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/minutesjrth-75x75.jpg" title="minutesjrth" width="75" height="75" /><p class="wp-caption-text">Nembo ya OneMinutesJr</p></div><br />
Mradi wa <a href="http://www.theoneminutesjr.org/">OneMinutesJr </a>unawapa vijana wa umri wa kati ya miaka 12 na 20 kutoka kona mbalimbali za dunia fursa ya kujieleza, kusema na kujifunza ujuzi wa kutengeneza kazi za sauti-na-kuoangalia ili kuwasiliana zaidi ya mipaka yao, lugha zao na umbali zaidi kwa kutumia video ya sekunde 60.</p>
<p>Mradi wa OneMinuteJr umetokana na jitihada za pamoja za <a href="http://www.eurocult.org/">Mfuko wa Utamaduni wa Ulaya</a>, <a href="http://www.theoneminutes.org/">Mfuko wa One Minutes Jr</a> na <a href="http://www.unicef.org/">Unicef</a>, vile vile na mashirika mwenza mengineyo. Katika wavuti yao, unaweza kuperuzi video za dakika moja moja zenye thamani ya mwaka mmoja  kutoka katika nchi mbalimbali, nyingine zikiwa zimetumwa na watu binafsi, na nyingine zimetokana na <a href="http://www.theoneminutesjr.org/?thisarticle=174">warsha</a> ambapo vijana wanafundishwa mbinu za kuandika, kupiga picha za video na kuhariri mawazo yao.</p>
<p>Video hizi fupi fupi zinaonyesha masuala, mawazo na ndoto za vijana wanaotokea asili tofauti tofauti, na kutupa kidirisha cha kuyachungulia maisha yao ya kila siku. Kwa mfano, kutoka <a href="http://www.theoneminutesjr.org/?thissection_id=10&#038;movie_id=200900283&#038;series_id=30">Poland, Ludmila Kierczak</a> anatengeneza video na kueleza yeye ni nani. Ili kuiangalia video, tafadhali bofya kwenye picha hapa chini <a href="http://www.theoneminutesjr.org/?thissection_id=10&#038;movie_id=200900283&#038;series_id=30">ili kwenda kwenye tovuti ya OneMinuteJr</a>.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/whoami.JPG" title="whoami" class="alignnone" width="239" height="209" /><br />
Huko Bangaladesh, Mobasshera Tarannum Adiba anaonyesha vifungu kadhaa kutoka <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Convention_on_the_Rights_of_the_Child">Makubaliano ya Haki za Mtoto</a>. Katika video yake, iitwayo <a href="http://www.youtube.com/watch?v=xyC8avD4Xlg">Nataka Uhuru</a>, anagusia Kifungu cha 12: Watoto wana haki ya kusikilizwa maoni yao na sauti zao ziheshimiwe na Kifungu cha 16 ambacho kinasema kwamba kila mtoto ana haki ya faragha.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/xyC8avD4Xlg&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/xyC8avD4Xlg&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kutoka Mongolia, <a href="http://www.youtube.com/watch?v=cZM87XL71jk">Tuvdenjamts (Tuvden) Altankhyag anaonyesha </a>haki ambayo kila mtoto anayo kwa utamaduni wake mwenyewe:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/cZM87XL71jk&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/cZM87XL71jk&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Na katika video hii inayofuata, Simon Tonge kutoka Antigua na Barbuda, anatumia haki yake ya uhuru wa kujieleza katika video iitwayo <a href="http://www.youtube.com/watch?v=QnBwfX9EtA0">Maungamo ya msichana aliyebalehe</a>:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/QnBwfX9EtA0&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/QnBwfX9EtA0&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Ibrahim Ide kutoka Niger anaonyesha haki ambayo watoto wanayo kwa familia inayowapenda na kuwalindia haki zao katika video ya <a href="http://www.youtube.com/watch?v=8QiDCP5l2x8">Pamoja au Pasipo</a>: </p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/8QiDCP5l2x8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/8QiDCP5l2x8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kwa video zaidi za dakika moja, unaweza kuangalia kwenye tovuti kuu kwa ajili ya mradi huo kwenye <a href="http://www.theoneminutesjr.org/">TheOneMinutesJr.org</a> au unaweza kutembelea <a href="http://www.youtube.com/user/UNICEFoneminutesjr">Idhaa ya UNICEF One minutes Jr kwenye Youtube</a> ili kuona video nyingi zaidi zenye sekunde 60 zilizotengenezwa na vijana kwenye mada ya Haki za Watoto.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/video-vijana-duniani-kote-wajieleza-kwa-sekunde-60/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Urusi: Jinsi Abiria wa &#8220;Nevsky Express&#8221; Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 01 Dec 2009 11:11:27 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Russian]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=738</guid>
		<description><![CDATA[Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/gregory-asmolov/">Gregory Asmolov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/29/russia-how-passengers-of-nevsky-express-tell-their-stories-through-social-media/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mamlaka nchini Urusi yanaendelea <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/28/russia-at-least-25-people-killed-in-the-neva-express-train-crash/">kuchunguza ajali ya treni la &#8220;Nevsky Express&#8221; </a>[ENG] ambayo ilitokea kati ya Moscow na St Petersburg usiku wa Ijumaa. Kwa mujibu wa maofisa, dhahama hiyo iliyochukua maisha ya angalau abiria 25 ilikuwa ni shambulio la kigaidi. Ajali hiyo imezua maswali mengi. Watu wengi wanauliza ni nini kilichotokea katika masaa ya mwanzo baada ya ajali na ni kwa nini ilichukua muda mrefu kuanza kutoa taarifa za ajali hiyo.</p>
<p>Kwa kuwa dhahama hiyo ilitokea mbali na maeneo yenye makazi ya watu, ilichukua muda mrefu kwa wanahabari kuwasili kwenye eneo la ajali. Na ndipo picha za kwanza na video zilipoanza kuonekana kila mahali. Je nini kilichoyatokea majukwaa ya uanahabari wa kijamii ambayo yalitaarifu vilivyo kuhusu <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/europe/7614951.stm">ajali ya ndege mjini Perm</a> [ENG] mwezi Septemba 2008.</p>
<p>Abira pekee ambaye alitoa taarifa mara moja kuhusu ajali ya “Nevsky Express” alikuwa mtumiaji wa Twita <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog</a>. Aliandika mara 12 kuhusu ajali hiyo kabla ya kuwasili nyumbani. Haya ndio aliyoandika: </p>
<blockquote><p>Nipo hai. Lakini nitaeleza kuhusu (ajali) baadaye. Kama mtu ataeleza chochote kwenye habari, tafadhali niandikie. Hawatuambii kila kitu hapa.</p></blockquote>
<p>Baadaye, abiria wengi kutoka mabehewa ya kwanza – ni mabehewa ya mwisho ambayo yaliteguliwa kutoka kwenye reli –walisema kuwa kwa saa zima baada ya ajali hawakufahamu chochote. <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy frog</a> alituma habari mpya za nyongeza: </p>
<blockquote><p>Tumepanda treni jingine. Nilifanya kila nilichoweza.</p>
<p>Hivi sasa tupo SAPSAN (treni mpya ambyo iliwachukua abiria kwenda St. Petersburg – G.A). Natamani ingekuwa inakwenda polepole.</p>
<p>Wametangaza sasa hivi kuwa watu walitayarishwa rasmi wangetulaki kwenye kituo cha treni.</p></blockquote>
<p>Siku iliyofuata baada ya dhahama, <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog </a>aliandika muhtasari wa uzoefu wake:</p>
<blockquote><p>Nilizihisi hisia za kwanza kuhusu kilichotokea wakati tulipofika karibu na Piter (St. Petersburg G.A). Sikuwa na wasiwasi nilipokuwa katika eneo la ajali. Nilikuwa na hofu kidogo na viatu vyangu – kulikuwa na tope kila mahali na mawe yenye ncha.</p></blockquote>
<p>Jumamosi habari nyingi zilijitokeza wakati abiria walipoanza kublogu kuhusu yaliyowakuta. Makala ya blogu maarufu zaidi inayohusiana na mada hii iliandikwa na mtumiaji wa LJ <em>paltus_mk</em> [RUS] ambaye alikuwemo ndani ya mabehewa ya mwisho yaliharibiwa vibaya na mlipuko. <a href="http://paltus-nk.livejournal.com/23747.html">Aliandika </a>[RUS]:</p>
<blockquote><p>Yote yanatokea ndani ya sekunde 10 wakati unapofahamu ni nini kitakachotokea. Nilikuwa na muda wa kutosha kuutayarisha mwili wangu. Lakini hakuna linaloweza kusaidia dhidi ya kanuni za Newton wakati dazeni za tani za vyuma zinaposimama mara moja wakati zikiwa katika mwendo wa kasi – ni bahati tu… kwa hiyo nilikuwa na bahati tu. Kaka yangu alikuwa na bahati, pia, ukiachilia mbali ukweli kuwa majeraha yake yalikuwa yanatisha kuliko yangu.<br />
[…]</p></blockquote>
<blockquote><p>Kila kitu ambacho kilikwenda mrama hadi kusimama kabisa kulichukua kama sekunde 30 hivi. Ilikuwa giza na kimya. Watu walioumia walianza kulia. Nilikuwa sakafuni, nimekandamizwa na miili mingine. Niliisogeza ile miili. Niliona kuwa nimelowana na damu lakini damu ile haikuwa yangu. Niliona kuwa ni mzima na miguu yangu na mikono vuinafanya kazi. Kichwani nilikuwa na jeraha linalovuja damu. Ilinibidi ninyanyuke na kusubiri kwa muda kiasi kabla ya watu wenye majeraha mado waliposafisha njia ya kutoka.<br />
[…]<br />
Mateso yalikuwepo kila mahali. Tulikuwa tumeketi mwishoni mwa behewa na mikoba yote ilipaa ikituelekea. Watu wengi waliojeruhiwa. Katika dakika chahce baada ya ajali, behewa lilikuwa ni kama fungu la miili, viti na sehemu za treni ambazo zilikuwa zimesambaa sawia kila mahali.</p></blockquote>
<p><em>Paltus_mk </em>anasimulia habari za uokoaji zenye maelezo ya kina kuanzia dakika za mwanzo baada ya ajali, lakini wakati huo huo anaepuka ufafanuzi ambao ungeweza kuwastua wasomaji. Anaandika kuwa abiria walianza kupeana huduma ya kwanza kwa ushujaa bila kuogopa. Anasema haikuwezekana kuhesabu ni wagtu wangapi waliofariki. Waokoaji waliwasili saa moja na nusu baada ya ajali. <em>Paltus_mk</em> na kaka yake hatimaye waliokolewa na kupelekwa kwenye hospitali jirani na baadaye aliwasili mjini St. Petersburg. </p>
<p>Hadithi nyingine ya kunusurika ilichapishwa na mwanablogu pancakyes katika huduma nyingine ya kublogu ya Kirusi Ya.Ru. behewa lake halikuharibiwa na mlipuko. Alichapisha makala yake ya kwanza saa 4:11 za usiku – nusu saa baada ya ajali – pale pale kwenye eneo la ajali.  Aliandika kuwa treni ilisimama kutokana na ajali ya namna fulani, mabehewa machache yaliteguliwa na kwamba angewasili nyumbani kwa uchelevu kuliko ilivyotarajiwa. Karibu saa zima baadaye, aliongeza kuwa kulikuwa na waathirika katika mabehewa mawili ya mwisho. Jumamosi,  <em>pancakyes</em> <a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442">alichapisha habari nzima kuhusu ajali</a> [RUS] kama alivyoshudia mwenyewe:</p>
<blockquote><p>Tulihisi mitetemo michache ambayo ilikuwa ikiongezeka nguvu. Vitu vilianza kuanguka kutoka mezani. Haikuwa wazi ni nini kilichotokea. Hapakuwa na matangazo. Kwanza tulidhani kuwa halikuwa jambo lenye uzito. Pengine kuna mtu aliyesimamisha treni kwa makosa. Lakini makondakta wenye sura zenye hofu walianza kukimbia kila mahali wakikusanya magodoro, vitambaa vya mezani na maji. Walitutaka tusiondoke kwenye viti vyetu isipokuwa kama ni madaktari. Tulisikia mambo mabaya kutoka kwenye redio zao. Uvumi ulianza kusambaa. Hatukuamini kuwa mabehewa mawili yalikuwa yametengana na yalikuwa mbali sana. Baadaye tuligundua kuwa ilikuwa kweli.</p>
<p>Tulitoka nje na tulitaka kusaidia. Tulikwenda mpaka behewa la tatu. […] hatukutaka kuwa waduwazi ambao wanaongeza wingi wa watu bila fursa yoyote ya kusaidia. Pia hatukutaka kuona yale ambayo watu waliotoka huko walikwishatueleza.</p></blockquote>
<p>Mara baada ya ajali, majukwaa ya uanahabari wa kijamii yalikuwa sehemu ya kwanza ambayo wanahabari wa Kirusi  walikuwa wakitafuta habari. Mwandishi kutoka Shirika la Habari la RIA-Novosty aliacha maoni kwenye blogu ya <em>pancakyes</em> na kumtaka mwanablogu huyo ampigie simu mara moja. Tatyana Landa (mtumiaji wa LJ mwenye jina la Elada) <a href="http://elada.livejournal.com/220534.html">aliandika kwenye blogu yake</a> [RUS] kuhusu rafiki aliyenusurika ambaye alikuwemo kwenye treni. Mara moja wanahabari wawili waliacha maoni ya kumtaka awasiliane nao. Baadaye Tatyana <a href="http://elada.livejournal.com/220866.html">alichapisha makala ya hasira</a> [RUS] ambamo alisema kuwa mwanahabari kutoka “Komsomolskaya pravda” (gazeti la udaku la Kirusi) alikuwa akijaribu kumpata kwa simu mara kadhaa usiku huo. Makala hiyo iligeukia mahali ambapo watu walianza kujadili kama wanahabari wanaweza kuwatumia wanablogu kama chanzo cha taarifa zinazohusu hii ajali ya treni. Wanahabari pia walijaribu kuwasiliana na mwanablogu ambaye <a href="http://naechst-naechst.livejournal.com/105582.html#comments">aliandika</a> [RUS] kuwa aliamua kutopanda treni la “Nevsky Express” katika dakika ya mwisho.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu <a href="http://tema.livejournal.com/509436.html">walieza kughafirika kwao </a>[RUS] na ukweli kuwa ni watu wachache mno kutoka kwenye treni walitumia vyombo vya habari vya kijamii kutoa taarifa za kile kilichokuwa kinatokea., Na, inavyoonekana, kuna fafanuzi kadhaa zinazoelea ni kwa nini  uanahabari wa kijamii haukuchukua nafasi kubwa katika upashaji wa habari za ajali ya “Nevsky express”.</p>
<p>Twita, jukwaa zuri la kublogu moja kwa moja, si maarufu nchini Urusi. Kwa mujibu wa <a href="http://twitter.com/twitRU">twitRU </a>[RUS], kuna watumiaji wa Twita 2,700 tu ambao wanaandika kwa lugha ya Kirusi. Wakati huo huo, majukwaa maarufu ya kublogu nchini Urusi kama vile Livejournal.com au ya.ru yangeweza kutumika ili kublogu moja kwa moja lakini, kama ilivyojadiliwa hapo juu, kuna mifano michache tu ya matumizi hayo.</p>
<p>Ufafanuzi wa pili unahusiana na nafasi ya zana za mkononi na uunganishaji. Zana za mkononi zinaongezeka nchini. Warusi zaidi na zaidi wanaweza kutumia mtandao wa intaneti na zana nyingine za mtandaoni. Tabia hii ina nguvu katika maeneo ya Moscow na St. Petersburg. Lakini ajali ilitokea mbali na maeneo ya mjini ambako, kama mashihidi walivyotaarifu, uwezo wa kupatikana kwa mawasiliano ya simu za mkononi ulikuwa mdogo. Mwanablogu  <em>pancakyes </em><a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442&#038;ncrnd=2805">anasimulia</a> tatizo la mawasiliano:</p>
<blockquote><p>
Mawasilian ya simu yalikuwa mabaya sana. Inawezekana kuwa kila mtu alijaribu kupiga simu kwa wakati mmoja na mtandao ulielemewa. Nilianza kupata jumba za maandishi pale tu nilipokuwa kwenye treni la pili (treni ambalo liliwachukua abiria kwenda Saint- Petersburg G.A.). Ningeliweza kutumia mtandao wa intaneti, lakini ilikuwa ni vigumu mno.</p></blockquote>
<p>Hii ni tofauti, ajali ya ndege kule Perm mwaka jana ambayo ilitoa fursa nyingi kwa uanahabari wa kiraia:</p>
<p>1. Ndege ilianguka ndani ya mipaka ya mji ambako watu wengi waliweza kuona ni nini kilichokuwa kinatokea kutokea madirishani. Ajali ya “Nevsky express”, kama ilivyoelezwa awali, ilitokea sehemu za vijijini.</p>
<p>2.Habari zilizoandikwa kwa uanahabari wa kijamii kule Perm zilitokana na maelezo ya walioishuhudia ajali ambao hawakuwamo katika ajali (kwa bahati mbaya, hapakuwa na walionusurika kutoka katika ile ndege). Mashahidi wote wa tukio la “Nevsky Express”  walikuwa ni abiria katika treni. </p>
<p>3. Watu wengi walituma habari mpya juu ya ajali ya ndege kule Perm kwa kutumia tarakilishi za nyumbani. Walionusurika kwenye “Nevsky Express” walitegemea zana za mikononi.</p>
<p>Tofauti hizi zinabainisha kwa nini vyombo vya habari vya kiraia vilikuwa mbele katika ajali ya  ndege na vilikaribia kutokuwepo kwenye tukio la “Nevsky Express.” </p>
<p>Pia inawezekana kudai kuwa urusi bado haijaendeleza utamaduni wa utoaji taarifa kupitia uanahabari wa kiraia. Na ndiyo sababu abiria wawili tu walikuwa na msukumo wakutosha kwenda kwenye mtandao na kujipa kazi ya uanahabari wa kijamii. Na pia inaweza kufafanua upinzani wa abiria na wanablogu kwa wanahabari ambao walikuwa wanatafuta taarifa za ajali kwenye vyombo vya habari vya kijamii. </p>
<p>Inaonekana kana kwamba ulimwengu wa blogu wa Kirusi bado uko mbali na kuwa chanzo kikuuu cha kutangaza habari mpya. Bado unabaki kuwa sehemu ya usambazaji wa habari na mijadala mipana inayohusu nini kilichotokea. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Malawi: Rais Ataka Nguvu Zaidi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/malawi-rais-ataka-nguvu-zaidi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/malawi-rais-ataka-nguvu-zaidi/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 25 Nov 2009 10:52:12 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Malawi]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=735</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Rais wa Malawi ataka nguvu zaidi!: &#8220;rais wa Malawi Bingu wa Mutharika, ambaye chama chake kina wabunge wengi katika bunge, anataka kunonesha nguvu zake kabla hajatoka kwenye ulingo wa siasa mwaka 2014.&#8221;
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/24/malawi-president-seeking-more-power/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://www.malawipolitics.com/news.php?extend.251">Rais wa Malawi ataka nguvu zaidi!</a>: &#8220;rais wa Malawi Bingu wa Mutharika, ambaye chama chake kina wabunge wengi katika bunge, anataka kunonesha nguvu zake kabla hajatoka kwenye ulingo wa siasa mwaka 2014.&#8221;</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/malawi-rais-ataka-nguvu-zaidi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afya Duniani: Siku ya Vyoo Duniani Yatoa Harufu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 25 Nov 2009 10:46:39 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Brunei]]></category>
		<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Ethiopia]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[India]]></category>
		<category><![CDATA[Oman]]></category>
		<category><![CDATA[Science]]></category>
		<category><![CDATA[Singapore]]></category>
		<category><![CDATA[Thailand]]></category>
		<category><![CDATA[United Kingdom]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=731</guid>
		<description><![CDATA[Ingawa inaweza kusikika kama masihara, Siku ya Vyoo Duniani inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwaza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/19/global-health-world-toilet-day-raises-a-stink/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/1019110937_99be0d6df3_m.jpg" title="Tiled Toilet" class="alignright" width="180" height="240" /><br />
Ingawa inaweza kusikika kama vile masihara, <a href="http://www.worldtoiletday.com/">Siku ya Vyoo Duniani</a> inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwanza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.</p>
<p>Watu wanaweza kuwa wanaona aibu kuongea wazi kuhusu hili suala, lakini kila mmoja hujisaidia, kwenye choo au la. Siku ya Vyoo Duniani inasaidia watu kusherehekea umuhimu wa usafi na kuwaelimisha watu bilioni 2.5 ambao hawana vyoo na mfumo wa usafi wenye uhakika. Video hii iliyotengenezwa na asasi isiyo ya kibiashara WaterAid <a href="http://www.youtube.com/watch?v=-T2eH7zrDJg">inaonyesha</a> starehe ya kuwa na choo.</p>
<p>Kusherehekea kopo lako kunaweza kuonekana kama ujinga, lakini kutokuwa na kopo siyo tu kunaweza kukusababishia aibu, kukosa heshima na masuala mengine ya kiusalama, bali pia kunaweza kukusababishia magonjwa yanayoweza kuzuilika na hata kifo. Pale watu wanapokosa vyoo, wanalazimika kujisaidia mitaani kweupe, kwenye viwanja au vichochoroni. Matokeo? Uchafuzi wa maji ya kunywa na vyanzo vya chakula, jambo ambalo linapelekea hatari nyingi za kiafya. Ukosefu wa mfumo wa usafi ndiyo sababu kubwa ya maambukizi na huua <a href="http://worldtoiletday.com/about.html">watu milioni 1.8</a>, hasa watoto, kila mwaka. Hata nchi zenye vyoo vya kutosha huwa zinakabiliana na matatizo yanayotokana na vyoo vichafu vya umma mpaka utupaji majitaka unaoharibu njia za maji.</p>
<p>Vanilla, anayeblogu kwenye <em>Let&#39;s Look At It This Way</em> kutokea Singapore, <a href="http://whatsayyouvanilla.blogspot.com/2009/11/world-toilet-day.html">anasema</a> kuwa watu wanapaswa kutilia maanani vyoo:</p>
<blockquote><p> “ Ninajua kwamba hii ni mada chafu kwa watu wengi. Ni bahati mbaya kwamba hii mada bado ni ‘mwiko’ kuiongelea wazi na watu wengi hawana uelewa kuhusu ukubwa wa tatizo. Ninashindwa kuelewa ni kwa jinsi gain hii inaweza kuwa mada isiyo na maana wakati, kwa wastani, huwa tunakwenda chooni mara 2500 kwa mwaka, au mara 6-8 kwa siku. Wakati wa maisha yetu, hutumia muda wa miaka 3 vyooni.&#8221; </p></blockquote>
<p>Chini ya maandalizi ya asasi isiyo ya kibiashara <a href="http://worldtoiletday.com/wto.html">The World Toilet Organisation</a>, Siku ya Vyoo Duniani inasherehekewa dunia nzima kwa matukio mbalimbali. Ili kuuelimisha umma zaidi, wiki hii WaterAid <a href="http://wateraidnews.blogspot.com/2009/11/launch-of-new-iphone-application-brings.html">ilitangaza</a> uzinduzi wa zana mpya ya Kutafutia Vyoo nchini Uingereza ya simu za mkononi za iPhone. Zana hiyo ya bure inawasaidia Waingereza kutafuta choo cha umma kilicho karibu zaidi  wakati pia inawakumbusha jinsi walivyo na bahati ya kuwa na vyoo safi na salama. Tukio kubwa zaidi leo, linaloitwa <a href="http://worldtoiletday.com/squat/">Mchuchumao Mkubwa</a>, linawataka watu wasimame na wachuchumae kwa dakika moja katika sehemu za umma ili kuongeza utambuzi. <a href="http://www.flickr.com/groups/1216217@N24/">Picha</a> hizi zinaonyesha watu waliochuchumaa dunia nzima, pamoja <a href="http://www.flickr.com/photos/25532596@N04/4116769214/in/pool-1216217@N24">na hii ya</a> watoto wa chekechea huko Singapore:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/4116769214_1b876f8640.jpg" title="Singapore Squat" class="aligncenter" width="500" height="273" /></p>
<p>Blogu inayotokea Brunei, <em>the world according to panyaluru </em>…, pia <a href="http://panyaluru.blogspot.com/2009/11/cut-paste-toilets.html">inaonyesha kuridhika</a> na vyoo kwa kuliweka suala hili kwenye muktadha sawia:</p>
<blockquote><p> “Fikiria ikiwa tunatembea mbele ya mlolongo wa maduka kule Kiulap au Gadong. Mara tu tumbo linaunguruma kama vile ambavyo haujawahi kusikia. Halisimami kukupa mapumziko. Linaunguruma na kuunguruma. Ngurumo. Taa ni ya manjano tayari kubadilika kuwa ya kijani. Lakini hakuna vyoo unavyoviona. Hakuna hata choo kimoja cha umma kwenye mlolongo wa maduka… ongezea pia kuwa hakuna maji, karatasi ya chooni, hakuna chochote! Hiyo inaweza kuwa siku mbaya zaidi katika maisha yako, jinamizi baya, au jinamizi baya zaidi ya yale yaliyowakuta watoto kwenye filamu za Elm Street. Katika siku hii, hebu na tuvienzi vyoo.”</p></blockquote>
<p>Ukiachilia mbali upande makini wa suala hili, watu wengi wametumia mzaha kuadhimisha siku ya Vyoo Duniani. Huko Uingereza blogu ya <em>London City Drains</em> imeweka chemsha bongo ya vyoo yenye maswali 10, wakati katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=zx2oVPjnUXs">video</a> hii mwalimu wa sekondari Matt Cheplic anaimba kuhusu siku hii.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu wanasema kuwa vyoo pekee vinaweza visiwe jibu. Sandhya, anayeblogu kwenye <em>Maradhi Manni </em>nchini India, <a href="http://maradhimanni.blogspot.com/2009/11/big-squat-to-take-stand-on-sanitation.html">anasema</a> wanaume wengi hawatumii vyoo vilivyopo:</p>
<blockquote><p>Kwenye mji kama Chennai, ambako hali ya hewa ni ya joto kwa karibu miezi 10 ya mwaka, huwaona wanaume wanakojoakando ya barabara kila wakati. Wkati wanawake wanaweza kujidhibiti  na kwenda nyumbani kujisaidia, kwa nini wanaume hawawezi kufanya hivyo, sijui kwa nini. Kwa hiyo, kwanza watu wote wanabidi wapigwe faini kali kwa kufanya kosa hili (naam, ni kosa) pale pale wanapokamatwa. Nimewahi kuwaona wakifanya hivyo kwenye ukuta wa vyoo vya umma! Kule Srinagam, nimewahi kuwaona wakikojoa kwenye ukutra wa boma la hekalu pamoja na kuwa kila mtaa unaolizunguka hekalu una vyoo, ambavyo vilikuwa visafi, lakini vya kulipia!”</p></blockquote>
<p>Wakati ukosefu wa mfumo wa usafi unaathiri kila mtu, miiko inayozunguka suala la vyoo inawaathiri vikubwa wanawake zaidi ya  wengine. <a href="http://worldtoiletday.com/squat">Katika baadhi ya nchi</a>, staha huwalazimisha wanawake kufanya shughuli zao kwenye makonde kabla ya jua kuchomoza au kujizuia mpaka mpaka baada ya jua kuzama, jambo ambalo linasababisha madhara ya kiusalama na kiafya. Joanne Sprague, anayeblogu kwenye <em>Overturning Boulders</em> nchini India, <a href="http://overturningboulders.blogspot.com/2009/11/but-where-do-women-do-their-business.html">anabaini</a> kuwa wanawake hawapo kwenye mzunguko wa kwenda haja asubuhi mijini Chennai, wakati huko Ethiopia blogu ya <em>AN ADVENTURE IN ADDIS</em> <a href="http://anadventureinaddis.com/2009/11/17/world-toilet-day/">inabaini </a>hali kama hiyo pia:</p>
<blockquote><p>“Nimekuwa nikisikia mara nyingi juu ya ukosefu wa vyoo kwa wanawake au ukosefu wa vyoo kwa ujumla; kwamba wasichana wa rika la kuwa wali huko mashambani huamka saa 10 za alfajiri kwenda nje kwenye giza kufanya shughuli zao ili wasitaniwe na wavulana shuleni au huacha kwenda shule kabisa. Wanaume hukojoa kila mahali, sigara mkononi na kuna kuna dhana kuwa wanawake hawapaswi kufanya hivyo, kama wanafikiriwa hata kidogo… ninataka kuona bango kubwa kwa lugha ya Ki-Amhara linalosema “wasichana nendeni pia’ lenye picha ya mwanasesere anayevutia wa kike aliyeketi chooni.” </p></blockquote>
<p>Kusherehekea Siku ya Vyoo Duniani, mwanablogu Jonathan Stray, anawachukua wasomaji kwenda <a href="http://jonathanstray.com/world-toilet-day">ziara ya kimataifa ya vyoo </a>ambavyo ameshawahi kuvizuru, kuanzia Thailand na Uingereza mpaka Afrika Magharibi na Oman, na anahitimisha:</p>
<blockquote><p> “Sisi watu wa Magharibi na vyoo vyetu vya kuvuta na karatasi za chooni na chemchemi zinazong’ara ni tofauti na wengine wengi; wengine wote waliobaki hufikiri kuwa bafu ni sehemu iliyolowana, inayonuka, ikiwa wanayo hayo mabafu. Choo kizuri kinamaanisha kuwa pengine una kiwango kizuri cha maisha, kwa hiyo burudika na choo chako. Siku njema ya Vyoo Duniani!  </p></blockquote>
<p><em>Picha ya <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/1019110937/">choo cha vigae</a> imepigwa na <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/">nedrichards</a> kwenye Flickr, Haki Miliki Huru.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Somalia: Kuufahamisha mtandao wa waandishi na wanablogu wa Kisomali</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 24 Nov 2009 12:45:45 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Somalia]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=705</guid>
		<description><![CDATA[Kituo cha habari cha Somalia ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/somalia-introducing-a-network-of-somali-journalists-and-bloggers/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://somalimedia.ning.com/">Kituo cha habari cha Somalia</a> ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari. </p>
<blockquote><p>Kituo cha Habari cha Somalia ni jukwaa linalojitegemea kwa ajili ya waandishi wa Kisomali ndani na nje ya nchi hiyo. (Kituo hicho) kimeanzishwa kukuza wasifu wa waandishi werevu, na wachapa kazi waliyoyatoa maisha yao kuwatumiakia watu dunia nzima.<br />
Somalia imekuwa ikichukuliwa kama nchi iliyoshindwa, nchi inayohusishwa na vifo, mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yasiyoisha, vita, ugaidi na uharamia wa kisasa. Lakini moja wapo ya habari za mafanikio kwa miaka mingi imekuwa ni kukua kwa uhuru wa habari na maoni. Hata hivyo, kuupa kipaumbele na kuutangaza ukweli huja kwa gharama kubwa.</p>
<p>Kituo hicho huchapisha blogu za waandishi hawa. Pia, kituo kinatawanya habari na taarifa za waandishi wa habari. Kituo pia kinaratibu waandishi wa Kisomali na wale wasio Wasomali. Kinawapa waandishi wasio Wasomali wanaoweza kuwa wanasafiri kwenda Somalia ushauri na mawasiliano ya awali. Kituo pia kinafanya kazi na mashirika makubwa ya kimataifa ya habari kwa ushirikiano, kuzalisha na kujazia habari na taarifa kuhusu Somalia na eneo lote la Pembe ya Afrika. </p></blockquote>
<p>Solana Larsen anaandika kuhusu <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/the-new-somali-media-centre">asili ya Mradi wa Kituo cha Habari cha Somalia</a>:</p>
<blockquote><p>Kama haujahisi bado, mimi si Msomali. </p>
<p>Katika shule ya Uandishi wa Habari jijini London mwaka 2002 nilikuwa na mwanafunzi mwenzangu aitwaye Harun Hassan ambaye nilizoea kumuuliza maswali mengi kuhusu maisha yake  ya Mogadishu na Siasa za Somalia. Baada ya kuhitimu, tulibaki kuwa marafiki na nilimfahamisha kuhusu uwezekano wa yeye kuandikia mtandao wa openDemocracy.net ambapo nilikuwa mhariri kwa miaka michache. Baadaye, nikawa mhariri mtendaji wa Global Voices Online, ambapo mara chache tulikuwa na habari kuhusiana na wanablogu wa kiSomali. </p>
<p>Harun alizoea kuniambia kuhusu mawazo aliyokuwanayo kwa ajili ya Mradi wa Habari uliojumuisha jamii ya Kisomali mjini London. Alianzisha gazeti la Kisomali, na wakati fulani alinifuata nimsaidie kutengeneza tovuti kwa ajili ya kitu alichokiita Kituo cha Habari cha Somalia.</p>
<p>Habari za jamii ya KiSomali kwenye vyombo vya habari nchini Uingereza zilikuwa hasi na zisizo sahihi, Harun alifikiria kuwa namna pekee ya kusahihisha hilo,ilikuwa ni kuwarahisishia waandishi wa Uingereza kuwapata waandishi wa Kisomali na watafiti wa kuongea nao.</p>
<p>Tulitengeneza tovuti na blogu, lakini baadae kidogo tukakabiliwa na kazi nyingine na mradi ukadumaa.</p>
<p>Wavuti unayoipitia sasa, ni jaribio letu  lapili la kutengeneza nyenzo ya mtandao kwa ajili ya waandishi wa Kisomali na wengine kuitumia ili kusaidia kuboresha uwelewa wa kidunia wa Wasomali na Somalia yenyewe.</p></blockquote>
<p>Hapa chini ni baadhi ya makala za blogu za hivi karibuni kabisa kutoka kwenye Kituo cha Habari cha Somalia: </p>
<p>Katika makala yenye kichwa cha habari, <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/affair-to-remember">Uzinifu wa Kukumbuka</a>, Fathia Absie anaandika kuhusu kushitakiwa kwa Joshua Asisam mlinzi wa amani katika Somalia, kwa kujihusisha na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa Kisomali:</p>
<blockquote><p>Mahakama ya Kijeshi ya Kampala ilimhukumu Joshua Asisa kifungo cha mwaka mmoja na nusu jela. Bw. Asisa ambaye ni mwanachama wa walinzi wa amani wa AMASOM nchini Somalia alipatiaka na hatia ya kujuhusisha na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa Kisomali aitwaye Nimco Omar na kumpa ujauzito baada ya kumuoa kwa kumdanganya kuwa alikuwa Mwislamu.<br />
Habari hii ilitokea mwaka uliopita huko Mogadisho lakini hakuna aliyesikia mpaka mwanamke huyu mdogo alipokwenda Kampala na kumshitaki Bw. Asisa mahakamani kwa kumdanganya. Mohamed Abubakar Ahmed ambaye ni mwandishi aliyeiibua habari hiyo aliniambia kuwa aliipata habari hiyo baada ya kuwa imeripotiwa na magazeti ya Uganda. Baada ya hapo, Bw. Ahmed alijaribu kuonana na viongozi wa jamii ya Kisomali waishio Kampala na akaweza kukutana na msichana huyo. Aliniambia kuwa Bi. Omar alimwambia kuhusu habari hiyo na jinsi alivyokutana na Bw. Asisa ambaye ni daktari. Alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali binafsi kwa ajili ya jeshi la Uganda mjini Mogadisho.</p></blockquote>
<p>“<a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/in-the-spirit-of-spreading-the">kwa nia ya kutawanya neno..</a>,” anaandika Idil Osman: </p>
<blockquote><p>Mafunzo ya kijeshi yanayofanyika katika makambi ya wakimbizi wa Kisomali huko Dadaab, Kaskazini mashariki ya Kenya yamechochea kelele zinazochanganya wengi ndani na nje ya eneo. Hata hivyo ninashangazwa sana na msimamo wa serikali ya Kenya. Nilifanya ripoti ya uchunguzi katika suala hili mapema kazini ambapo waziri wa ulinzi wa Kenya alidai kwa msimamo kwamba Kenya haikutoa ruhusa kwa mafunzo haya kufanyika.<br />
Wakati huo huo mashahidi na wanaharakati wa haki za binadamu wanarekodi na kuweka kumbukumbu za ushahidi wa vijana hawa wanaowekwa  katika magari ya kijeshi ya Kenya na kusafirishwa kwa magari kwenda kwenye vyuo vya mafunzo ya Kijeshi vya Kenya.<br />
Wengi wa vijana hawa wanachukuliwa kwa kudanganywa na kuahidiwa mshahara mzuri pamoja na kazi inayoaminika kwenye miradi ya kijeshi ya Umoja wa Mataifa/Umoja wa Ulaya/Umoja wa Afrika..<br />
Kiukweli wanafunzwa kwenda na kupigana kwenye vita ile ile waliyoikimbia na kuwafanya wawe wakimbizi. Wengi wa wakimbizi hawa vijana wanaarifiwa kuwa chini ya umri unaotakikana na wamechukuliwa bila ridhaa ya wazazi wao.<br />
Imevunja haki zao za kimataifa za binadamu kama wakimbizi kwa mujibu wa tangazo la kwenye vyombo vya habari lilitolewa hivi karibuni na Shirika la Human Rights Watch, kwa sababu wakimbizi wanatakiwa kuwekwa kwenye mazingira ya kiraia. </p></blockquote>
<p>Solana anajadili suala la ‘chanzo kisichotaka kufahamika’ katika taarifa za vyombo vya habari vya Kimagharibi kwenye makala yake aliyoipa jina la “<a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/when-local-sources-go-unnamed">Wakati vyanzo vya mahali vinapochagua kutokuwa na jina</a>”</p>
<blockquote><p>nimechukua toleo la hivi karibuni la jarida la National Geographic Magazine kwa habari yao inayohusu ‘Somalia iliyovunjika’. Picha za Mogadishu zilizopigw ana Pascal Maitre ni nzuri, ingawa zinaonyesha uharibifu mkubwa. Na mwandishi, Robert Draper anatoa muhtasari wa haki na wenye mguso kuhusu historia tata. Pia anaziweka wazi changamoto za upashaji habari wa kigeni.  </p>
<p>Katika hali inayoacha maswali, mwandishi wa Kisomali Harun Hassan anatajwa kwa jina kwenye maelezo ya picha inayomwonyesha mlinzi wa barabarani mjini Mogadishu, lakini kwa kiwango ninachoona haionekani kwenye habari yenyewe. Kwa nini kuna ugumu wa kuweka wazi chanzo?  Kama Draper alihangaika kuwasiliana na kuvihoji vyanzo vya Habari vya Somalia, kwa nini asiwaeleze wasomaji wake habari hiyo?</p>
<p>Je, huu ndio uzoefu wa wandishi wa Kisomali wanaowasaidia waandishi wa Kimagharibi kuhabarisha? Ninatumainii wanachama wa Kituo cha Habri cha Somalia watasaida kutupa mwanga wa jinsi inavyokuwa kwenye sehemu hiyo ya timu inayotengeneza ripoti.  </p></blockquote>
<p>Unaweza kuona orodha ya wanachama waliopo wa Kituo hicho <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/members/">hapa</a>.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika: Haki za Wanawake</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-haki-za-wanawake/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-haki-za-wanawake/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 11:30:25 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=721</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Sokari anaandika kuhusu Toleo Maalum la Masuala ya Wanawake la Pambazuka linaloangalia miaka 15 iliyopita tangu mkutano au Jukwaa la Vitendo mjini Beijing pamoja na mustakabali wa haki za wanawake barani.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/22/africa-womens-rights-across-africa/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Sokari anaandika kuhusu <a href="http://www.blacklooks.org/2009/11/womens_rights_across_africa.html">Toleo Maalum la Masuala ya Wanawake la Pambazuka</a> linaloangalia miaka 15 iliyopita tangu mkutano au Jukwaa la Vitendo mjini Beijing pamoja na mustakabali wa haki za wanawake barani.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-haki-za-wanawake/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika Kusini: Kikaragosi Kiliochoathirika na VVU Kwenye Kipindi cha Sesame Chaelimisha Kuhusu Ukimwi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 10:38:13 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=696</guid>
		<description><![CDATA[Wakati kipindi cha watoto cha Mtaa wa Sesame (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/11/south-africa-sesame-streets-hiv-positive-muppet-raises-awareness/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Kami22.jpg" title="Kami" class="alignright" width="200" height="260" /><br />
Wakati kipindi cha watoto cha <a href="http://www.sesamestreet.org/home/">Mtaa wa Sesame</a> (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. </p>
<p>Wakati kipindi cha Sesame Street kinatazamwa katika zaidi ya <a href="http://www.sesameworkshop.org/newsandevents/sesameupdates/sesame_40thbirthday">nchi 140</a>, kila toleo huzungumzia masuala yanayotokea kwenye jamii husika na kwa kumtumia vikaragosi tofauti. <a href="http://muppet.wikia.com/wiki/Kami">Kami</a> mwenye rangi ya Njano-dhahabu alionekana kwa mara ya kwanza kwenye kipindi mwenza cha Sisame Street cha Afrika Kusini kinachoitwa <a href="http://www.schooltv.co.za/TakHome.htm">Takalani Sesame</a>, mwaka 2002 kujibu matatizo ya nchi yanayohusiana na UKIMWI. Kama kikaragosi cha kwanza duniani chenye VVU, kinasaidia kuwaelimisha watoto kuhusu ugonjwa na kushughulikia masuala yanayohusiana na kuwa mwathirika wa UKIMWI. Jina la Kami <a href="http://www.sesameworkshop.org/aroundtheworld/southafrica">linatoka</a> kwenye neno la kiSetswana “Kamogelo”, lenye maana ya “kukubalika.” Sunshinestar110, anayeblogu kwenye <em>U dont Like My Opinion&#8230;That’s Fine!</em> <a href="http://thatsfine2009.blogspot.com/2009/11/happy-birthday-to-you.html">anazungumzia zaidi</a> kuhusu Kami:</p>
<blockquote><p>“Kami ni mwathirika wa VVU mwenye afya, yatima wa miaka mitano mwenye bashasha ambaye ana aibu kidogo lakini huchangamka akijongelewa kwa njia ya kirafiki, pia anajua mengi kuhusu Virusi vya UKIMWI, alimpoteza mama yake kwa ugonjwa huo. Kami alipozinduliwa, akiwa na nywele zake za kahawia na pia alivaa fulana, na kutembea kwenye mtaa wa Susame na kujiuliza huku akihofu kama wenyeji watataka kucheza nae. Hakuwa na haja ya kuogopa kwa sababu vikaragosi vingine vilimpokea kwa bashasha”</p></blockquote>
<p>Kami aliletwa kuwasaidia watoto wengi wa Afrika Kusini wanaotaabika na janga la VVU/UKIMWI. Inaaminika kuwa Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya watu walio na VVU duniani – inakadiriwa kuwa watu <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">milioni 5.7</a> Kwa makadirio, kati ya walioathirikia, 280,000 ni watoto wa umri wa miaka chini ya 14 na kuna yatima milioni 1.4 nchini kutokana na UKIMWI. Zaidi ya madhara ya kimwili ya kuwa na VVU, vilevile kuna unyanyapaa na miiko inayotokana na kuwa na ugonjwa, ambayo husababisha ugumu kwa watu kupata matibabu stahiki na msaada. Takalani Sesame, ambayo inajumuisha lugha zote rasmi 11 za Afrika Kusini, inajaribu kuwasaidia watoto kuyatazama masuala haya kwa ujasiri kupitia Kami.</p>
<p>Hata hivyo, kulikuwa na mkanganyiko wakati Kami alipoanza kuonyeshwa, hasa hasa nchini Marekani, ambapo wengi walikasirishwa na kuwa kipindi cha watoto kinanamchezesha mhusika mwenye VVU. <em>Haven on Earth</em> <a href="http://haven-on-earth.spaces.live.com/blog/cns!C13DE188EF218F14!382.entry?sa=500695506">anafafanua</a> mjadala huo:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ilitaarifiwa kuwa ujio wa Kami kwenye kipindi cha Sesame Street nchini Afrika Kusini ulikuwa unakaribishwa.(Nina wakati mgumu kukubaliana na ukweli huu kwa sababu kiwango kikubwa cha kukataa bado kipo), kulikuwa na mkanganyiko ulio wazi hapa Marekani. Ninakumbuka kusoma kuhusu suala hili (hii ni sababu ya mimi kufurahia kukutana na kipindi kikirushwa kutokea Afrika Kusini – nisingelifikiria kukitafuta). Iliondokea kuwa kundi la wabunge wa Congress wa chama cha Republican walituma barua kwa Rais wa Shirika la Utangazaji la Umma (PBS) linalorusha kipindi cha Sesame Street. Barua ilidai kwamba mipango ya kuleta mhusika kama huyo ambaye ni mwathirika wa UKIMWI nchini Marekani haikuwa sahihi, kwa kuzingatia umri wa watazamaji. Walipendekeza kwamba hatua hiyo ingeathiri ufadhili wa umma kwa Shirika hilo (PBS).”</p></blockquote>
<p>Kami hajawahi kuonekana kwenye kipindi cha Sesame Stree cha Marekani, ingawa amedhihirisha kuwa mhusika aliyefanikiwa sana kwenye kipindi cha Takalani Sesame na zaidi. Mwaka 2003, UNICEF <a href="http://www.unicef.org/media/media_16631.html">ilimteua</a> kuwa “Shujaa wa Watoto” duniani. Katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=9eXlNn-C8BY">video</a> hii, anaungana na Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton kutoa ujumbe kuhusu VVU/UKIMWI. Jamie, anayeblogu kwenye <em>No day but Today</em>&#8230;, <a href="http://phaino.blogspot.com/2006/12/world-according-to-sesame-street.html">anajadili</a> mafanikio mengine ya Kami:</p>
<blockquote><p> “Kwa sababu watoto wengi wa Afrika Kusini wanamfahamu mtu fulani mwenye UKIMWI, mhusika huyo amekuwa shujaa wa taifa, anayependwa na watu wa nchi hiyo. Kami ameonekana kwenye Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia na alihojiwa na Katie Couric. Ameteuliwa kuwa balozi wa UNICEF wa watoto na ameonekana kwenye vipande vya onyesho la Takalami pembeni mwa Desmond Tutu na Nelson Mandela.”</p></blockquote>
<p>Pamoja na mafanikio ya Kami, wanablogu wengine bado wanaamini kuwa si mhusika sahihi kwa toleo la Kimarekani la Sesame Street. Emily Meyer, anayeblogu kwa ajili ya darasa lake la heshima, <a href="http://hons101fall09eem.blogspot.com/2009/10/kami-hiv-muppet.html">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ni muhimu kwa Wamerekani kufahamu kuhusu VVU/UKIMWI na hatari ya ugonjwa wenyewe, nadhani kuwafundisha watoto katika umri wa miaka miwili na mitatu ni kwenda mbali sana. Watoto wadogo kiasi hiki hawataweza kuelewa kuhusu VVU na hawataelewa madhara yake. Kama Kami alitakiwa aletwe Marekani kama njia kueneza elimu na kudhibiti UKIMWI, sidhani kama matokeo yaliyokusudiwa yangetokea&#8230;Watoto nchini Marekani hawalazimishwi kuhusika na masuala ya UKIMWI katika umri huo mdogo. Nadhani wakati sahihi kwa watoto nchini Marekani kujifunza kuhusu hatari ya virusi vya UKIMWI ni wanapokuwa wakubwa, kadri ya miaka kumi ama kumi na moja au wakati mwanafunzi anapoanza kujihusisha na vitendo vya mapenzi kimwili”</p></blockquote>
<p>Bado, wanablogu wengi, kama huyu hapa <a href="http://beckyluz.wordpress.com/2008/12/16/kami-the-hiv-positive-muppet/">anayeandika kwenye</a> <em>Muppets and History</em>, anamwona Kami kama mfano mwingine wa namna Sesame Street inavyosukuma mipaka. Wengine <a href="http://joburgjoblog.blogspot.com/2006/03/celebrating-aids-research.html">wanaonyesha upendo</a> wao kwa kikaragosi huyo na ujumbe anaowaletea watoto. Na wengine wanadhani anatakiwa atumike kwenye matoleo mengine ya Sesame Street. Katika blogu yake binafsi, Steisha Pintado <a href="http://steishapintado.wordpress.com/2008/12/18/final-grades-kami/">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Anawaonyesha watoto kwamba ni sawa kumkumbatia mtu mwenye virusi vya UKIMWI, na anaeleza nini cha kufanya anapokuwa na kidonda kwenye kidole chake au kama umejikata mwenyewe. Anaifundisha hadhira ya watoto wadogo kuhusu kukabiliana na kuumwa na kupotelewa&#8230;.Ingawa ngono huwa haitajwi kamwe katika kuzungumzia hali ya Kami, watu wengine wamesema kuwa kuwepo kwa mhusika mwenye virusi vya UKIMWI lisingekuwa jambo sahihi kwa hadhira ya watazamaji wadogo. Mbunge mmoja hata alidai kuwa Warsha ya Sesame ingepoteza msaada wa kifedha kutoka serikalini kama ingerusha kipindi chenye mhusika huyo kwenye nchi yetu. Inashangaza kusikia maneno haya. Wazazi wanatumia muda mfupi (na unaopungua kila siku) na watoto wao, na wanaruhusu runinga kuwaelimisha zaidi na zaidi. Ni wazi wazazi wengi hawawafundishi watoto wao namna ya kuyakabili masuala nyeti  ya uelewa na kukubalika. Wazazi tayari wamewaruhusu Warsha ya Sesame kuingiza suala la kukubalika kwa wale wenye ulemavu na kuugua, na pia kwa wale wenye rangi na dini tofauti. Je, hii ina tofauti gani? </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Azerbaijan: Baada ya Hukumu ya Wanablogu wa Video</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/azerbaijan-baada-ya-hukumu-ya-wanablogu-wa-video/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/azerbaijan-baada-ya-hukumu-ya-wanablogu-wa-video/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 10:21:01 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Azerbaijan]]></category>
		<category><![CDATA[Blogger News]]></category>
		<category><![CDATA[Central Asia & Caucasus]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=694</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naOnnik Krikorian  &#183; Imetafsiriwa na Christian Bwaya &#183;  Angalia ujumbe mama 

Siku chache baada ya hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa  sauti juu ya kifungo cha Adnan Hajizade na Emin Milli. Wanaharakati hawa wa mtandaoni watatumikia vifungo vya miaka miwili [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/onnik-krikorian/">Onnik Krikorian</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/more-reaction-to-blogger-trial-verdict/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/hands_off12.jpg" class="alignleft" width="177" height="187" /><br />
Siku chache baada ya <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/11/azerbaijan-bloggers-sentenced/">hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video</a> huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa  sauti juu ya kifungo cha <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/blogger/adnan-hajizada">Adnan Hajizade </a>na <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/blogger/emin-milli">Emin Milli</a>. Wanaharakati hawa wa mtandaoni watatumikia vifungo vya miaka miwili na mwingine miaka miwili na nusu gerezani baada ya mashitaka ambayo wengi wanayaona kama yenye nguvu za kisiasa na ni katika kujaribu kuwanyamazisha wasemaji kwenye nchi hiyo.</p>
<p>Wanaungana na wengine kama <a href="http://www.se2009.eu/en/meetings_news/2009/11/12/presidency_statement_on_azerbaijan">Urais wa Jumuiya ya Ulaya</a>, <a href="https://wcd.coe.int//ViewDoc.jsp?Ref=PR839%282009%29&#038;Language=lanEnglish&#038;Ver=original&#038;BackColorInternet=F5CA75&#038;BackColorIntranet=F5CA75&#038;BackColorLogged=A9BACE">Baraza la Bunge la Ulaya</a>, <a href="http://www.osce.org/item/41288.html">Shirika la Usalama na Ushirika la Ulaya</a>, Shirika la kupingania Haki za Binadamu la <a href="http://www.hrw.org/en/news/2009/11/12/azerbaijan-young-bloggers-jailed">Human Rights Watch</a>, <a href="http://www.amnesty.org/en/library/asset/EUR55/009/2009/en/655ee814-8957-4c08-b4f3-16772a16d9c2/eur550092009en.html">Amnesty International </a>na <a href="http://www.rsf.org/spip.php?page=article&#038;id_article=34972">Waandishi wasio na mipaka </a>na wengine wengi wanaoishutumu hukumu hiyo.</p>
<p>Shirika la Amnesty International vilevile <a href="http://www.amnesty.org/en/library/asset/EUR55/009/2009/en/655ee814-8957-4c08-b4f3-16772a16d9c2/eur550092009en.html">limewatangaza vijana hao wawili kama wafungwa wa dhamira</a>. <em>Interesing times</em>, “mradi wa mtandaoni unaofuatilia jitihada  za kudhibiti na kuzuia upatikanaji huru wa mtandao duniani kote,” <a href="http://www.i-times.org/interesting_times/2009/11/azerbaijans-government-intensifies-its-war-on-free-expression.html">waliyaweka mashtaka katika muktadha</a>. </p>
<blockquote><p>matumizi ya mabavu ya hivi karibuni yaliyoonyeshwa na nguvu za dola nchini Azerbaijan hayaachi shaka yoyote kwamba wote, waandishi na wanablogu wanatumia haki yao ya kujieleza kwa uhuru ilhali wanajua hatari inayowakabili. </p>
<p> […]</p>
<p>Shukrani kwa shinikizo la kimataifa kama vile barua ya WPFC na nyingine nyingi,  serikali ya Azeri imelazimishwa kuwatoa waandishi hao gerezani.</p>
<p>Lakini kitendo hiki cha hivi karibuni cha uonevu dhidi ya wanablogu wawili hakiachi tena wasiwasi kwamba, kama wakiachwa wenyewe, maafisa wa serikali wa Azerbaijan wataendelea na njia zao za kinyanyasaji.</p></blockquote>
<p><em>Notes from Abroad</em> naye pia <a href="http://gedirem.blogspot.com/2009/11/long-prison-sentences-for-two-azeri.html">hashangazwi na hukumu  hiyo</a>:</p>
<blockquote><p>Jumanne, wanablogu wawili vijana walihukumiwa kifungo jela –mmoja kwa miaka miwili na nusu, na mwingine kwa maika miwili– kwa mashitaka ya kipuuzi ya uhuni. Suala zima ni aibu –likiendeshwa na malengo ya kisiasa, lakini haishangazi.</p>
<p>[…]</p>
<p>Kwa kuwa Azerbaijan ni utawala wenye utajiri mkubwa wa mafuta, nchi za Magharibi zimekuwa makini mno katika majibu yake kwa kitendo hiki kisichokuwa cha kidemokrasia kilichofanywa na serikali ya Azeri.</p>
<p>Serikali ya Azeri ni lazima ikemewe kwa nguvu zote na nchi zote za demokrasia duniani kwamba tabia ya aina hii hikubaliki.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu <em>The Blogar</em>, hata hivyo, <a href="http://theblogar.blogspot.com/2009/11/emin-and-adnan-in-prison.html">anakaribia kukosa maneno</a>:</p>
<blockquote><p>Kwa hiyo hukumu imetolewa.<br />
Emin na Adnan sasa ni rasmi kwamba ni ‘wahuni’.<br />
Ninakosa cha kusema hapa.<br />
Kama inavosemekana kuwa vyombo vya habari vya jamii vilihusika katika kuwatia ndani, vilihusika na kueneza habari mitaani kuhusu uvunjifu wa haki lakini havikuweza kubadili akili za mfumo wa sheria uliooza wa Azerbaijan.<br />
Usicheze na Ilham.</p>
<p> […] Mawazo yangu yako na fanilia zao pamoja na wao wenyewe.</p></blockquote>
<p>Hata hivyo, kukiwa na rufaa inayokaribia kukatwa na uwezekano wa hatua zitakazochukuliwa na Mahamakama ya Haki za Binadamu ya Ulaya, <em>L4L</em>, blogu mpya ya lugha ya Kiingereza ya Azeri, <a href="http://sympathy4thedevil.wordpress.com/2009/11/13/beginning/">inasema kwamba huu ni mwanzo tu</a>:</p>
<blockquote><p>Nini cha kufanya baada ya hapa? Awali ya yote tusikome. Tuendelee kufanya kazi kuelekea uhuru wa marafiki zetu na kuelekea kwenye uhuru wa raia wote wa Azerbaijan [&#8230;] Adnan na Emin hawakuonyesha woga na sisi hatupaswi kuwa chochote chini ya majasiri na wenye kutia moyo.</p>
<p>[…]</p>
<p>Huu hauwezi kuwa mwisho. Vyote vinaanza sasa.</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/parvana.jpg" class="aligncenter" width="440" height="294" /><br />
<em>Parvana Persiani na David Sasaki wa Jukwaa la Dunia la kublogu la Global Voices on lin, Bucharest, Romania © Onnik Krikorian / Oneworld Multimedia 2009</em></p>
<p>Wakati huo huo, kwenye pembe za Kongamano la Dunia la Kublogu mjini Bucharest, Romania, <em>Global Voices Online</em> ilifanya mahojiano yaliyoshindikana na Parvana Persiani, Mjumbe wa Heshima wa Bodi ya OL! Vuguvugu la vijana wa Azerbaijani ambalo rafiki yake wa kiume, Adnan Hajizade aliyefungwa sasa, ni mshiriki mwanzilishi.</p>
<p><object width="720" height="450"><param name="movie" value="http://dotsub.com/static/players/portalplayer.swf?plugins=dotsub&#038;uuid=4fe42f66-8f9b-42f3-85de-69e92c748374&#038;type=video&#038;lang=none"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowscriptaccess" value="always"></param><embed src="http://dotsub.com/static/players/portalplayer.swf?plugins=dotsub&#038;uuid=4fe42f66-8f9b-42f3-85de-69e92c748374&#038;type=video&#038;lang=none" type="application/x-shockwave-flash" allowscriptaccess="always" allowfullscreen="true" width="420" height="347"></embed></object></p>
<p>Habari mpya zitakuwa zilitundikwa kila zikipatikana. Wakati huo huo, habari kamili ya kukamatwa,  mashitaka na kufungwa kwa Adnan Hajizade na Emin Milli zinapatikana kwenye <a href="http://globalvoicesonline.org/-/world/central-asia-caucasus/azerbaijan/">sehemu ya Azerbaijan </a>ya <em>Global Voices Online </em>na kwenye blogu ya OL! (Kwa <a href="http://ol-en.blogspot.com/">Kiingereza</a> na <a href="http://ol-az.blogspot.com/">Kiazeri</a>). Alama ya <a href="http://twitter.com/#search?q=%23EminAdnan">#EminAdnan </a>pia inatumika kwenye Twitter.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/emin_adnan_poster.jpg" class="aligncenter" width="440" height="570" /><br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/poster.jpg" title="poster" class="aligncenter" width="440" height="525" /></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/azerbaijan-baada-ya-hukumu-ya-wanablogu-wa-video/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>China: Obama ni Mshabiki Mkubwa wa Kutokuchuja Habari</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 17 Nov 2009 10:06:54 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[China]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=690</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naOiwan Lam  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa &#8220;Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari&#8220;.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/oiwan/">Oiwan Lam</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/17/china-obama-as-a-big-supporter-of-non-censorship/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa &#8220;<a href="http://shanghaiscrap.com/?p=3920">Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari</a>&#8220;.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Karibea: Tuzo za Fasihi ya Kifaransa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/karibea-tuzo-za-fasihi-ya-kifaransa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/karibea-tuzo-za-fasihi-ya-kifaransa/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 12:20:17 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Canada]]></category>
		<category><![CDATA[Diaspora]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[France]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Guadeloupe]]></category>
		<category><![CDATA[Haiti]]></category>
		<category><![CDATA[Language]]></category>
		<category><![CDATA[Literature]]></category>
		<category><![CDATA[Martinique]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Senegal]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=680</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naFabienne Flessel  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/fabienne-flessel/">Fabienne Flessel</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/06/caribbean-french-literary-prizes/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, <a href="http://www.alterpresse.org/spip.php?article8952">katika makala hii kutoka Haiti</a>, na <a href="http://indiscretions.over-blog.fr/article-le-goncourt-pour-marie-n-diaye-04-11-09-38785480-comments.html#comment50651606">hii kutoka Guadeloupe</a> na <a href="http://www.montraykreyol.org/spip.php?article3183">hii kutoka Martinique</a> [Fr]. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/karibea-tuzo-za-fasihi-ya-kifaransa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
