Habari kuhusu Kiingereza kutoka Februari, 2013
Mgomo wa Nchi Nzima Wamshitua Rais wa Malawi
Rais wa Malawi Joyce Banda atupilia mbali shinikizo la kujiuzulu mara baada ya mamia ya maelfu ya wafanyakazi wa umma kuandamana kwa wiki mbili kuishinikiza serikali kuongeza mishahara, hali iliyopelekea kufungwa kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Malawi na kusababisha hali ya taharuki mahospitalini na mashuleni.
Uhuru wa Vyombo vya Habari Nchini Myanmar Bado ni Giza
Uamuzi wa Myanmar wa kuivunja bodi katili ya ukaguzi ilisifiwa na makundi mbalimbali ya watu kama njia ya kuelekea kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini humo. Lakini, waangalizi wa uhuru wa vyombo vya habari waliainisha vitisho na mashambulio wanayokabiliana nayo waandishi wa habari wanaoishi nchini Myanmar.
Vurugu Zinazofadhiliwa na Serikali Nchini Angola
Mwanablogu Claudio Silva anaandika kwenye makala yake Africa Ni Nchi kwamba mtazamo wa kina juu ya vurugu zinazofadhiliwa na serikali (kufukuzwa watu mijini na kupigwa kwa waandamanaji) unahitajika ili kuelewa video mbili zilizosambaa sana mtandaoni na kuleta sintofahamu kubwa nchini (tazama habari maalumu za Global Voices). Anaandika “vurugu za Angola...
Bangladeshi: Raia Wakutana Kudai Haki Itendeke
Kidogo kidogo, makutano ya Shahbag katika mji mkuu wa Bangladesh, Dhaka yamefurika watu wenye lengo la kutaka haki kufuatia ukatili uliofanywa mnamo mwaka 1971 wakati wa harakati za vita vya kutafuta uhuru pamoja na kudai hukumu ya kifo kwa wahalifu wa vita.Drop by drop, the Shahbag intersection in Bangladesh's capital city Dhaka has become an ocean of people, demanding justice for the atrocities committed during the country's 1971 liberation war and death penalty for war criminals.
Wakati Papa Anajiuzulu, Warusi Wajiuzulu kwa Putin
Pasipokutaka kujua matokeo ya kujiuzulu kwa Papa Benedict na athari yake kwa imani ya Kikatoliki au tafsiri ya hatua hiyo kufuatia kashfa ya udhalilishaji iliyowakabili kwa watawa, RuNet walioweka habari hiyo kwenye safu za vichekesho.
Costa Rica Yakumbwa na Tetemeko la Ardhi wa Ukubwa wa 7.6
Wananchi wa Costa Rica wamekuwa wakitwiti kuhusiana na tetemeko la ardhi lililoikumba nchi hiyo tarehe 5 Septemba saa 2:42 asubuhi, kwa kutumia alama habari #temblorcr and #terremotocr kuhabarishana yanayoendelea.
Hali ya Hatari kwa Watoto nchini Syria: Namna Utakavyo Saidia.
Hadi sasa,inakadiriwa watoto 4,355 wameshauawa katika mgogoro unaoendelea hivi sasa nchini Syria. Mapema wiki hii, tulitoa taarifa juu ya madhila wanayokabiliana nayo watoto wa Syria kufuatia vita hii inayoisambaratisha nchi yao vipande vipande. Leo tunaangalia namna ambavyo watu wanaweza kusaidia kukabiliana na baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo.
PICHA: Maandamano ya Pamoja ya Watu wa Shia Nchini kote Pakistan Yamalizika Kwa Amani.
Baada ya milipuko ya mabomu huko Quetta kuua zaidi ya watu 100, maanadamano ya watu wa jamii ya Hazara ya Shia yalisambaa kama moto katika maeneo mbalimbali ya Pakistani. Watu kutoka katika makundi makuu ya dini na makabila mbalimbali waliungana kwa pamoja na watu wa Hazara wakiimba kwa kurudiarudia#Sisi sote ni watu wa Hazara. Maandamano ya kuishinikiza serikali kusikiliza madai yao yalianzishwa katika zaidi ya majiji 100 na miji.
Blogu 10 Bora za Mapishi ya ki-Afrika
MyWeku anatengeneza orodha ya Blogu 10 bora za Mapishiya ki- Afrika kwa mwaka 2013: “Inaonekana kuna blogu milioni moja zinazozungumzia mapishi, lakini ni chache sana zinazoonyesha vyakula vya Kiafrika. Pamoja na hayo imekuwa kazi ngumu kuchagua 10 kati ya nyingi nzuri kwa mwaka huu 2013.”