Habari kuhusu Kiingereza kutoka Novemba, 2012
Mkanganyiko wa Makubaliano ya OIC Kuanzisha Ofisi Nchini Myanmar
Shirika la Ushirikiano wa Kiislam (OIC) limependekeza kuanzisha ofisi nchini Myanmar kwa lengo la kukisaidia kikundi kidogo cha Waislamu nchini humo. Serikali ilishakubaliana na mpango huu lakini ilibadili uamuzi huu mara baada ya kutokea maandamano ya kupinga uamuzi huo katika maeneo mengi ya nchi.
Uharibifu Nchini Syria Katika Picha
Wapiga picha wa Syria wanatumia mitandao ya kijamii kuweka taswira ya uharibifu katika maeneo mbalimbali na kwenye mitaa. Pamoja na ufinyu wa vitendea kazi vya utoaji wa habari, habari zinazotoka Syria zinaonesha hali ya kutisha ya uharibifu inayoikabili nchi ya Syria.
Maelfu Watia Saini Pendekezo la Zawadi ya Nobel na Kusherehekea Siku ya Malala
Mwanaharakati wa elimu mwenye umri wa miaka 15 -- Malala Yousufzai -- aliyepigwa risasi mnamo tarehe 9 Oktoba 2012 na wanamgambo wa TTP, anaendelea kupata nafuu japo polepole. Mnamo tarehe 10 Novemba, watu kote ulimwenguni walimpongeza Malala kama kielelezo kwa ajili ya wasichana wapatao milioni 32 ambao hawapati fursa ya kwenda shulen.