Habari kuhusu Kiingereza kutoka Julai, 2010
Niger: Njaa ya Kimya Kimya
Janga la njaa ambalo kwa kiasi kikubwa haliripotiwi ipasavyo huko Sahel limechukua sura kubwa ya kutisha kufuatia kiasi cha watu milioni 2.5 nchini Naija hivi sasa kuathirika na uhaba wa chakula. Wanablogu nchini Naija wanatafakari janga jingine la chakula baada ya lile la mwaka 2005.
Thailand: Vurugu Zinazotokana na Ujumbe Mfupi wa Maneno wa Waziri Mkuu
Wakati Waziri mkuu wa Thailand Abhisit Vejjajiva alipotwaa madaraka mwaka 2008, alituma ujumbe mfupi wa maneno kwa mamilioni ya wateja wa simu za viganjani wa Thailand akiwataka wawe na umoja. Hivi sasa anakabiliwa na makosa ya ufisadi kwa kupokea "zawadi" kutoka mashirika ya mawasiliano. Kadhalika anashutumiwa kwa kuvunja mipaka ya ya faragha za wateja wa simu za viganjani.
Asia ya Kusini Mashariki : Ngono na Udhibiti wa Mtandao
Uratibu wa maudhui katika intaneti unaonekana kana kwamba ni kinyume na demokrasia lakini serikali za Kusini Mashariki mwa Asia zinaweza kuhalalisha kitendo hicho kwa kuzusha haja ya kuwaokoa vijana kutoka kwenye janga la tabia za ngono holela.
Rwanda: Wanaomuunga Mkono wa Paul Kagame Wabaini Nguvu ya Twitter, Facebook na Blogu
Waungaji mkono wa rais Paul Kagame wa Rwanda wameanza kutumia nguvu ya ushawishi ya Facebook, Twitter na blogu ili kumsaidia kushinda uchaguzi wa rais unaotarajiwa kufanyika tarehe 9 Agosti 2010.
Afrika ya Kusini: Dakika 67 za Mabadikio – Siku ya Mandela
Nelson Mandela alitumikia kifungo cha miaka 27 jela kule katika Kisiwa cha Robben, Afrika Kusini. Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba Madiba (kama ambavyo wengi wanapenda kumwita huko Afrika ya Kusini) alitumia miaka 67 ya maisha yake katika kupiga vita ubaguzi wa rangi na umaskini. Jumapili hii Julai 18 2010, kutakuwa na maadhimisho ya miaka yake 92 - na pia Siku ya Mandela - siku ambayo watu duniani kote watajitolea dakika 67 ili kuifanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi kwa wote.
Ghana: Je Una Chumba cha Ziada kwa Ajili ya Rais wa Zamani Rawlings?
Rais wa zamani wa Ghana Jerry Rawlings hana pa kuishi. Anahitaji nyumba ya kupanga katika mji mkuu wa Ghana Accra. yafuatayo ni maoni ya wanablogu wa Ghana pamoja na wasomaji wao.
Cameroon: Vyombo vya Habari Vyachochea Demokrasia
Célestin Lingo anaonyesha uhusiano kati ya vyombo vya habari na mchakato wa demokrasi nchini Cameroon.
China: Kashfa ya Wizi wa Kitaaluma Uliofanywa na Wang Hui, Mtazamo wa Kimataifa
Kuna kashfa ya wizi wa kitaaluma iliyoibuka mwezi Machi katika duru za kitaaluma za Kichina pale Profesa wa Fasihi wa Chuo Kikuu cha Nanjing, Wang Binbin, alipotuhumu kwamba kazi ya uzamizi ya Wang Hui kuhusu Lu Xun – Kugomea Kukata Tamaa – ina aya kadhaa ambavyo vimenukuliwa moja kwa moja...
Uganda: Wanablogu Washtushwa na Milipuko ya Mabomu
Mashabiki wa soka kote ulimwenguni walikusanyika kwenye kumbi za baa na migahawa ili kushuhudia mechi ya fainali za Kombe la Dunia usiku wa Jumapili iliyopita. Nchini uganda usherehekeaji huu ulikatishwa pale milipuko ya mabomu iliposambaratisha maeneo mawili maarufu kwa sherehe za mpaka majogoo jijini Kampala, mji mkuu wa nchi hiyo.
Naijeria: Nani Amemfanya Rais Abadili Msimamo — Facebook au FIFA?
Baada ya kupokea mamia ya maoni kwenye ukurasa wake wa Facebook page, Rais wa Naijeria alibadili uamuzi wake tata wa kuifungia timu ya taifa ya nchi hiyo. Lakini je ni kweli kwamba kubadilika huku kwa moyo wa Jonathan kulitokana na maoni ya raia waliopaaza sauti zao zenye hasira katika Facebook? Au ulitokana na msukumo wa shirikisho lenye nguvu la mpira wa miguu?