Habari kuhusu Kiingereza kutoka Novemba, 2009
Malawi: Rais Ataka Nguvu Zaidi
Rais wa Malawi ataka nguvu zaidi!: “rais wa Malawi Bingu wa Mutharika, ambaye chama chake kina wabunge wengi katika bunge, anataka kunonesha nguvu zake kabla hajatoka kwenye ulingo wa siasa mwaka 2014.”
Afya Duniani: Siku ya Vyoo Duniani Yatoa Harufu
Ingawa inaweza kusikika kama masihara, Siku ya Vyoo Duniani inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwaza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.
Somalia: Kuufahamisha mtandao wa waandishi na wanablogu wa Kisomali
Kituo cha habari cha Somalia ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari.
Afrika: Haki za Wanawake
Sokari anaandika kuhusu Toleo Maalum la Masuala ya Wanawake la Pambazuka linaloangalia miaka 15 iliyopita tangu mkutano au Jukwaa la Vitendo mjini Beijing pamoja na mustakabali wa haki za wanawake barani.
Afrika Kusini: Kikaragosi Kiliochoathirika na VVU Kwenye Kipindi cha Sesame Chaelimisha Kuhusu Ukimwi
Wakati kipindi cha watoto cha Mtaa wa Sesame (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI.
Azerbaijan: Baada ya Hukumu ya Wanablogu wa Video
Siku chache baada ya hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa sauti juu ya kifungo cha Adnan Hajizade na Emin Milli. Wanaharakati hawa wa mtandaoni watatumikia vifungo vya miaka miwili na mwingine miaka miwili na nusu gerezani baada ya mashitaka ambayo...
China: Obama ni Mshabiki Mkubwa wa Kutokuchuja Habari
Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa “Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari“.
Karibea: Tuzo za Fasihi ya Kifaransa
Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, katika makala hii kutoka Haiti, na hii kutoka Guadeloupe na hii...
Finland: Suala la Lugha
Nordic Voices anaandika kuhusu ‘suala la lugha” huko Finland.
Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini
Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens, ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.