Habari kuhusu Kiingereza kutoka Oktoba, 2009
Caribbean: Tafakari Mpya Kuhusu Uchapishaji wa Mtandaoni
Wanablogu wa ukanda wa Karibea wanawaza kuanzisha jumuiya ya uandishi na uchapishaji ya mtandaoni ikitumia njia za mawasiliano zilizo shirikishi ili kukabiliana na ugumu wa uchapishaji vitabu unaoukabili ukanda wao.
Haiti, Jamhuri ya Dominica: Hali Mbaya Yaongezeka
Repeating Islands anaripoti kuhusu mauaji ya Wahaiti wanne katika Jamhuri ya Dominica
Palestina: IDF Yachoma Moto Magari Ya Wapalestina
Kwenye Do Unto Others, Samuel Nichols anaandika kuwa doria ya jeshi la Israel imeanza kuchoma moto magari ambayo yanakamatwa yakijaribu kuvuka mpaka kutoka Ukanda wa Magharibikuingia Israel. Ametundika video hapa.
Malayasia: Serikali ya Jimbo Yaja na Sera ya ‘Msala Mmoja’
Kwa kuiga chapa ya Malaysia1, serikali ya Jimbo la Terengganu hivi majuzi ilikuja na sera ya ‘msala 1’ kama hatua kwa walimu na wanafunzi (wa jinsia moja) kuchangia misala (vyoo) ili kukuza hisia za umoja. Kumekuwepo na maoni mchanganyiko katika ulimwengu wa blogu kuhusiana na sera hii.
Misri: Watawala Wa Kiimla na Wake Zao
Baada ya kuziangalia picha za mke wa Rais wa Cameroon, Mmisri Zeinobia anasema: “Sijui ni ni kiasi gani cha pesa alichotumia kwa ajili ya nywele zake na muonekano wake lakini ninafahamu kuwa watu wa Camerron wanazihitaji zaidi hizo pesa.”
Trinidad & Tobago: Kampeni ya 350
“Trinidad na Tobago ni kisiwa tajiri na nchi inayoendelea tajiri kwa mafuta na gesi asilia. Lakini pia tunashuhudia madhara mabaya ya maendeleo ya haraka kwenye nyanja za viwanda katika visiwa vyetu. Hii ni fursa ya sauti za wanawake kusikika”: Attillah Springer anajihusisha na kampeni ya hali ya hewa 350.
Cambodia: Tuzo yamuenzi aliyenusurika na utumwa wa ngono
Sina Vann alikuwa na umri wa miaka 13 wakati alikupoja Cambodia kutoka Vietnam kwa kile kilichopaswa kuwa likizo. Badala yake, aliuzwa kama mtumwa kwa ajili ya ngono na alitumia miaka miwili iliyofuata ndani ya danguro. Alikombolewa wakati Somaly Mam, mwanaharakati wa kupinga utumwa na sura ya Taasisi ya Somaly Mam,...
Japan: Uchunguzi Mpya Juu ya Umaskini Waharibu Soga za Utajiri
Mjapani mmoja kati ya sita anaishi katika umasikini inasema ripoti mpya ya Wizara ya Ustawi wa Jamii [en]. Kwa mujibu wa takwimu za OECD, Japan ina kiwango kikubwa zaidi cha umasikini katika dunia iliyoendelea na ni ya 4 baada tu ya Mexico, Uturuki na Marekani. Mnamo mwezi wa Septemba, Makoto...
Bhutan: Mpito Usio na Mikwaruzo Kuelekea Demokrasi
Tshering Tobgay, kiongozi wa chama cha upinzani katika Bunge la Taifa la Bhutan, anatoa maoni kuwa: “mpito wetu kuelekea demokrasi, kwa hakika, umetukia bila mikwaruzo. Umetukia bila mikwaruzo kiasi kwamba wengi wetu walikuwa hata hawaufuatilii.”
Marekani: Wanandoa wa rangi tofauti wanyimwa cheti cha ndoa
Juma lililopita huko Hammond, Louisiana, wapenzi wawili walituma maombi ya kibali cha kufunga ndoa na walikataliwa kwa misingi ya rangi zao tofauti. Afisa wa kutathmini na kuandikisha nyaraka (Muamuzi wa Amani) alidai kuwa “ndoa baina ya watu wa rangi hazidumu” na alisema kuwa anafanya hivyo “kwa ajili ya watoto.”