GlobalVoices katika

English

Hifadhi ya lugha Katika Makundi · 474 jumbe


Below are posts about citizen media in English. Don't miss Global Voices, where Global Voices posts are translated into English! Read about our Lingua project to learn more about how Global Voices content is being translated into other languages.

Habari mpya Kuhusu English

7 Mei 2013

Michoro ya Dar: Sanaa kwa Maendeleo Endelevu

Dar Sketches (Michoro ya Dar) ni sehemu ya mradi unaoanzia ngazi ya Mtaa jijini Dar Es Salaam, Tanzania ulioanzishwa na msanii na mchoraji Sarah Markes:

Ni katika kuenzi urithi wa kitamaduni na wa sanaa ya ubunifu wa majengo kwa jiji la Dar Es Salaam sambamba na juhudi za kukuza uelewa kwa wananchi juu ua tishio la urithi huu linalotokana na kasi kubwa ya kupanuka holela kwa jiji hilo.

5 Mei 2013

Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska

Habari Mpya:  Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito.

Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana wasiotarajiwa wamejitokea kuwania kiti hicho. Wakati wagombea wa awali walikuwa wapya kabisa wasiofahamika sana, wanasiasa wachache machachari wanaofahamika wanatarajiwa kugombea akiwemo rais wa zamani Didier Ratsiraka, rais wa sasa wa mpito Andry Rajoelina [fr] na mke wa rais wa zamani Ravalomanana, anayeitwa Lalao Ravalomanana.

4 Mei 2013

Wabunge wa Ukraine Wataka Utoaji Mimba Upigwe Marufuku Kisheria

Soma makala hii.

Mapema mwezi Aprili, Wabunge watatu kutoka kambi ya Upinzani iitwayo“Svoboda” walipeleka mswada bungeni wenye lengo la kupiga marufuku utoaji mimba nchini Ukraine. Tetyana Bohdanova anataarifu mwitikio wa watumiaji wa mtandao kufuatia hatua hii ya Bunge la Ukraine.

28 Aprili 2013

Uganda: Kukumbuka milipuko ya mabomu ya 2010

Soma makala hii.

Wananchi wa Uganda wameutumia mtandao wa Twita na Facebook kuwakumbuka wahanga 2010 wa milipuko yha mabomu iliyotokea kwenye klabu ya Rugby huko Kyaddondo na katika baa ya Kijiji cha Kiethiopia jijini Kampala Uganda.Mashambulizi hayo yalitokea wakati ambao wapenzi wa kandanda walikuwa wakitazama mpambano wa fainali kati ya Uhispania na Uholanzi uliofanyika nchini Afrika Kusini.

24 Aprili 2013

Washindi wa Tuzo za Kwanza za Uandishi wa Kiraia Nchini Ghana

Soma makala hii.

Tumepata matokeo ya Tuzo za kwanza kabisa za Uandishi wa Kiraia nchini Ghana.

16 Aprili 2013

Uturuki: Polisi Watumia Mabomu ya Machozi Kuwatawanya AkinaMama Waandamanaji

Soma makala hii.

Wafungwa wa kisiasa wa Kikurdi wamefikia siku yao ya 55 ya mgomo wa kula. Kuna mamia ya wafungwa wa kisiasa walio kwenye mgomo wa kula nchini Uturuki, na hii imesababisha maandamano mshikamano katika bara la Ulaya, na hususani ndani ya Uturuki. Mapema jana [4 Novemba 2012], wanawake ambao ni mama wa baadhi ya wafungwa wa kisiasa walifanya maandamano ya kukaa, na walijikuta wakipambana na mabomu ya machozi, pamoja na kunyunyuziwa maji ya kuwasha. Wa- Kurdi duniani kote wanapinga kimya kinachotumika kushughulikia adha yao.

15 Aprili 2013

Asasi za Kiraia za Urusi “Zakaguliwa” na Mwendesha Mashitaka

Soma makala hii. RuNet Echo

Wanaharakati wa DemVybor katika jiji kuu la eneo la Voronezh waliripoti kwenye blogu ya DemVybor[ru] kwamba Asasi Zisizo ki-Serikali zinakaguliwa na ofisi ya mwendesha mashitaka wa umma wa jiji hilo. Mashirika...

11 Aprili 2013

Photos jumbe Video jumbe
Bahrain: ‘Kususia michezo ya Olimpiki’

Soma makala hii.

Wa-Bahraini wengi wanatoa mwito wa kususuia michezo ya Olympics. Kwanza, mwana wa mfalme, ambaye amekuwa akituhumiwa kwa kujihusisha na utesaji wa wanariadha, anahudhuria michezo hiyo. Pili, sehemu kubwa ya timu ya nchi hiyo imetengenezwa na wanariadha wa ki-Afrika.

2 Aprili 2013

Tanzania: Ghorofa Laporomoka jijini Dar Es Salaam

Pernille anaweka picha mtandaoni zinazoonyesha ghorofa lililoporomoka jijini Dar Es Salaam, Tanzania siku ya Ijumaa, 29 Machi 20013: “Karibu kabisa na jengo hilo kuna uwanja wa kandanda unaotumiwa na watoto. Zaidi ya watu 60, pamoja na watoto, wanaripotiwa kupotea kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha ITV. Hakuna kauli rasmi iliyotolewa mpaka sasa.”

12 Machi 2013

Ramani za Mpaka wa Kikoloni wa Sudan Kusini Ziko Wapi?

Joseph Edward anazungumzia kupotea kwa ramani za mpaka wa Sudan Kusini za enzi za ukoloni: “Majadiliano yameibuka kuhusu ramani ambazo zilidaiwa kuchukuliwa na Waingereza baada ya Sudan kupata uhuru mnamo mwaka wa 1956. Huku baadhi a watu wanaamini kwamba nyaraka hizo za kihistoria zinaweza kupunguza migogoro ya mpaka inayoendelea, watafiti wanatilia shaka uwepo wa ramani hizo.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha