GlobalVoices katika

Arabic

Hifadhi ya lugha Katika Makundi · 60 jumbe


Below are posts about citizen media in Arabic. Don't miss Global Voices الأصوات العالمية, where Global Voices posts are translated into Arabic! Read about our Lingua project to learn more about how Global Voices content is being translated into other languages.

Habari mpya Kuhusu Arabic

28 Januari 2013

Mauritania:Ghadhabu Dhidi ya Kauli ya Balozi wa Marekani

Picha ya maandamano dhidi ya Ubalozi wa Marekani mjini Nouakchott – Iliwekwa kwenye ukurasa wa Facebook ya Vijana wa Kukusanya Nguvu ya Kidemokrasia

zaidi »

27 Oktoba 2012

Misri: Ushauri kwa Waandamanaji wa Kuwait

Soma makala hii.

Wakati watu wa Kuwait walipoanzisha maandamano makubwa ambayo hayakuwahi kutokea ya kuonesha waziwazi kutokukubaliana na mabadiliko ya sheria ya uchaguzi yaliyopitishwa chini ya mtawala wa kurithi kufuatia kuvunjwa kwa bunge, watu wa Misri wametumia muda wao mwingi katika Twita wakitoa ushauri kwa watu wa Kuwait kuhusiana na yapi ya kufanya na yapi ya kutokufanya.

8 Oktoba 2012

Tunisia: Mgomo Waanza jijini Thala

Kupitia mtandao wa twita, Tounsia Hourra (m-Tunisia huru) anasema [ar] kuna mgomo mkubwa umeanza jijini Thala, kwenye jimbo la Kasserine, leo [Oktoba 8, 2012]. Mgomo huo umekuja kama hatua ya kupinga kukua kwa kasi kwa ukosefu wa ajira na kuzorota kwa maendeleo ya jiji hilo.


@tounisiahourra
: اضراب عام في تالة ( ولاية القصرين ) اليوم احتجاجا على ارتفاع معدلات البطالة واهمال صيانة المدينة

@tounisiahourra: Mgomo mkubwa jijini Thala (jimbo la Kasserine) leo kupinga kuongezeka kwa ukosefu wa ajira na kuzorota kwa maendeleo ya jiji hilo.

Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala

Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati.

18 Septemba 2012

Italia Yalaumiwa kwa Ukiukaji wa Haki za Wakimbizi wa Kiafrika

Soma makala hii.

Februari 23, Mahakama ya Haki za Binadamu ya Ulaya huko Strasbourg ilikuja na hukumu ya kihistoria kwamba Italia imevujna Tamko la Ulaya la Haki za Binadamu kwa kuwazuia na kuwarudisha wakimbizi wa ki-Eritrea na Somalia kwenda Libya. Abdoulaye Bah anaripoti.

23 Agosti 2012

Photos jumbe
Mauritania: Wafanyakazi wa Migodini Wapinga ‘Aina Mpya ya Utumwa’

Soma makala hii.

Zaidi ya wafanyakazi 2,300 wako kwenye mgomo nchini Mauritania katika mji wa kaskazini wa Zouerat, jambo ambalo limesababisha kuzorota kwa maeneo mengine kumi ya Kampuni la Taifa la Madini na Viwanda, huku kazi zikiwa kwenye mvurugiko mkubwa. Madai yamejikita katika suala zima la maslahi bora ya wafanyakazi.

20 Agosti 2012

Saudi Arabia: Mwanaharakati Reema Al Joresh Atiwa Kizuizini katika Sikukuu ya Idi

Soma makala hii.

"Hamjambo? Polisi wamenikamata mimi na watoto wangu." - Reema Al Joresh, mke wa mfungwa ambaye amekuwa kizuizini kwa miaka nane bila kufunguliwa mashtaka, alikuwa akielekea msikitini ili kutoa zawazi 500 pamoja na barua ya kueneza taarifa kuhusu itiaji nguvuni wa kiholela katika ufalme huo.

18 Agosti 2012

Video jumbe
Syria: Mafunzo ya Silaha na Namna ya Kupigana Katika Mtandao wa Intaneti

Soma makala hii.

Waasi nchini Syria wameanza kutumia YouTube ili kupeana mafunzo hasa kupitia 'Free Syrian Army Help' yaani 'Msaada wa Jeshi la Kuikomboa Syria'. Chaneli hiyo ina picha za video zipatazo 80 zikiliezea mbinu kama vile vita ya uso-kwa-uso, jinsi ya kutengeneza mabomu ya kutupwa kwa mkono, na jinsi ya kuwavizia maadui.

Photos jumbe
Morocco: Wanafunzi Wadai Marekebisho kwenye Mfumo wa Elimu

Soma makala hii.

Mwezi Julai, kikundi cha wanafunzi wa nchini Morocco kilizindua ukurasa wa Facebook ulioitwa "Umoja wa Wanafunzi wa Morocco kwa ajili ya Mabadiliko ya Mfumo wa Elimu". Pungufu ya mwezi mmoja, kikundi hiki kilivuta uungwaji mkono mkubwa hasa kupitia mitandao ya kijamii.

15 Julai 2012

Photos jumbe
Misri: Waandamanaji Watuma Ujumbe Dhidi ya Udhalilishaji wa Kijinsia.

Soma makala hii.

Since the revolution took place, more and more Egyptians are speaking up and demanding their rights, including women's rights. In this photo post we look at a recent protest against sexual harassment held in Cairo.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha