The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Arabic Hifadhi ya lugha Katika Makundi

Kiungo cha RSS kwa Arabic

2009-11-16

Misri: Haki ya Kijerumani kwa Marwa El Sherbini

Muuaji wa Marwa El-Sherbini, mwanamke wa Kimisri ambaye alichomwa visu mpaka kufa na muhamiaji mwenye asili ya Urusi na Ujerumani, Alex Wiens, ndani ya mahakama huko Ujerumani, amehukumiwa kifungo cha maisha, bila uwezekano wa kuachiwa mapema. Haki hatimaye imetolewa na muuaji anaadhibiwa, wanasema wanablogu wa Misri.

2009-11-15

Algeria-Misri: Ugomvi Juu ya pambano la Mpira kwenye MtandaoPhotos postVideo post

Hali tete kati ya mashabiki wa mpira wa miguu wa Misri na Algeria inazidi kukua kabla ya pambano litakalofanyika mjini Cairo tarehe 14 Novemba. Mchuano huo utaamua ipi kati ya timu hizo zitafaulu kwenda kwenye Kombe la Dunia la FIFA Afrika ya kusini mwaka ujao. Misri inahitaji japo ushindi wa magoli mawili ili kulazimisha mchezo wa kukata shauri katika uwanja wa nchi nyingine ambapo Algeria, ambayo imeshindwa kufaulu kwenda kombe la dunia tangu 1986, itapambana ili kutunza nafasi yake ya sasa ya kuongoza katika kundi la wanaogombania nafasi ya kufaulu. Wakati wa kuelekea pambano la Jumamosi, mashabiki washindani wamekuwa wakijiandaa nje ya mtandao wa intaneti, kadhalika katika malumbano makali ya mtandaoni, ambayo yamekua na kugeuka “vita-vya-mikwara-kwenye-mtandao”

2009-10-27

Uchaguzi Tunisia: haki Bila Ya Upendeleo!!?

Rais wa Tunisia Zine Al Abidine Ben Ali ameshinda uchaguzi kwa kipindi cha tano kwa asilimia 89.62 ya kura zote. Chama chake cha Democratic Constitutional Rally kilishinda viti vya bunge 161 katika viti 214. Wanablogu wa Tunisia wanatoa maoni katika makala hii.

2009-10-25

Middle East & North Africa

Omar Mushawah ameripoti [ar] kukamatwa kwa Haytham al-Maleh, mwanasheria wa Ki-Syria na mtetezi wa haki za binaadamu ambaye pia alitumia muda wa miaka 6 jela kati ya 1980 na 1986 kwa kudai mabadiliko ya kikatiba. Al-Maleh pia ni mwanzilishi mwenza wa Jumuiya ya Haki za Binaadamu ya Syria.

2009-05-27

Tajiri Wa Kimisri Ahukumiwa Kifo

Wamisri walishuhudia hukumu isiyotarajiwa katika historia ya vyombo vya sheria nchini humo: Bilionea Hesham Talaat Moustafa, pamoja na mamluki wake (mpiga risasi wa kukodi) Mohsen El Sokari wamehukumiwa adhabu ya kifo kutokana na kuhusika kwao katika mauaji ya mwimbaji wa Kilebanoni Suzanne Tameem. Mauaji hayo ya kinyama yalitokea huko Dubai, UAE, na hukumu iliyotolewa Alhamisi imesababisha mshtuko na mshangao wakati wanablogu walipojaribu kukubaliana na yaliyotukia.

2009-02-02

Mashariki ya Kati: Vikwazo kama Silaha ya Kisiasa

Watu wengi wa Mashariki ya Kati wamesusia bidhaa za Israeli na Marekani kama jibu la mashambulizi ya Israeli huko Gaza. Tarek Amr anapitia yale wanablogu wanayosema kuhusu suala hili.

2009-01-07

Palestina: Gaza Haitafuti Aspirini Kwa Ajili Ya Kidonda Chake

Wapalestina wachache na wanaharakati wageni bado wanaweza kutuma ripoti za kile kinachoendelea kwenye ukanda wa Gaza kwa kutumia umeme wa jenereta pale inapobidi. Zifuatazo ni jumbe za blogu katika masaa 24 yaliyopita.

2008-10-26

Bahrain: Raha na Karaha za Kusoma Ng'ambo

Ingawa Bahrain ina idadi kadhaa ya vyuo vikuu, vya umma na binafsi, raia wengi wa nchi hiyo hupata fursa ya kwenda ng'ambo kwa masomo ya shahada ya kwanza na hata zile za juu, mara nyingi kwa kutegemea ufadhili. Moja ya matatizo ya kwanza wanayokumbana nayo huko ughaibuni ni kwamba watu wachache tu hufahamu ni wapi Bahrain ilipo. Katika makala hii tunafuatilia uzoefu wa wanablogu watatu ambao ndiyo kwanza wamekwenda ng'ambo kwa masomo: kule Japan, Uingereza na Marekani na mwanablogu wa nne ambaye anasoma India kwa kipindi fulani hivi sasa.