Victoria Munene · Juni, 2012

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Victoria Munene kutoka Juni, 2012

Umuhimu wa Kongamano La Sauti za Dunia (Global Voices Summit) hapa Nairobi

  27 Juni 2012

Kuanzia tarehe mbili mwezi wa Julai hadi tarehe nne mwezi huo huo, familia ya Sauti za Dunia (Global Voices, GV) pamoja na washiriki wao wa kimataifa, raia wapendao vyombo vya habari na watazamaji watakusanyika pamoja katika hoteli ya Pride-Inn mjini Nairobi kwa kongamano la GV. Bila shaka tukio hili ni la kusisimua na ambalo limekuwa likitarajiwa na wengi kwa shauku kuu.

Brazili: Jarida Lawapa Nafasi Wasio na Makazi

  12 Juni 2012

Jarida la Ocas linalosambazwa katika mitaa ya mjini São Paulo pamoja na Rio de Janeiro tangu 2002, ni jarida ambalo husheheni habari ambazo hulitofautisha na vyombo vikuu vya habari nchini Brazil. Na linakwenda zaidi ya hapo. Aidha huwapa mwanzo mpya na fursa za kazi watu ambao hawana makazi na ambao wamo katika hatari ya kuangamia kijamii.

Kitabu kipya cha michezo ya watoto kutoka nchi mbalimbali

  7 Juni 2012

Blogu changamfu la Kimataifa, PocketCultures limechapisha limechapisha kitabu kuhusu michezo kumi na tano ya watoto kutoka nchi mbalimbali na amabayo inaweza kuchezwa kwa urahisi na msomaji. Kitabu kinaitwa ‘Games for Kids of the World’ na kinaweza kupatikana kwa bure kwenye iPad, Mac au kwenye kompyuta.