Blogu changamfu la Kimataifa, PocketCultures limechapisha limechapisha kitabu kuhusu michezo kumi na tano ya watoto kutoka nchi mbalimbali na amabayo inaweza kuchezwa kwa urahisi na msomaji. Kitabu kinaitwa ‘Games for Kids of the World’ na kinaweza kupatikana kwa bure kwenye iPad, Mac au kwenye kompyuta.
makala mpya zaidi ya Victoria Munene
30 Septemba 2012
Mbinu za Kugundua Dawa Bandia katika Nchi Zinazoendelea
Watu 700,000 hufa kila mwaka kwa kutumia dawa bandia za malaria na saratani pekee. Shirika la Afya Duniani, WHO linasema katika ripoti yake kuwa, mapato kutoka kwa dawa hizi kila mwaka hukaribia dola bilioni 200.
19 Septemba 2012
Kocha Mfaransa Ateuliwa Kuongeza Bahati ya Kenya Kwenye Kandanda
Shirikisho la Kandanda nchini Kenya FKF, limemchagua Kocha mpya wa timu ya taifa la Kenya ambaye ni Mfaransa, Henri Mchel. Wanakamati hao, wana matumaini kuwa anaweza kuwa 'bahati' ya Kenya katika mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ya 2013 na Kombe la Dunia la 2014.
21 Julai 2012
Matangazo ya Mkutano wa Sauti za Dunia (Sehemu ya 1)
Sauti za waliowakilisha GV katika warsha mjini Nairobi, Kenya.
15 Julai 2012
Afrika: Ujuzi wa Matumizi ya Zana za Habari za Kijamii kwa Vijana Wanaoishi na Ulemavu.
Warsha ya vijana walemavu kutoka kote barani Afrika lafanyika Dakar, Senegali. Warsha hii ilipangwa na DRI na YI. Imeandikiwa na Haute Haiku.
27 Juni 2012
Umuhimu wa Kongamano La Sauti za Dunia (Global Voices Summit) hapa Nairobi
Kuanzia tarehe mbili mwezi wa Julai hadi tarehe nne mwezi huo huo, familia ya Sauti za Dunia (Global Voices, GV) pamoja na washiriki wao wa kimataifa, raia wapendao vyombo vya habari na watazamaji watakusanyika pamoja katika hoteli ya Pride-Inn mjini Nairobi kwa kongamano la GV. Bila shaka tukio hili ni la kusisimua na ambalo limekuwa likitarajiwa na wengi kwa shauku kuu.
12 Juni 2012
Kenya: Intani walipwe au wasilipwe?
Mada hapa ni kuhusu kama inafaaa au haifai kwa intani kulipwa,mjadala ulioanzishwa na @RobertAlai.
Brazili: Jarida Lawapa Nafasi Wasio na Makazi
Jarida la Ocas linalosambazwa katika mitaa ya mjini São Paulo pamoja na Rio de Janeiro tangu 2002, ni jarida ambalo husheheni habari ambazo hulitofautisha na vyombo vikuu vya habari nchini Brazil. Na linakwenda zaidi ya hapo. Aidha huwapa mwanzo mpya na fursa za kazi watu ambao hawana makazi na ambao wamo katika hatari ya kuangamia kijamii.
7 Juni 2012
Kenya: Wanaharakati wapigana vita dhidi ya ufisadi kwa intaneti
I Paid a Bribe ni njia mojawapo inayotumiwa na wanaharakati dhidi ya ufisadi nchini, kwa kutumia teknolojia mpya ili kuwawezesha kupata ripoti za utoaji wa hongo.' I paid a Bribe' imefuatia muundo wa ‘India Anti-Corruption Portal (IPAB)' na ni ushirkiano kati ya IPAB na Wamani Trust ya Kenya ili kuleta IPAB katika Afrika Mashariki na Kati.

Marekani: Kumbukumbu la Walters Art lachapisha Mkusanyiko wa Picha
Jumba la Kumbukumbu la The Walters Art lililoko Baltimore, Maryland limechapisha zaidi ya picha elfu kumi na tisa kwenye mkusanyiko wa Wikimedia Commons na kuziweka chini ya leseni Creative-Commons. Jumba lenyewe lina mkusanyiko wa michoro kutoka Roma na Ulaya.




























Kiungo cha RSS kwa Victoria Munene







mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...