<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Deogratias Simba</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Paraguay: Wenyeji Wanyunyiziwa Dawa za Kuua Wadudu kwa Ndege</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/paraguay-wenyeji-wanyunyiziwa-dawa-za-kuua-wadudu-kwa-ndege/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/paraguay-wenyeji-wanyunyiziwa-dawa-za-kuua-wadudu-kwa-ndege/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 17 Nov 2009 09:56:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Agriculture]]></category>
		<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Indigenous]]></category>
		<category><![CDATA[Paraguay]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=685</guid>
		<description><![CDATA[Huko Mashariki mwa Paraguay, jumla ya watu 217 wa jumuiya ya wenyeji ya Ava Guaraní walianza kusumbuliwa wakionyesha dalili mbalimbali za kiafya zinazoaminika zilisababishwa na unyunyiziaji wa makusudi wa dawa za kuua wadudu hasa baada ya wao kuwa wamegoma kuhama kutoka katika ardhi waliyoirithi kutoka kwa mababu zao.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/eduardo-avila/">Eduardo Avila</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/12/paraguay-indigenous-group-sprayed-aerially-with-pesticides/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Huko Mashariki mwa Paraguay, jumla ya watu 217 wa jumuiya ya wenyeji ya Ava Guaraní walianza kusumbuliwa wakionyesha dalili mbalimbali za kiafya zinazoaminika zilisababishwa na unyunyiziaji wa makusudi wa dawa za kuua wadudu hasa baada ya wao kuwa wamegoma kuhama kutoka katika ardhi waliyoirithi kutoka kwa mababu zao.</p>
<p>Watendaji wa serikali wamethibitisha kwamba baadhi ya sehemu za ardhi ya wenyeji iliyo katika Wilaya ya Itakyry katika <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Alto_Paran%C3%A1_Department">Idara ya Alto Paraná</a> ilinyunyiziwa wakati ambapo <a href="http://www.ultimahora.com/notas/272060-Ministra-confirma-que-fumigaron-tierras-sin-cultivo-en-Itakyry">hakukuwa na mazao yoyote </a>[es]. Ishara nyingi zinaelekezwa kwa walima maharage ya soya wa KiBrazili kwamba ndiyo wanaohusika na unyunyiziaji huo, kwani kwa kiasi kikubwa ardhi iliyo mikononi mwa jamii za wenyeji ingefaa sana kwa zao hilo na kwamba hawa wamekuwa katika mgogoro na Ava Guaraní kuhusu <a href="http://interparaguay.blogspot.com/2009/11/ministros-comprobaron-la-fumigacion.html">umiliki wa takribani hekta 3,000</a>, kwa mujibu wa blogu ijulikanayo <em>Interparaguay [es]</em>.</p>
<blockquote><p>José Ángel López Barrios wa Bienvenidos! [es] akielezea eneo la jamii lililo mbali na mengine ambapo tukio hilo lilitokea:<br />
Itakyry es uno de los distritos del Departamento de Alto Paraná, distante a unos 450 kilómetros de Asunción, capital de la Republica, se llega a el por caminos no pavimentados, su época de esplendor se dio en la época de las explotaciones yerbateras. Que termino al cabo de 100 años abriendo paso a la explotación de la soja en estos últimos tiempos……</p></blockquote>
<div class="translation">
Itakyry ni moja ya wilaya za Idara (Mkoa wa) Alto Paraná, iliyo umbali wa kilomita 450 kutoka katika mji mkuu wa Asunción. Kufika huko mtu huna budi kutumia barabara za vumbi, katika kilele cha mafanikio yake ilikuwa ni wakati wa ulimaji wa yerba maté. Jambo hilo lilikoma baada ya miaka 100, na kupisha ulimaji soya katika miaka ya hivi karibuni……</div>
<p>Ni mahitaji ya maharage ya soya na bei yake inayozidi kupanda ambayo inaifanya ardhi hiyo kuwa inayofaa kwa zao hili lenye kipato kikubwa sasa. Sehemu ya ardhi hii iko kwenye ardhi ya kurithi ya mababu wa jamii za wenyeji, kama vile <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Guaran%C3%AD">Guaraní</a>. Mwanablogu Carlos Rodríguez wa <em>Rescatar [es]</em> <a href="http://rescatar.blogspot.com/2009/11/soja-y-genocidio-fumigan-indigenes.html">hafikiri kwamba tukio la unyunyiziaji dawa dhidi ya makundi ya wenyeji ni tukio dogo, analiita tendo hilo kama &#8220;mauaji ya halaiki</a>&#8220;: </p>
<blockquote><p>Hubo un tiempo en que en Paraguay los aborígenes no eran considerados seres humanos. Eran cazados como animales y sus crías rescatadas como trofeos.<br />
(…)<br />
Otros fueron apropiándose a bala y sangre de sus tierras y como los indígenas no hacían gestiones ante las instituciones encargadas de titular las tierras que siempre les pertenecieron, el hombre blanco si lo hizo y se plantea el contrasentido de que los legítimos dueños de estas tierras, hoy son “los invasores”.<br />
Y siguen siendo tratados como animales. Sólo así se puede entender que los productores de soja les envíen aviones fumigadores para lanzarles venenos encima, tal como lo ha comprobado el Ministerio de Salud que socorre en estos momentos a los indígenas intoxicados por plaguicidas para soja.</p></blockquote>
<div class="translation">Kuna kipindi hapa Paraguay ambapo WaAborigino hawakudhaniwa kuwa ni binadamu. Waliwindwa kama wanyama na watoto wao walichukuliwa kama mapambo fulani hivi.<br />
(…)<br />
Sehemu ya ardhi yao iliporwa kwa risasi na damu, na hasa kwa kuwa wenyeji hawa hawakwenda kwenye mamlaka zinazohusika na utoaji hati miliki za ardhi kuhusu ardhi ambayo daima wameimiliki, Wazungu hawakwenda kwenye taasisi hizo, na katika jambo ambalo ni la kushangaza, hawa wanaochukuliwa kwamba wao ndiyo wamiliki wa ardhi hiyo ni hawa &#8220;wavamizi&#8221;.<br />
Wanaendelea kutendewa kama wanyama. Ni kwa njia hii tu ambapo mtu anaweza kuelewa kwa namna gani wazalishaji wa soya wanaweza kutuma ndege za kunyunyiza dawa ya sumu dhidi ya wenyeji, jambo ambalo limethibitishwa na Wizara ya Afya, ambayo sasa inajaribu kuwasaidia wenyeje walioathiriwa na sumu hiyo. </div>
<p>López Barrios <a href="http://lopezbarrios.blogspot.com/2009/11/matte-larangeira-la-industrial.html">pia anaona aibu kwa hitoria ya vitendo vibaya vinavyofanywa na jamii za wenyeji huko Paraguay [es]. </a>Kama mtoto wa wahamiaji kwenye nchi hii, anaandakika kwamba matukio hayo &#8220;yanamfanya atamani kurejea Ulaya&#8230; lakini kwa kweli &#8230;angependa wanyonyaji hao waondoke zao.&#8221;</p>
<blockquote><p>
Ensañarse con un pueblo indígena que tiene más de 38 siglos de existencia en sus propios y verdaderos territorios, no me parece apropiado…. Si no respetamos a nuestros mayores nuestros días se acortaran sobre la tierra y si anteponemos la avaricia a cualquier otra virtud caeremos sin remedio…..</p></blockquote>
<div class="translation">Kuwachukia wenyeji ambao wameishi hapo kwa zaidi ya karne 38 kwenye ardhi yao wenyewe, si jambo la kukubalika kwangu &#8230;. Kama hatuwaheshimu wakubwa zetu, basi siku zetu duniani zitafupishwa, na kama choyo (tamaa) ikiwekwa mbele ya kitu chochote, ipo siku tutaangamia &#8230;. </div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/paraguay-wenyeji-wanyunyiziwa-dawa-za-kuua-wadudu-kwa-ndege/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Marekani: Mauaji ya Fort Hood Yasababisha Kumulikwa kwa Waislamu Walio Jeshini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/marekani-mauaji-ya-fort-hood-yasababisha-kumulikwa-kwa-waislamu-walio-jeshini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/marekani-mauaji-ya-fort-hood-yasababisha-kumulikwa-kwa-waislamu-walio-jeshini/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 14 Nov 2009 09:35:25 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Racism]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=641</guid>
		<description><![CDATA[Shambulizi la upigaji risasi la kushtukiza lililofanywa na mwanajeshi wa Jeshi la Marekani, Meja Nidal Malik Hassan, na kusababisha vifo vya watu 13 na kujeruhi wengine 31 katika kambi ya kijeshi ya Fort Hood, jimbo la Texas, kwa mara nyingine limesababisha Waislamu nchini Marekani kumulikwa - hasa wale wanolitumikia jeshi. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/bhumika-ghimire/">Bhumika Ghimire</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/12/usa-fort-hood-massacre-puts-spotlight-on-muslims-in-army/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Fort_Hood">Shambulizi la upigaji risasi la kushtukiza</a> lililofanywa na mwanajeshi wa Jeshi la Marekani, Meja Nidal Malik Hassan, na kusababisha vifo vya watu 13 na kujeruhi wengine 31 katika kambi ya kijeshi ya Fort Hood, jimbo la Texas, kwa mara nyingine limesababisha Waislamu nchini Marekani kumulikwa - hasa wale wanaolitumikia jeshi. </p>
<p>Kitambo kifupi baada ya Meja Hassan kutangazwa kama mfyatuaji aliyetuhumiwa, kulikuwa na kukosa raha kuliko wazi kabisa miongoni mwa warusha habari na watoa maoni kuhusu usuli wake wa kidini na asili yake.  Iliripotiwa pia kwa wingi kwamba wanajeshi wengine wa Kiislamu mara nyingine walikabiliana na mashambulizi kutoka kwa wanajeshi wenzao.</p>
<p>Howard M. Friedman, Profesa Mwandamizi wa Sheria katika Chuo Kikuu cha Toledo, anasema katika blogu yake ijulikanayo kama <em><a href="http://religionclause.blogspot.com/2009/11/muslim-soldiers-in-us-military-face.html">ReligionClause</a></em>:</p>
<blockquote><p> “Jeshi limekuwa likiandikisha Waislamu walio na ujuzi wa lugha na welewa wa utamaduni, vitu vinavyohitajika ili kupigana vita huko Iraki na Afganistani. Hata hivyo, Waislamu walio jeshini sasa wanatiliwa shaka na baadhi ya maofisa wao.&#8221;</p></blockquote>
<p>Bila kujali mashaka dhidi ya wanajeshi Waislamu yaliyokuwapo kabla ya shambulizi hili, mtu anaweza kuwa na hofu kwamba mashaka hayo yamepata msukumo mpya baada ya mauaji ya watu kule Fort Hood. Maswali bado yanaendelea kuibuliwa endapo Meja Hassan alikuwa mwenye siasa kali na ambaye alifanya mashambulizi hayo kwa msukumo wa itikadi ya kidini au labda tu alikuwa na tatizo la kiakili. </p>
<p>Kule Kanada, mwandishi Gwynne Dyer wa gazeti huru la kila wiki la Vancouver kupitia mtandao wa <em><a href="http://www.straight.com/article-269513/gwynne-dyer-us-media-overlook-obvious-explanation-maj-nidals-mass-murder">Straight.com</a></em>, anabuni kwamba kuelekeza fikra kwenye dini ya muuaji ni kufumbia macho baadhi ya masuala mengine muhimu:</p>
<blockquote><p>“Baada ya siku chache wakati watoa maoni wakisitasita kutoa maelezo yanayoshindana, vyombo vya habari vinaanza kujikita katika maelezo kwamba ilikuwa ni unyanyasaji wa kirangi/kiasili/kidini ndiko kulikomsukuma Nidal kupata ukichaa. Watu wabaya, wanaofanya vitu kinyume na Wamarekani mwisho wa siku ndiyo wenye kuhusika na msiba huo, na kuna mwisho wake. </p>
<p>Maelezo yanayokwepwa ni kwamba vita vya Wamarekani vinavyoendeshwa ng&#39;ambo katika ardhi za Waislamu vinawajenga Waislamu nyumbani kuchukua msimamo mkali. Usijali sana kwamba magaidi wa Kiislamu waliokuzwa nyumbani walioshambulia mfumo wa usafiri jijini Landani mwaka 2005, na wafanya njama wa Kiislamu kadhaa ambao wamekamatwa katika nchi za Magharibi kabla njama zao hazijazaa matunda, wote wamelaumu uvamizi unaofanywa na mataifa ya Magharibi kwenye nchi za Kiislamu kama kitendo kilichowasukuma wao kuwa na msimamo mkali. Zaidi sana, usijali kwamba kile kilichowafanya kuwa na msimamo mkali ni ukweli kwamba uvamizi huo haukuwa na maana kwa masuala ya usalama wa Magharibi.&#8221;</p></blockquote>
<p>Fox News, ambayo mara nyingi hukosolewa kwa kuelemea kwake upande mmoja katika masuala yanayohusiana na uhamiaji na siasa mgando, inasemekana kuitisha wazo la <a href="http://www.salon.com/news/politics/war_room/2009/11/06/fox_friends/index.html">&#8220;uchunguzi kwa Waislamu&#8221; </a>walio jeshini. Katika tovuti ya <em><a href="http://www.veteranstoday.com/modules.php?name=News&#038;file=article&#038;sid=9280">Veterans Today</a></em>, ofisa mstaafu wa Jeshi la Ulinzi wa Pwani ya Marekani, United States Coast Guard, Tom Barnes, anasema chombo hicho cha habari kinachochea mtazamo uleule wa siku zote kwa kujaribu kujenga imani potofu ya &#8220;sisi dhidi ya wao&#8221;:</p>
<blockquote><p>
“… chombo hicho cha habari kinazidi kuwa &#8220;kisichosaidia&#8221;, yaani kwa lugha nyepesi, hasa kama swali hili la msingi linageuka kuwa vita nyingine ya Fox Channel dhidi &#8220;yao&#8221;.  Taarifa kama hizi siyo tu zinazidi kupitwa na wakati bali ni za hatari pia. <a href="http://www.salon.com/news/politics/war_room/2009/11/06/fox_friends/index.html">Hapa</a> ndipo palipo na habari nzima.</p>
<p>Kama nilivyoonyesha hapo kabla, jambo kama hili limewahi kutokea katika Jeshi la Ulinzi la Marekani. Ninazidi kuchoshwa na habari za Fox News zinazoniambia kuwa adui zangu ni akina nani. Kila wakati. Bila kukoma. Sikuwa na habari kwamba &#8220;wao&#8221; wapo wengi!&#8221;</p></blockquote>
<p><a href="http://news.google.com/news/url?sa=t&#038;ct2=us%2F0_0_s_0_0_t&#038;usg=AFQjCNFUhLnrNP-D9fmObNIMr6pSA-X1sg&#038;cid=1465293836&#038;ei=oXL4Spi5FIqGmQfJnPI9&#038;rt=SEARCH&#038;vm=STANDARD&#038;url=http%3A%2F%2Fwww.csmonitor.com%2F2009%2F1108%2Fp02s08-usmi.html">Magazeti mengi</a> hivi sasa yanachunguza ni kwa namna gani vitendo vya Hassan vitawaathiri Waislamu wanaotumikia katika Jeshi la Marekani, na wakazi Waislamu wanaoishi karibu na kambi ya Fort Hood.</p>
<p>Hapa kuna taarifa ya habari ya video ya <em><a href="http://www.youtube.com/watch?v=N8Azg9TxYkM">euroamericannews</a></em> katika YouTube kuhusu maoni ya Waislamu walio Fort Hood kuhusiana na tukio hilo.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/N8Azg9TxYkM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/N8Azg9TxYkM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Wakati ambapo uchunguzi wa mauaji hayo unaendelea, bila shaka jicho litaendelea kutupwa wa Waislamu wanaotumikia jeshi.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/marekani-mauaji-ya-fort-hood-yasababisha-kumulikwa-kwa-waislamu-walio-jeshini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Video: Dunia Yaadhimisha Kuanguka kwa Ukuta wa Berlini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/video-dunia-yaadhimisha-kuanguka-kwa-ukuta-wa-berlini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/video-dunia-yaadhimisha-kuanguka-kwa-ukuta-wa-berlini/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 11 Nov 2009 12:50:28 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Cyprus]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Film]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[German]]></category>
		<category><![CDATA[Germany]]></category>
		<category><![CDATA[History]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Mexico]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=620</guid>
		<description><![CDATA[Leo ni Kumbukumbu ya 20 ya kuanguka kwa Ukuta wa Berlini, kizingiti madhubuti cha kiusalama ambacho kiliwahi kuligawa jiji la Berlini katika pande mbili za Mashariki na Magharibi huko Ujerumani. Leo tunaonyesha baadhi ya picha za video zinazotoka pande mbalimbali za dunia zinazopandishwa ili kusherehekea siku hii na nini ukuta huo ulimaanisha siyo Ujerumani tu bali duniani kote. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/09/video-the-world-commemorates-the-fall-of-the-berlin-wall/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption aligncenter" style="width: 310px"><img alt="Ukuta wa Berlini na Natalie Maynor" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/127094076_0624cc7780-300x214.jpg" title="Berlin Wall by Natalie Maynor" width="300" height="214" /><p class="wp-caption-text">Ukuta wa Berlini na Natalie Maynor</p></div><br />
Leo ni <a href="http://www.mauerfall09.de/">Kumbukumbu ya 20 ya kuanguka kwa Ukuta wa Berlini</a>, kizingiti madhubuti cha kiusalama ambacho kiliwahi kuligawa jiji la Berlini katika pande mbili za Mashariki na Magharibi huko Ujerumani. Leo tunaonyesha baadhi ya picha za video zinazotoka pande mbalimbali za dunia zinazopandishwa ili kusherehekea siku hii na nini ukuta huo ulimaanisha siyo Ujerumani tu bali duniani kote. </p>
<p>Huko Ujerumani, mfululizo wa mifano ya vipande vya mchezo wa domino iliundwa kutumia maboya na kisha kunyanyuliwa ili baadaye yaangushwe kama ishara ya kumaliika kwa zama za Vita Baridi. <a href="http://www.youtube.com/watch?v=rsDNfQqnET4">Video hii iliyotayarishwa na NoCommentTV</a> inaonyesha vipande hivyo vya domino, ambavyo <a href="http://www.spiegel.de/international/germany/0,1518,615014,00.html">vilichorwa na watoto huko Ujerumani</a> na p<a href="http://www.heiditrautmann.com/category.aspx?CID=2676368777">ia na wasanii wanaoishi maeneo mengine ambapo kuna migawanyiko na kuta</a>, vikisimamishwa. Kipande cha kukupa vitu vya kuchagua kimezuiwa kufanya kazi, lakini <a href="http://www.youtube.com/watch?v=0y5eGXy_laQ">unaweza kuona jinsi vipande hivyo vya domino vilivyoangushwa kwa kubofya kiungo hiki ili kuiona katika ukurasa wake wa YouTube</a>.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/rsDNfQqnET4&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/rsDNfQqnET4&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kule <a href="http://www.youtube.com/watch?v=hDCHrnZdwcs">Kolombia</a>, wanafunzi waliigiza uangukaji wa ukuta huo, kwa kupokezana kuvunjilia mbali ukuta wa zege:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/hDCHrnZdwcs&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/hDCHrnZdwcs&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kutoka Ujerumani, mshabiki wa kuangusha domino <a href="http://www.youtube.com/watch?v=dKLiooarpkA">Annodomino2007</a> amepandisha mtandaoni domino yake mwenyewe ili kuenzi kuanguka kwa ukuta huo, na pia kama kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 10 tangu alipoanza mapenzi yake makubwa kwa michezo ya domino:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/dKLiooarpkA&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/dKLiooarpkA&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p><a href="http://www.youtube.com/watch?v=UF_o1KYQIWU">Kule Marekani</a>, wanachuo waliinua mfano wa Ukuta wa Berlini ambao mtu angeweza kuandika juu yake, yaani kama njia ya kuiamsha jamii:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/UF_o1KYQIWU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/UF_o1KYQIWU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kutoka Mexico, <a href="http://www.youtube.com/watch?v=kffLolfYcfU">VarinVxx alipandisha picha ya video</a> ikionyesha ukuta mwingine ambao bado uko imara, <em>Si Berlini, si Palestina, bali ni kwenye mpaka wa Marekani na Mexico, Ukuta wa Aibu huko Marekani</em>:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/kffLolfYcfU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/kffLolfYcfU&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p><a href="http://www.youtube.com/watch?v=cGpVyCovo70">Krista Schyler</a> pia analinganisha ukuta ulio kwenye mpaka wa Mexico na Marekani na ule wa Berlini, safari hii siyo tu kukazia kuhusu madhara ya uhamaji wa binadamu, lakini kutoka kwa mtazamo wa utunzaji wanyama pori pia:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/cGpVyCovo70&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/cGpVyCovo70&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Mradi huu wa majaribio (Mradi Rubani) kwa ajili ya <a href="http://www.youtube.com/watch?v=7QeaIChuJ4c">makala ya video ya Ziashere</a> inaonyesha kuta nyingine ambazo bado ziko imara, mojawapo ikiwa kule Ireland:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/7QeaIChuJ4c&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/7QeaIChuJ4c&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Video hiyo ya mwisho ina umri wa miaka 2 sasa, lakini bado ujumbe wake una maana: <a href="http://www.youtube.com/watch?v=Pu4OztB_Zyo">mtengeneza filamu Adam</a> aliwahoji vijana kutoka pande zote mbili za ukuta Kaskazini na Kusini mwa Cyprus, ukanda wa kijani unaolindwa na vikosi vya helmeti za kibuluu vya Umoja wa Mataifa ambao unatenganisha WaCyprus wa Kituruki na Wacyprus wa Kigiriki, jambo linaoufanya mji huo uwe na heshima ya kuwa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Nicosia">mji wa mwisho uliogawanyika</a>.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/Pu4OztB_Zyo&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/Pu4OztB_Zyo&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/video-dunia-yaadhimisha-kuanguka-kwa-ukuta-wa-berlini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ofisa Aweka Wazi Ufisadi wa Polisi kupitia Mtandao</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 10 Nov 2009 11:10:26 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=595</guid>
		<description><![CDATA[Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko Novorossiysk alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/vadim-isakov/">Vadim Isakov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/09/officer-exposes-police-corruption-using-the-web/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/YouTube-%D0%92%D0%B8%D0%B4%D0%B5%D0%BE%D0%BE%D0%B1%D1%80%D0%B0%D1%89%D0%B5%D0%BD%D0%B8%D0%B5-%D0%BC%D0%B0%D0%B9%D0%BE%D1%80%D0%B0-%D0%BC%D0%B8%D0%BB%D0%B8%D1%86%D0%B8%D0%B8-%D0%BA-%D0%9F%D1%83%D1%82%D0%B8%D0%BD%D1%83-1_1257748652019-75x75.jpg" title="YouTube - Видеообращение майора милиции к Путину (#1)_1257748652019" class="alignleft" width="75" height="75" /> Mnamo tarehe 6 Novemba, afisa wa polisi katika Idara ya Mambo ya Ndani huko <a href="http://maps.google.com/maps?q=Novorossiysk&#038;oe=utf-8&#038;rls=org.mozilla:en-US:official&#038;client=firefox-a&#038;um=1&#038;ie=UTF-8&#038;hq=&#038;hnear=Russian+Federation,+Region+of+Krasnodar,+Novorossiysk&#038;gl=us&#038;ei=aa73SouZJZDR8QbxpNDzCQ&#038;sa=X&#038;oi=geocode_result&#038;ct=title&#038;resnum=1&#038;ved=0CAoQ8gEwAA">Novorossiysk</a> alitumia tovuti yake binafsi kuwasiliana na Waziri Mkuu Vladimir Putin na kuzungumzia matatizo lukuki yanayowakabili maafisa wa polisi nchini Urusi. </p>
<p>Kwenye ujumbe wake wa video unaopotakina katika anwani hii ya mtandaoni <a href="http://www.dymovskiy.ru/">www.dymovskiy.ru</a> na YouTube (<a href="http://www.youtube.com/watch?v=2G3KbBfpg24&#038;feature=related">sehemu ya I</a> na <a href="http://www.youtube.com/watch?v=2dJkMLxvulw">sehemu ya II</a> [RUS]), Aleksey Dymovskiy anaonekana kuwa mtulivu na anayejieleza kwa usahihi mkubwa. Anazungumzia juu ya kushuka kwa hadhi ya polisi, rushwa, ufisadi na jinsi gani malipo duni yanavyokuwa kama sumu inayowala maafisa wengi wa polisi nchini Urusi.</p>
<blockquote><p>Nafikiri watu wengi watanielewa. Nataka kuchapa kazi, lakini nimechoshwa na mipango ya kingano ambapo tunalazimishwa kupeleleza jinai ambazo hazipo.  Nimechoshwa na mipango ya kutunga ambapo tunaambiwa tuwafunge watu fulani. Nimechoshwa na jinai za kutunga zinazoandaliwa ili kuwatupa watu fulani gerezani. </p></blockquote>
<p>Akiendelea kuweka wazi mambo mbalimbali, Dymovskiy anakiri kumtupa mtu asiye na hatia gerezani kwa sababu ya kulazimishwa na mkubwa wake kazini:</p>
<blockquote><p>Mkurugenzi wa Idara ya mambo ya Ndani alinitunukia cheo cha Meja, ambacho nilikipata mwezi Mei, kwa sababu tu nilimwahidi kutumpa mtu asiye na hatia gerezani. Siogopi kueleza jambo hili. Naelewa kuwa naweza kuadhibiwa kwa sababu hii. Lakini ni ukweli nami ninaukiri.</p></blockquote>
<p>Dymovsky pia anamwomba Waziri Mkuu Vladimir Putin kupeleleza matatizo hayo na kumalizia mbali tatizo la ufisadi katika jeshi la polisi.<br />
Video yake hiyo ilipata watembeleaji wengi sana muda mfupi tu tangu ichapishwe na vilevile maelfu waliibofya kwenye YouTube. Ilichukuliwa pia sana na kuchapishwa na vyombo vikuu vya habari za Urusi na kujadiliwa sana katika blogu nyingi. Ni mfano mmoja kati ya kadhaa ya kwanza ambapo raia wa Urusi wanafaulu vema kabisa kutumia miundo mipya ya majukwa ya habari ili kuwasiliana na serikali hasa kuhusu masuala nyeti yanayoikabili nchi. </p>
<p>Upekee wa &#8220;hotuba za kiraia kwa njia ya video&#8221; nchini Urusi inaelezwa vema zaidi kwa maoni yenye tahadhari kutoka katika moja ya blogu maarufu zaidi nchini inayoitwa <a href="http://dolboeb.livejournal.com/1696532.html">dolboeb</a>:</p>
<blockquote><p>Risala yenye nguvu ya pekee. Sitashangaa kama itageuka kuwa mbinu ambukizi ya utafutaji masoko. Mhusika mkuu anaonekana kama mtu wa kutoka sayari nyingine.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu mwingine <a href="http://marchenk.livejournal.com/191686.html">marchenk</a> anaandika:</p>
<blockquote><p>Hakuna hata mmoja wetu aliye malaika&#8230; simhusudu [Dymovskiy] kama askari mwaminifu na mpenda ukweli (mwenyewe amekiri kwamba alitunukiwa cheo cha Meja kwa kumfunga mtu asiye na hatia gerezani).  […] Hata hivyo, nampa heshima kwa ajili ya ujasiri wake wa kuwa mkweli. Kwa hiyo, kumbe kuna maafisa wengine wa polisi walio waaminifu. Kwa sababu yao, ni muhimu kuhakikisha kunakuwepo na mabadiliko katika jeshi la polisi. </p>
<p>Ninamwombea Mungu ili kwamba uwekaji wake wazi huu wa mambo umpe kinga na atendewe haki katika hali yake. </p></blockquote>
<p>Siku ya Jumapili, tarehe 8 Novemba, Rashid Nurgaliev, Waziri wa Urusi wa Mambo ya Ndani, alitangaza ukaguzi wa jeshi la polisi huko Novorossiysk. Wakati huohuo, Dymovskiy amefukuzwa kazi kwa sababu ya “uzushi na vitendo ambavyo vinaharibu sifa” ya polisi.</p>
<p>Katika mahojiano yake na kituo cha redio cha Urusi, “<a href="http://www.echo.msk.ru/">Ekho Moskvy</a>,” Dymovskiy alisema kwamba amekuwa akifuatiliwa na kwa hiyo alikuwa akifikiria kuhamishia familia yake jijini Moscow kwa sababu za kiusalama. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ofisa-aweka-wazi-ufisadi-wa-polisi-kupitia-mtandao/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Bolivia: Uhaba wa Maji Kwa Sababu ya Theluji Inayoyeyuka</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/bolivia-uhaba-wa-maji-kwa-sababu-ya-theluji-inayoyeyuka/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/bolivia-uhaba-wa-maji-kwa-sababu-ya-theluji-inayoyeyuka/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 07 Nov 2009 12:55:48 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Bolivia]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=572</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naEduardo Avila  &#183; Imetafsiriwa na Deogratias Simba &#183;  Angalia ujumbe mama 
Safu ya milima ya Chacaltaya ina baadhi ya vilele ambavyo ni alama zenye maana katika safu ya milima Andes iliyopo Bolivia. Kwa kuwa ilikuwa ni sehemu moja pekee ambapo mchezo wa kuteleza barafuni uliweza kufanyika katika nchi hii ya milimamilima, [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/eduardo-avila/">Eduardo Avila</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/02/bolivia-water-shortages-due-to-melting-glaciers/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Chacaltaya">Safu ya milima ya Chacaltaya</a> ina baadhi ya vilele ambavyo ni alama zenye maana katika safu ya milima Andes iliyopo Bolivia. Kwa kuwa ilikuwa ni sehemu moja pekee ambapo mchezo wa kuteleza barafuni uliweza kufanyika katika nchi hii ya milimamilima, milima hii ni maarufu sana kwa wale walio kwenye Idara ya La Paz, na pia kwa wageni wapenda kuvumbua mambo mapya. Ni katika milima hiyohiyo ambapo zilifanyika mechi za soka za hisani ambazo kwazo Rais Evo Morales alishiriki ili kuthibitisha kwamba michezo inaweza kuchezwa katika maeneo ya ukanda wa juu.</p>
<p>Hata hivyo, theluji ya Chacaltaya imeanza kupungua kwa kasi inayotisha na kali sana. Athari ya mabadiliko ya hali ya hewa kwa barafu iliyoko kwenye mlima huu na mingine iliyo katika eneo hili zimekuwa zikichunguzwa na Profesa wa Chuo Kikuu cha San Andrés, Edson Ramírez, <a href="http://revistavirtual.redesma.org/vol5/articulo6.php?id=c1">ambaye anahitimisha kwa kusema kwamba kuna uhusiano wa moja kwa moja</a> kati ya kuongezeka kwa kiwango cha joto na kutokweka kwa theluji au barafu hiyo.</p>
<p>Ramírez na timu yake wamekuwa pia wakitafiti barafu iliyoko kwenye  mlima mwingine ambao nao umekuwa ukipatwa na athari zinazofanana na huo mwingine na madhara ya mwenendo huo kwa jamii inayoishi maeneo ya jirani. barafu iliyoko kwenye  mlima unaoitwa Tuni Condoriri glacier unayeyuka katika kasi kubwa, hivyo kuwaathiri wapenzi wa alpine, lakini pia hali hiyo inaathiri jamii za wahamiaji walio katika hatari ambao huitegemea ili kujipatia maji ya kunywa na kwa ajili ya shughuli za kilimo. </p>
<p>Tenki la kuhifadhia maji yanayotoka <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/americas/6496429.stm">kwenye barafu iliyoko kwenye  mlima huo hutoa kiasi cha 80% cha maji ya kunywa kwa jiji la El Alto na vitongoji vyake vya La Paz</a>. Kwa mujibu wa sensa ya hivi karibuni, <a href="http://es.wikipedia.org/wiki/El_Alto">El Alto ina jumla ya watu wapatao 827,000 [es]</a>,ambapo idadi hiyo inakua kwa 5.1% kila mwaka. Kwa mujibu wa mwandishi wa habari na mwanablogu Mónica Oblitas, <a href="http://monioblitas.blogspot.com/2008/06/glaciar-nuestro-tesoro-se-derrite.html">kiwango hiki ni zaidi ya mara mbili ya wastani wa taifa [es]</a>. Wataalamu wanabashiri uhaba wa maji na kulipia maji, ambapo <a href="http://observadorglobal.com/bolivia-un-futuro-sin-agua-informe-especial-n45.html">watu wengine wanabashiri kwamba suala la mgao wa maji limekaribia [es]</a>. <em>Timu kutoka Observador Global [es]</em> (Wafuatiliaji wa Ulimwengu) <a href="http://observadorglobal.com/bolivia-un-futuro-sin-agua-informe-especial-n45.html">waliandaa makala ya video yenye sehemu sita kuonyesha madhara ya upungufu wa maji katika eneo hilo</a>.</p>
<p>Jiji hilo ni <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/El_Alto">makazi ya wahamiaji kutoka jamii za wenyeji wa Aymara  katika Altiplano ya Bolivia</a>, ambao huhamia katika jiji la El Alto, mara nyingi wakiwa katika hali ya umaskini uliokithiri. Mwanablogu wa Ki-Bolivia, Cristina Quisbert anayeandika katika blogu ya <em>Indigenous Bolivia</em> <a href="http://boliviaon.blogspot.com/2009/09/our-mountains-melt.html">anaelezea hali inayowakabili wakaazi wengi hususani kuhusu maji salama ya kunywa</a>:</p>
<blockquote><p>Kuna mambo mengine yanayochangia katika ugumu wa kupata maji. Watu wengi wanafika kutoka vijijini kuingia katika jiji la El Alto na kuanzisha makazi pale wanapoweza kufanya hivyo. Kwa sababu ya ukosefu wa fedha, wanaishi popote pale mara nyingi ambapo hapana maji ya kunywa wala hakuna mfumo wa maji taka. Baadhi yao huchimba visima vifupi vya hadi mita tatu hivi hadi wapate maji. Kwenye mwezi Novemba hivi, mvua za mwanzo huanza kunyesha, hivyo kufanya uwezekano wa kupata maji kwa majirani hawa. Mwishowe, uhaba wa maji huchangia katika kuongeza umaskini na vyote hivyo husababisha maradhi.</p>
<p>Kuna hali fulani ya mambo mbalimbali na tofauti kuwa pamoja . Mimi napata maji nyumbani lakini jirani zangu hawapati. Hili ni jambo zito kwa familia. Kwa upande wangu, ninawagawia maji familia nyingine. Basilio naJuana wana watoto wanne. Wanaishi katika nyumba ya kupanga. Nyumba wanamoishi haina maji yanayofaa kunywa. Kila wanapoyahitaji, basi hawana budi kutumia mpira ili kupata maji kutoka nyumbani kwangu na mwisho wa mwezi basi tunagawana gharama kadiri ya ankra. </p></blockquote>
<p>Hata hivyo, siyo tu kwamba Tuni Condoriri hutoa maji ya kunywa kwa ajili ya jiji hilo tu, lakini pia hutoa maji kwa ajili ya shughuli za kilimo kwenye safu za Altiplano. Endapo uendelezaji wa shughuli za kilimo utapungua kwa sababu ya uhaba wa maji, watu wengi zaidi kutoka maeneo ya vijijini watatiririka kwenda El Alto kujitafutia maisha, ambapo watakumbana na tatizo lile lile la uhaba wa maji na papo hapo wakiongeza mahitaji ya maji. </p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Wanaharakati wa 350.org wakikwea kwenye mlima barafu Chacaltaya huko Bolivia kufanya maandalizi ya tukio kubwa mnamo tarehe 24 Oktoba. Picha imetumika chini ya leseni ya haki miliki huru." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/chacaltaya.jpg" title="chacaltaya" width="400" height="268" /><p class="wp-caption-text">Wanaharakati wa 350.org wakikwea kwenye &#39;mlima&#39; barafu Chacaltaya huko Bolivia kufanya maandalizi ya tukio kubwa mnamo tarehe 24 Oktoba. Picha imetumika chini ya leseni ya haki miliki huru.</p></div>
<p>Ni sura inayopewa kipa umbele ya barafu iliyoko kwenye mlima wa Chacaltaya ndiyo inayovuta usikivu wa ofisa wa serikali za mitaa na vikundi vingine vya wanaharakati ili kutazama tatizo la mabadiliko ya hali ya hewa katika ukanda wa Bolivia. <a href="http://www.facebook.com/event.php?eid=173999981920&#038;ref=nf">Tukio lililotokea mahali hapo siku za hivi karibuni lililohusiana na kampeni ya 350.org lilitangazwa katika Facebook [es]</a>, likiwaalika raia wa Bolivia kutembelea &#8216;mlima&#39; barafu wa Chacaltaya kujionea wenyewe madhara yanayofanyika. </p>
<p>Hatimaye, Oblitas <a href="http://monioblitas.blogspot.com/2008/06/glaciar-nuestro-tesoro-se-derrite.html">anahitimisha kwa swali hili lifuatalo [es]</a>:</p>
<blockquote><p>Chacaltaya ya no está y pronto dejarán de existir otros glaciares, ¿está el país preparado para esas pérdidas?, ¿somos conscientes de la importancia de tomar un rol activo e inmediato contra el calentamiento? Para muchos, el cambio climático no es un fenómeno global y no creen sentirse afectados, pero lo cierto es que absolutamente todos estamos en riesgo y no todos podemos enfrentarlo en las mismas condiciones. La lucha continúa, aunque ya sea tarde para lugares como Chacaltaya.</p></blockquote>
<div class="translation">&#8216;Mlima&#39; barafu wa Chacaltaya haupo tena, vilevile hivi karibuni &#8216;milima&#39; barafu mingine nayo itatoweka. Je, nchi iko tayari kupata hasara hii? Je, tunatambua umuhimu wa kuchukua wajibu wa haraka wa kushiriki kukabili kuongezeka kwa joto duniani? Kwa walio wengi, mabadiliko ya hali ya hewa si tatizo la kiulimwengu na hawajihisi kuathiriwa, kila mmoja yuko kwenye hatari ingawa si kila mmoja anaweza kukabiliana na hatari hiyo kwa namna moja. Mapambano yanaendelea, hata kama tayari tumechelewa katika maeneo kama Chacaltaya.</div>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/bolivia-uhaba-wa-maji-kwa-sababu-ya-theluji-inayoyeyuka/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Irani: Vuguvugu la Kijani Laupinga Utawala Tena</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/irani-vuguvugu-la-kijani-laupinga-utawala-tena/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/irani-vuguvugu-la-kijani-laupinga-utawala-tena/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:29:03 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Farsi]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Iran]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=552</guid>
		<description><![CDATA[Upande wa upinzani wa Vuguvugu la Kijani nchini Irani mnamo tarehe 4 Novemba uliendesha maandamano makubwa ambapo maandamano hayo yalikabiliwa na matumizi makubwa ya nguvu ya kuyazuia yaliyofanywa na vikosi vya usalma. Kama ambavyo sasa inatarajiwa, uandishi wa habari wa kiraia nchini Irani haukukosa kitu kwani ulirekodi 'historia' hiyo kupitia simu zao za mikononi. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/hamid-tehrani/">Hamid Tehrani</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/iran-green-movement-defies-regime-again/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/13aban.jpg" class="alignleft" width="200" height="269" /><br />
Upande wa upinzani wa Vuguvugu la Kijani nchini Irani mnamo tarehe 4 Novemba mwaka huu (13 ya Abani) <a href="http://www.guardian.co.uk/world/blog/2009/nov/04/iran-student-day-protests">uliendesha</a> maandamano makubwa ya mitaani, baada ya kutumia fursa ya maandamano rasmi yaliyoendeshwa siku hiyo ya kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 30 ya ukaliaji wa Ubalozi wa Marekani jijini Teherani.  Maandamano hayo ya upinzani yalikabiliwa na matumizi ya nguvu kupita kiasi ya kuyavunja yaliyofanywa na vikosi vya usalama.</p>
<p>Kama ambavyo sasa imekuwa jambo la kutarajiwa, vyombo vya habari vya kiraia vya Irani vilirekodi &#8216;historia&#39; hiyo kupitia simu zao za mkononi.</p>
<p>Waandamanaji jijini Teherani walikanyagakanyaga picha ya Kiongozi Mkuu wa Kidini nchini humo, Ayatollah Ali Khamenei, kitendo ambacho wala kisingefikiriwa miezi michache tu iliyopita. </p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/ROBiaGs7OYo&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/ROBiaGs7OYo&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Ujumbe kwa Obama: Ama uko upande wetu au uko upande wao.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/x-yLLZ3JGfM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/x-yLLZ3JGfM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kiongozi wa upinzani, Mehdi Karoubi, akiwa katikati ya watu.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/UuGNPxkIXU4&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/UuGNPxkIXU4&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Vikosi vya Usalama vikishambulia waandamanaji.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/AIiAopKXE7w&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/AIiAopKXE7w&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/irani-vuguvugu-la-kijani-laupinga-utawala-tena/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Amerika ya Kati: Kasi Kubwa ya Ueneaji wa Jangwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:24:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Chile]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=556</guid>
		<description><![CDATA[Ueneaji wa jangwa unasambaa kimyakimya lakini kwa kasi kubwa mahali pengi duniani na Amerika ya Kati haijaweza kukwepa hali hii iliyo na athari mbaya za kutisha. Wakati ambapo majangwa ni maumbo ya asili, ueneaji wa jangwa ni mchakato wa kuharibika kwa nyanda za ardhi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu unaofanywa na binadamu. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/belen-bogado/">Belen Bogado</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/  '>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Pengine maneno ueneaji jangwa yanaweza kusikika sawa na jangwa, lakini kuna tofauti kubwa ya msingi kati ya maneno hayo: wakati ambapo majangwa ni moja kati ya maumbo mazuri ya kipekee ya asili, ueneaji jangwa ni mchakato wa kuharibika ambako kanda za ardhi hupitia baada ya kuathiriwa vibaya na mabadiliko ya hali ya hewa, shughuli za binadamu na majanga ya asili mpaka hatimaye zinageuka na kuwa majangwa.</p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/desertification.jpg" title="desertification" width="400" height="258" /><p class="wp-caption-text">Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons.</p></div>
<p>Ingawa athari ya mabadiliko ya hali ya hewa katika ueneaji jangwa bado haijaeleweka vema, yaani kwa mujibu wa GreenFacts, inafahamika kwamba <a href="http://www.greenfacts.org/en/desertification/index.htm">viwango vya juu vya joto vinavyotokana na kuongezeka kwa viwango vya dioksidii ya kaboni kunaweza kuwa na athari mbaya kutokana na kuongezeka kwa upotevu wa maji kutoka ardhini na kupungua kwa viwango vya mvua katika maeneo yenye ukame</a>. Wakati huohuo ueneaji jangwa nao huchangia katika mabadiliko ya hali ya hewa kwa kuruhusu kaboni iliyohifadhiwa kwenye mimea ya maeneo yenye ukame na udongo kurushwa kwenye anga.</p>
<p>Ueneaji jangwa unazidi kuwa na athari mahali pote duniani. Kwa sasa hivi ueneaji huo unaathiri mavuno, unasababisha kupanda kwa bei za vyakula vilivyopo, na katika baadhi ya maeneo, hata wanyama wanakufa. Watu wanalazimika kuhamia maeneo mengine ya mbali na nyumbani kwao, kama anavyoeleza mwanablogu Miguel Angel Alvarado anayetokea El Salvador <a href="http://www.ecoportal.net/content/view/full/61308/">kuhusu mpango wa kuhamisha makazi ya rais kwa sababu ya ueneaji jangwa[es]</a>:</p>
<blockquote><p>El traslado de casa presidencial, del Barrio san Jacinto al local en donde estaba el Ministerio de Relaciones exteriores, según informes extrajudiciales, obedece a la prevención del ejecutivo ante un posible hundimiento del suelo generado por cárcavas en este sector.</p></blockquote>
<div class="translation">Kwa mujibu wa nyaraka zisizo rasmi kisheria, kuhamishwa kwa makazi ya rais kutoka maeneo ya San Jacinto kwenda ilipokuwa Wizara ya Mambo ya Nje hapo awali, ilikuwa ni hatua ya kujihami iliyofanywa na mhimili wa dola ili kuepuka kutitia kwa ardhi kutokana na makorongo yaliyotokea pale.</div>
<p>Bara lililoathiriwa zaidi ni Afrika, na jambo hili linaweza kuonekana zaidi nchini Kenya, ambapo moja ya sekta zinazoweza kupata athari kubwa za ueneaji jangwa na ukame ni wasichana. Pale maji yaliyohifadhiwa kwenye matenki yalipokuwa yametumika yote katika Nyumba ya Watoto Yatima ya Dago Dala Hera huko Magharibi mwa Kenya, akina mama wanaojitolea na watoto wanalazimika kuteka maji yasiyo salama kutoka katika mto ulio karibu kwa ajili ya kupikia na kunywa. <a href="http://us.oneworld.net/article/367320-africa-famine-deepens-drought-worst-decades">“Kwenda mtoni kuteka maji peke yao nyakati za jioni kunawaweka wasichana katika hatari ya kukumbana na wanaume wanaoweza kuwanyanyasa kingono,”</a> alisema Edwin Odoyo, ambaye mama yake anayeitwa Pamela ndiye aliyeanzisha makazi hayo ya watoto yatima.</p>
<p>Ingawa ueneaji jangwa una athari kubwa zaidi barani Afrika, hali ya mazingira ya Amerika ya Kati nayo inapitia mabadiliko makubwa, kama ilivyojadiliwa siku za karibuni katika Mkutano wa Tisa wa Kongamano kuelekea Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Kukabili Ueneaji Jangwa uliofanyika jijini Buenos Aires, Ajentina. Mtaalamu wa Kiitaliano, Massimo Candelori, aliyekuwa mwakilishi wa Mkataba wa Kukabili Uenejaji Jangwa, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=esp&#038;idnews=3422">alisema katika mahojiano na  Tierramerica</a> kwamba hali ilivyo Amerika ya Kati inatisha kwa kuzingatia kwamba hakuna taarifa za kutosha kuhusu kiwango cha ueneaji jangwa katika eneo hilo. “Hatuna takwimu za sasa hivi. Moja ya lengo lililojadiliwa katika Mkutano wa Tisa lilikuwa ni kupata viashirio vinavyoturuhusu kuelewa vizuri zaidi hali halisi &#8230; takwimu tulizonazo mpaka sasa ni zile za miaka kumi iliyopita,” alisema Candelori.</p>
<p>Katika nchi za Amerika ya Kati ambapo kilimo na ufugaji ni moja ya sekta kuu za uchumi, ueneaji jangwa unaweza kuwa wa kimyakimya, lakini wenye madhara makubwa kama mnyama hatari mwindaji. Walau <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">asilimia 25 ya sehemu ya eneo zima</a> tayari imeharibiwa na wakati huohuo watu wanazidi kuwa na wasiwasi juu ya suala hili, kama inavyojionyesha katika blogu mbalimbali. </p>
<p><em>Eco Briefings [pt]</em>, blogu ya KiBrazili, inaonyesha kwamba <a href="http://ecobriefings.com/2009/10/05/desertificao/">WaBrazili waishio Kaskazini Mashariki mwa nchi wanashuhudia ueneaji wa kasi sana wa jangwa[pt]</a>:</p>
<blockquote><p>Mais um alerta está ligado. Temos pouco tempo para corrigir as coisas. (…)</p>
<p>No Brasil a desertificação tem avançado na caatinga, e zonas do polígono da seca no Nordeste e Norte de Minas Gerais, e também em Estados que antes não tinham áreas secas ou desertificadas como o Rio Grande do Sul. O Rio Amazonas viveu já uma grande seca a pouco tempo, grande com mortandade de peixes.</p></blockquote>
<div class="translation">Kiitia hatari kingine kinanguruma. Tuna muda mfupi sana wa kurekebisha mambo (…)</p>
<p>Nchini Brazili, ueneaji jangwa umeongezeka sana katika Caatinga, katika ukanda wa maeneo kame Kaskazini Mashariki na Kaskazini mwa jimbo la Minas Gerais, na vilevile katika majimbo ambayo hayakukumbwa na ukame wala ueneaji jangwa hapo kabla kama vile Rio Grande do Sul. Mto Amazon umepitia ukame mkubwa kabisa katika kipindi kifupi kilichopita, jambo lililosababisha samaki kufa kwa idadi kubwa.</p></div>
<p>Ajentina nayo ina maeneo kadhaa yaliyoathiriwa. Katika mkoa wa Valles Aridos, Kaskazini Mashariki, ambapo shughuli kuu ya kiuchumi ni ufugaji kondoo, inakadiriwa kwamba <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/www.inta.gov.ar/salta/info/documentos/Desertificaci%C3%B3n.pdf">katika miaka 100 iliyopita, walau watu 180,000 walilazimika kuhama. [es] (katika mfumo wa .pdf)</a>. Kusini mwa nchi ya Ajentina nako hakujapona na ueneaji jangwa. Mwanablogu Ailen Romero, anaandika maoni katika blogu inayoitwa <em>Geoperspectivas [es]</em> <a href="http://geoperspectivas.blogspot.com/2009/06/dia-mundial-de-la-desertificacion-2009.html">kwamba katika mkoa wa Patagonia, juhudi za serikali za kukabili ueneaji jangwa bado hazitoshi</a>:</p>
<blockquote><p>En la Patagonia, la amplitud del problema es de tal magnitud que ha comenzado a adquirir estado público. Pocos ignoran el tema, pero pocos tienen la posibilidad de actuar de alguna forma o con el conocimiento para hacerlo. El problema de la desertificación en el caso de la Patagonia supera a los planes que se han elaborado para combatirlo. Es por eso que no deben ahorrarse esfuerzos, ni limitar la imaginación de soluciones alternativas.”Si la geografía es la manifestación de la sociedad en el espacio físico, un espacio físico deteriorado refleja una sociedad deteriorada” afirman del Valle y Coronato(investigadores del Centro Nacional Patagónico)</p></blockquote>
<div class="translation">Katika Patagonia, ukali wa tatizo ni mkubwa kiasi kwamba umma wote umetambua tatizo hilo. Ni watu wachache tu ndiyo wanaolipuuza na ni wachache tu walio na nafasi au maarifa ya kufanya juhudi kulikabili. Tatizo la ueneaji jangwa huko Patagonia unazidi mipango iliyokwishaainishwa kulikabili. Ndiyo sababu kila juhudi haina budi kufanywa, wala kusiwe na mipaka katika kufikiria ufumbuzi mwingine wowote. ‘Kama Jiografia ni kielelezo cha jamii katika nafasi halisia, kuharibika kwa nafasi halisia huko kunaakisi kuharibika kwa jamii, wanasema  Valle na Coronato (watafiti kutoka katika Kituo cha Taifa cha Patagonia).</div>
<p>Huko Chile, ambapo <a href="http://www.conaf.cl/?seccion_id=8ad00d8dd61d22aa152575a1e5c08e58&#038;unidad=0&#038;PHPSESSID=db19e79870c9e01418e62b8576a26daf">takribani asilimia 62 ya eneo la taifa tayari imeathiriwa na ueneaji jangwa [es]</a>, mwanablogu Alfredo Erlwein alieleza wasiwasi kupitia katika blogu inayoitwa <em>El Ciudadano [es]</em>(Raia) kuhusu jinsi gani watu <a href="http://www.elciudadano.cl/2009/03/26/desertificacion-y-sequia-el-gran-problema-ambiental-de-chile-y-el-mundo/">wasiyo na maarifa ya kutosha kuhusu ueneaji jangwa</a>.</p>
<blockquote><p>
Efectivamente la desertificación es el problema ambiental más grave de Chile y muy poco conocido. Existen grandes zonas, como en la costa de la octava región, donde la erosión severa supera el 50% de la superficie: esto es que literalmente más de la mitad de los suelos se ha perdido por completo. En esas zonas se encuentran cárcavas de más de 50 metros de profundidad. Una tasa normal de formación de suelo puede ser de 0.2 cm por año, lo que evidencia la gravedad del asunto.</p></blockquote>
<div class="translation">Ueneaji jangwa kwa hakika ni tatizo kubwa kabisa lakini lisilofahamika miongoni mwa matatizo ya kimazingira nchini Chile. Kuna maeneo makubwa, kama vile pwani ya Nane ya Mkoa, ambapo mmomonyoko mkali wa udongo unazidi asilimia 50 ya ardhi: hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya ardhi imepotea, huo ndiyo ukweli. Katika maeneo hayo kuna makorongo yenye kina cha mpaka mita 50. Kiwango cha kawaida cha utengenezekaji ardhi ni kama sm 0.2 kwa mwaka, huo ndiyo uthibitisho wa ukali wa tatizo lililopo.</div>
<p>Kwa mujibu wa mtaalamu Mwitaliano Candelori, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">kutumia udongo katika soko la Kaboni kutasaidia kupambana na ueneaji jangwa</a>; jambo hili pengine litaamuliwa katika Kongamano litakalofanyika jijini Copenhagen. Tayari kongamano hilo limeanza kuhesabiwa siku na ulimwengu unalisubiri kwa hamu.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kutambulisha Sauti Zinazotishwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kutambulisha-sauti-zinazotishwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kutambulisha-sauti-zinazotishwa/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:08:01 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Announcements]]></category>
		<category><![CDATA[Blogger News]]></category>
		<category><![CDATA[Blogger Profiles]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Projects]]></category>
		<category><![CDATA[Software & Tools]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=554</guid>
		<description><![CDATA[Leo, kitengo cha utetezi cha Global Voices, kinazindua tovuti mpya inayoitwa Threatened Voices, yaani, Sauti Zinazotishwa ili kusaidia kufuatilia unyamazishaji wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni. Inaonyesha ramani ya dunia na mwingiliano wa saa unaosaidia kuonyesha taarifa za vitisho na ukamataji unaofanywa dhidi ya wanablogu duniani kote, na ni mhimili mkuu wa kukusanyia taarifa kutoka katika asasi na wanaharakati walioamua kujitoa muhanga kwelikweli. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/sami-ben-gharbia/">Sami Ben Gharbia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/03/introducing-threatened-voices/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/threatened-logo-1.gif" title="threatened-logo" class="aligncenter" width="352" height="77" /><br />
Haijawahi kutokea hapo kabla kwamba watu wengi kiasi hicho wametishwa au kutupwa gerezani kwa sababu ya maneno wanayoandika kwenye mtandao.</p>
<p>Kwa kuwa wanaharakati wengi na raia wa kawaida wameongeza sana utumiaji wa Intaneti ili kutoa maoni yao na kuwasiliana na wengine, serikali nyingi pia zimeongeza ufuatiliaji wa kichunguzi, kujipenyeza, uchukuaji wa hatua za kisheria na unyanyasaji. Matokeo mabaya zaidi ya vitendo hivyo yanapata hasa msukumo wa kisiasa na hivyo kusababisha ukamataji wa wanablogu na waandishi wengine wa mtandaoni kutokana na shughuli zao za mtandaoni na nje ya mtandao, katika baadhi ya matukio ya kusikitisha hata vifo vimetokea. Waandishi wa habari wa mtandaoni na wanablogu wanawakilisha <a href="http://cpj.org/imprisoned/cpjs-2008-census-online-journalists-now-jailed-mor.php">asilimia 45 ya wanahabari </a>walio magerezani duniani kote.</p>
<p>Leo, <a href="http://advocacy.globalvoicesonline.org/">kitengo cha utetezi cha Global Voices</a>, kinazindua tovuti mpya inayoitwa <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/">Threatened Voices</a>, yaani, Sauti Zinazotishwa ili kusaidia kufuatilia unyamazishaji wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni. Inaonyesha ramani ya dunia na mwingiliano wa saa unaosaidia kuonyesha taarifa za vitisho na ukamataji unaofanywa dhidi ya wanablogu duniani kote, na ni mhimili mkuu wa kukusanyia taarifa kutoka katika asasi na wanaharakati walioamua kujitoa muhanga kwelikweli, zikiwemo <a href="http://www.committeetoprotectbloggers.org/">Committee to Protect Bloggers</a> (Kamati ya Kuwalinda Wanablogu), <a href="http://www.anhri.net/en/">The Arabic Network for Human Rights Information</a> (Mtandao wa Kiarabu wa Haki za Binadamu kwa Taarifa), <a href="http://rsf.org/">Wanahabari Wasio na Mipaka</a>, <a href="http://hrw.org/">Shrika la Kuchunguza Haki za Binadamu</a>, B<a href="http://cyberlaw.org.uk/">logu ya Sherika za Mitandao</a>, <a href="http://www.amnesty.org/">Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu</a>, <a href="http://www.cpj.org/">Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari</a>, <a href="http://advocacy.globalvoicesonline.org/">Kitengo cha Utetezi cha Global Voices</a>.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/threatened_voices1.jpg" title="threatened_voices" class="aligncenter" width="450" height="352" /></p>
<p><strong>Mwanablogu yupi, wapi?</strong></p>
<p>Kupata taarifa sahihi kuhusu wanablogu na waandishi wa mitandaoni waliokamatwa ni jambo gumu kwa sababu mbalimbali.</p>
<p>Kwanza, usiri unaotawala udhibiti wa mtandaoni na ukandamizaji unafanya taarifa sahihi liwe jambo gumu sana. Hakuna wiki inayopita bila kuwepo habari za kukamwatwa kwa mwandishi au mwanaharakati mwingine wa mtandaoni katika nchi kama vile Misri au Irani, lakini undani na sababu mara nyingi hugubikwa na utata usioelezeka.</p>
<p>Pili, bado kuna mkanganyiko kuhusu ufafanuzi wa &#8220;Mwanablogu&#8221; ni nani. Wanahabari mahiri wanazidi kuhamia katika matumizi ya vyombo vya habari vya mtandaoni na blogu ili kutafuta uhuru zaidi, hivyo kufanya ufafanuzi uliokuwepo hapo kabla kuingia ukungu. Na wengi kati ya wale wanaoitwa watukutu wa mitandaoni huko Uchina, Tunisia, Vietinamu, au Irani, hawana blogu zao binafsi. Katika nyakati nyingine, wanablogu hukamatwa kwa sababu ya shughuli zao zilizo nje ya mtandao, kuliko yale waliyoyachapishwa kwenye mtandao.</p>
<p>Mkanganyiko huu mara nyingine umefanya iwe vigumu kwa watetezi wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni kuja na mkakati na ushirikiano wa kuwatetea wanablogu na wanaharakati wa mtandaoni, lakini haikutokea kuwa ni muhimu zaidi kujaribu.</p>
<p><strong>Tushirikiane</strong></p>
<p>Katika <a href="http://globalvoicesonline.org/">Global Voices</a> tunawashirikisha waandishi, wahariri, na watafsiri, ambao hutufahamisha kuhusu ukiukwaji wa uhuru wa kujieleza na haki za binadamu.  Kwa kuanzisha <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/">Threatened Voices</a> tunakusudia <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/submit">kufungua mchakato wa kutolea taarifa</a> hata kwa mtu mwingine zaidi aliye na taarifa fulani.</p>
<p>Tunatoa wito kwa wale wote ambao rafiki, ndugu, wenzao, au wapiganaji wenzao wametishwa kwa namna moja au nyingine ili kusaidia <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/submit">kutengeneza</a> na kutoa taarifa mpya kuhusu wale waliopotea au waliokamatwa, ili kwamba tutafute vyanzo zaidi ili kuthibitisha na kuunganisha na kampeni za mtandaoni zinazolenga kuhakikisha wanaachiwa huru.</p>
<p>Katika mchakato, tunataraji kujifunza zaidi kuhusu ni lini, wapi na kwa kiasi gani wanablogu wanatendewa vibaya katika nchi mbalimbali, ili tuweze kuwashirikisha taarifa hizi waandishi wa habari, watafiti, na wanaharakati, na kujaribu kupigania uwepo wa Intaneti ambamo kila mmoja anaweza kutumia uhuru wake wa kujieleza, na mahali ambapo wanablogu walio magerezani hawasahauliwi.</p>
<p><strong>Saidia kueneza neno. Twiti, blogu na toa taarifa mpya kwenye facebook kuhusu <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/">Sauti Zinazotishwa</a>! </strong></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kutambulisha-sauti-zinazotishwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Watu 10 Wenye Ushawishi Zaidi Nchini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-watu-10-wenye-ushawishi-zaidi-nchini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-watu-10-wenye-ushawishi-zaidi-nchini/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 04 Nov 2009 10:42:30 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Business]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[Elections]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=517</guid>
		<description><![CDATA[Mtoto wa Rais wa Misri, Hosni Mubarak, anayitwa Gamal Mubarak, -- na ambaye anatarajiwa kumrithi baba yake nafasi hiyo -- aliibuka kama mmoja wa washindi 100 wa TIME. Wanablogu wa Ki-Misri wana ya kueleza kuhusu jambo hili. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/marwa-rakha/">Marwa Rakha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/29/egypt-the-top-10-most-influential-people/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mwanablogu <em>Ahmed Shokeir</em> aliendesha <a href="http://shokeir.blogspot.com/2009/10/2009.html">taftishi</a> ya kutafuta watu 10 wenye ushawishi zaidi nchini Misri baada ya <a href="http://shokeir.blogspot.com/2009/10/2009.html">kushangazwa </a>na matokeo ya <em><a href="http://globalvoicesonline.org/2009/08/16/egypt-gamal-mubarak-why-not/">Gamal Mubarak</a></em>, mtoto wa Rais Hosni Mubarak wa Misri - kama mmoja wa <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1886141,00.html">washindi 100 wa mwisho wa mwaka 2009 wa TIME</a>.</p>
<p>Shokeir anaandika: </p>
<blockquote><p>
المفاجأة الحقيقة كانت في إسم الشخصية العربية التالية والتي تظهر في القائمة أيضا للمرة الأولى وتحتل المركز الثامن عشر بفارق بسيط عن الشيخ أحمد وتحصل على ثمانمائة وثلاثون ألف صوت بمتوسط 31 نقطة وهو جمال مبارك متقدماً على أسماء مثل بريتني سبيرز التي حلت في المركز الثلاثون وباراك أوباما في المركز السابع والثلاثون
</p></blockquote>
<div class="translation">Jambo la kushangaza sana lilikuwa kwamba Mwarabu wa pili mwenye ushawishi zaidi baada ya Shehe <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1884132,00.html">Ahmed bin Zayed Al Nahyan</a>, ambaye ni mkurugenzi wa Abu Dhabi Investment Authority, aliyeshika nafasi ya 13 baada ya kupata kura 839,000. Kwa mara ya kwanza <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1885482,00.html">jina la Gamal Mubarak</a> limejitokeza katika nafasi ya 18 ya orodha baada ya kupata kiasi cha kura 832,593. Gamal Mubarak alimshinda <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1884106,00.html">Britney Spears</a> (aliyeshika nafasi ya 30) na <a href="http://www.time.com/time/specials/packages/article/0,28804,1883644_1883653_1883950,00.html">Barack Obama</a> (nafasi ya 37). </div>
<p><em>Zeinobia</em> <a href="http://egyptianchronicles.blogspot.com/2009/10/shokeirs-100-egyptian-2009.html">alikuja na orodha ya watu 10 wenye ushawishi zaidi nchini Misri</a> kwa mujibu wa taftishi ya Shokeir: </p>
<blockquote><p>Kwanza kabisa huwa hatuna aina hii ya ushindanishaji nchini Misri mara kwa mara, pili huna budi kutambua kwamba jambo hili liliendeshwa kwenye blogu ya nchini Misri, washiriki wanaweza kusemwa kwamba ilikuwa ni sampuli ndogo sana katika jamii ya Wa-Misri &#8220;Zaidi ya washiriki 120 kwenye blogu yake na <a href="http://www.facebook.com/event.php?eid=139748076249">zaidi ya washiriki 300 kwenye tukio katika face book</a>&#8221; na kwa hiyo baadhi ya watu huenda watasema kwamba sampuli haikuwa wakilishi vya kutosha, hata hivyo, kwa namna ya kushangaza kabisa, baadhi ya majibu yanawakilisha maoni ya Wa-Misri walio wengi. </p></blockquote>
<p>Akitunza kile kizuri ili kukitoa mwishoni kabisa, <em>Zeinobia</em> alianza na washindi bora 9: </p>
<blockquote><p>Katika nafasi ya 10 yenye pointi 168 yupo kocha wa timu ya taifa ya soka ya Misri Hassan Shahata.<br />
Katika nafasi ya 9 yenye pointi 181 ni mfanyabiashara Naguib Sawiris.<br />
Katika nafasi ya 8 yenye pointi 200 ni Rais Hosni Mubarak. &#8220;kura 26&#8243;<br />
Katika nafasi ya 7 yenye pointi 200 ni mwandishi wa habari Ibrahim Eissa. &#8220;Kura 46&#8243;<br />
Katika nafasi ya 6 yenye pointi 202 ni mfanyabiashara Ahmed Ezz.<br />
Katika nafasi ya 5 yenye pointi 215 ni mwanasayansi Ahmed Zowail.<br />
Katika nafasi ya 4 yenye pointi 262 ni mwendesha kipindi cha TV Mona El-Shazely.<br />
Katika nafasi ya 3 yenye pointi 325 ni mcheza soka Mohamed Abu-Tarika.<br />
Katika nafasi ya 2 yenye pointi 364 ni Gamal Mubarak.</p></blockquote>
<p>Sasa kuhusu mtu mwenye ushawishi zaidi nchini Misri, </p>
<blockquote><p>Na kwa mshangao wangu mkubwa:</p>
<p>Katika nafasi ya 1 yenye pointi 496 ni Mhubiri wa dini ya Kiislamu kwenye TV Amr Khalid.<br />
Hakuna shaka kwamba hao wengine tisa ukitoa Ahmed Zoweil wamekuwa na nafasi ya pekee katika maisha yetu katika mwaka 2009,lakini Amr Khalid!!??</p></blockquote>
<p>Zeinobia anatambua kwamba: </p>
<blockquote><p>Taftishi hii ilikuja katika kilele cha matukio ya Khalid hasa kwa umaarufu wake kutokana na vipindi vyake vya TV vya wakati wa Ramadhani, hivyo hicho kilichangia sana matokeo hayo na bila shaka nafasi ya dini katika maisha yetu. </p></blockquote>
<p>Hata hivyo, bado anajiuliza kama kweli alistahili kushika nafsi ya kwanza kwenye orodha hiyo.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-watu-10-wenye-ushawishi-zaidi-nchini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Japan: Mkeo anapougua</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/japan-mkeo-anapougua/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/japan-mkeo-anapougua/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 02 Nov 2009 12:26:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Japan]]></category>
		<category><![CDATA[Japanese]]></category>
		<category><![CDATA[Labor]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=494</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naTomomi Sasaki  &#183; Imetafsiriwa na Deogratias Simba &#183;  Angalia ujumbe mama 
Pale utamaduni wa &#8220;mifugo ya mashirika&#8221; au kwa maneno mengine “utamaduni wa ujumla wa wafanyakazi” (社蓄 shachiku) na maadili ya ndoa vinapogongana - zaidi ya watu 300 walitoa majibu kuhusiana na swali lililoulizwa kwenye jukwaa kubwa la mijadala lijulikanalo kama [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/tomomi-sasaki/">Tomomi Sasaki</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/29/japan-when-your-wife-is-sick/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Pale utamaduni wa &#8220;mifugo ya mashirika&#8221; au kwa maneno mengine “utamaduni wa ujumla wa wafanyakazi” (社蓄 <em>shachiku</em>) na maadili ya ndoa vinapogongana - zaidi ya watu 300 walitoa majibu kuhusiana na swali lililoulizwa kwenye jukwaa kubwa la mijadala lijulikanalo kama Hatsugen Komachi: <a href="http://komachi.yomiuri.co.jp/t/2009/1010/267719.htm?o=0&#038;p=0">Je, mwanaume aombe ruhusa kazini pale mkewe anapougua?<br />
</a><br />
<strong>Hali ilivyokuwa</strong></p>
<p>Rina amekuwa akiishi kwenye ndoa kwa miaka 8 sasa na binti yake anasoma darasa la tatu. Anataka kutalikiana na anarejea tukio moja katika ndoa yake ambalo limebaki katika akili yake tangu wakati huo. </p>
<p>Wakati binti yao alipokuwa akingali mchanga, Rina alinyong&#39;onyea sana kwa sababu ya kukosa usingizi kutokana na kulia sana kwa binti yao nyakati za usiku. Alipatwa na homa kali kiasi cha kushindwa kumhudumia binti yao mchanga, lakini mumewe alikataa katakata kuchukua likizo yenye malipo na alikataa pia kurejea nyumbani mapema kuliko ilivyo kawaida. Rina alihuzunika sana kwamba hata simu mumewe alikuwa hapigi. Ilimchukua takribani miezi miwili kwa hali yake kutengemaa tena na anashindwa kabisa kusahau jinsi mumewe alivyoshindwa kumsaidia katika kipindi hicho. </p>
<p><strong>Swali</strong></p>
<blockquote><p>
ここういう状態の場合、会社を休めないまでもせめて定時で帰ってきてほしいというのはわがままでしょうか。<br />
みなさんのご家庭はどうですか？妻が病気の時、夫は会社を休んで子供の世話をしてくれますか？また、会社で「妻が病気だから」と言って休んでいる人をどう思いますか？ </p></blockquote>
<div class="translation">
Katika hali ya namna hii, je, nitakuwa mbinafsi kwa kutaka mume wangu walau arejee nyumbani mapema pasipo kufanya kazi saa za ziada, kama si kuomba ruhusa siku nzima?<br />
Je, hali ikoje katika familia zenu? Je, mume wako huomba ruhusa kazini siku nzima ili kuwatunza watoto pale mke anapougua? Je, kuna watu kwenye kampuni yenu ambao huomba ruhusa kutokuwepo kazini kwa sababu mke wake anaumwa?  </div>
<p><strong>Majibu</strong></p>
<p>Mara moja, wanawake wengi wazazi wa muda mrefu walituma simulizi zao kuhusu nyakati kadhaa ambapo walikuwa wagonjwa lakini walijikokota kutoka kitandani ili kujitunza na kuwatunza watoto wao pasipo msaada wa waume zao - si kwa sababu walitarajia au walitaka msaada kutoka kwao.</p>
<p>‘Aliyeolewa na mwenye watoto wawili&#39; alisema:  </p>
<blockquote><p>
インフルエンザで寝込んでいるときも、４０度の熱が三日間下がらない時も、一週間３８度から熱が下がらずいた時も夫に休ん で欲しいと思ったことはありませんでした。夫の職種が営業だったので客先と約束があれば休めないのも仕方がないし、客先と急に約束が入ったら帰れないのも 仕方がないので。会社に勤めてお給料を頂いている以上会社に損害を与えるような休暇をとれないのは当たり前。<br />
トピ主様のご主人の業種がわかりませんが当人の体調不良と家族の体調不良はまた別でしょう。夫の風邪を理由に仕事を休む妻というのもありえないと思いますがどう思いますか？</p></blockquote>
<div class="translation">Hata wakati nilipokuwa hoi kitandani kwa sababu ya mafua, au nilipokuwa na homa kali ya nyuzi joto 40 kwa siku tatu mfululizo, au nyuzi joto 38 kwa wiki nzima, haikuwahi kupita akilini mwangu kuhitaji mume wangu akae nyumbani. Yeye ni bwana mauzo kwa hiyo hana budi kukutana na wateja wake na nyakati za usiku hakuwezi kuwepo na msaada kama kuna dharura.<br />
Ni wazi kwangu kwamba kama mtu anapokea mshahara, hawezi kupumzika baadhi ya siku, kwani jambo hilo litakuwa na athari mbaya kwa kampuni. Sina hakika mumeo anafanya kazi gani, lakini kuugua kwake na kuugua kwa mwanafamilia mwingine ni vitu viwili tofauti. Nashindwa kuamini kwamba kuna mwanamke anayetaka mumewe akae nyumbani siku yeye (mke) akiugua. Unawaza nini hapo? </div>
<p>Miri anasema, huna budi kuzingatia sifa ya mumeo. </p>
<blockquote><p>
旦那さんのお仕事の形態にもよると思いますが、急なお休みは周りにとても迷惑をかける事となります。それに自分(妻）の管理が出来ていない事で夫の会社に迷惑をかけるなぞ夫の評価を下げる事と思って居ます。<br />
妻が病気(入院する様な病気以外）夫が会社休むは普通とは思えません。ヘルパーさん頼むとか考えます。</p></blockquote>
<div class="translation">Kwanza inategemea kazi aliyonayo mumeo, lakini kuomba ruhusa za ghafla kazini kwa kawaida husababisha usumbufu mkubwa kwa wafanyakazi wenzake na kwa wateja. Kukosa kwako nidhamu ya kuchunga afya yako kunampunguzia sifa mumeo kazini kwa kusababisha usumbufu kwenye kampuni. Sidhani kama ni jambo la kawaida kwa mume kutofika kazini kwa sababu mkewe anaumwa, labda kama inampasa kulazwa hospitalini. Mimi ningewaza kumwajiri nesi au mhudumu. </div>
<p>Teardrop naye anakumbuka jambo kama hilo. Mumewe alikwenda zake kunywa na marafiki zake akimwacha yeye anaumwa, jambo lililosababisha ugomvi mkubwa. </p>
<blockquote><p>
でももっとびっくりしたのはこの話をした時の女性達の反応！「そんなことで・・・。」という反応なんですよね。ウチなんてもっとひどいわよ～って。<br />
妻たちはみんなこういう仕打ちに慣れてしまって、感覚がマヒしてしまっているんだなぁって、悲しく思ったことを覚えています。<br />
でもあれから数年・・・完全に私もマヒしてます。</p></blockquote>
<div class="translation">Kilichonishangaza zaidi (kuliko ukweli kwamba alikwenda zake kunywa) ilikuwa ni vitendo vya mashoga zangu! Waliniambia, &#8220;Je, umekasirika kwa sababu hiyo tu? Mimi nina tatizo kubwa zaidi!&#8221; Nakumbuka kuwaza jinsi gani ilivyo huzuni kwamba wake wanalazimika kuzoea unyanyasiaji huu kiasi cha kuwafanya wasiwe na hisia tena. Ni miaka michache imepita…. Na hisia zangu zimekufa kabisa. </div>
<p>Kanon anasema kwamba mumewe huonyesha mapenzi yake kwa njia nyingine. </p>
<p>夫の会社の激務や夫の社内での立場を思えば「体調悪いから帰ってきて！」とは言えません。私の体調の悪い時に夕飯を外で済ませてきてくれる。駅の自販機でポカリを買ってきてくれる。私にはそれだけで十分に優しい夫です。 </p>
<p>Ile kuwaza tu kuhusu kazi nyingi zinazomkabili mume wangu na jinsi wanavyomchukulia ofisini kwake, kwa kweli siwezi tu kusema “Tafadhali rudi nyumbani mapema kwa sababu sijisikii vizuri!”. Ninapoumwa, yeye hula chakula chake cha usiku mgahawani. Ananinunulia vinywaji baridi kwenye mashine ya vinywaji mtaani. Kwangu mimi huyu ni mume anayenijali kwa kufanya vitendo hivi. </p>
<p>‘Kengyo-shufu&#39; (mama wa nyumbani anayefanya kazi) anasema: </p>
<blockquote><p>
ちゃんと仕事をしたことないから言える言葉だと思います。<br />
ご主人だって休みたいんだと思います。でも休めないんですよ。自分が体調悪くて休むのは周りに風邪をうつしてはいけないとかそういったことではないですか?<br />
簡単に休めないという現在の多くの日本の企業が問題だと思いますが休めないのが現実です。</p></blockquote>
<div class="translation">Haya ni maneno ya mtu ambaye hajawahi kufanya kazi kamwe. Nafikiri mumeo anataka kukaa nyumbani, lakini anashindwa.<br />
Ukweli kwamba wafanyakazi wana wakati mgumu kupumzika siku moja moja ni tatizo linaloyakabili makampuni mengi makubwa ya Kijapani, lakini ukweli ni kwamba hawezi kujichukulia mapumziko tu. </div>
<p>Wapo wengine wanaomwonea huruma, kama nabe. </p>
<blockquote><p>
リナさんの言うことは正しいです。全然わがままではありません。<br />
　私はもちろん休んでいます。 […] 妻が病気になっても働く時代は終わってます。<br />
二人で力を合わせて生活守って時代です</p></blockquote>
<div class="translation">Rina, unachokisema ni sahihi. Hiyo wala si ubinafsi! Huwa ninaomba ruhusa ya kumpumzika pale mke wangu anapougua. […] Zama ambapo wanaume huwaacha nyumbani wake zao walio wagonjwa na wao kwenda kazini zimepita. Sasa, hatuna budi kuungana na kulinda uhai wetu.</div>
<p>Pochi anashangazwa na jinsi kila mmoja alivyo mkali, na kwa kukebehi anauliza kama <em>wanafanya</em> kazi kwa saa 15 - 16 kila siku katika mwaka mzima. </p>
<blockquote><p>家族がせっぱつまった状態のときに、仕事のほうがどうにか都合がつきそうだったら、少々遅刻して病院につれていくとか、コ ンビニで食料を調達するとか、残業はせずに急いで帰ってくるとかするのは社会人失格？頭から「休めるわけない！！」と決めつけるのは、ストイックな姿を会 社の人に見せたいから？自分の楽しみのために有給をとることもあるでしょう。（有給をとって友人とゴルフにいく上司をなんども見てます）</p></blockquote>
<div class="translation">Ikiwa ninampeleka hospitali mwanafamilia yangu na kuchelewa kufika kazini, au ninakwenda dukani kununua vyakula, au ninaharakisha kurejea nyumbani bila kufanya kazi katika saa za ziada pale hali inaporuhusu, je, hii ina maana kwamba mimi si mwanajumuiya kamili? Je, mnatangaza rasmi mapema kuwa “Siwezi kwamwe kupumzika hata siku moja!” kwa sababu tu unataka kujionyesha jinsi ulivyo na bidii kwa wenzako? Watu huchukua likizo zenye malipo kwa ajili ya kujiburudisha, au siyo? (Nimeona mara nyingi mabosi wakichukua likizo zenye malipo ili kwenda kucheza mchezo wa gofu na rafiki zao.)</div>
<p>Tokumei anasema inategemea unaumwa kiasi gani na anaongeza kusema: </p>
<blockquote><p>
結婚生活を快適に過ごすこつは、お互いに相手に期待しないことではないかともうすぐ銀婚式の私は思っています。期待すると裏切られたと思うし、期待しなければ些細な優しさもありがたく感じられます。再婚の際の参考までに</p></blockquote>
<div class="translation">Hivi karibuni nitasherehekea miaka 25 ya ndoa yangu, na ninaweza kukuambia kwamba siri ya kuwa na maisha yasiyo na mivutano mingi katika ndoa ni kutokuwa na matarajio makubwa sana kwa mwenzako. Kama hutarajii, basi akikufanyia hata jambo dogo jema basi litakufurahisha. Huu ni ushauri tu kama utatokea kuolewa tena. </div>
<p>Huu ni ushauri wa Echika: </p>
<blockquote><p>うちの会社の場合、男性が家庭の事情で会社を休むと、上司はあまりよく言いません。なので、私も自分の体調不良と偽って休暇をとり、妻の看病をしました。</p></blockquote>
<div class="translation">Bosi wangu huwa hawawafikirii vyema wanaume wanaoomba ruhusa kwa sababu ya matatizo ya kifamilia. Ninachofanya ni kuwaambia ofisini kwamba mimi ndiye ninayeumwa, kwa hiyo hukaa nyumbani na kumtunza mke wangu. </div>
<p>‘Usuaji&#39; anasema kwamba jambo hilo kwamwe haliwezekani katika kampuni anayofanyia kazi. </p>
<blockquote><p>
でも、文句を言い続けて一生夫婦であり続けることよりも、離婚と言う手段を選んだトピ主さんの勇気は素晴らしいと思います。</p></blockquote>
<blockquote><p>Pamoja na yote, nakupongeza kwa kuchagua kutalikiana na mumeo, kuliko kuishi naye maisha yote huku ukinung&#39;unika. </p></blockquote>
<p>Nya anasema kwamba inaweza kuwa ni jambo la kusumbua, lakini wanaume hawawezi kubahatisha kujua wanachokitaka wanawake, mpaka kielezwe bayana. </p>
<blockquote><p>妻が病気の時、「食事を作るのは難しいだろうから、外食して帰るよ」という夫さん、よくいますよ。高熱で起きられない妻の 食事は??思いつきません。面倒だけど「作れないのでコレコレを買ってきて(何か買ってとまかせると、こってりしたコンビニ弁当とか買ってきてしまう)」</p></blockquote>
<blockquote><p>
Kuna wanaume wengi ambao husema “Nitakula kabisa chakula cha usiku kabla ya kufika nyumbani kwa sababu najua itakuwa vigumu kwako kupika”. Yaani haiwaingii akilini kwamba mke mwenye homa kali naye anahitaji kula. Japokuwa ina usumbufu lakini huna budi kusema “Siwezi kupika leo, kwa hiyo tafadhali ninunulie hiki na kile”. Kama ukiwaachia, watakwenda kwenye duka ambapo watanunua kifurushi cha  chakula chenye mafuta mengi kutoka kwenye duka la walaji au chochote kile. </p></blockquote>
<p>Hatuna budi kutambua kwamba Hatsugen Komachi ana mwelekeo wa kike ua hata ule wa mwanamke mama wa nyumbani. Nyongeza ya kuvutia katika simulizi hili ni majibu kutoka kwa Hatena,ambaye ana mtazamo wa kiume zaidi, ambaye alitofautiana kabisa (<a href="http://b.hatena.ne.jp/entry/kusoshigoto.blog121.fc2.com/blog-entry-303.html">Hakuna kazi duniani iliyo muhimu zaidi ya afya yangu au ya familia yangu.</a> 自分、もしくは家族の健康にも優先する仕事なんてこの世に一つもない。) kama ilivyokuwa kwenye mjadala kuhusu utaalamu katika SNS LinkedIn (<a href="http://www.linkedin.com/news?viewArticle=&#038;articleID=78146724&#038;gid=1848408&#038;articleURL=http%3A%2F%2Fkusoshigoto%2Eblog121%2Efc2%2Ecom%2Fblog-entry-303%2Ehtml&#038;urlhash=uuar&#038;trk=news_discuss">ruhusa inatakiwa:Wafanyabiashara wa Kijapani wanatoa kafara familia zao</a>), lakini hiyo ni simulizi kwa ajili ya siku nyingine. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/japan-mkeo-anapougua/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
