Mosi Simba · Julai, 2010

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mosi Simba kutoka Julai, 2010

Thailand: Vurugu Zinazotokana na Ujumbe Mfupi wa Maneno wa Waziri Mkuu

  27 Julai 2010

Wakati Waziri mkuu wa Thailand Abhisit Vejjajiva alipotwaa madaraka mwaka 2008, alituma ujumbe mfupi wa maneno kwa mamilioni ya wateja wa simu za viganjani wa Thailand akiwataka wawe na umoja. Hivi sasa anakabiliwa na makosa ya ufisadi kwa kupokea "zawadi" kutoka mashirika ya mawasiliano. Kadhalika anashutumiwa kwa kuvunja mipaka ya ya faragha za wateja wa simu za viganjani.

Palestina: Mateso ya Kuwa Uhamishoni

Wakimbizi wa Kipalestina ni miongoni mwa watu ambao wamejikuta wakikimbilia uhamishoni ulimwenguni kote, Umoja wa Mataifa unatoa msaada kwa jumla ya wakimbizi waliosajiliwa wapatao milioni 4.7 katika ukanda unaokaliwa kwa nguvu huko Palestina, Jordan, Lebanoni na Syria. Mamilioni ya wakimbizi wa Kipalestina na wale walioteguliwa kutoka kwenye makazi yao wanaishi sehemu mbalimbali duniani. However, their Hata hivyo, watu hawa daima mioyo yao ipo nyumbani kwao, au kwa wazazi au mababu na mabibi zao waliobaki nyuma. Wanablogu wawili wa huko Gaza wameandika kuhusu mateso ya kuwa uhamishoni.

Ivory Coast: Mwanablogu na Mwandishi wa Habari Théophile Kouamouo Akamatwa Pamoja na Timu Yake Tangu Julai 13

Waandishi wa habari watatu wa Le Nouveau Courrier d'Abidjan walitiwa mbaroni na polisi baada ya kukataa kueleza vyanzo vya habari vya uandishi wao wa kipelelezi kuhusu biashara ya usafirishaji kahawa na kakao kwenda nje ya nchi. Yafuatayo ni maoni kutoka kwa raia na vyombo vya habari nchini Ivory Coast huku wenzao watatu wakiendelea kupigania kuachiwa kwa wanahabari hao.

Afrika ya Kusini: Dakika 67 za Mabadikio – Siku ya Mandela

Nelson Mandela alitumikia kifungo cha miaka 27 jela kule katika Kisiwa cha Robben, Afrika Kusini. Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba Madiba (kama ambavyo wengi wanapenda kumwita huko Afrika ya Kusini) alitumia miaka 67 ya maisha yake katika kupiga vita ubaguzi wa rangi na umaskini. Jumapili hii Julai 18 2010, kutakuwa na maadhimisho ya miaka yake 92 - na pia Siku ya Mandela - siku ambayo watu duniani kote watajitolea dakika 67 ili kuifanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi kwa wote.

Uganda: Wanablogu Washtushwa na Milipuko ya Mabomu

Mashabiki wa soka kote ulimwenguni walikusanyika kwenye kumbi za baa na migahawa ili kushuhudia mechi ya fainali za Kombe la Dunia usiku wa Jumapili iliyopita. Nchini uganda usherehekeaji huu ulikatishwa pale milipuko ya mabomu iliposambaratisha maeneo mawili maarufu kwa sherehe za mpaka majogoo jijini Kampala, mji mkuu wa nchi hiyo.