Joyce Maina · Aprili, 2013

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Joyce Maina kutoka Aprili, 2013

Urusi: Wapinzani Wapumbazwa na Uchaguzi wa Awali, Wapoteza Uchaguzi Halisi

RuNet Echo  30 Aprili 2013

Mwezi Agosti (mwaka 2012), Mtandao wa Sauti za Dunia uliripoti habari za wanaharakati kadhaa wanaohusika na vuguvugu la maandamano nchini Urusi wanaogombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa. Walitumaini itakuwa rahisi kushinda uchaguzi huo mdogo, ambao ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. Oktoba 14, 2012 huku idadi ya ndogo ya wapiga kura wakiojitokeza tena ndani ya madai ya siku nyingi ya wizi wa kura katika uchaguzi, Warusi walishiriki kwa maelfu katika uchaguzi nchini kote, kupiga kura kuwachagua mameya wa miji, madiwani, na wabunge wa mikoa.

Irani: Je, Dola Inamwogopa Msichana wa Miaka 13?

Kuwapiga watu marufuku kusafiri nje ya nchi yamekuwa mazoea ya serikali ya Irani  kwa makusudi ya kuwaghasi wanaharakati wa asasi za kisiasa na zile za kiraia kwa miaka mingi. Lakini, mahakama ya usalama iliwasha moto upya kwa kumpiga marufuku kusafiri nje ya nchi mume wa mwanasheria wa haki za binadamu aliyefungwa Nasrin Sotoudeh pamoja na binti yao mwenye umri wa miaka kumi na mitatu, Mehraveh Khandan. Nasrin Stoudeh amehukumiwa miaka kumi na moja gerezani.

Uganda: Kukumbuka milipuko ya mabomu ya 2010

Wananchi wa Uganda wameutumia mtandao wa Twita na Facebook kuwakumbuka wahanga 2010 wa milipuko yha mabomu iliyotokea kwenye klabu ya Rugby huko Kyaddondo na katika baa ya Kijiji cha Kiethiopia jijini Kampala Uganda.Mashambulizi hayo yalitokea wakati ambao wapenzi wa kandanda walikuwa wakitazama mpambano wa fainali kati ya Uhispania na Uholanzi uliofanyika nchini Afrika Kusini.

Iran: Wakati Matetemeko yanaua, “Televisheni Zinafundisha Sala”

Matetemeko makubwa mawili ya ardhi yalilitikisa eneo la kaskazini magharibi nchini Iran, Mashariki jimbo la Azarbaijan mnamo Jumamosi (Agosti 11, 2012), na kuua watu 250 na kujeruhi karibu 1800. Matetemeko ya ardhi kipimo cha 6.4 na 6.3 katika ukubwa, na kusababisha uharibifu mkubwa na mateso. Wa-Irani waliingia kwenye mtandao wa intaneti ili kuwaombolezea wahanga na kuomba watu kujitolea damu na msaada. Pia walionyesha hasira zao kwa televisheni ya kitaifa ya Iran, ambayo hutangaza vipindi vya dini, badala ya kutoa taarifa kwa watazamaji kuhusu matetemeko ya ardhi na jinsi ya kusaidia.

Misri: Mubarak ahukumiwa kifungo cha maisha

Dunia ilishuhudia wakati mahakama ya Misri  ilipomhukumu aliyekuwa Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak na Waziri wake wa Mambo ya Ndani Habib Al Adly kifungo cha maisha hivi leo kufuatia kukutwa na hatia ya kuhusika na mauaji ya waandamanaji.  Hukumu hiyo ilifikiwa baada ya vikao 49,  masaa 250, na kuandikwa katika kurasa 60,000.

Uturuki: Polisi Watumia Mabomu ya Machozi Kuwatawanya AkinaMama Waandamanaji

Wafungwa wa kisiasa wa Kikurdi wamefikia siku yao ya 55 ya mgomo wa kula. Kuna mamia ya wafungwa wa kisiasa walio kwenye mgomo wa kula nchini Uturuki, na hii imesababisha maandamano mshikamano katika bara la Ulaya, na hususani ndani ya Uturuki. Mapema jana [4 Novemba 2012], wanawake ambao ni mama wa baadhi ya wafungwa wa kisiasa walifanya maandamano ya kukaa, na walijikuta wakipambana na mabomu ya machozi, pamoja na kunyunyuziwa maji ya kuwasha. Wa- Kurdi duniani kote wanapinga kimya kinachotumika kushughulikia adha yao.

Bahrain: Nani Aliyesikia Milipuko ya Bomu na Nani ni Waathirika?

Wakuu wa Serikali nchini Bahrain wametangaza leo kwamba wafanyakazi wawili wa kigeni wameuawa na wa tatu akijeruhiwa vibaya katika milipuko mitano tofauti kwenye maeneo ya Gudaibiya na Adliya, kwenye mji mkuu Manama. kwenye mtandao wa twita, habari hizi zilipokelewa kwa mashaka, kutokuamini na kusababisha mwito kwa utatuzi wa kisiasa wa kumaliza hali ya ghasia katika nchi hiyo, kufuatilia kusambaa kwa maandamano ya kuipinga serikali yaliyoanza terehe 14 Februari, 2011.