GlobalVoices katika

Joyce Maina

Wasifu wa mwandishi · 19 jumbe · alijiunga 7 Juni 2012

Kiungo cha RSS kwa Joyce Maina Kiungo cha RSS kwa Joyce Maina

Am a Kenyan citizen living in Nairobi. Graduated in tourism and currently working as a Tour Operator.

Anwani ya Barua Pepe Joyce Maina

makala mpya zaidi ya Joyce Maina

30 Aprili 2013

Urusi: Wapinzani Wapumbazwa na Uchaguzi wa Awali, Wapoteza Uchaguzi Halisi

Soma makala hii. RuNet Echo

Mwezi Agosti (mwaka 2012), Mtandao wa Sauti za Dunia uliripoti habari za wanaharakati kadhaa wanaohusika na vuguvugu la maandamano nchini Urusi wanaogombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa. Walitumaini itakuwa rahisi kushinda uchaguzi huo mdogo, ambao ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita. Oktoba 14, 2012 huku idadi ya ndogo ya wapiga kura wakiojitokeza tena ndani ya madai ya siku nyingi ya wizi wa kura katika uchaguzi, Warusi walishiriki kwa maelfu katika uchaguzi nchini kote, kupiga kura kuwachagua mameya wa miji, madiwani, na wabunge wa mikoa.

Irani: Je, Dola Inamwogopa Msichana wa Miaka 13?

Soma makala hii.

Kuwapiga watu marufuku kusafiri nje ya nchi yamekuwa mazoea ya serikali ya Irani  kwa makusudi ya kuwaghasi wanaharakati wa asasi za kisiasa na zile za kiraia kwa miaka mingi. Lakini, mahakama ya usalama iliwasha moto upya kwa kumpiga marufuku kusafiri nje ya nchi mume wa mwanasheria wa haki za binadamu aliyefungwa Nasrin Sotoudeh pamoja na binti yao mwenye umri wa miaka kumi na mitatu, Mehraveh Khandan. Nasrin Stoudeh amehukumiwa miaka kumi na moja gerezani.

29 Aprili 2013

Ujasiriamali,Utamaduni na Mshikamano katika Afrika

Soma makala hii.

Pamoja na ukuaji mkubwa wa kiuchumi, bara la Afrika bado linahangaika kukuza kada ya wajasiriamali wazawa watakaoweza kudhibiti viwanda vya kimkakati. Wasomi na watafiti wengi wa ki-Afrika wanajaribu kuelewa atahri za tabia za kimila katika ujasiriamali barani humo.

28 Aprili 2013

Uganda: Kukumbuka milipuko ya mabomu ya 2010

Soma makala hii.

Wananchi wa Uganda wameutumia mtandao wa Twita na Facebook kuwakumbuka wahanga 2010 wa milipuko yha mabomu iliyotokea kwenye klabu ya Rugby huko Kyaddondo na katika baa ya Kijiji cha Kiethiopia jijini Kampala Uganda.Mashambulizi hayo yalitokea wakati ambao wapenzi wa kandanda walikuwa wakitazama mpambano wa fainali kati ya Uhispania na Uholanzi uliofanyika nchini Afrika Kusini.

21 Aprili 2013

Iran: Wakati Matetemeko yanaua, “Televisheni Zinafundisha Sala”

Soma makala hii.

Matetemeko makubwa mawili ya ardhi yalilitikisa eneo la kaskazini magharibi nchini Iran, Mashariki jimbo la Azarbaijan mnamo Jumamosi (Agosti 11, 2012), na kuua watu 250 na kujeruhi karibu 1800. Matetemeko ya ardhi kipimo cha 6.4 na 6.3 katika ukubwa, na kusababisha uharibifu mkubwa na mateso. Wa-Irani waliingia kwenye mtandao wa intaneti ili kuwaombolezea wahanga na kuomba watu kujitolea damu na msaada. Pia walionyesha hasira zao kwa televisheni ya kitaifa ya Iran, ambayo hutangaza vipindi vya dini, badala ya kutoa taarifa kwa watazamaji kuhusu matetemeko ya ardhi na jinsi ya kusaidia.

18 Aprili 2013

Misri: Mubarak ahukumiwa kifungo cha maisha

Soma makala hii.

Dunia ilishuhudia wakati mahakama ya Misri  ilipomhukumu aliyekuwa Rais wa zamani wa Misri Hosni Mubarak na Waziri wake wa Mambo ya Ndani Habib Al Adly kifungo cha maisha hivi leo kufuatia kukutwa na hatia ya kuhusika na mauaji ya waandamanaji.  Hukumu hiyo ilifikiwa baada ya vikao 49,  masaa 250, na kuandikwa katika kurasa 60,000.

16 Aprili 2013

Uturuki: Polisi Watumia Mabomu ya Machozi Kuwatawanya AkinaMama Waandamanaji

Soma makala hii.

Wafungwa wa kisiasa wa Kikurdi wamefikia siku yao ya 55 ya mgomo wa kula. Kuna mamia ya wafungwa wa kisiasa walio kwenye mgomo wa kula nchini Uturuki, na hii imesababisha maandamano mshikamano katika bara la Ulaya, na hususani ndani ya Uturuki. Mapema jana [4 Novemba 2012], wanawake ambao ni mama wa baadhi ya wafungwa wa kisiasa walifanya maandamano ya kukaa, na walijikuta wakipambana na mabomu ya machozi, pamoja na kunyunyuziwa maji ya kuwasha. Wa- Kurdi duniani kote wanapinga kimya kinachotumika kushughulikia adha yao.

11 Aprili 2013

Photos jumbe Video jumbe
Bahrain: ‘Kususia michezo ya Olimpiki’

Soma makala hii.

Wa-Bahraini wengi wanatoa mwito wa kususuia michezo ya Olympics. Kwanza, mwana wa mfalme, ambaye amekuwa akituhumiwa kwa kujihusisha na utesaji wa wanariadha, anahudhuria michezo hiyo. Pili, sehemu kubwa ya timu ya nchi hiyo imetengenezwa na wanariadha wa ki-Afrika.

8 Aprili 2013

Bahrain: Nani Aliyesikia Milipuko ya Bomu na Nani ni Waathirika?

Wakuu wa Serikali nchini Bahrain wametangaza leo kwamba wafanyakazi wawili wa kigeni wameuawa na wa tatu akijeruhiwa vibaya katika milipuko mitano tofauti kwenye maeneo ya Gudaibiya na Adliya, kwenye mji mkuu Manama. kwenye mtandao wa twita, habari hizi zilipokelewa kwa mashaka, kutokuamini na kusababisha mwito kwa utatuzi wa kisiasa wa kumaliza hali ya ghasia katika nchi hiyo, kufuatilia kusambaa kwa maandamano ya kuipinga serikali yaliyoanza terehe 14 Februari, 2011.

30 Septemba 2012

Kenya: Wito wa Mshikamano Baada ya Mashambulizi ya Kigaidi

Siku chache kabla ya ufunguzi  wa GV2012 mjini nairobi, Kenya ilikumbwa na milipuko na utekaji nyara huko Mombasa na mjini Garissa. Mlipuko ulitokea katika sehemu ya burudani mnano Juni 24 na kuwauwa watu watatu siku moja baada ya ubalozi wa marekani kuonya mamlaka ya Kenya kuhusu mashambulizi hayo jijini. Umati huo ulikuwa umekusanyika katika kilabu kutazama robo fainali  kati ya Uingereza na Italia.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha