<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; j nambiza tungaraza</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Urusi: Jinsi Abiria wa &#8220;Nevsky Express&#8221; Walivyoeleza Habari Kupitia Vyombo Vya Habari Vya Kijamii</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 01 Dec 2009 11:11:27 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Russian]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=738</guid>
		<description><![CDATA[Ajali ya treni la "Nevsky Express" ilitokea mbali na makazi ya watu. Ilichukua masaa kadhaa kwa wanahabari kufika kwenye eneo. Na hapo ndio picha na video za kwanza zilipoanza kuonekana kila mahali. je nini kilichotokea kwenye upashanaji habari wa kiraia ambao uliongoza njia ya kupashana habari wakati wa ajali ya ndege huko Urusi mwaka mmoja uliopita?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/gregory-asmolov/">Gregory Asmolov</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/29/russia-how-passengers-of-nevsky-express-tell-their-stories-through-social-media/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mamlaka nchini Urusi yanaendelea <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/28/russia-at-least-25-people-killed-in-the-neva-express-train-crash/">kuchunguza ajali ya treni la &#8220;Nevsky Express&#8221; </a>[ENG] ambayo ilitokea kati ya Moscow na St Petersburg usiku wa Ijumaa. Kwa mujibu wa maofisa, dhahama hiyo iliyochukua maisha ya angalau abiria 25 ilikuwa ni shambulio la kigaidi. Ajali hiyo imezua maswali mengi. Watu wengi wanauliza ni nini kilichotokea katika masaa ya mwanzo baada ya ajali na ni kwa nini ilichukua muda mrefu kuanza kutoa taarifa za ajali hiyo.</p>
<p>Kwa kuwa dhahama hiyo ilitokea mbali na maeneo yenye makazi ya watu, ilichukua muda mrefu kwa wanahabari kuwasili kwenye eneo la ajali. Na ndipo picha za kwanza na video zilipoanza kuonekana kila mahali. Je nini kilichoyatokea majukwaa ya uanahabari wa kijamii ambayo yalitaarifu vilivyo kuhusu <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/europe/7614951.stm">ajali ya ndege mjini Perm</a> [ENG] mwezi Septemba 2008.</p>
<p>Abira pekee ambaye alitoa taarifa mara moja kuhusu ajali ya “Nevsky Express” alikuwa mtumiaji wa Twita <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog</a>. Aliandika mara 12 kuhusu ajali hiyo kabla ya kuwasili nyumbani. Haya ndio aliyoandika: </p>
<blockquote><p>Nipo hai. Lakini nitaeleza kuhusu (ajali) baadaye. Kama mtu ataeleza chochote kwenye habari, tafadhali niandikie. Hawatuambii kila kitu hapa.</p></blockquote>
<p>Baadaye, abiria wengi kutoka mabehewa ya kwanza – ni mabehewa ya mwisho ambayo yaliteguliwa kutoka kwenye reli –walisema kuwa kwa saa zima baada ya ajali hawakufahamu chochote. <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy frog</a> alituma habari mpya za nyongeza: </p>
<blockquote><p>Tumepanda treni jingine. Nilifanya kila nilichoweza.</p>
<p>Hivi sasa tupo SAPSAN (treni mpya ambyo iliwachukua abiria kwenda St. Petersburg – G.A). Natamani ingekuwa inakwenda polepole.</p>
<p>Wametangaza sasa hivi kuwa watu walitayarishwa rasmi wangetulaki kwenye kituo cha treni.</p></blockquote>
<p>Siku iliyofuata baada ya dhahama, <a href="http://twitter.com/lazy_frog">Lazy Frog </a>aliandika muhtasari wa uzoefu wake:</p>
<blockquote><p>Nilizihisi hisia za kwanza kuhusu kilichotokea wakati tulipofika karibu na Piter (St. Petersburg G.A). Sikuwa na wasiwasi nilipokuwa katika eneo la ajali. Nilikuwa na hofu kidogo na viatu vyangu – kulikuwa na tope kila mahali na mawe yenye ncha.</p></blockquote>
<p>Jumamosi habari nyingi zilijitokeza wakati abiria walipoanza kublogu kuhusu yaliyowakuta. Makala ya blogu maarufu zaidi inayohusiana na mada hii iliandikwa na mtumiaji wa LJ <em>paltus_mk</em> [RUS] ambaye alikuwemo ndani ya mabehewa ya mwisho yaliharibiwa vibaya na mlipuko. <a href="http://paltus-nk.livejournal.com/23747.html">Aliandika </a>[RUS]:</p>
<blockquote><p>Yote yanatokea ndani ya sekunde 10 wakati unapofahamu ni nini kitakachotokea. Nilikuwa na muda wa kutosha kuutayarisha mwili wangu. Lakini hakuna linaloweza kusaidia dhidi ya kanuni za Newton wakati dazeni za tani za vyuma zinaposimama mara moja wakati zikiwa katika mwendo wa kasi – ni bahati tu… kwa hiyo nilikuwa na bahati tu. Kaka yangu alikuwa na bahati, pia, ukiachilia mbali ukweli kuwa majeraha yake yalikuwa yanatisha kuliko yangu.<br />
[…]</p></blockquote>
<blockquote><p>Kila kitu ambacho kilikwenda mrama hadi kusimama kabisa kulichukua kama sekunde 30 hivi. Ilikuwa giza na kimya. Watu walioumia walianza kulia. Nilikuwa sakafuni, nimekandamizwa na miili mingine. Niliisogeza ile miili. Niliona kuwa nimelowana na damu lakini damu ile haikuwa yangu. Niliona kuwa ni mzima na miguu yangu na mikono vuinafanya kazi. Kichwani nilikuwa na jeraha linalovuja damu. Ilinibidi ninyanyuke na kusubiri kwa muda kiasi kabla ya watu wenye majeraha mado waliposafisha njia ya kutoka.<br />
[…]<br />
Mateso yalikuwepo kila mahali. Tulikuwa tumeketi mwishoni mwa behewa na mikoba yote ilipaa ikituelekea. Watu wengi waliojeruhiwa. Katika dakika chahce baada ya ajali, behewa lilikuwa ni kama fungu la miili, viti na sehemu za treni ambazo zilikuwa zimesambaa sawia kila mahali.</p></blockquote>
<p><em>Paltus_mk </em>anasimulia habari za uokoaji zenye maelezo ya kina kuanzia dakika za mwanzo baada ya ajali, lakini wakati huo huo anaepuka ufafanuzi ambao ungeweza kuwastua wasomaji. Anaandika kuwa abiria walianza kupeana huduma ya kwanza kwa ushujaa bila kuogopa. Anasema haikuwezekana kuhesabu ni wagtu wangapi waliofariki. Waokoaji waliwasili saa moja na nusu baada ya ajali. <em>Paltus_mk</em> na kaka yake hatimaye waliokolewa na kupelekwa kwenye hospitali jirani na baadaye aliwasili mjini St. Petersburg. </p>
<p>Hadithi nyingine ya kunusurika ilichapishwa na mwanablogu pancakyes katika huduma nyingine ya kublogu ya Kirusi Ya.Ru. behewa lake halikuharibiwa na mlipuko. Alichapisha makala yake ya kwanza saa 4:11 za usiku – nusu saa baada ya ajali – pale pale kwenye eneo la ajali.  Aliandika kuwa treni ilisimama kutokana na ajali ya namna fulani, mabehewa machache yaliteguliwa na kwamba angewasili nyumbani kwa uchelevu kuliko ilivyotarajiwa. Karibu saa zima baadaye, aliongeza kuwa kulikuwa na waathirika katika mabehewa mawili ya mwisho. Jumamosi,  <em>pancakyes</em> <a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442">alichapisha habari nzima kuhusu ajali</a> [RUS] kama alivyoshudia mwenyewe:</p>
<blockquote><p>Tulihisi mitetemo michache ambayo ilikuwa ikiongezeka nguvu. Vitu vilianza kuanguka kutoka mezani. Haikuwa wazi ni nini kilichotokea. Hapakuwa na matangazo. Kwanza tulidhani kuwa halikuwa jambo lenye uzito. Pengine kuna mtu aliyesimamisha treni kwa makosa. Lakini makondakta wenye sura zenye hofu walianza kukimbia kila mahali wakikusanya magodoro, vitambaa vya mezani na maji. Walitutaka tusiondoke kwenye viti vyetu isipokuwa kama ni madaktari. Tulisikia mambo mabaya kutoka kwenye redio zao. Uvumi ulianza kusambaa. Hatukuamini kuwa mabehewa mawili yalikuwa yametengana na yalikuwa mbali sana. Baadaye tuligundua kuwa ilikuwa kweli.</p>
<p>Tulitoka nje na tulitaka kusaidia. Tulikwenda mpaka behewa la tatu. […] hatukutaka kuwa waduwazi ambao wanaongeza wingi wa watu bila fursa yoyote ya kusaidia. Pia hatukutaka kuona yale ambayo watu waliotoka huko walikwishatueleza.</p></blockquote>
<p>Mara baada ya ajali, majukwaa ya uanahabari wa kijamii yalikuwa sehemu ya kwanza ambayo wanahabari wa Kirusi  walikuwa wakitafuta habari. Mwandishi kutoka Shirika la Habari la RIA-Novosty aliacha maoni kwenye blogu ya <em>pancakyes</em> na kumtaka mwanablogu huyo ampigie simu mara moja. Tatyana Landa (mtumiaji wa LJ mwenye jina la Elada) <a href="http://elada.livejournal.com/220534.html">aliandika kwenye blogu yake</a> [RUS] kuhusu rafiki aliyenusurika ambaye alikuwemo kwenye treni. Mara moja wanahabari wawili waliacha maoni ya kumtaka awasiliane nao. Baadaye Tatyana <a href="http://elada.livejournal.com/220866.html">alichapisha makala ya hasira</a> [RUS] ambamo alisema kuwa mwanahabari kutoka “Komsomolskaya pravda” (gazeti la udaku la Kirusi) alikuwa akijaribu kumpata kwa simu mara kadhaa usiku huo. Makala hiyo iligeukia mahali ambapo watu walianza kujadili kama wanahabari wanaweza kuwatumia wanablogu kama chanzo cha taarifa zinazohusu hii ajali ya treni. Wanahabari pia walijaribu kuwasiliana na mwanablogu ambaye <a href="http://naechst-naechst.livejournal.com/105582.html#comments">aliandika</a> [RUS] kuwa aliamua kutopanda treni la “Nevsky Express” katika dakika ya mwisho.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu <a href="http://tema.livejournal.com/509436.html">walieza kughafirika kwao </a>[RUS] na ukweli kuwa ni watu wachache mno kutoka kwenye treni walitumia vyombo vya habari vya kijamii kutoa taarifa za kile kilichokuwa kinatokea., Na, inavyoonekana, kuna fafanuzi kadhaa zinazoelea ni kwa nini  uanahabari wa kijamii haukuchukua nafasi kubwa katika upashaji wa habari za ajali ya “Nevsky express”.</p>
<p>Twita, jukwaa zuri la kublogu moja kwa moja, si maarufu nchini Urusi. Kwa mujibu wa <a href="http://twitter.com/twitRU">twitRU </a>[RUS], kuna watumiaji wa Twita 2,700 tu ambao wanaandika kwa lugha ya Kirusi. Wakati huo huo, majukwaa maarufu ya kublogu nchini Urusi kama vile Livejournal.com au ya.ru yangeweza kutumika ili kublogu moja kwa moja lakini, kama ilivyojadiliwa hapo juu, kuna mifano michache tu ya matumizi hayo.</p>
<p>Ufafanuzi wa pili unahusiana na nafasi ya zana za mkononi na uunganishaji. Zana za mkononi zinaongezeka nchini. Warusi zaidi na zaidi wanaweza kutumia mtandao wa intaneti na zana nyingine za mtandaoni. Tabia hii ina nguvu katika maeneo ya Moscow na St. Petersburg. Lakini ajali ilitokea mbali na maeneo ya mjini ambako, kama mashihidi walivyotaarifu, uwezo wa kupatikana kwa mawasiliano ya simu za mkononi ulikuwa mdogo. Mwanablogu  <em>pancakyes </em><a href="http://pancakyes.ya.ru/replies.xml?item_no=30442&#038;ncrnd=2805">anasimulia</a> tatizo la mawasiliano:</p>
<blockquote><p>
Mawasilian ya simu yalikuwa mabaya sana. Inawezekana kuwa kila mtu alijaribu kupiga simu kwa wakati mmoja na mtandao ulielemewa. Nilianza kupata jumba za maandishi pale tu nilipokuwa kwenye treni la pili (treni ambalo liliwachukua abiria kwenda Saint- Petersburg G.A.). Ningeliweza kutumia mtandao wa intaneti, lakini ilikuwa ni vigumu mno.</p></blockquote>
<p>Hii ni tofauti, ajali ya ndege kule Perm mwaka jana ambayo ilitoa fursa nyingi kwa uanahabari wa kiraia:</p>
<p>1. Ndege ilianguka ndani ya mipaka ya mji ambako watu wengi waliweza kuona ni nini kilichokuwa kinatokea kutokea madirishani. Ajali ya “Nevsky express”, kama ilivyoelezwa awali, ilitokea sehemu za vijijini.</p>
<p>2.Habari zilizoandikwa kwa uanahabari wa kijamii kule Perm zilitokana na maelezo ya walioishuhudia ajali ambao hawakuwamo katika ajali (kwa bahati mbaya, hapakuwa na walionusurika kutoka katika ile ndege). Mashahidi wote wa tukio la “Nevsky Express”  walikuwa ni abiria katika treni. </p>
<p>3. Watu wengi walituma habari mpya juu ya ajali ya ndege kule Perm kwa kutumia tarakilishi za nyumbani. Walionusurika kwenye “Nevsky Express” walitegemea zana za mikononi.</p>
<p>Tofauti hizi zinabainisha kwa nini vyombo vya habari vya kiraia vilikuwa mbele katika ajali ya  ndege na vilikaribia kutokuwepo kwenye tukio la “Nevsky Express.” </p>
<p>Pia inawezekana kudai kuwa urusi bado haijaendeleza utamaduni wa utoaji taarifa kupitia uanahabari wa kiraia. Na ndiyo sababu abiria wawili tu walikuwa na msukumo wakutosha kwenda kwenye mtandao na kujipa kazi ya uanahabari wa kijamii. Na pia inaweza kufafanua upinzani wa abiria na wanablogu kwa wanahabari ambao walikuwa wanatafuta taarifa za ajali kwenye vyombo vya habari vya kijamii. </p>
<p>Inaonekana kana kwamba ulimwengu wa blogu wa Kirusi bado uko mbali na kuwa chanzo kikuuu cha kutangaza habari mpya. Bado unabaki kuwa sehemu ya usambazaji wa habari na mijadala mipana inayohusu nini kilichotokea. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/urusi-jinsi-abiria-wa-nevsky-express-walivyoeleza-habari-kupitia-vyombo-vya-habari-vya-kijamii/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Malawi: Rais Ataka Nguvu Zaidi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/malawi-rais-ataka-nguvu-zaidi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/malawi-rais-ataka-nguvu-zaidi/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 25 Nov 2009 10:52:12 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Malawi]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=735</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Rais wa Malawi ataka nguvu zaidi!: &#8220;rais wa Malawi Bingu wa Mutharika, ambaye chama chake kina wabunge wengi katika bunge, anataka kunonesha nguvu zake kabla hajatoka kwenye ulingo wa siasa mwaka 2014.&#8221;
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/24/malawi-president-seeking-more-power/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://www.malawipolitics.com/news.php?extend.251">Rais wa Malawi ataka nguvu zaidi!</a>: &#8220;rais wa Malawi Bingu wa Mutharika, ambaye chama chake kina wabunge wengi katika bunge, anataka kunonesha nguvu zake kabla hajatoka kwenye ulingo wa siasa mwaka 2014.&#8221;</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/malawi-rais-ataka-nguvu-zaidi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afya Duniani: Siku ya Vyoo Duniani Yatoa Harufu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 25 Nov 2009 10:46:39 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Brunei]]></category>
		<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Ethiopia]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[India]]></category>
		<category><![CDATA[Oman]]></category>
		<category><![CDATA[Science]]></category>
		<category><![CDATA[Singapore]]></category>
		<category><![CDATA[Thailand]]></category>
		<category><![CDATA[United Kingdom]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=731</guid>
		<description><![CDATA[Ingawa inaweza kusikika kama masihara, Siku ya Vyoo Duniani inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwaza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/19/global-health-world-toilet-day-raises-a-stink/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/1019110937_99be0d6df3_m.jpg" title="Tiled Toilet" class="alignright" width="180" height="240" /><br />
Ingawa inaweza kusikika kama vile masihara, <a href="http://www.worldtoiletday.com/">Siku ya Vyoo Duniani</a> inatilia maanani kwenye suala ambalo si la mzaha linalowakwanza karibu nusu ya watu wote duniani – ukosefu wa vyoo na mfumo wa usafi.</p>
<p>Watu wanaweza kuwa wanaona aibu kuongea wazi kuhusu hili suala, lakini kila mmoja hujisaidia, kwenye choo au la. Siku ya Vyoo Duniani inasaidia watu kusherehekea umuhimu wa usafi na kuwaelimisha watu bilioni 2.5 ambao hawana vyoo na mfumo wa usafi wenye uhakika. Video hii iliyotengenezwa na asasi isiyo ya kibiashara WaterAid <a href="http://www.youtube.com/watch?v=-T2eH7zrDJg">inaonyesha</a> starehe ya kuwa na choo.</p>
<p>Kusherehekea kopo lako kunaweza kuonekana kama ujinga, lakini kutokuwa na kopo siyo tu kunaweza kukusababishia aibu, kukosa heshima na masuala mengine ya kiusalama, bali pia kunaweza kukusababishia magonjwa yanayoweza kuzuilika na hata kifo. Pale watu wanapokosa vyoo, wanalazimika kujisaidia mitaani kweupe, kwenye viwanja au vichochoroni. Matokeo? Uchafuzi wa maji ya kunywa na vyanzo vya chakula, jambo ambalo linapelekea hatari nyingi za kiafya. Ukosefu wa mfumo wa usafi ndiyo sababu kubwa ya maambukizi na huua <a href="http://worldtoiletday.com/about.html">watu milioni 1.8</a>, hasa watoto, kila mwaka. Hata nchi zenye vyoo vya kutosha huwa zinakabiliana na matatizo yanayotokana na vyoo vichafu vya umma mpaka utupaji majitaka unaoharibu njia za maji.</p>
<p>Vanilla, anayeblogu kwenye <em>Let&#39;s Look At It This Way</em> kutokea Singapore, <a href="http://whatsayyouvanilla.blogspot.com/2009/11/world-toilet-day.html">anasema</a> kuwa watu wanapaswa kutilia maanani vyoo:</p>
<blockquote><p> “ Ninajua kwamba hii ni mada chafu kwa watu wengi. Ni bahati mbaya kwamba hii mada bado ni ‘mwiko’ kuiongelea wazi na watu wengi hawana uelewa kuhusu ukubwa wa tatizo. Ninashindwa kuelewa ni kwa jinsi gain hii inaweza kuwa mada isiyo na maana wakati, kwa wastani, huwa tunakwenda chooni mara 2500 kwa mwaka, au mara 6-8 kwa siku. Wakati wa maisha yetu, hutumia muda wa miaka 3 vyooni.&#8221; </p></blockquote>
<p>Chini ya maandalizi ya asasi isiyo ya kibiashara <a href="http://worldtoiletday.com/wto.html">The World Toilet Organisation</a>, Siku ya Vyoo Duniani inasherehekewa dunia nzima kwa matukio mbalimbali. Ili kuuelimisha umma zaidi, wiki hii WaterAid <a href="http://wateraidnews.blogspot.com/2009/11/launch-of-new-iphone-application-brings.html">ilitangaza</a> uzinduzi wa zana mpya ya Kutafutia Vyoo nchini Uingereza ya simu za mkononi za iPhone. Zana hiyo ya bure inawasaidia Waingereza kutafuta choo cha umma kilicho karibu zaidi  wakati pia inawakumbusha jinsi walivyo na bahati ya kuwa na vyoo safi na salama. Tukio kubwa zaidi leo, linaloitwa <a href="http://worldtoiletday.com/squat/">Mchuchumao Mkubwa</a>, linawataka watu wasimame na wachuchumae kwa dakika moja katika sehemu za umma ili kuongeza utambuzi. <a href="http://www.flickr.com/groups/1216217@N24/">Picha</a> hizi zinaonyesha watu waliochuchumaa dunia nzima, pamoja <a href="http://www.flickr.com/photos/25532596@N04/4116769214/in/pool-1216217@N24">na hii ya</a> watoto wa chekechea huko Singapore:</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/4116769214_1b876f8640.jpg" title="Singapore Squat" class="aligncenter" width="500" height="273" /></p>
<p>Blogu inayotokea Brunei, <em>the world according to panyaluru </em>…, pia <a href="http://panyaluru.blogspot.com/2009/11/cut-paste-toilets.html">inaonyesha kuridhika</a> na vyoo kwa kuliweka suala hili kwenye muktadha sawia:</p>
<blockquote><p> “Fikiria ikiwa tunatembea mbele ya mlolongo wa maduka kule Kiulap au Gadong. Mara tu tumbo linaunguruma kama vile ambavyo haujawahi kusikia. Halisimami kukupa mapumziko. Linaunguruma na kuunguruma. Ngurumo. Taa ni ya manjano tayari kubadilika kuwa ya kijani. Lakini hakuna vyoo unavyoviona. Hakuna hata choo kimoja cha umma kwenye mlolongo wa maduka… ongezea pia kuwa hakuna maji, karatasi ya chooni, hakuna chochote! Hiyo inaweza kuwa siku mbaya zaidi katika maisha yako, jinamizi baya, au jinamizi baya zaidi ya yale yaliyowakuta watoto kwenye filamu za Elm Street. Katika siku hii, hebu na tuvienzi vyoo.”</p></blockquote>
<p>Ukiachilia mbali upande makini wa suala hili, watu wengi wametumia mzaha kuadhimisha siku ya Vyoo Duniani. Huko Uingereza blogu ya <em>London City Drains</em> imeweka chemsha bongo ya vyoo yenye maswali 10, wakati katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=zx2oVPjnUXs">video</a> hii mwalimu wa sekondari Matt Cheplic anaimba kuhusu siku hii.</p>
<p>Baadhi ya wanablogu wanasema kuwa vyoo pekee vinaweza visiwe jibu. Sandhya, anayeblogu kwenye <em>Maradhi Manni </em>nchini India, <a href="http://maradhimanni.blogspot.com/2009/11/big-squat-to-take-stand-on-sanitation.html">anasema</a> wanaume wengi hawatumii vyoo vilivyopo:</p>
<blockquote><p>Kwenye mji kama Chennai, ambako hali ya hewa ni ya joto kwa karibu miezi 10 ya mwaka, huwaona wanaume wanakojoakando ya barabara kila wakati. Wkati wanawake wanaweza kujidhibiti  na kwenda nyumbani kujisaidia, kwa nini wanaume hawawezi kufanya hivyo, sijui kwa nini. Kwa hiyo, kwanza watu wote wanabidi wapigwe faini kali kwa kufanya kosa hili (naam, ni kosa) pale pale wanapokamatwa. Nimewahi kuwaona wakifanya hivyo kwenye ukuta wa vyoo vya umma! Kule Srinagam, nimewahi kuwaona wakikojoa kwenye ukutra wa boma la hekalu pamoja na kuwa kila mtaa unaolizunguka hekalu una vyoo, ambavyo vilikuwa visafi, lakini vya kulipia!”</p></blockquote>
<p>Wakati ukosefu wa mfumo wa usafi unaathiri kila mtu, miiko inayozunguka suala la vyoo inawaathiri vikubwa wanawake zaidi ya  wengine. <a href="http://worldtoiletday.com/squat">Katika baadhi ya nchi</a>, staha huwalazimisha wanawake kufanya shughuli zao kwenye makonde kabla ya jua kuchomoza au kujizuia mpaka mpaka baada ya jua kuzama, jambo ambalo linasababisha madhara ya kiusalama na kiafya. Joanne Sprague, anayeblogu kwenye <em>Overturning Boulders</em> nchini India, <a href="http://overturningboulders.blogspot.com/2009/11/but-where-do-women-do-their-business.html">anabaini</a> kuwa wanawake hawapo kwenye mzunguko wa kwenda haja asubuhi mijini Chennai, wakati huko Ethiopia blogu ya <em>AN ADVENTURE IN ADDIS</em> <a href="http://anadventureinaddis.com/2009/11/17/world-toilet-day/">inabaini </a>hali kama hiyo pia:</p>
<blockquote><p>“Nimekuwa nikisikia mara nyingi juu ya ukosefu wa vyoo kwa wanawake au ukosefu wa vyoo kwa ujumla; kwamba wasichana wa rika la kuwa wali huko mashambani huamka saa 10 za alfajiri kwenda nje kwenye giza kufanya shughuli zao ili wasitaniwe na wavulana shuleni au huacha kwenda shule kabisa. Wanaume hukojoa kila mahali, sigara mkononi na kuna kuna dhana kuwa wanawake hawapaswi kufanya hivyo, kama wanafikiriwa hata kidogo… ninataka kuona bango kubwa kwa lugha ya Ki-Amhara linalosema “wasichana nendeni pia’ lenye picha ya mwanasesere anayevutia wa kike aliyeketi chooni.” </p></blockquote>
<p>Kusherehekea Siku ya Vyoo Duniani, mwanablogu Jonathan Stray, anawachukua wasomaji kwenda <a href="http://jonathanstray.com/world-toilet-day">ziara ya kimataifa ya vyoo </a>ambavyo ameshawahi kuvizuru, kuanzia Thailand na Uingereza mpaka Afrika Magharibi na Oman, na anahitimisha:</p>
<blockquote><p> “Sisi watu wa Magharibi na vyoo vyetu vya kuvuta na karatasi za chooni na chemchemi zinazong’ara ni tofauti na wengine wengi; wengine wote waliobaki hufikiri kuwa bafu ni sehemu iliyolowana, inayonuka, ikiwa wanayo hayo mabafu. Choo kizuri kinamaanisha kuwa pengine una kiwango kizuri cha maisha, kwa hiyo burudika na choo chako. Siku njema ya Vyoo Duniani!  </p></blockquote>
<p><em>Picha ya <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/1019110937/">choo cha vigae</a> imepigwa na <a href="http://www.flickr.com/photos/nedrichards/">nedrichards</a> kwenye Flickr, Haki Miliki Huru.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afya-duniani-siku-ya-vyoo-duniani-yatoa-harufu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Brazil: Je, Milango ya Benki Hubaini vyuma au Rangi za Watu?</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-je-milango-ya-benki-hubaini-vyuma-au-rangi-za-watu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-je-milango-ya-benki-hubaini-vyuma-au-rangi-za-watu/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 24 Nov 2009 12:35:02 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Portuguese]]></category>
		<category><![CDATA[Racism]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=724</guid>
		<description><![CDATA[Benki nyingi nchini Brazil zinatumia milango inayozunguka yenye vifaa vya kubaini vyuma. Je, milango hiyo inatumika kama kisingizio cha kubagua watu? Video ya uandishi wa kiraia inaonyesha moja ya matukio hayo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/paulagoes/">Paula Góes</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/19/brazil-do-banks-have-metal-or-melanin-detector-doors/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Usiku wa mkesha wa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Black_Pride">Siku ya Kujivunia Weusi</a> nchini Brazil – inayosherehekewa tarehe 20 Novemba, wakati nchi inapofufua vita vinavyoendelea dhidi ya ubaguzi - <em><a href="http://www.circovoador.com.br/">Circo Voador Audiovisual Collective</a></em> ilifanya jaribio. Waliwarekodi wanachama wao wawili katika filamu, ambao wana rika moja na waliovalia mavazi yanayofanana, wakijaribu kuingia benki katika benki moja katika nyakati tofauti, huku wakiwa wamebeba mikoba iliyojaa vyuma – funguo, sarafu, simu za mkononi. Mmoja wao alichukua sekunde chache kuingia bila ya matatizo yoyote; mwingine hakuweza kuingia, alizuiwa na mlango unaozunguka, ambao ni kitu cha kawaida katika mabenki mengi nchini Brazil. Kijana wa kwanza alikuwa mzungu, wa pili, mtu mweuzi. Angalia matokeo:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/LQee_J0K4BY&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en_US&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/LQee_J0K4BY&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en_US&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kwa mujibu wa waliotengeneza filamu, jaribio hili limeonyesha kuwa milango yenye vifaa vinavyobaini vyuma huwa inawashwa na walinda usalama kwenye mabenki. Kwa maneno mengine, taratibu za ulinzi ambazo benki inazitumia hivi sasa zinategemea maamuzi ya watumishi, maamuzi ambayo mara nyingi hugubikwa na dhana zilizokuwepo kabla ya tukio, imani potofu na ubaguzi dhidi ya watu wa aina fulani. Kwenye blogu yao, <em><a href="http://novasdocirco.blogspot.com/2009/11/sobre-o-video-do-manifesto.html">Circo Voador</a></em> [Sarakasi inayopaa, pt] anawakaribisha wasomaji kujiunga, kwa kutuma video zao za watu weusi tofauti tofauti wengi inavyowezekana. Wnafafanua jaribio hilo:</p>
<blockquote><p>Na primeira cena aparecem várias pessoas ao redor da bolsa. Todas elas fizeram o teste com a mesma bolsa, algumas foram barradas outras não. Em nenhum momento alguém alterou o conteúdo dos pertences na bolsa. A escolha da imagem do MC Shackal não se deveu ao fato dele ser negro e sim, por termos nos utilizado de câmeras escondidas e o momento em que o registramos, não sofreu interferências externas, como carros ou pessoas paradas na frente da câmera.</p></blockquote>
<div class="translation">Katika sehemu ya kwanza ya filamu kuna watu wengi waliokuwepo karibu na mkoba. Wote walifanya jaribio kwa kuubeba mkoba ule ule mmoja, wengine walizuiwa na wengine hawakuzuiwa. Hakuna aliyebadilisha vitu vilivyokuwemo ndani ya mkoba. Tumeamua kuijumusha sehemu ya filamu tuliyoipiga na MC Shackal siyo kwa kuwa yeye ni mtu mweusi lakini ni kwa sababu tulitumia kamera iliyofichwa na wakati tuliponpiga picha, hapakuwa na vitu vilivyoingilia, kama vile magari au watu waliosimama mbele ya kamera.</div>
<p>Watu wengi walitoa maoni kwenye kisanduku cha maoni cha blogu ya Circo Voador. Baadhi ya wasomaji walishawahi kukutwa na mikasa inayofanana na huu kama <a href="http://novasdocirco.blogspot.com/2009/11/video-flagrante-manifesto-porta-na-cara.html?showComment=1258104506110#c6353301951423238337">Dona Biologia</a> [pt], ambaye ni mwalimu:</p>
<blockquote><p>Coloquei chaves, celular, bolsinha de moedas no local indicado e a porta apitava e travava. Por fim, o rapaz chamou um pseudo gerente que atravessou a porta e, dentro do caixa eletrônico da agência, me fez abrir a bolsa de provas e quando não viu nada que justificasse, teve a audácia de dizer que fora a minha bolsinha de lápis. Me arrependo até hoje de não ter processado o banco pelo constrangimento.</p></blockquote>
<div class="translation">Niliweka funguo, simu ya mkononi, pochi ya sarafu katika sehemu iliyoelekezwa na bado mlango uliwasha king’ora na kujifunga. Hatimaye, yule kijana alimuita meneja uchwara ambaye alipita mlangoni na, katika mashine ya kutolea pesa, akanitaka nifungue mkoba wangu [wa mwanafunzi] wa makaratasi ya insha na aliposhindwa kukuta chochote kilichoweza kuhalalisha [tabia yake] alikuwa na ujasiri wa kuniambia kuwa sababu ilikuwa ni kasha langu la penseli. Bado ninasikitika kwa kutoishitaki benki kwa kunizuia.</div>
<p><a href="http://novasdocirco.blogspot.com/2009/11/video-flagrante-manifesto-porta-na-cara.html?showComment=1258029603026#c6288412453615633717">Christiano J. Jabur</a> [pt], ambaye aliwahi kuzuiwa katika mlango wenye vifaa vya kung’amua vyuma mjini Sao Paulo kwa sababu ya kubeba kamera ya kidijitali, anadai kuwa ubaguzi dhidi ya watu kwenye milango ile ile ya kuzunguka hutokea kwenye mabenki bila kujali rangi ya ngozi:</p>
<blockquote><p>Tive que colocá-la numa caixinha para conseguir entrar no banco. Mas uma senhora de idade, também branca, que tentou entrar na agência da Nossa Caixa, na mesma cidade, foi barrada e não conseguiu entrar de jeito nenhum, mesmo chamando a polícia. O gerente do banco ininuou que ela poderia ser criminosa, pois existem muitas pessoas hoje, acima dos 50 e 60 anos de idade, cometendo crimes (o que não deixa de ser verdade). Não vou dizer que não exista preconceito contra negros e pardos nos bancos, por parte de vigilantes e atendentes. Mas dizer que são só os negros que são barrados nas portas giratórias é uma bela de uma mentira.</p></blockquote>
<div class="translation">
Ilinibidi niiweke [kamera] katika kasha ili niweze kuingia ndani ya benki. Lakini mwanamke mzee, mzungu, alijaribu kuingia katika tawi la Nossa Caixa kwenye mji ule ule alizuiwa na hakuweza kuingia kabisa, hata baada ya kuwapigia simu polisi. Benki iliashiria kuwa angeweza kuwa jambazi, kwa sababu kuna watu wengi wenye zaidi ya miaka 50 mpaka 60 ambao hufanya makosa siku hizi (jambo ambalo ni kweli). Siwezi kusema kuwa walinzi wa usalama na wahudumu kwenye mabenki hawana ubaguzi dhidi ya watu weusi na wale wenye rangi ya kahawia. Lakini kusema kwamba watu ni weusi pekee ambao huzuiliwa katika milango inayozunguka ni uongo.</div>
<p>Katika upande mwingine, mlinzi wa usalama aitwaye <a href="http://novasdocirco.blogspot.com/2009/11/manifesto-porta-na-cara.html?showComment=1258434725779#c6445085889139836208">Leandro</a> [pt] anafafanua katika kisanduku hicho hicho cha maoni jinsi mfumo unavyofanya kazi, na anakosoa namna ambayo video ile ilivyotafsiriwa na baadhi (ya watu):</p>
<blockquote><p>Sou Vigilante (segurança), e posso afirmar, este sistema é falho, mas este vídeo esta sendo usado para sujar a imagem de profissionais que estão apenas cumprindo ordens… os ‘controles’ podem sim travar e destravar as portas giratórias, mas isso não é valido para todas as agencias, são sistemas diferenciados pra cada agencia ou cada porta giratória… e não temos controle sobre o “Nível de travamento“ de cada porta (isso é de responsabilidade do gerente), que costuma variar de 4 a 7 níveis, por isso vc pode entrar em uma agencia e ficar travado e em outra passar sem problema algum…<br />
Sei que intenção de vc&#39;s não é esta, li o que estão propondo e apoio totalmente, mas não esta sendo divulgado desta forma, outros sites e meios de comunicação estão colocando informações “picadas”, pela metade… eu mesmo recebi um Email como Titulo: “Vigilantes racistas?”</p></blockquote>
<div class="translation">Mimi ni mlinzi wa usalama na ninaweza kukwambia kuwa mfumo huu una makosa, lakini video hii inatumika kuichafua sifa ya wafanyakazi ambao wanafuata amri tu… kuna ‘vidhibiti’ ambavyo kwa hakika huweza kufunga au kufungua milango inayozunguka, lakini hii si kweli katika matawi yote, mfumo ni tofauti kwa kila tawi au kila mlango unaozunguka… hatuna uwezo wa kudhibiti ‘ngazi ya ufungaji’ wa kila mlango ambayo huwa kati ya ngazi ya 4 mpaka 7 (huu ni wajibu wa meneja), na hii ndiyo sababu inayokufanya ukamatwe kwenye mlango wa tawi moja lakini ukaweza kuingia ndani ya tawi jingine bila ya matatizo…<br />
Ninajua kuwa haikuwa nia yako, nimesoma kile unachokusudia kukisema na nikiunga mkono kabisa, lakini (kile ulichokusudia) hakisambazwi hivyo, tovuti nyingine na vyombo vya habari vimechapisha vipande vya taarifa nusu… mimi binafsi nimepokea barua pepe yenye kichwa cha habari: “Walinzi wa usalama wabaguzi?”</div>
<p>Kadhalika video hiyo imeenea haraka kwenye ulimwengu wa blogu. <a href="http://meujazz.wordpress.com/2009/11/12/manifesto-porta-na-cara/">Rafael Cesar</a> [pt] anasema kwamba milango kujifunga kwa watu weupe au weusi si kiini cha suala hili:</p>
<blockquote><p>A questão é que sabemos que aquele detector de metais é muito mais uma desculpa para os seguranças fazerem o controle da forma como julgam apropriada do que qualquer outra coisa. O que trava, mesmo, é aquele controlezinho que eles carregam. Comigo é rotineiro, sem qualquer exagero, passar por aquela porra sem metal nenhum na mochila (já deixei até estojo naquela caixinha ao lado por causa de lapiseira) e me travarem. Ou seja: o que volta e meia detectam em mim é um meliante em potencial, porque por várias vezes não havia qualquer metal a ser detectado. Se eu não tinha metal, por que ‘a porta’ travou? E, se eu tenho metal, por que logo em seguida ‘a porta’ destrava?E nessa de o crivo da segurança passar pelos olhos dos seguranças, é claro que o indivíduo negro leva a pior. Assim como leva a pior com a polícia, com emprego etc.</p></blockquote>
<div class="translation">Kiini cha suala ni kuwa tunafahamu kwamba  vifaa vya kung’amua vyuma, zaidi ya yote, ni kisingizio cha walinzi wa usalama walio kwenye zamu kutumia uamuzi wao katika njia wanayoona sawa. Milango hufungwa, kwa kutumia kifaa kidogo wanachokibeba cha kuwashia na kuzima. Kwangu ni tabia, bila ya kutaka kujikuza, kupita katika upumbavu ule bila ya chuma chochote kwenye mkoba wangu wa mgongoni (nimewahi hata kuacha kasha pembeni kwa sababu ya kichongeo cha penseli cha chuma) hata hivyo nilizuiwa. Kwa maneno mengine: kitu wanachokiona kwangu kila wakati ni kuwa nina uwezo wa kuwa mwizi, kwani mara kadhaa sikuwa na chuma ambacho kingeweza kubainiwa. Ikiwa sikubeba chuma chochote, kwa nini mlango ulijifunga? Na kama nimebeba chuma, kwa nini basi mara tu milango hujifungua? Kwa kuwa hatua za usalama huchujwa kwa kutumia macho ya walinzi wa usalama, bila ya shaka mtu mweusi ana wakati mgumu zaidi. Kwa namna sawa sawa na mbavyo ana wakati mgumu zaidi na polisi, kwenye kuomba kazi n.k…</div>
<p><a href="http://helioventura.blogspot.com/2009/10/portas-giratorias-detectores-de-metais.html">Helio Ventura</a> [pt] anachukua fursa kuchapisha maandishi yaliyochapwa kwanza mwezi Machi 2007 na kuuliza kama milango hubaini vyuma au melanin (chembe hai zinazosababisha kuwa na ngozi nyeusi) baada ya mteja mweusi kuuwawa ndani ya benki jijini Rio de Janeiro:</p>
<blockquote><p>Rio de Janeiro, sexta-feira, 22 de dezembro de 2006, 13 horas e 20 minutos. O micro-empresário negro Jonas Eduardo Santos de Souza, 34 anos, estava na fila da agência do banco Itaú da Av. Rio Branco, da qual era cliente há 10 anos, para operações de rotina. Mas ele foi vítima do racismo que persiste em existir em nosso país, apesar de muitas vozes da elite e da intelectualidade negarem. Ele foi morto com um tiro no peito por Natalício de Souza Marins, 29 anos, vigilante da agência.<br />
Ao tentar entrar na agência bancária, Jonas foi parado pela conhecida e constrangedora porta giratória. Ele foi abordado por Natalício e obrigado a pôr na bandeja todos os objetos que possuía. Como a porta continuava travando, Jonas foi obrigado a tirar inclusive o cinto. O gerente foi acionado por Natalício, e só autorizou o acesso do jovem micro-empresário à agência após exigir que Jonas provasse ser cliente da agência, mostrando um cartão do banco. Após o constrangimento, já dentro da agência, Jonas e Natalício continuaram a discutir, até que o vigilante, demonstrando total despreparo para o exercício da função, sacou seu revólver e matou Jonas, que não teve chance de defesa. […]<br />
Assim como também poderíamos estar do outro lado, o de Natalício, também negro, um pai de família que teve suprimidas as oportunidades de acessar uma profissão que pudesse dar melhores condições à sua filha de 5 anos, que se viu obrigado a pleitear apenas funções que exigem menor qualificação, como a de vigilante. Ele também foi atingido pelo racismo estrutural que assola este país. Isso em nada muda o fato dele ter agido equivocadamente: é um homicida e deve receber as sanções legalmente previstas. E ser também negro não atenua o crime. Mas nos faz perguntar: que sistema é este que coloca dois semelhantes em lados opostos, fazendo com que um tire a vida do outro? Até quando fatos como este acontecerão? Percebemos o quão perverso é este “racismo à brasileira”, uma política de extermínio silenciosa, disfarçada de risco social e fatalidade.</p></blockquote>
<div class="translation">Rio de Janeiro, Ijumaa, Disemba 22, 2006, saa 7:20 mchana. Mjasiriamali mweusi Jonas Eduardo Santos de Souza, umri mika 34, alikuwa amepanga foleni ili kupata huduma ya kawaida katika tawi la benki ya Itau katika Rio Branco, ambako alikuwa mteja kwa muda wa miaka 10. Lakini alikuwa muathirika wa ubaguzi ambao unaendelea kuwepo katika nchi yetu, pamoja na kukataa kuwa ubaguzi haupo, kukataa ambako kunatoka kwa makundi mengi ya wataalamu na wasomi. Aliuwawa kwa kupigwa risasi kifuani na mlinzi wa usalama kwenye tawi hilo, Natalício Marins de Souza, 29.<br />
Wakati akijaribu kuingia kwenye tawi hilo, Jonas alizuiwa na milango inayozunguka  inayojulikana vyema kwa kuwatia watu aibu. Alijongelewa na Natalicio na kulazimishwa kuweka vitu vyake vyote kwenye sinia. Mlango ulikuwa bado umefungwa, Jonas alilazimishwa hata kuvua mkanda wake. Natalicio akamuita meneja, ambaye alimruhusu huyu mjasiriamali kijana baada ya kumtaka Jonas kuthibitisha kuwa alikuwa ni mteja wa wa tawi lile, kwa kuonyesha kadi yake. Baada ya aibu ile, ndani ya benki, Jonas na mlinzi wa usalama waliendelea kubishana mpaka mlinzi yule wa usalama, alipodhihirisha kuwa hakuwa na uwezo wa kuifanya kazi yake, alitoa bunduki na na kumuua Jonas, ambaye hakuwa na uwezo wa kujikinga. […]<br />
Tunaweza kuwa upande wa Natalicio, ambaye pia ni mweusi, baba wa familia ambaye hakuwa na fursa ya kupata taaluma ambayo ingemwezesha kumpa mazingira bora binti yake wa miaka 5, hivyo kulazimika kuomba kazi ambazo zinahitaji vigezo vya chini zaidi, kama vile kazi ya ulinzi wa usalama. Na yeye naye alikumbwa na ubaguzi wa kimfumo unaoisibu nchi hii. Hii haibadili ukweli kuwa alifanya makosa; ni muuaji na anapaswa kupokea adhabu zinazotolewa na sheria. Kadhalika kuwa mweusi hakupunguzi kosa. Lakini inatufanya tujiulize: huu ni mfumo wa namna gain unaowaweka watu wawili walio sawa kwenye pande tofauti, na kumsababisha mmoja kuchukua maisha ya mwingine? Mpaka lini matukio kama haya yataendelea kutokea? Tunaona gani ‘ubaguzi’ ulivyo mbaya katika Brazil, sera ya kimya kimya inayomaliza watu, iliyojificha kama hatari ya kijamii na ajali isiyozulika.</div>
<p><a href="http://naoinviabilize.blogspot.com/2009/11/olha-faaaaaaca.html">Andréia Freitas</a> [pt], ambaye aliwahi kufanikiwa kuingia ndani ya benki bila bugudha na kisu cha jikoni ambacho alikuwa amekinunua kabla, anasema kuwa hitimisho la kusikitisha ni kuwa watu huona sura ya nje tu ya watu wengine:</p>
<blockquote><p>Por que será que cresceram os assaltos a banco realizados por homens de terno e gravata? Por que será que hoje existe o roubo de carros em estacionamentos e os assaltantes chegam no local pra assaltar de carro importado? Golpes de estelionatários em hotéis de luxo, em lojas de grife, em restaurantes cinco estrelas…</p>
<p>A resposta é óbvia: O mundo é movido por “aparências”! Sim… se você é considerada uma pessoa “bem apessoada” a vida fica mais fácil pra você em todos os aspectos. Agora… se você não está tão “bem vestido”, ou seu cabelo “acordou” num dia ruim, ou seu sapato tá meio surrado, pode apostar que a vida não será bolinho pra você.</p>
<p>O ser humano vê as aparências! Se as portas dos bancos fossem realmente controladas por uma máquina, por um dispositivo eletrônico de segurança, os dois caras do vídeo do YouTube tinham sido barrados! E nada mais justo do que barrar OS DOIS, que portavam objetos de metal.
</p></blockquote>
<div class="translation">Ni kwa nini ujambazi katika mabenki unafanywa na watu waliovalia suti na tai? Kwa nini siku hizi magari huibwa kwenye sehemu za maegesho na majambazi huwasili katika magari yaliyoagizwa kutoka nje ya nchi? Utapeli kwenye mahoteli ya kifahari, maduka ya wabunifu, migahawa ya nyota tano…</p>
<p>Jibu liko wazi: dunia inaendeshwa na “wajihi au jinsi unavyoonekana”! Naam… kama unaonekana ni kijana mwenye sura nzuri, maisha ni rahisi kwako kwa kila hali. Sasa… kama wewe si “mtanashati”, au kama uan siku ya nywele mbaya, au kama viatu vyako vimechakaa kidogo, unaweza kutabiri kuwa maisha hayatukuwa mepesi kwako.</p>
<p>Binaadamu huona jinsi watu wanavyoonekana! Kama milango ya benki ingekuwa inaendeshwa na mashine kati maana halisi, mashine ya umeme, vijana wawili walioonyeshwa kwenye video ya YouTube wangezuiwa! Na hakuna jingine lililo sawa zaidi ya kuwazuia WOTE WAWILI, kwani wote walikuwa wamebeba vifaa vya chuma.</p></div>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/logo_portanacara.png" title="logo_portanacara" class="aligncenter" width="400" height="135" /></p>
<p>Kuna <a href="http://www.petitiononline.com/porta/petition.html">kampeni ya kwenye mtandao</a> [pt] iliyoanzishwa na jaribio linalozitaka benki za Brazil kuacha kutumia milango inayozunguka na kuwekeza kwenye mfumo wa mionzi (X-ray) au vifaa vya usalama ambavyo vinaonyesha vitu alivyonavyo mteja, kampeni hiyo imesainiwa na zaidi ya watu 2,000 mpaka sasa. Wito wa kampeni hiyo ni kuwa kila mtu anapaswa kuhudumiwa kwa heshima na kila benki. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-je-milango-ya-benki-hubaini-vyuma-au-rangi-za-watu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika: Haki za Wanawake</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-haki-za-wanawake/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-haki-za-wanawake/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 11:30:25 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=721</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Sokari anaandika kuhusu Toleo Maalum la Masuala ya Wanawake la Pambazuka linaloangalia miaka 15 iliyopita tangu mkutano au Jukwaa la Vitendo mjini Beijing pamoja na mustakabali wa haki za wanawake barani.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/22/africa-womens-rights-across-africa/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Sokari anaandika kuhusu <a href="http://www.blacklooks.org/2009/11/womens_rights_across_africa.html">Toleo Maalum la Masuala ya Wanawake la Pambazuka</a> linaloangalia miaka 15 iliyopita tangu mkutano au Jukwaa la Vitendo mjini Beijing pamoja na mustakabali wa haki za wanawake barani.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-haki-za-wanawake/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Brazil: Mtazamo wa Wakazi wa Vitongoji Maskini</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-mtazamo-wa-wakazi-wa-vitongoji-maskini/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-mtazamo-wa-wakazi-wa-vitongoji-maskini/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 11:21:58 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Portuguese]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=716</guid>
		<description><![CDATA[Katika makala hii, tunasikia mitazamo ya wanahabari raia kutoka mradi wa Viva Favela kuhusiana ya vurugu inayotokana na mihadarati huko Rio de Janeiro na jinsi inavyofagia makazi ya walalahoi, kama wanavyoiona mbele ya milango ya nyumba zao.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/diego-casaes/">Diego Casaes</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/01/brazil-a-view-from-slum-dwellers-on-rios-drugs-war/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wiki iliyopita, picha za vita kati ya wasafirishaji na wafanyabiashara ya madawa ya kulevya mjini Rio de Janeiro zilitapakaa duniani. Tarehe 17 Oktoba, mapambano kati ya magenge yanayotokea vilima vya Morro Sao Joao na Morro dos Macacos yaliwatisha watu. Mamia ya askari wa jimbo walipelekwa katika juhudi za kudhibiti magenge hayo yanayoshindana lakini haikusaidia: ugomvi kati ya wafanyabiashara wa madawa ya kulevya na polisi yalipelekea kutunguliwa kwa helikopta ya polisi na vifo vya polisi watatu, na kuchukua maisha ya zaidi ya watu 30 wengine, miongoni mwao wakiwemo watu wanaotuhumiwa kuwa wanachama wa magenge na wapiti njia. </p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 610px"><img alt="Wakati helikopta inalipuka. Picha na Taiane Oliveira kwenye Twitpic." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/36736952.jpg" title="The moment the helicopter exploded. Photo by Taiane Oliveira On Twitpic." width="600" height="450" /><p class="wp-caption-text">Wakati helikopta inalipuka. Picha na Taiane Oliveira kwenye Twitpic.</p></div>
<p>Blogu ya <em><a href="http://inblogs.com.br/censurado/">Censurado</a></em> inaukosoa mtizamo wa gavana katika mgogoro huu, baada ya kusikia habari zinazoashiria kuwa <a href="http://inblogs.com.br/censurado/politicanacional/carnaval-fora-de-epoca-no-rio-de-janeiro-chove-bala-rio-2016-socorro-ja">polisi hawakujua chochote juu a uvamizi</a>:</p>
<blockquote><p>Vocês viram as cenas na televisão este fim de semana? Helicóptero caindo, policial morrendo queimado, inocente metralhado nas ruas e traficante invadindo a favela do outro em plena luz do dia, uma verdadeira cena de filme de guerra. Dizem no Rio que até o serviço secreto israelense sabia que um morro atacaria o outro, mas mesmo assim o governador Sérgio Cabral diz que a policia carioca não sabia de nada? Acho que ele anda passando muito tempo com o Lula. Só isso explica essa ‘ignorância&#39; sobre o tema.</p></blockquote>
<div class="translation">Je uliiona habari katika televisheni mwishoni mwa juma hili? Helikopta akianguka, polisi wanaungua moto, watu wasio na hatia wanapigwa kwa risasi mitaani na wauza madawa ya kulevya wakivamia vitongoji vya wauzaji wengine mchana kweupe; kama picha kutoka kwenye sinema ya vita. Mjini Rio, watu wanasema kuwa hata shirika la kijasusi la Israel lilikuwa linafahamu kuwa wauza madawa ya kulevya wangeeenda kuwashambulia wauzaji wengine, lakini bado gavana Sergio Cabral alisema kuwa polisi wa carioca walikuwa hawafahamu lolote? Nadhani anatumia muda mwingi na [rais wa Brazil] Lula. Hiyo ndiyo sababu pekee ya “kutokufahamu kwake” juu ya suala hili.</div>
<p>Mwanablogu <em><a href="http://anamvc.blogspot.com/">Ana Maria</a> </em>[pt] anasema kuwa kuitungua helikopta siyo kazi rahisi na kuonyesha kuwa huu unaweza ukawa ni mwanzo tu. <a href="http://anamvc.blogspot.com/2009/10/desespero-do-trafico.html">Anasema</a>[pt]:</p>
<blockquote><p>Mas os senhores do tráfico, donos dos morros cariocas possuem não apenas as armas capazes disso, possuem indivíduos capazes de manuseá-las e causar um desastre como o do sábado.<br />
Isso vai ficar marcado para sempre na memória da PM e do cidadão de bem, morador do estado do Rio de Janeiro.<br />
Se eles podem fazer isso com um helicóptero da polícia tripulado por homens treinados, que dão a vida pela segurança pública, o que podem fazer com o cidadão comum?<br />
Não vou “tapar o sol com peneira”.<br />
As coisas podem piorar.</p></blockquote>
<div class="translation">Sio tu vigogo wa madawa ya kulevya, bali pia wamiliki wa makazi ya masikini katika carioca, wanazo bunduki zenye uwezo wa kufanya jambo kama hilo mikononi mwao, na pia wanao watu waliofundishwa kuzitumia na kusababisha janga kama la Jumamosi iliyopita.<br />
Tukio hili litaacha lama katika kumbukumbu za Polisi na raia wa kawaida, wakazi wa jimbo la Rio de Janeiro.<br />
Kama wanaweza kufaifanyia hivi helikopta inayoendeshwa na watu waliofuzu, ambao wametoa maisha yao ili kutoa usalama kwa umma, je wanaweza kufanya nini kwa raia wa kawaida?<br />
Siwezi “kulificha jua kwa chujio”.<br />
Mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi.</div>
<p><strong><br />
Maelezo ya wakazi juu ya vita vya madawa ya kulevya</strong></p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Mwanamke aliyembeba mtoto anatembea bila kujali mbele ya maofisa wa polisi wanaofanya doria katika Morro dos Macacos" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-010.jpg" title="Macacos-010" width="400" height="300" /><p class="wp-caption-text">Mwanamke aliyembeba mtoto anatembea bila kujali mbele ya maofisa wa polisi wanaofanya doria katika Morro dos Macacos</p></div>
<p>Mradi wa habari wa jamii <em><a href="http://www.vivafavela.com.br/">Viva Favela</a></em> [pt] unatoa <a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46399&#038;sid=87">maelezo ya wakazi walioshuhudia kwa macho ugomvi huu</a>. Waandishi wao wa kiraia – ambao wote wanaishi katika mstari wa mbele wa mapambano – wamekusanya maoni kutoka kwa wakazi wa kwenye maeneo hayo na picha za siku ambayo vita vya madawa ya kulevya vilianza jijini Rio de Janeiro.</p>
<p>Mtu wa kwanza kusikilizwa na <em>Viva Favela</em> alikuwa Hugo Mattos, ambaye anaishi kwenye mtaa ambao ndio njia ya kuelekea kwenye eneo ambalo matukio yalijiri (Morro dos Macacos). Alisema kuwa wauza madawa ya kulevya walitumia bunduki zenye nguvu ya juu na akaongeza kuwa kuna aina fulani ya hofu ya jumla kwamba ikiwa polisi watalichukua tena eneo linalokaliwa na wauza madawa ya kulevya, patazuka machafuko mabaya kama jibu kutoka kundi linalotawala Morro dos Macasos: </p>
<blockquote><p>O tiroteio começou por volta das duas da manhã e só terminou às oito horas, quando a policia chegou. Muita gente teve que dormir fora de casa nesse dia.</p>
<p>As pessoas dizem que ninguém deve sair de casa depois das 10 horas, porque algo pode acontecer.</p></blockquote>
<div class="translation">Kutupiana risasi kulianza kwenye majira ya saa 8 za usiku na kumalizika saa 2 asubuhi wakati polisi walipowasili. Iliwabidi watu wengi walale nje ya nyumba zao usiku ule. Watu wanasema kuwa hakuna anayepaswa kutoka nyumbani kwake baada ya saa 4 za usiku, kwa kuwa lolote linaweza kutokea.</div>
<p>Kwa mujibu wa <em>Viva Favela</em>, taarifa kama hizi huletwa wakati wote kutoka kwa wakazi wa maeneo hayo, ambao hawana uwezo wa kufanya lolote. Jioni ya Jumanne tarehe 20 Oktoba, wakazi wa Morro Sao Joao waliandamana kutokana na hofu ya kuvamiwa kama majibu (ya wauza madawa walioshambuliwa awali), hofu ambayo ilitajwa kuwa haikuwa na msingi wowote na Mkuu wa jeshi la Polisi, Kanali Mario Sergio Duarte. Hata hivyo, watu walikwishaingiliwa na hofu. Mkazi mwingine wa Morro dos Macacos, Karen Carolina Nascimento anasema kuwa kutupiana risasi kati ya wauza madawa ya kulevya na polisi kumekuwa kukiendelea kwa miezi miwili. Anahofu mgogoro mpya:</p>
<blockquote><p>Já era praticamente uma rotina, mas no último sábado foi diferente. O confronto aconteceu por causa de uma tentativa de invasão e não foi a primeira vez que os traficantes do Morro São João tentam. O comentário que se escuta no morro é que a facção rival deu uma ordem para tomar o Morro dos Macacos até dezembro e que esses bandidos tiveram ajuda de policiais para tentar invadir.</p>
<p>O policiamento não está reforçado e os moradores estão muito apreensivos com medo de uma outra invasão. Eu trabalho no pé do Morro São João e vou para a minha casa andando. Ontem só havia um único carro com dois policiais dentro parado em uma esquina. Em cima do morro não existe policiamento nenhum. Uma vez ou outra um carro blindado sobe e faz uma ronda. Estamos com muito medo porque com certeza a facção rival vai tentar tomar novamente.</p></blockquote>
<div class="translation">[Vita vya Magenge] vimekuwa ni kama kama kawaida, lakini jumamosi hii ilikuwa tofauti. Mgogoro ulianza kwa sababu ya jaribio la kuivamia Morro dos Macacos lililofanywa na wauza madawa ya kulevya kutoka Morro Sao Joao, na hili halikuwa jaribio la kwanza. Neno lililokuwa kwenye kwenye makazi ni kuwa kundi shindani limetoa amri ya kuiteka Morro dos Macacos ifikapo mwezi Desemba na kwamba maofisa wa polisi walikuwa wanawaunga mkono wauzaji hao.<br />
Doria ya polisi haitekelezwi na wakazi wana wasiwasi mkubwa, wanahofia uvamizi mpya. Ninafanya kazi chini ya bonde la Morro Sao Joao na hutembea ninaporudi nyumbani. Jana, kulikuwa na gari moja tu lililokuwa na maofisa wawili wa polisi ndani yake lililoegeshwa kwenye kona. Hakuna doria ya polisi juu kwenye makazi. Mara moja moja kwa nadra gari iliyokingwa (mithili ya gari ya jeshi) huja huku juu na kufanya doria. Tumo kwenye hofu kubwa kwani tuna hakika kuwa kundi shindani litajaribu kulikomboa eneo.</div>
<p><em><a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46400&#038;sid=87">Viva Favela</a></em> [pt] pia inatoa maoni ya <em>Wagner da Silva de Barros</em>, mwenye umri wa miaka 29 ambaye ni mkazi wa Vila Penheiro kutoka Complexo da Mare, anayesema kuwa athari za mgogoro katika Morro dos Macacos umefika mbali kiasi hiki kwa sababu ya helikopta iliyotunguliwa na anaongeza kuwa vita hii itaenea pia kwenye  jamii nyingine nyingi:</p>
<blockquote><p>A queda do helicóptero e a morte dos três policiais chocou parte da população, mas na Maré, durante cinco meses, nós vivemos um confronto entre facções que matou muita gente, inclusive moradores que nada tinham a ver com o tráfico, e não teve nem metade da divulgação que esse tiroteio dos Macacos está tendo.</p>
<p>Esses tiroteios reforçam de que na favela só existe bandido e violência, mas o que muitas pessoas ignoram é que trabalhadores morrem durante os conflitos e são logo identificados como traficantes pela polícia.</p></blockquote>
<div class="translation">Kuanguka kwa helikopta na vifo vya maofisa watatu wa polisi kulishtua sehemu ya wakazi wa kwenye vitongoji, lakini Mare [vitongoji hivyo vya hali ya chini], kwa miezi mitano, tumeishi katika ugomvi baina ya makundi ambao umeua watu wengi zaidi, pamoja na wakazi ambao hawakuwa na uhusiano wowote na biashara ya madawa ya madawa ya kulevya, na hawa hawakupata hata nusu ya habari zilizotangazwa na vyombo vya habari juu ya mapambano ya risasi katika Morro dos Macacos.<br />
Mapambano haya ya risasi yanasisitiza ukweli kuwa katika maeneo ya maskini (favelas) kuna majambazi na machafuko, ila jambo ambalo watu wengi hawafahamu ni kuwa wafanyakazi hufariki wakati wa machafuko na haraka polisi huwatangaza kama wauza madawa ya kulevya.</div>
<p>Kwa mujibu wa <em><a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46400&#038;sid=87">Viva Favela</a></em> [pt], katika kesi ya Morro dos Macacos, vijana watatu wa kiume wasio na hatia ambao waliuwawa kwa risasi walijumuishwa kwenye orodha ya majambazi waliouwawa. Katibu wa Usalama Jose Mariano Beltrame alijirudi na kuomba msamaha kwa familia za Marcelo Costa Gomes, 26, Leonardo Fernandes Paulino, 27, na Francisco Haílton Vieira Silva, 24. Walikuwa wanarudi nyumbani kutokea kwenye hafla wakati uvamizi ulipotokea. Kijana wa nne, mhudumu wa hoteli Francisco Alaílton Vieira da Silva, 22, aliokolewa na wakazi na hivi sasa yuko hospitali katika kitengo cha huduma maalum. Mpenzi wake wa kike ni mjamzito wa miezi 3.</p>
<p>Walter Mesquista wa <em>Viva Favela</em> pia <a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=46399&#038;sid=87">anatoa picha za mgogoro huo</a> zilizopigwa na mpiga picha <em>Guillermo Planel</em> siku ambayo watu wanaiita “Vita vya Mihadarati”.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-001.jpg" title="Macacos-001" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-002.jpg" title="Macacos-002" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-003.jpg" title="Macacos-003" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-004.jpg" title="Macacos-004" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-005.jpg" title="Macacos-005" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-006.jpg" title="Macacos-006" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-007.jpg" title="Macacos-007" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-008.jpg" title="Macacos-008" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/Macacos-009.jpg" title="Macacos-009" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/macacos011_trat.jpg" title="macacos011_trat" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/macacos012_trat.jpg" title="macacos012_trat" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/macacos013_trat.jpg" title="macacos013_trat" class="aligncenter" width="400" height="300" /></p>
<p>Kuna mauaji takriban 6,000 kwa mwaka katika jimbo zima la Rio, ambalo lina wakazi milioni 14. Operesheni “Eneza Amani” yenye doria ya kudumu imekuwa ikitekelezwa kwa mwaka mzima katika vitongoji vitano. Ongezeko la uwepo wa polisi vitongojini kunayalazimisha magenge kupigania maeneo mengine.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/viva_favela_logoweb-300x136.jpg" title="viva_favela_logoweb" class="alignnone" width="300" height="136" /></p>
<p><em><a href="http://www.vivafavela.com.br/publique/cgi/cgilua.exe/sys/start.htm?infoid=40489&#038;sid=74">Viva Favela</a> ni mradi wa uanahabari wa kijamii ambao unafanya kazi na wanablogu malum pamoja na wapiga picha ambao wanaishi katika maeneo maskini ya Rio de Janeiro. Mradi huo uko chini ya uongozi wa Mhariri <a href="http://twitter.com/rodrigonogueira">Rodrigo Nogueira</a>. Unaweza kupata taarifa zaidi katika <a href="http://twitter.com/vivafavela">akaunti yao rasmi ya Twita</a></em> [pt] <em>na katika <a href="http://www.orkut.com.br/Main#Community?cmm=33684890">jamii </a>ya Orkut </em>[pt].</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/brazil-mtazamo-wa-wakazi-wa-vitongoji-maskini/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ufaransa: Tuzo ya Fasihi Yaja na Masharti</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ufaransa-tuzo-ya-fasihi-yaja-na-masharti/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ufaransa-tuzo-ya-fasihi-yaja-na-masharti/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 19 Nov 2009 06:32:14 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[France]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Literature]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=700</guid>
		<description><![CDATA[Mwanzo wa msimu wa Fasihi ya Kifaransa mwaka huu ulishuhudia mwandishi wa riwaya na michezo ya kuigiza mwenye asili ya Kisenegali na Kifaransa Marie N’Diaye akipewa tuzo iliyosuburiwa sana ya Prix Goncourt. Lakini, N’Diaye na familia yake walikwishahamia mjini Berlin miaka miwili iliyopita, hasa kutokana na siasa za rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy. Mwaka jana, jopo la tuzo hii yenye hadhi walizusha hisia kali pale walipomchagua mwandishi wa Kiafghani Atim Rahimi, kwa kitabu chake cha Kifaransa, Syngué Sabour. Je hii itakuwa ni fursa nyingine ya kusherehekea mchanganyiko wa aina mbalimbali katika jamii inayobadilika ya Kifaransa? Au itakuwa ni wasaa utakaoharibiwa na utete wa tukio?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/suzanne-lehn/">Suzanne Lehn</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/france-does-prestigious-literary-award-entail-a-duty-of-restraint/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mwanzo wa msimu wa Fasihi ya Kifaransa mwaka huu ulishuhudia mwandishi wa riwaya na michezo ya kuigiza mwenye asili ya Kisenegali na Kifaransa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Marie_NDiaye">Marie N’Diaye</a> akipewa tuzo iliyosuburiwa sana ya <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Goncourt_Prize">Prix Goncourt</a>. Lakini, N’Diaye na familia yake walikwishahamia mjini Berlin miaka miwili iliyopita, hasa kutokana na siasa za rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy. Mwaka jana, jopo la tuzo hii yenye hadhi walizusha hisia kali pale walipomchagua mwandishi wa Kiafghani Atim Rahimi, kwa kitabu chake cha Kifaransa, <em>Syngué Sabour</em>. Je hii itakuwa ni fursa nyingine ya kusherehekea mchanganyiko wa aina mbalimbali katika jamii inayobadilika ya Kifaransa? Au itakuwa ni wasaa utakaoharibiwa na utete wa tukio?</p>
<p>DW-World <a href="http://www.dw-world.de/dw/article/0,,4884146,00.html">anaeleza</a>:</p>
<blockquote><p>Katika mahojiano na gazeti la “Inrockuptibles” kiangazi kilichopita, N’Diaye alisema kuwa aliamua kuondoka Ufaransa na kuhamia Berlin mwaka 2007 ‘kwa kiwango kikubwa kutokana na Sarkozy”</p>
<p>Sakata hilo lilianza baada ya Eric Raoult, mtungasheria na mwanachama wa chama tawala cha Sarkozy, UMP, aliandika barua kwa waziri wa utamaduni wiki iliyopita akishauri kuwa N’Diaye akumbushwe “wajibu wa kujiheshimu” ambao unaambatana na tuzo ya Goncourt. </p>
<p>Katika kutoa majibu, wenye nguvu katika sekta ya utamaduni walishutumu kuwa kuna uchujaji katika malumbano haya. Bernard Pivot, mwanachama katika jopo la Goncourt, alimshutumu Raoult kuwa hafahamu chochote katika uwanja wa fasihi.</p></blockquote>
<p>N’Diaye, aliyezaliwa mwaka 1967 na mama Mfaransa na baba Msenegali, alishinda tuzo ya Goncourt kutokana na riwaya yake “Trois femmes puissantes” (”Wanawake watatu wenye nguvu”), hadithi inayohusu wanawake waliojikuta katikati ya Ufaransa na Senegal na katika mkasa wa dhiki mbaya ya uhamiaji usio halali kutokea Afrika.</p>
<p>“Hadithi ya hawa wahamiaji imesimuliwa mara nyingi kabla, lakini kama hii itawasaidia watu kufahamu hatima yao vyema zaidi, basi nitafurahi,” alisema N’Diaye.</p>
<p>Ni kitu gain kilichochochea hasira ya Eric Raoult? Si pungufu ya mahojiano ya mwanamke huyu mwandishi, wakati alipojibu swali la <a href="http://www.lesinrocks.com/actualite/actu-article/t/1257862620/article/raoultndiaye-on-nest-plus-en-1942/">gazeti la Les Inrocks</a>: “Je unajisikia vizuri katika Ufaransa ya Sarkozy?” alisema [Fr]:</p>
<blockquote><p>« Je trouve cette France-là monstrueuse. Le fait que nous (avec son compagnon l’écrivain Jean-Yves Cendrey, et leurs trois enfants – ndlr) ayons choisi de vivre à Berlin n’est pas étranger à ça. (…) Je trouve détestable cette atmosphère de flicage, de vulgarité… »</p></blockquote>
<div class="translation">Naiona aina hiyo ya Ugfaransa kuwa mbaya isiyovumilika. Ukweli kuwa sisi (N’Diaye, mpenzi wake, mwandishi Jean-Yves Cendrey, pamoja na watoto wao watatu) tuliamua kuishi mjini Berlin unahusiana na hili. (…) Naiona hali hii ya ulinzi mkali na tabia chafu inakifu…”</div>
<p>Mwanablogu wa sheria anayejulikana <em><a href="http://www.maitre-eolas.fr/post/2009/11/12/Prix-Busiris-pour-Éric-Raoult">Maître Eolas</a></em> anayabomoa bomoa madai ya Bw. Raoult katika makala ya kejeli iliyoandikwa kwa mantiki nzuri [Fr], na hatimaye anamtunukia tuzo ya “Prix Busiris” (“buse” inaweza ikatafsiriwa kama “upumbavu”)</p>
<p>Kwanza anasahihisha makosa ya sarufi:</p>
<blockquote><p>Tout d’abord, et le ministre de la culture et de la communication aura rectifié de lui-même, le devoir de réserve ne peut en tout état de cause être dû aux lauréats mais dû par les lauréats : cette erreur de préposition fait du lauréat le créancier alors que dans  la tête du député, il en serait évidemment le débiteur.</p></blockquote>
<div class="translation">Kwa kuanzia, na Waziri wa Utamaduni na Mawasiliano hawezi kusahau kujisahihisha, wajibu wa kujizuia hauwezi katika mfano wowote kuwapa wajibu waliopokea tuzo, lakini badala yake huwajibika kwa waliopokea tuzo; mapendekezo haya yenye makosa yanamfanya aliyepokea tuzo kuwa kama mkopaji wakati katika mawazo ya mbunge anakuwa kama vile ni mkopeshaji.</div>
<p>Na kisheria? Kati ya maandishi, mwanablogu ananukuu <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Declaration_of_the_Rights_of_Man_and_of_the_Citizen">Tamko la Haki za Mtu na za Raia la mwaka 1789 </a>pamoja na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/European_Convention_on_Human_Rights">Makubaliano ya Haki za Binaadamu ya Nchi za Ulaya</a>. Na “Wajibu wa Kujizuia au Kujiheshimu” huwa unawawajibisha watumishi wa umma?</p>
<blockquote><p>Le devoir de réserve est souvent invoqué à tort et à travers par des gens qui n’y ont rien compris comme interdisant à un fonctionnaire de s’exprimer, y compris parfois sur des affaires purement privées.</p></blockquote>
<div class="translation">Wajibu wa Kujizuia auKujiheshimu huwa unatolewa hovyo hovyo na watu ambao hawafahamu lolote juu ya wito huo, kama vile kumkataza mtumishi wa umma asiongee, mara nyingine hata kuhusu  mambo binafsi.</div>
<p>Mwanasheria anahitimisha kwa kutoaminika kwa mbunge, kabla ya kutoa pigo la mwisho:</p>
<blockquote><p>Ajoutons à cela qu’en 2005, en tant que maire du Raincy, lors des émeutes de l’automne, il fut le premier à proclamer l’état d’urgence dans sa commune pourtant épargnée par les actes de violence afin de griller la politesse au premier ministre, ce qui montre une certaine tendance à la gesticulation inutile pour attirer l’attention sur lui.<br />
Ce qui établit en même temps le mobile d’opportunité politique, et emporte la décision.</p></blockquote>
<div class="translation">Hebu tuongeze juu ya yote haya ukweli kwamba mnamo mwaka 2005, kama Meya wa Le Raincy, wakati wa machafuko ya kipupwe, alikuwa wa kwanza kutoa tamko la hali ya dharura ndani ya mji wake, na aliponusurika na machafuko hayo, alimzunguka Waziri Mkuu, jambo ambalo linanyonyesha tabia yake ya vitendo visivyo na maana ili watu wamuangalie.</p>
<p>Jambo ambalo wakati huo huo linathibitisha kuwa sababu kubwa ya kuchukua uamuzi ni kutaka kunufaika kisiasa. </p></div>
<p>Wanablogu wengine pia walikuwa na maneno makali.</p>
<p>Kwenye <em>Art contemporain, la peau de l&#39;ours</em>, Philippe Rillon <a href="http://rillon.blog.lemonde.fr/2009/11/10/marie-ndiaye-eric-raoult-et-le-devoir-de-reserve/">anaandika </a>[Fr]: </p>
<blockquote><p>Nous comprenons fort bien que le devoir de réserve s’impose à tout serviteur de l’Etat; mais depuis quand la littérature et les auteurs sont ils assimilés aux fonctionnaires avec leurs droits et devoirs?<br />
Nous avions déjà une “Culture administrée”, nous voici maintenant “artistes fonctionnaires” comme si Paris était Berlin-est d’avant la chute du mur…<br />
(…)<br />
Il serait quand même étonnant qu’au lendemain d’une hyper-médiatique commémoration de la chute du mur, ce godillot vienne gâcher le spectacle idylique des dominos qui tombent.</p></blockquote>
<div class="translation">Tunaelewa vyema kuwa wajibu wa kujizuia ni sheria kwa kila mfanyakazi wa dola; lakini tangu lini fasihi na waandishi wamewekwa kwenye kundi sawa na watumishi wa umma pamoja na haki na wajibu wao?<br />
Tayari tunao “utamaduni wa serikali”, na sasa tumegeuka kuwa “wasanii wa dola”, kana kwamba mji wa Paris umekuwa Berlini ya Mashariki kabla ya ukuta kuvunjwa…<br />
(…)<br />
Je isingekuwa jambo la ajabu siku baada ya kusherehekea kuanguka kwa ukuta, mshabiki huyu angeliweza kuharibu muonekano mzuri wa kete zilizokuwa zinaanguka.</div>
<p>Wakati huo huo, Marie N’Diaye baada ya jitihada za kushusha ukali wa maneno yake katika <a href="http://www.europe1.fr/Culture/Ndiaye-revient-sur-ses-propos-excessifs-sur-Sarkozy/%28gid%29/253818">mahojiano na Radio Station Europe 1</a>, ambayo katikati ya mzozo watu hawakuyaona, alimuomba Waziri wa Utamaduni wa Ufaransa, Frederic Miterrand. Waziri huyo <a href="http://www.leparisien.fr/flash-actualite-culture/marie-ndiaye-persiste-et-signe-frederic-mitterrand-juge-la-polemique-anecdotique-et-ridicule-12-11-2009-708919.php">ameuchukulia</a> mzozo huo kuwa ni kitu kigogo na cha kijinga” [Fr], na <a href="http://www.lefigaro.fr/flash-actu/2009/11/13/01011-20091113FILWWW00566-ndiaye-raoult-ne-regrette-rien.php">wahusika wakuu </a>wameshikilia <a href="http://www.marianne2.fr/Marie-NDiaye-ou-la-fable-de-l-ecrivain-rebelle_a182772.html?com">misimamo yao</a>. [Fr]</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ufaransa-tuzo-ya-fasihi-yaja-na-masharti/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>China: Obama ni Mshabiki Mkubwa wa Kutokuchuja Habari</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 17 Nov 2009 10:06:54 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[China]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=690</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naOiwan Lam  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa &#8220;Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari&#8220;.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/oiwan/">Oiwan Lam</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/17/china-obama-as-a-big-supporter-of-non-censorship/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Adam Minter amesikitishwa na maoni ya Obama kwenye Mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Jiji la Shanghai, hasa, maelezo yake kuwa &#8220;<a href="http://shanghaiscrap.com/?p=3920">Mimi ni muunga mkono mkubwa wa kutokuchuja habari</a>&#8220;.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/china-obama-ni-mshabiki-mkubwa-wa-kutokuchuja-habari/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Karibea: Tuzo za Fasihi ya Kifaransa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/karibea-tuzo-za-fasihi-ya-kifaransa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/karibea-tuzo-za-fasihi-ya-kifaransa/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 12:20:17 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Canada]]></category>
		<category><![CDATA[Diaspora]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[France]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Guadeloupe]]></category>
		<category><![CDATA[Haiti]]></category>
		<category><![CDATA[Language]]></category>
		<category><![CDATA[Literature]]></category>
		<category><![CDATA[Martinique]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Senegal]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=680</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naFabienne Flessel  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/fabienne-flessel/">Fabienne Flessel</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/06/caribbean-french-literary-prizes/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, <a href="http://www.alterpresse.org/spip.php?article8952">katika makala hii kutoka Haiti</a>, na <a href="http://indiscretions.over-blog.fr/article-le-goncourt-pour-marie-n-diaye-04-11-09-38785480-comments.html#comment50651606">hii kutoka Guadeloupe</a> na <a href="http://www.montraykreyol.org/spip.php?article3183">hii kutoka Martinique</a> [Fr]. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/karibea-tuzo-za-fasihi-ya-kifaransa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Finland: Suala la Lugha</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/finland-suala-la-lugha/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/finland-suala-la-lugha/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 16 Nov 2009 12:09:09 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[Finland]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[History]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Language]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Literature]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sweden]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=677</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naVeronica Khokhlova  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Nordic Voices anaandika kuhusu &#39;suala la lugha&#8221; huko Finland. 
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/neeka/">Veronica Khokhlova</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/16/finland-the-language-issue/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Nordic Voices <a href="http://nordicvoices.blogspot.com/2009/11/land-of-one-language.html">anaandika</a> kuhusu &#39;suala la lugha&#8221; huko Finland. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/finland-suala-la-lugha/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
