2009-11-06
2009-11-05
Sub-Saharan Africa
Marvin anaandika kuhusu Afripot, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua kasi na kupamba moto. Ni nani ajuaye, inaweza kutengeneza joto la kutosha na kulazimisha mabadiliko tuayoyahitaji sana.”
2009-11-04
Georgia: Aibu Katika Kanisa la Orthodox
Sub-Saharan Africa
Mradi wenye lengo la kutengeneza ramani mpya ya wazi ya kitongoji cha Kibera mjini Nairobi, Kenya: “Na jana tulimaliza siku nzima pale MS Action Aid kenya, ambako wanafunzi wa ki-Denmark pamoja na wengine waliotokea kwenye mashirika mbalimbali kama vile Ushahidi, UNICEF, Umande Trust na World Bike, walipoonyeshwa mbinu za kutengeneza ramani.”
Middle East & North Africa
Kwa mujibu wa Kian majeshi ya usalama yaliwashambulia waandamanaji katika viwanja vya hafteh tir mjini Teheran na kuwajeruhi watu kadhaa.
Central Asia & Caucasus
Mwanablogu wa Emotions on Air, Mind Mute anatafakari marajio ya jamii kwamba wanawake watabakia mabikira mpaka watakapofunga ndoa. Japokuwa ipo nchini Azerbaijan, blogu hiyo inabaini mfumo unaofanana wa maadili katika eneo lote la Caucasus na inaongelea kuhusu dhana na taratibu za namna hiyo za mfumo dume.
South Asia
Mohammad Malick anatoa maoni juu ya shambulizi la kigaidi la hivi karibuni kwenye soko la watu wa tabaka chini na la kati huko Peshawar: “limeonyesha kuwa hii ni vita ambyo magaidi wanasimama upande mmoja wa mstari wa damu, na sisi wananchi upande mwingine.”
2009-11-03
Middle East & North Africa
Katika Th!nk About It, Adela anaandika kuhusu Siku ya Kimataifa ya Bahari Nyeusi.







