<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; charahani</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Saudi Arabia: Kina Mama Huru</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/09/saudi-arabia-kina-mama-huru/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/09/saudi-arabia-kina-mama-huru/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 06 Sep 2008 01:57:04 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Humor]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[TOPICS]]></category>
		<category><![CDATA[TYPE]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=16</guid>
		<description><![CDATA[WAKATI kukiwa hakuna shaka kwamba kuna vizuizi kwa wanawake waishio Saudi Arabia, havifanani na taswira iliyojengwa na wageni dhidi ya taifa hilo. Katika makala hii tunao ushauri kwa wakina mama wanaotaka kutembelea jiji la Jeddah wakiwa peke yao, kuna muhtasari wa hoteli za kina mama pekee jijini Riyadh, na wito kwa wageni wote wanajihisi kuzungumza kwa niana ya kina mama wanaokandamizwa wa Saudia.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ayesha-saldanha/">Ayesha Saldanha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/29/saudi-arabia-independent-women/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>WAKATI kukiwa hakuna shaka kwamba kuna vizuizi kwa wanawake waishio Saudi Arabia, havifanani na taswira iliyojengwa na wageni dhidi ya taifa hilo. Katika makala hii tunao ushauri kwa wakina mama wanaotaka kutembelea jiji la Jeddah wakiwa peke yao, kuna muhtasari wa hoteli za kina mama pekee jijini Riyadh, na wito kwa wageni wote wanajihisi kuzungumza kwa niana ya kina mama wanaokandamizwa wa Saudia.</p>
<p>Tunaanza na Hala, ambaye anaishi Marekani hivi sasa na anablogu katika blogu yake HALA_IN_USA, anayetoa ushauri kwa marafiki zake akinamama wasio na waume watakaotaka kutembelea jiji la <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jeddah">Jeddah</a> kwa mara yao ya <a href="http://hala1.wordpress.com/2008/08/27/visiting-jeddah-a-single-woman-perspective/">kwanza</a>:</p>
<blockquote><p>Wanawake katika jiji la Jeddah huvaa gauni lijulikanalo kama &#8220;<a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Abaya">Abaya</a>&#8220;, gauni hili hupaswa kuvaliwa juu ya mavazi mengine hivyo vaa nguo nyepesi za ndani haswa wakati wa majira ya kiangazi. Ushungi si lazima kwa akina mama wageni lakini ni vazi linalopendekezwa kuvaliwa (kwa ajili ya usalama na kuepuka usumbufu usiokuwa wa lazima) katika maeneo ya kiutamaduni.</p>
<p>Kuna maeneo mbalimbali ya kuyaona jijini Jeddah, ninapendekeza Balad, jiji la kale la Jeddah, likiwa na majengo yaliyosanifiwa kizamani, Jengo la Naseef ni mfano mmojawapo wa majengo ya kale. Unaweza kununua bidhaa za kitamaduni za kale kutoka katika maduka ya kizamani na ukafurahia marashi ya Kiarabu kama vile Udi Bukhour, vilevile kuna bidhaa za kazi za mikono za kitamaduni kama balbu, [fanusi], tende, pipi na vitambaa vya rangi mbalimbali.</p>
<p>Pia kuna <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jeddah_Corniche">barabara maarufu jijini Jeddah iliyokatiza ufukweni mwa bahari </a>. Napendekeza upite katika barabara hiyo mapema alfajiri au jioni saa 12 ili uweze kujionea maumbile ya kupendeza baharini, pia kuna chemchem ya baharini, moja ya chemchem zilizoko juu zaidi kuliko nyingine yoyote duniani. Kuna machaguo mbalimbali ya vyakula katika barabara ya kupendeza ufukweni mwa bahari, kuanzia migahawa ya ya anasa mpaka maduka ya vyakula vya haraka au hata vijiduka vidogo vya biskuti na chipsi. Wenyeji hukuketi katika ufukweni kwa masaa na watoto wao wakicheza karibu yao huku wakiwaangalia wapita njia.</p></blockquote>
<p>Kwa ushauri zaidi wa Hala kuhusiana na unachotaka kukiona jijini Jeddah, angalia <a href="http://hala1.wordpress.com/2008/08/27/visiting-jeddah-a-single-woman-perspective/">hapa</a>.</p>
<p>Wakati huo huo bloga <em>American Bedu</em>, ambaye ni Mmarekani anayeishi Saudi Arabia, anatueleza kile anachokifikiri kuhusiana na hoteli za kina mama pekee jijini <a href="http://americanbedu.com/2008/08/28/so-what-if-riyadh-has-a-women-only-hotel/">Riyadh</a>.</p>
<blockquote><p>Hoteli ya <a href="http://www.luthanspa.com/default.htm">Al Luthan</a> na bafu lake ni hoteli ya kwanza kabisa ya wanawake pekee ya aina yake jijini Riyadh. Ni hoteli ya kifahari na ina bafu la chemchem maalumu kwa wanawake pekee. Ni hoteli ya huduma zote yenye kutoa huduma za uhakika na yenye kutoa malazi salama. Al Luthan inapokea wageni wa kike kutoka Saudia na wasio Wasudia. Hivi sasa baadhi ya wanawake wamezungumza na vyombo vya abari wakisema kuwa kuzinduliwa Al Luthan ni mojawapo ya upigani hatua nyuma.  Kwa mujibu wa wanawake hawa, wanaona kama ni kupiga hatua kuelekea nyuma kwa ufalme wa taifa hilo kutokana na ukweli kwamba tayari kuna ubaguzi na siyo tu kwamba wanawake wana haki kidogo lakini kwa kushabikia na kuafiki uanzishwaji wa hoteli ya wanawake peke yao yenye eneo la kuogea inarudisha nyuma harakati za kina mama kudai haki. Pengine nimo kwenye kundi dogo katika jamii, lakini nachukua mtazamo mbadala. Al Luthan siyo hoteli ya kipekee ikilinganishwa na hoteli nyingine duniani. Hoteli za wanawake au hoteli zinazotenga safu nzima ya ghorofa kwaa jili ya wanawake zipo karibu katika kila jiji kubwa (na hata kwenye miji isiyo mikubwa) duniani. Siku za nyuma wakati nilipokuwa nikisafiri safari nyingi za kimataifa, nilikuwa nikifurahia kupanga katika hoteli zenye safu maalumu kwa ajili ya wanawake pekee. Haswa katika  majiji ya kigeni ambayo hayakuzoea kuwa na wafanyabiashara wanawake wanaosafiri peke yao. Kwa hiyo mimi sioni kama kuanzishwa kwa hoteli hii maalumu kwa wanawake kuwa ni hatua ya kurudi nyuma asilani bali chaguo jema kwa wanawake kuwa nalo ndani ya falme.</p></blockquote>
<p>Bloga kutoka Riyadh, <em>Sweet Anger</em> amechoshwa na wageni wanaodhani kuwa wanawake wa Kisaudia wanakandamizwa, wakati hawajui lolote kuhusu maisha yao au <a href="http://sweetangerksa.blogspot.com/2008/08/saudi-arabia.html">jamii</a>: </p>
<blockquote><p>Basi, nilikuwa nikitafiti mtandaoni kitu kimoja au kingine nikakutana na ujumbe kuhusu ripota aliyekuwa Saudia ambaye ni mwanamke na hivyo hakuruhusiwa kukaa kwenye sehemu ya wanaume ndani ya mgahawa wa Starbucks.umm boo hoo hoo. Kitu kilichonishika zaidi siyo ile makala yenyewe, lakini maoni. […] Nataka ieleweke kwamba Saudi siyo mahema machache yanayounganishwa na ngamia wanaorandaranda, na wanaume wenye vilemba waimbao &#8220;Allah o akbar&#8221; huku wakiwabaka wanawake kwa sababu ni haki yao na wanamiliki nyumba ya harimu yenye vigoli si  chini ya 20. Oh, na pia  hatutahiri wanawake wetu, hilo ni jambo la hovyo na ni kosa katika ngazi nyingi.  Wanawake hawafungiwi nyumbani na yeyote yule ambaye kwamba hilo ni jambo la  utamaduni wa familia na siyo nchi, upo? Vyema. Hatuko nyuma nyie mafidhuli, sisi ni wahafidhina, yaani, kama unapotaka kwenda kujichanganya na mtu wa jinsia tofauti kuna maeneo maalumu. […] Sasa hoja yangu ya msingi hapa ni kwamba hivi tangu lini mmeanza kuhukumu watu: &#8220;Fungeni Starbucks!! Zisiwe na sehemu zinazokaribisha familia&#8221; – umm, hapana samahani? Silalamiki na ninahitaji kahawa yangu, tuache utani, POTEENI MBALI, sikukodi mtu yeyote awe msemaji wangu.</p>
<p>Kwa wale ambao bado mnashawishika kwamba sisi ni taifa kandamizi na kwamba sisi wanawake masikini tunahitaji kufunzwa namna ya kupambana na kama sivyo vyema vyema endeleeni kutupigania, ngojeni niwape maelezo mafupi namna siku ya kawaida inavyokuwa jijini Riyadh. Jana niliamka nikatengeneza kahawa yangu… nikatinga vazi langu la abaya (kama unaona hili linatisha kufikirika, lifikirie kama jaketi), nikamchukua malaika wangu mdogo, nikaingia ndani ya gari yangu iendeshwayo na dereva ndani yake, nikamshusha binti yangu, halafu nikaenda kazini. Mida ya saa 7:30 napata chakula cha mchana na marafiki zangu wa kike kutoka mgahawa wa Subway, halafu nikarejea kazini na kutoka saa 10:30 jioni, narejea nyumbani, napumzika, naoga natinga mavazi yangu, namsubiri dereva anipeleke mgahawa wa Wachina kwani nilikuwa nimewakaribisha marafiki zangu wa kike. Nafika pale mida ya saa 3:45 hivi halafu naondoka kama saa 6, nafika nyumbani, naingia mtandaoni, naangalia facebook na hotmail, halafu naingia kitandani saa 8. MUNGU WANGU, JINAMIZI GANI HILI, NINAWEZAJE KUISHI MAISHA YA KIKANDAMIZWA NAMNA HII, AAAAHHHHHH!!!! […] Hoja yangu ni kwamba baadhi ya watu hawana welewa kuhusu nini kinaendelea ndani ya maisha yetu na bado wanafikiri wana haki ya kuamua na kuwa wakuu. Tuko tofauti, naam, na kwa kuwa tuko tofauti na vile ambavyo unafikiri ni sawa haitufanyi sisi kuwa wabaya au wenye makosa inatufanya sisi kuwa sisi. Kabiliana na ukweli huo au jitoe.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/09/saudi-arabia-kina-mama-huru/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Angola, Brazil: Mshituko na Utengano wa Kitamaduni</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/angola-brazil-mshituko-na-utengano-wa-kitamaduni/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/angola-brazil-mshituko-na-utengano-wa-kitamaduni/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 31 Aug 2008 07:39:18 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Angola]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Business]]></category>
		<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[Diaspora]]></category>
		<category><![CDATA[Elections]]></category>
		<category><![CDATA[Ethnicity]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Portuguese]]></category>
		<category><![CDATA[Racism]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=14</guid>
		<description><![CDATA[Mahusiano maalum kati ya Angola na Brazili yanamaanisha kwamba biashara kati ya makoloni haya mawili ya zamani ya Ureno inashamiri - kadhalika uhamiaji kutoka pande zote za Atlantiki. Lakini, ni vipi hawa watoto wawili wanavyoishi? Ujumbe huu unatoa mitazamo ya wote, kutoka kwa bloga wa Kiangola na wa Kibrazili waishio Luanda.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/paulagoes/">Paula Goes</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href=' http://globalvoicesonline.org/2008/08/17/angola-brazil-a-culture-shock-divide/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/08/47276853_eaf456fb02.jpg' alt='' class='alignnone' /><br />
<strong>Kinyago cha mtumwa mweusi kilichochongwa na Luiz Paulino da Cunha. Picha kwa hisani ya </strong><a href="http://www.carfweb.net/">Asasi  ya Watoto Walio Hatarini</a>. </p>
<p>Angola na Brazil zina <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Angolaâ??Brazil_relations">uhusiano maalum</a> baina yao, kutokana na matumizi ya lugha moja na pamoja na historia yao ya kutawaliwa huko nyuma - nchi hizi mbili zilikuwa sehemu ya <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Portuguese_Empire">himaya ya Wareno </a>– na utamaduni wa pamoja unaotoka na historia ya asili moja. Tangu mwaka 2000, biashara kati ya mataifa haya mawili ilianza kukuwa na sasa inachanua. Kwa mujibu wa Chama cha Makampuni ya KiBrazili nchini Angola (AEBRAN), <a href="http://ipsnews.net/news.asp?idnews=40040">biashara kati ya mataifa mawili</a> haya imekuwa kwa mara sita zaidi tangu mwaka 2002. </p>
<p>Kutokana na kuongezeka huko kwa biashara, uwepo wa makampuni ya Brazili nchini Angola pia kumeongezeka. Kumepelekea, pia ongezeko la uhamiaji kutoka Brazili kwenda Angola kwa kadri ya asilimia 70 kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita. <a href="http://www.migrationinformation.org/Profiles/display.cfm?ID=311">Inakadiriwa kuwa kuna Wabrazili 5,000 waliosajiliwa nchini Angola</a> haswa wanaojishughulisha na masuala ya ujenzi, uchimbaji madini na biashara za mazao ya kilimo. Maendeleo haya mapya katika historia ya Angola, nchi iliyozoea kuwa na uhamiaji kuelekea ng&#39;ambo nyingine ya Atlantiki, yanapelekea kwenye mtikisiko wa kiutamaduni usioweza kuepukika kwa wote, Wabrazili na Waangola pia.</p>
<p>Hapa chini kuna habari zilizopachikwa katika kurasa za blogu mbili zikionyesha mitazamo tofauti baina ya watu wawili kwa kuibua masuala muhimu kama uhamiaji, ubaguzi wa rangi, ukabila na heshima miongoni mwa watu. Zaidi ya yote, wanabainisha mahusiano ya namna mbalimbali na yenye mchanganyiko - kwa kuwianisha yale yanayofanana na yanayotofautiana - miongoni mwa watoto hao waliotenganishwa na bahari wakati wa makuzi yao. </p>
<p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/08/47276856_812db9808b.jpg' alt='' class='alignnone' /><br />
<strong>Kinyago cha mtumwa mweusi kilichochongwa na Luiz Paulino da Cunha. Picha kwa hisani ya </strong><a href="http://www.carfweb.net/">Asasi  ya Watoto Walio Hatarini</a>. </p>
<p><a href="http://casadeluanda.blogspot.com/2008/08/em-contagem-decrescente.html">Migas</a> [pt], Mbrazili anayeishi Luanda, anasema yafuatayo:</p>
<blockquote><p>Nimekuwa nikiuangalia uchaguzi wa Septemba kwa mtazamo chanya. Nina matumaini kwamba matukio ya vurumai yaliyowahi kutokea huko nyuma hayatatokea tena. Kila mmoja anakubaliana kuwa taifa linahitaji amani ili kuweza kufuatilia makuzi ya uchumi, maendeleo, hali bora ya maisha. Labda maisha bora ni lengo lililokwishasahaulika. Hata hivyo, tukio linakaribia. Septemba 5 ni siku iliyochaguliwa na kila mmoja anasubiri kwa hamu awe raia wa Angola au wa nje.</p></blockquote>
<blockquote><p>Ninaishi katika eneo ambalo mimi peke yangu ni mgeni kutoka nje ya nchi. wengine wote ni watu weusi, waliopo katika tabaka ambalo siwezi kujitambulisha nalo. Siyo matajiri na wala siyo masikini. Lakini hawako kwenye tabaka la kati pia. Naweza kusema ni masikini zaidi kuliko matajiri, kwa mujibu wa viwango vyangu. Hata hivyo, ni matajiri kiasi kuweza kuwa na hifadhi za maji, majenereta, magari na vyakula katika meza zao. Katika moja ya wikiendi zilizopita, kulikuwa na sherehe katika kaya mojawapo.  Ilikuwa ni hafla ya kuadhimisha kuzaliwa. Ninajuta kushinda nyumbani siku hiyo.</p></blockquote>
<blockquote><p>Hafla hiyo iliendelea mpaka mapambazuko na mcheza santuri (DJ) alichagua miziki kabambe. Nilijijutia kwa sababu nilikuwa nimekwishaamua kubaki nyumbani na kulala mapema. Baada ya kurejea nyumbani nikitokea dukani majira ya saa nne hivi usiku, nikaona gari moja likiwa limeegesha katika sehemu yangu ya maegesho.  Sikuwaambia waondoe gari lao, lakini nikatafuta &#8220;suluhisho la haraka&#8221; (katika desturi nzuri ya kaskazini) ili kwamba [magari] yaendelee kuwepo pale. [gari] langu na lile la mgeni. Mgeni, ambaye ni wazi alikuwa amelewa, aliniacha nikisubiri na akarejea kwenye hafla, kwa madai ya kutafuta funguo za gari. Dakika chache baadaye, alisahau ombi langu na alikuwa akisakata muziki wa dansi na watu wengine.</p></blockquote>
<blockquote><p>Nilimudu kukabiliana na suala lile angalau kidogo, lakini ni lazima nikiri sikupenda tabia yao. Habari hii inabainisha hofu zangu.  Sina shaka kwamba uchaguzi utaleta kiwango kikubwa cha ulevi, hafla kadhaa na tabia za hovyo. Na hilo linanitia hofu miye. Kama mpaka sasa sijapata kuhisi kukosa raha kwa kuishi kwenye maeneo ambayo nyumba yangu pekee ndiyo makazi ya mtu mweupe, niligundua usiku ule kwamba hafla zinazochangamshwa na pombe zinaweza kuleta matukio ya usumbufu, hata katika sehemu tunazojihisi vyema. </p></blockquote>
<p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/08/47263530_65f92c74bb.jpg' alt='' class='alignnone' /><br />
<strong><a href="http://www.flickr.com/photos/beija-flor/47263530/">Mtoto wa miaka 12 Naomi Leonardo de Queiros</a>, Picha kwa hisani ya <a href="http://www.carfweb.net/">Asasi  ya Watoto Walio Hatarini</a>.</strong></p>
<p>Hapa chini kuna mtizamo tofauti, kuhusu hafla nyingine na taswira nzima ya uhamiaji huu mpya na <a href="http://patriciaguinevere.blogspot.com/2008/08/enigmas-racismo-no-brasil.html">Gil Gonçalves </a>[pt], raia wa Angola:</p>
<blockquote><p>Jijini Luanda, Kampuni za Brazil zinajihusisha na ubeberu wa Marekani. Brazil ni koloni la Marekani. Wengi, kwa kweli raia wengi wa Brazili wameshawasili na wanazidi kuwasili Luanda kama samaki wa kopo.</p></blockquote>
<blockquote><p>Kule Movicel, kuna kampuni ya mawasiliano ambako wanashikilia imara idara ya masoko, wanawaleta kaka na dada zao kama vile ni wataalamu wenye ujuzi wa juu wa masuala ya teknolojia. Watu wa Luanda ndiyo wanawafundisha jinsi ya kufanya kazi, kwa sababu masikini watu hao wamefika hapa wakiwa hawajui kusoma. Nchini Brazili inaonekana kama vile hakuna Vyuo Vikuu au kama vipo basi havifanyi kazi. Wanapata mishahara katika maalfu ya dola za kimarekani na wana haki ya kupata maalfu marupurupu ya anasa.  Na wa-Luanda wanalipwa dola kiduchu. Mfumo wa kikoloni lazima udumishwe.</p></blockquote>
<blockquote><p>Wanaume na wanawake wa Kibrazili wamevamia hoteli, iko kwa ajili ya miliki yao tu. Wanavuta sana (sigara), wanfanana na volkeno inayolipuka wakati wote. Kila mara wanaangusha pati kwenye kiwambaza. Kama watu wasio na elimu ya masuala ya kijamii wanapiga wanaporomosha miziki miovu  inayowakosesha usingizi watwana wa Luanda. Hawajui, wanajifanya hawajui , kwamba jijini Luanda uchafuzi wa mazingira kwa kupiga kelele ni kinyume cha sheria na ni kosa la jinai., Wageni wasioheshimu sheria za nchi walizofikia wanastahili kutimuliwa. Lakini kwa kuwa [hoteli] inamilikiwa nao na baadhi ya marafiki zao kutoka Luanda…</p></blockquote>
<blockquote><p>Cha kushangaza katika yote haya ni kwamba Wabrazil… wote ni weupe. Wako wapi wanaume weusi? Wananawake weusi? Je wamekimbia kutoka <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Zumbi"><em>Zumbi quilombo?</em></a> Hivi walipelekwa katika makambi ya ya maangamizi ya Nazi? Au wamejificha katika misitu ya Amazoni? Au wameangamizwa? Je hivi hawatakiwi au ni haramu? Au wanapamba maonyesho ya wanyama mwitu? Au wametupwa baharini?</p></blockquote>
<blockquote><p>Kwanini pasiwe na ujasiri wa kusema hadharani kwamba hakuna Wabrazili weusi huko Brazili!</p></blockquote>
<p>Picha inayoelezea kisa hiki zinatoka katika mtandao wa picha wa <a href="http://www.flickr.com/photos/beija-flor/sets/1030536/">Symbols and Symbolism Flickr photo set</a> kwa hisani <a href="http://www.carfweb.net/">Asasi ya Watoto Wanaoishi katika Mazingira Hatari </a>na unatumiwa chini ya leseni ya mfumo Huru wa Haki Miliki. Zinaonyesha picha za historia ya miaka 300 ya utumwa nchini Brazil na athari zake ndani ya nchi hiyo, kama vile urithi wa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/CandomblÃ©">Candomblé</a>. Hapa chini ni maelezo ya picha hiyo:</p>
<blockquote><p>Mtu mweusi aling&#39;olewa kutoka katika ardhi yake na kuuzwa kama bidhaa, utumwani. Aliwasili nchini Brazili kama mtumwa, kifaa; kutoka katika ardhi yake alitoka kama mtu huru. Wakati wa safari, safari ya utumwani, alipoteza utu wake, lakini utamaduni wake, historia yake, nchi yake, na uzoefu wake  alikuja navyo. </p>
<p>Miaka 300 ya historia ya utumwa wa mtu mweusi nchini Brazili imeacha athari kubwa ndani ya nchi hiyo. Candomblé ni mojawapo ya athari hizo, dini iliyojawa na siri nyingi, ishara za matambiko yanayofahamika tu kwa wanaopitipia matambiko hayo lakini pia ni ni sehemu muhimu ya utamaduni wa Brazili.  Hakuna idadi kamili kuhusiana na watu wangapi wanaabudu Candomblé. Serikali inakadiria, kihafidhina, kwamba kuna vituo zaidi ya 300,000 vya kuabudia imani za Wabrazili wenye asili ya Afrika, ambavyo vinajumuisha  Candomblé. Wanaoshiriki katika imani hizo wanadhaniwa kufikia angalau theluthi moja ya watu wote wa Brazili wanaokaribia milioni 170. Wengi wanaabudu katika Ukatoliki na Candomblé.</p>
<p>Bahia, jimbo ambalo lina asilimia kubwa zaidi ya watu  weusi, ndiyo makao makuu ya dini hii, ambayo inafuata kwa karibu asili yake ya Kiafrika na hasa tamaduni za Kiyoruba za Nigeria na za Kibantu za Angola na Kongo. Tamaduni za Kiyoruba zinazojumuisha majina yanayotumika sana ya Orisha (miungu ya mahekalu ya Kiafrika), bado inatawala sana. Hivi sasa Candomblé inatambulika rasmi na inalindwa na serikali ya Brazil. Hata hivyo, enzi za utumwa na miongo mingine iliyofuata baada ya kukomeshwa kwa biashara hiyo ya watu nchini Brazil mwaka 1888, ibada za Candomblé zilipigwa marufuku na serikali na kanisa Katoliki, na wafuasi wake waliadhibiwa vikali.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/angola-brazil-mshituko-na-utengano-wa-kitamaduni/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Arabeyes: Rais wa Mauritania Aliyepinduliwa Katika mapinduzi ya Kijeshi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 17 Aug 2008 23:10:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Algeria]]></category>
		<category><![CDATA[Arabic]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[French]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Iraq]]></category>
		<category><![CDATA[Mauritania]]></category>
		<category><![CDATA[Morocco]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Western Sahara]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=10</guid>
		<description><![CDATA[ &#183; Imetafsiriwa na charahani &#183;  Angalia ujumbe mama 

MAKAMANDA wa jeshi wamemuondoa madarakani Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi, rais wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em> &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/06/arabeyes-mauritanian-president-ousted-in-military-coup-detat/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/08/457px-sidi_mohamed_ould_cheikh_abdallahi2.jpg' alt='' class='alignright' /><br />
MAKAMANDA wa jeshi <a href="http://www.abc.net.au/news/stories/2008/08/07/2326564.htm">wamemuondoa</a> madarakani <a href="http://www.answers.com/President%20Sidi%20Ould%20Cheikh%20Abdallahi">Rais Sidi Ould Cheikh Abdallahi</a>, rais <a href="http://www.answers.com/Mauritania">wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi huru katika miongo miwili</a>, katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanywa Jumatano iliyopita baada ya mtafaruku wa kisiasa uliotokana na rais huyo kuwatimua kazi majenerali wanne wa ngazi za juu wa jeshi.  Makamanda wa jeshi walitangaza kuundwa kwa Baraza jipya la taifa na kiongozi wake, <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Mohamed_Ould_Abdel_Aziz">Jenerali Mohamed Ould Abdel Aziz </a>(mmoja kati ya majenerali wanne wa jeshi waliotimuliwa), kwenye radio na vituo vya televisheni vya serikali. Jenerali Abdel Aziz ni miongoni mwa walioshiriki <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/2005_Mauritanian_coup_d%27%C3%A9tat">mapinduzi ya kijeshi nchini Mauritania mwaka 2005</a>.</p>
<p>Bloga kutoka Algeria <em>The Moor next Door</em> amekuwa <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/the-president-will-not-be-taking-calls-today/">akiblogu</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/china-and-mauritania/">habari</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/coup-snapshots/">hii</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/developing-story/">kwa kina</a> <a href="http://themoornextdoor.wordpress.com/2008/08/06/summer-time-coups/">anaripoti</a>:</p>
<blockquote><p>Ninapozungumza na Wa-Mauritania wanaojua, baadhi yao walihisi kutokea kwa mapinduzi wakati wa kiangazi kama ilivyotokea, wakati wa kipupwe au isingeweza kutokea kabisa. Hisia zangu mara zote zilikuwa zikinielekeza kwamba mapinduzi haya yangefanyika majira ya kiangazi (Sijawahi kuandika bayana juu ya hili, lakini nimelielezea hili katika majadiliano na sikutaka kuchangia lolote kuhusiana na sakata hili. (1) kwa sababu Western Sahara Info. taarifa za kutoka Sahara Magharibi zilielezea kinaganaga na hakukuwa na haja ya kushindana ikiwa wewe ni mmoja wa mabloga wawili au watatu  unakuwa miongonimwa  wanaofuatilia sakata hili kwa karibu sana. (2) nilitaka kuhakikisha kwamba kama &#8216;ningetabiri&#39; jambo hili nisingekosea; Ningeweza kutabiri kuwa &#8216;Mwishoni mwa miezi ya Mei, Juni, Julai na Agosti Serikali ya Rais Sidi, isingelikuwapo tena&#39; na ningekuwa nimekosea; mimi si mtabiri wa hali ya hewa, na (3)  sijawahi kukutana na raia wa Mmauritania ambaye lolote jema la kumzungumza kuhusu Sidi, ukiachilia mbali uzuri wa wajihi wake.) Mojawapo ya mashinikizo yaliyomfanya Rais Sidi afanye alivyofanya ni kuwapo tishio la kuundwa tume huru ya kuchunguza mapesa ya mfuko wa maendeleo wa mkewe, tume ambayo ingemuweka hata yeye mwenyewe pabaya zaidi. Tume hiyo pia ingeufanya utawala wa Rais Sidi kituko kutokana na matumizi mabaya ya fedha za umma. Kwa mfano, nimeambiwa kuwa, safari zake za ndege za nje ziliigharimu serikali zaidi ya dola za Marekani mbili bilioni, kwa kukodisha ndege za kifahari yeye na familia yake na ujumbe wake pamoja na anasa zingine zisizokuwa za lazima. Kwa hakika alikuwa katika wakati mgumu: Ama angelazimika kujiuzulu (kwa mujibu wa Olmert) katika aibu kubwa au angelazimika kuvunja bunge na hivyo kuunda serikali yake upya, hali ambayo ingempeleka katika mapinduzi kama haya tuliyoyoyashuhudia, ambayo angalau imeficha aibu yake kisiasa. Alibanwa pande zote na alikuwa hana pa kutokea zaidi ya kukumbana na hatima yake.</p></blockquote>
<p><em>Western Sahara Info</em> amekuwa akiblogu mgogoro huu tokea ulipoanza, na leo <a href="http://w-sahara.blogspot.com/2008/08/military-coup-in-mauritania.html">ametuletea</a> habari za mapinduzi hayo ya kijeshi kama zinavyotokea dakika kwa dakika, pamoja na muhtasari wa unyambuzi: </p>
<blockquote><p>Uchambuzi wa harakaharaka, ambao naweza kuujutia: balaa kwa demokrasia ya Mauritania, kwa upande mmoja, (demokrasia) ambayo haikuwa na nafasi, lakini muhimu zaidi ni kuwa (mapinduzi haya) yamerudisha nyuma nafasi iliyokuwepo kwa maendeleo ya kisiasa. Ingawa, Rais Abdellahi na washirika wake si malaika, lakini Majenerali Ghazouani na Abdelaziz wanawakilisha kundi baya la kinyonyaji katika utawala wa Mauritania, kwa kukataa kuruhusu utawala wa kiraia kutulia madarakani kwa kuwatishia kung&#39;oa kabisa utawala wa kiraia hatimaye. Kama mapinduzi ya mwisho ya kijeshi yaliyotokea Agosti 2005, yangalieleweka na Jumuiya ya Kimataifa baada ya kung&#39;olewa kwa Rais Ould Tayaa, na hatimaye kupelekea mabadiliko makubwa, mapinduzi haya ya juzi yalikuwa tofauti saana. Kilichotokea mwaka 2005 ilikuwa kwamba madikteta wa kijeshi walioegemea katika ukabila waling&#39;atuliwa na nafasi ilijitokeza ikasimika badala yake utawala wa kiraia uliokuwa na muundo wa nusu-mabavu ambao uliruhusu desturi nyingi za kidemokrasia kwa muda mwingi zaidi, (utawala huo) ulishughulikia zaidi muwafaka wa kitaifa, urejeshwaji wa wakimbizi na maendeleo ya kiuchumi; ingawa siyo hema, lakini ilikuwa bora. Mabadiliko haya hivi sasa yanageuzwa. Wapinduaji - japokuwa wengine ni miongoni mwa wale waliofanya mwaka 2005 - - ni lazima walaumiwe na matokeo ya mapinduzi yabatilishwe kama inawezekana; Mauritania ilikuwa na fursa ya pekee kuweza kuvunja mzunguko huu usiokwisha, na sasa (fursa hiyo ya pekee) inaponyoka.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <em>Roads To Iraq</em>, katikaujumbe wenye kichwa cha habari &#8220;Wamarekani walipanga mapinduzi nchini Mauritania,&#8221; <a href="http://www.roadstoiraq.com/2008/08/06/american-orchestrated-coup-in-mauritania/">inaripoti</a> habari hiyo vile vile: </p>
<blockquote><p>Mambo yanabadilika kwa kasi sana nchini Mauritania, imeanza na mapinduzi asubuhi hii, kwa kutoa &#8220;taarifa nambari moja&#8221; katika kituo cha televisheni cha Mauritania, Mkuu wa kituo hicho cha televisheni<br />
alibadilishwa sababu alikataa kushirikiana na mkuu wa jeshi aliyeandaa mapinduzi na kumtangaza mtawala mpya wa kijeshi.</p></blockquote>
<p>Huko Misri, <em>Bella</em> [Ar]<a href="http://afkaar-bella.blogspot.com/2008/08/blog-post.html">anasema</a> kilichotokea Mauritania kimedhihirisha kuwa Waarabu hawakupangwa kwa demokrasia.</p>
<blockquote><p>Inaonekana demokrasia haikuumbwa kwa watu kama sisi - ambao hatuwezi kupumua nje ya tawala za kijeshi.</p></blockquote>
<p>Baada ya kutupa historia fupi ya demokrasia changa ya Mauritania <em>Bella</em> anaandika: </p>
<blockquote><p>Kwa njia hii, Mauritania, ambayo ilikuwa ianze kuvuna matunda ya demokrasia katika msukumo wa kiasisi ambao eneo lote la mataifa ya jirani yalikuwa yanaungalia kwa shauku, mambo yamerejea kule yalikotoka kiasili, na wanajeshi wakaingilia kati na mapinduzi kutokea.</p></blockquote>
<p>Bloga wa Kuwaiti <em>Wild Il Deera</em> <a href="http://wildildeera.blogspot.com/2008/08/blog-post_06.html">anahoji maswali machache </a>kuhusiana na mapinduzi haya. Anauliza:</p>
<blockquote><p>Jumuiya ya Kiarabu ina msimamo gani kuhusu viongozi wa mapinduzi haya?<br />
Hivi huyu kiongozi wa Mauritania hakuchaguliwa na watu wake?<br />
Hivi inawezekanaje kundi la kisiasa, kama Jumuiya ya Kiarabu, ambayo inataka kuheshimiwa katika jamii ya Kiarabu na katika ulingo wa kimataifa ikaruhusu mapinduzi kama haya kufanyika katika moja ya mataifa wanachama wake?</p></blockquote>
<p>Bloga maarufu nchini Morocco Larbi [Fr] alipachika kiungo cha makala ya ya habari, <a href="http://www.larbi.org/post/2008/08/Mauritanie%3A-Coup-d-Etat-en-cours">kisemacho</a>: </p>
<blockquote><p>Unaweza kusema: Afrika ni bara lililolaaniwa!</p></blockquote>
<p>Habari yake hiyo imepata maoni mengi. <em>Citoyen</em> anatoa maoni kwamba:</p>
<blockquote><p>Ni kweli mapinduzi hayatabiriki Afrika… Nashangaa, ingawa, kama kwa mara nyingine tena, Mashirika ya Moroko yamekatizwa kama yalivyokuwa mwezi Ogasti 2005? </p></blockquote>
<p>Mwishoni KABOBfest, ambaye huwa anaingiza vichekesho katika kila hali, <a href="http://www.kabobfest.com/2008/08/kickin-it-old-skool.html">anatoa maoni</a> yenye mzaha: </p>
<blockquote><p>Wakati utamaduni wa mapinduzi katika mataifa mengi ni utamaduni uliopitwa na wakati (kama vile Syria hakujapata kutokea mapinduzi kwa miongo kadhaa sasa) Baadhi ya mataifa yanapendelea mitindo ya kizamani,  rejea pale ambapo ianonekana palikuwa na mapinduzi kama juma moja lililopita sehemu fulani hapa duniani. Wakati Mauritania siyo Fiji, wanadumisha utamaduni usio na maana wa mapinduzi katika dunia ya Waarabu.</p></blockquote>
<p>Blogu ya Arabdemocracy pia anayo <a href="http://www.arabdemocracy.com/2008/08/mauritaniaobituary-for-young-democracy.html">taarifa ya maombolezo</a> ya iliyokuwa demokrasia changa.</p>
<p><em>Picha ya hapo juu ni ya Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallahi iliyopigwa na <a href="http://www.agenciabrasil.gov.br/media/imagens/2007/09/27/1254MCMauritania1.jpg/view">Marcello Casal Jr./Abr</a> (Septemba 2007)</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/arabeyes-rais-wa-mauritania-aliyepinduliwa-katika-mapinduzi-ya-kijeshi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Msumbiji: 2038?</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/msumbiji-2038/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/msumbiji-2038/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 08 Aug 2008 16:51:00 +0000</pubDate>
		<dc:creator>charahani</dc:creator>
				<category><![CDATA[Agriculture]]></category>
		<category><![CDATA[Business]]></category>
		<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[Economics]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Language]]></category>
		<category><![CDATA[Mozambique]]></category>
		<category><![CDATA[Portuguese]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=7</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naPaula Góes  &#183; Imetafsiriwa na charahani &#183;  Angalia ujumbe mama 
Msumbiji itakuwaje katika miaka 30 ijayo? Mwana sosiolojia Carlos Serra [pt] anatoa mitizamamo tisa ya falme zilizokufa za Kirumi  yaani (Byzantine) na anawakaribisha wasomaji wake kurekebisha mitizamo hivyo kwa kadri ya wanavyoona ni sawa: 
1. Lugha ya kireno itakuwa ni [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/paulagoes/">Paula Góes</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/charahani/'>charahani</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/02/mozambique-2018/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Msumbiji itakuwaje katika miaka 30 ijayo? Mwana sosiolojia <a href="http://">Carlos Serra </a>[pt] anatoa mitizamamo tisa ya falme zilizokufa za Kirumi  yaani (Byzantine) na anawakaribisha wasomaji wake kurekebisha mitizamo hivyo kwa kadri ya wanavyoona ni sawa: </p>
<blockquote><p>1. Lugha ya kireno itakuwa ni mabaki, itazidiwa na lugha ya kiingereza, itakayokuwa ikitumika kiufasaha katika maeneo ya mijini. Kireno kitakuwa lugha ya kisomi, itakayozungumzwa katika makundi mahususi, huku ikiungwa mkono na mchanganyiko mtamu wa lugha za kiholela katika sehemu za nyika.<br />
2. Madini ya chuma yataendeshwa na Wachina, Warusi, Brazil, na hatimaye Wahindi. Bonde la Mto Zambezi litakuwa na migodi ya Wachina na Wa-Brazil.<br />
3. Kama tukibahatika, patakuwa na mafuta, ambayo Wamarekani na Wakanada watakuwa wakiyavuna.<br />
4. Misitu, kama itabaki, itamilikiwa na Wachina.<br />
5. Itakuwa ni nchi ya nishati-mimea, itakayoendeshwa kwa biashara ya ubia wa namna mbalimbali, ikikumbatiwa na kilimo kidogo cha kuhamahama, kinachosaidiwa na maghala maalum ya nafaka yanayolindwa kwa ajili ya  kusafirishwa nje (kwenda Uchina na India).<br />
6. Biashara, ya jumla na ya rejareja,  itatawaliwa na Wachina na Wahindi, kama-katika-urembo na mapambo.<br />
7. Ulaya itamiliki fukwe za bahari za kitalii, zilizo na Wazungu-wa-Kimarekani watakaokuwa wanalilia na kukumbatia kumbukumbu za Ulaya inayokaribia kukata roho na Marekani isiyo-ubeberu.<br />
8. Simu za mikononi zitakuwa zikitengenezwa ndani (Msumbiji), zikiwa na makasha ya Nokia na roho za Kichina, magari yatakuwa ya Kichina na Kikorea, yenye maumbo ya Kimarekani.<br />
9. Wizara yetu itakayovutia zaidi, wizara-kabambe, itakuwa ni ile ya Biashara na Mambo ya Nje (Hebu angalia ukubwa wao wa sasa hapahapa jijini Maputo uweze kupata taswira ya itakavyokuwa huko mbeleni).</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/msumbiji-2038/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
