<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Christian Bwaya</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Video: Vijana duniani kote wajieleza kwa sekunde 60</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/video-vijana-duniani-kote-wajieleza-kwa-sekunde-60/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/video-vijana-duniani-kote-wajieleza-kwa-sekunde-60/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Antigua and Barbuda]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Bangla]]></category>
		<category><![CDATA[Bangladesh]]></category>
		<category><![CDATA[Central Asia & Caucasus]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Film]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Mongolia]]></category>
		<category><![CDATA[Niger]]></category>
		<category><![CDATA[Poland]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=743</guid>
		<description><![CDATA[mradi wa OneMinuteJr unawapa vijana......]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/30/video-worldwide-youth-express-themselves-in-60-seconds/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption alignleft" style="width: 85px"><img alt="Nembo ya OneMinutesJr" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/minutesjrth-75x75.jpg" title="minutesjrth" width="75" height="75" /><p class="wp-caption-text">Nembo ya OneMinutesJr</p></div><br />
Mradi wa <a href="http://www.theoneminutesjr.org/">OneMinutesJr </a>unawapa vijana wa umri wa kati ya miaka 12 na 20 kutoka kona mbalimbali za dunia fursa ya kujieleza, kusema na kujifunza ujuzi wa kutengeneza kazi za sauti-na-kuoangalia ili kuwasiliana zaidi ya mipaka yao, lugha zao na umbali zaidi kwa kutumia video ya sekunde 60.</p>
<p>Mradi wa OneMinuteJr umetokana na jitihada za pamoja za <a href="http://www.eurocult.org/">Mfuko wa Utamaduni wa Ulaya</a>, <a href="http://www.theoneminutes.org/">Mfuko wa One Minutes Jr</a> na <a href="http://www.unicef.org/">Unicef</a>, vile vile na mashirika mwenza mengineyo. Katika wavuti yao, unaweza kuperuzi video za dakika moja moja zenye thamani ya mwaka mmoja  kutoka katika nchi mbalimbali, nyingine zikiwa zimetumwa na watu binafsi, na nyingine zimetokana na <a href="http://www.theoneminutesjr.org/?thisarticle=174">warsha</a> ambapo vijana wanafundishwa mbinu za kuandika, kupiga picha za video na kuhariri mawazo yao.</p>
<p>Video hizi fupi fupi zinaonyesha masuala, mawazo na ndoto za vijana wanaotokea asili tofauti tofauti, na kutupa kidirisha cha kuyachungulia maisha yao ya kila siku. Kwa mfano, kutoka <a href="http://www.theoneminutesjr.org/?thissection_id=10&#038;movie_id=200900283&#038;series_id=30">Poland, Ludmila Kierczak</a> anatengeneza video na kueleza yeye ni nani. Ili kuiangalia video, tafadhali bofya kwenye picha hapa chini <a href="http://www.theoneminutesjr.org/?thissection_id=10&#038;movie_id=200900283&#038;series_id=30">ili kwenda kwenye tovuti ya OneMinuteJr</a>.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/whoami.JPG" title="whoami" class="alignnone" width="239" height="209" /><br />
Huko Bangaladesh, Mobasshera Tarannum Adiba anaonyesha vifungu kadhaa kutoka <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Convention_on_the_Rights_of_the_Child">Makubaliano ya Haki za Mtoto</a>. Katika video yake, iitwayo <a href="http://www.youtube.com/watch?v=xyC8avD4Xlg">Nataka Uhuru</a>, anagusia Kifungu cha 12: Watoto wana haki ya kusikilizwa maoni yao na sauti zao ziheshimiwe na Kifungu cha 16 ambacho kinasema kwamba kila mtoto ana haki ya faragha.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/xyC8avD4Xlg&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/xyC8avD4Xlg&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kutoka Mongolia, <a href="http://www.youtube.com/watch?v=cZM87XL71jk">Tuvdenjamts (Tuvden) Altankhyag anaonyesha </a>haki ambayo kila mtoto anayo kwa utamaduni wake mwenyewe:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/cZM87XL71jk&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/cZM87XL71jk&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Na katika video hii inayofuata, Simon Tonge kutoka Antigua na Barbuda, anatumia haki yake ya uhuru wa kujieleza katika video iitwayo <a href="http://www.youtube.com/watch?v=QnBwfX9EtA0">Maungamo ya msichana aliyebalehe</a>:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/QnBwfX9EtA0&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/QnBwfX9EtA0&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Ibrahim Ide kutoka Niger anaonyesha haki ambayo watoto wanayo kwa familia inayowapenda na kuwalindia haki zao katika video ya <a href="http://www.youtube.com/watch?v=8QiDCP5l2x8">Pamoja au Pasipo</a>: </p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/8QiDCP5l2x8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/8QiDCP5l2x8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es_ES&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kwa video zaidi za dakika moja, unaweza kuangalia kwenye tovuti kuu kwa ajili ya mradi huo kwenye <a href="http://www.theoneminutesjr.org/">TheOneMinutesJr.org</a> au unaweza kutembelea <a href="http://www.youtube.com/user/UNICEFoneminutesjr">Idhaa ya UNICEF One minutes Jr kwenye Youtube</a> ili kuona video nyingi zaidi zenye sekunde 60 zilizotengenezwa na vijana kwenye mada ya Haki za Watoto.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/12/video-vijana-duniani-kote-wajieleza-kwa-sekunde-60/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Somalia: Kuufahamisha mtandao wa waandishi na wanablogu wa Kisomali</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 24 Nov 2009 12:45:45 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Somalia]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=705</guid>
		<description><![CDATA[Kituo cha habari cha Somalia ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/somalia-introducing-a-network-of-somali-journalists-and-bloggers/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://somalimedia.ning.com/">Kituo cha habari cha Somalia</a> ni jukwaa la waandishi na wanablogu wa Kisomali wanaoishi ndani na nje ya Somalia. Kituo kinasambaza machapicho ya habari na kuchapisha blogu zilizoandikwa na waandishi wa habari. </p>
<blockquote><p>Kituo cha Habari cha Somalia ni jukwaa linalojitegemea kwa ajili ya waandishi wa Kisomali ndani na nje ya nchi hiyo. (Kituo hicho) kimeanzishwa kukuza wasifu wa waandishi werevu, na wachapa kazi waliyoyatoa maisha yao kuwatumiakia watu dunia nzima.<br />
Somalia imekuwa ikichukuliwa kama nchi iliyoshindwa, nchi inayohusishwa na vifo, mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yasiyoisha, vita, ugaidi na uharamia wa kisasa. Lakini moja wapo ya habari za mafanikio kwa miaka mingi imekuwa ni kukua kwa uhuru wa habari na maoni. Hata hivyo, kuupa kipaumbele na kuutangaza ukweli huja kwa gharama kubwa.</p>
<p>Kituo hicho huchapisha blogu za waandishi hawa. Pia, kituo kinatawanya habari na taarifa za waandishi wa habari. Kituo pia kinaratibu waandishi wa Kisomali na wale wasio Wasomali. Kinawapa waandishi wasio Wasomali wanaoweza kuwa wanasafiri kwenda Somalia ushauri na mawasiliano ya awali. Kituo pia kinafanya kazi na mashirika makubwa ya kimataifa ya habari kwa ushirikiano, kuzalisha na kujazia habari na taarifa kuhusu Somalia na eneo lote la Pembe ya Afrika. </p></blockquote>
<p>Solana Larsen anaandika kuhusu <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/the-new-somali-media-centre">asili ya Mradi wa Kituo cha Habari cha Somalia</a>:</p>
<blockquote><p>Kama haujahisi bado, mimi si Msomali. </p>
<p>Katika shule ya Uandishi wa Habari jijini London mwaka 2002 nilikuwa na mwanafunzi mwenzangu aitwaye Harun Hassan ambaye nilizoea kumuuliza maswali mengi kuhusu maisha yake  ya Mogadishu na Siasa za Somalia. Baada ya kuhitimu, tulibaki kuwa marafiki na nilimfahamisha kuhusu uwezekano wa yeye kuandikia mtandao wa openDemocracy.net ambapo nilikuwa mhariri kwa miaka michache. Baadaye, nikawa mhariri mtendaji wa Global Voices Online, ambapo mara chache tulikuwa na habari kuhusiana na wanablogu wa kiSomali. </p>
<p>Harun alizoea kuniambia kuhusu mawazo aliyokuwanayo kwa ajili ya Mradi wa Habari uliojumuisha jamii ya Kisomali mjini London. Alianzisha gazeti la Kisomali, na wakati fulani alinifuata nimsaidie kutengeneza tovuti kwa ajili ya kitu alichokiita Kituo cha Habari cha Somalia.</p>
<p>Habari za jamii ya KiSomali kwenye vyombo vya habari nchini Uingereza zilikuwa hasi na zisizo sahihi, Harun alifikiria kuwa namna pekee ya kusahihisha hilo,ilikuwa ni kuwarahisishia waandishi wa Uingereza kuwapata waandishi wa Kisomali na watafiti wa kuongea nao.</p>
<p>Tulitengeneza tovuti na blogu, lakini baadae kidogo tukakabiliwa na kazi nyingine na mradi ukadumaa.</p>
<p>Wavuti unayoipitia sasa, ni jaribio letu  lapili la kutengeneza nyenzo ya mtandao kwa ajili ya waandishi wa Kisomali na wengine kuitumia ili kusaidia kuboresha uwelewa wa kidunia wa Wasomali na Somalia yenyewe.</p></blockquote>
<p>Hapa chini ni baadhi ya makala za blogu za hivi karibuni kabisa kutoka kwenye Kituo cha Habari cha Somalia: </p>
<p>Katika makala yenye kichwa cha habari, <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/affair-to-remember">Uzinifu wa Kukumbuka</a>, Fathia Absie anaandika kuhusu kushitakiwa kwa Joshua Asisam mlinzi wa amani katika Somalia, kwa kujihusisha na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa Kisomali:</p>
<blockquote><p>Mahakama ya Kijeshi ya Kampala ilimhukumu Joshua Asisa kifungo cha mwaka mmoja na nusu jela. Bw. Asisa ambaye ni mwanachama wa walinzi wa amani wa AMASOM nchini Somalia alipatiaka na hatia ya kujuhusisha na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke wa Kisomali aitwaye Nimco Omar na kumpa ujauzito baada ya kumuoa kwa kumdanganya kuwa alikuwa Mwislamu.<br />
Habari hii ilitokea mwaka uliopita huko Mogadisho lakini hakuna aliyesikia mpaka mwanamke huyu mdogo alipokwenda Kampala na kumshitaki Bw. Asisa mahakamani kwa kumdanganya. Mohamed Abubakar Ahmed ambaye ni mwandishi aliyeiibua habari hiyo aliniambia kuwa aliipata habari hiyo baada ya kuwa imeripotiwa na magazeti ya Uganda. Baada ya hapo, Bw. Ahmed alijaribu kuonana na viongozi wa jamii ya Kisomali waishio Kampala na akaweza kukutana na msichana huyo. Aliniambia kuwa Bi. Omar alimwambia kuhusu habari hiyo na jinsi alivyokutana na Bw. Asisa ambaye ni daktari. Alikuwa akifanya kazi kwenye hospitali binafsi kwa ajili ya jeshi la Uganda mjini Mogadisho.</p></blockquote>
<p>“<a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/in-the-spirit-of-spreading-the">kwa nia ya kutawanya neno..</a>,” anaandika Idil Osman: </p>
<blockquote><p>Mafunzo ya kijeshi yanayofanyika katika makambi ya wakimbizi wa Kisomali huko Dadaab, Kaskazini mashariki ya Kenya yamechochea kelele zinazochanganya wengi ndani na nje ya eneo. Hata hivyo ninashangazwa sana na msimamo wa serikali ya Kenya. Nilifanya ripoti ya uchunguzi katika suala hili mapema kazini ambapo waziri wa ulinzi wa Kenya alidai kwa msimamo kwamba Kenya haikutoa ruhusa kwa mafunzo haya kufanyika.<br />
Wakati huo huo mashahidi na wanaharakati wa haki za binadamu wanarekodi na kuweka kumbukumbu za ushahidi wa vijana hawa wanaowekwa  katika magari ya kijeshi ya Kenya na kusafirishwa kwa magari kwenda kwenye vyuo vya mafunzo ya Kijeshi vya Kenya.<br />
Wengi wa vijana hawa wanachukuliwa kwa kudanganywa na kuahidiwa mshahara mzuri pamoja na kazi inayoaminika kwenye miradi ya kijeshi ya Umoja wa Mataifa/Umoja wa Ulaya/Umoja wa Afrika..<br />
Kiukweli wanafunzwa kwenda na kupigana kwenye vita ile ile waliyoikimbia na kuwafanya wawe wakimbizi. Wengi wa wakimbizi hawa vijana wanaarifiwa kuwa chini ya umri unaotakikana na wamechukuliwa bila ridhaa ya wazazi wao.<br />
Imevunja haki zao za kimataifa za binadamu kama wakimbizi kwa mujibu wa tangazo la kwenye vyombo vya habari lilitolewa hivi karibuni na Shirika la Human Rights Watch, kwa sababu wakimbizi wanatakiwa kuwekwa kwenye mazingira ya kiraia. </p></blockquote>
<p>Solana anajadili suala la ‘chanzo kisichotaka kufahamika’ katika taarifa za vyombo vya habari vya Kimagharibi kwenye makala yake aliyoipa jina la “<a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/blogs/when-local-sources-go-unnamed">Wakati vyanzo vya mahali vinapochagua kutokuwa na jina</a>”</p>
<blockquote><p>nimechukua toleo la hivi karibuni la jarida la National Geographic Magazine kwa habari yao inayohusu ‘Somalia iliyovunjika’. Picha za Mogadishu zilizopigw ana Pascal Maitre ni nzuri, ingawa zinaonyesha uharibifu mkubwa. Na mwandishi, Robert Draper anatoa muhtasari wa haki na wenye mguso kuhusu historia tata. Pia anaziweka wazi changamoto za upashaji habari wa kigeni.  </p>
<p>Katika hali inayoacha maswali, mwandishi wa Kisomali Harun Hassan anatajwa kwa jina kwenye maelezo ya picha inayomwonyesha mlinzi wa barabarani mjini Mogadishu, lakini kwa kiwango ninachoona haionekani kwenye habari yenyewe. Kwa nini kuna ugumu wa kuweka wazi chanzo?  Kama Draper alihangaika kuwasiliana na kuvihoji vyanzo vya Habari vya Somalia, kwa nini asiwaeleze wasomaji wake habari hiyo?</p>
<p>Je, huu ndio uzoefu wa wandishi wa Kisomali wanaowasaidia waandishi wa Kimagharibi kuhabarisha? Ninatumainii wanachama wa Kituo cha Habri cha Somalia watasaida kutupa mwanga wa jinsi inavyokuwa kwenye sehemu hiyo ya timu inayotengeneza ripoti.  </p></blockquote>
<p>Unaweza kuona orodha ya wanachama waliopo wa Kituo hicho <a href="http://somalimedia.ning.com/profiles/members/">hapa</a>.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/somalia-kuufahamisha-mtandao-wa-waandishi-na-wanablogu-wa-kisomali/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika Kusini: Kikaragosi Kiliochoathirika na VVU Kwenye Kipindi cha Sesame Chaelimisha Kuhusu Ukimwi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 10:38:13 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=696</guid>
		<description><![CDATA[Wakati kipindi cha watoto cha Mtaa wa Sesame (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/11/south-africa-sesame-streets-hiv-positive-muppet-raises-awareness/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Kami22.jpg" title="Kami" class="alignright" width="200" height="260" /><br />
Wakati kipindi cha watoto cha <a href="http://www.sesamestreet.org/home/">Mtaa wa Sesame</a> (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. </p>
<p>Wakati kipindi cha Sesame Street kinatazamwa katika zaidi ya <a href="http://www.sesameworkshop.org/newsandevents/sesameupdates/sesame_40thbirthday">nchi 140</a>, kila toleo huzungumzia masuala yanayotokea kwenye jamii husika na kwa kumtumia vikaragosi tofauti. <a href="http://muppet.wikia.com/wiki/Kami">Kami</a> mwenye rangi ya Njano-dhahabu alionekana kwa mara ya kwanza kwenye kipindi mwenza cha Sisame Street cha Afrika Kusini kinachoitwa <a href="http://www.schooltv.co.za/TakHome.htm">Takalani Sesame</a>, mwaka 2002 kujibu matatizo ya nchi yanayohusiana na UKIMWI. Kama kikaragosi cha kwanza duniani chenye VVU, kinasaidia kuwaelimisha watoto kuhusu ugonjwa na kushughulikia masuala yanayohusiana na kuwa mwathirika wa UKIMWI. Jina la Kami <a href="http://www.sesameworkshop.org/aroundtheworld/southafrica">linatoka</a> kwenye neno la kiSetswana “Kamogelo”, lenye maana ya “kukubalika.” Sunshinestar110, anayeblogu kwenye <em>U dont Like My Opinion&#8230;That’s Fine!</em> <a href="http://thatsfine2009.blogspot.com/2009/11/happy-birthday-to-you.html">anazungumzia zaidi</a> kuhusu Kami:</p>
<blockquote><p>“Kami ni mwathirika wa VVU mwenye afya, yatima wa miaka mitano mwenye bashasha ambaye ana aibu kidogo lakini huchangamka akijongelewa kwa njia ya kirafiki, pia anajua mengi kuhusu Virusi vya UKIMWI, alimpoteza mama yake kwa ugonjwa huo. Kami alipozinduliwa, akiwa na nywele zake za kahawia na pia alivaa fulana, na kutembea kwenye mtaa wa Susame na kujiuliza huku akihofu kama wenyeji watataka kucheza nae. Hakuwa na haja ya kuogopa kwa sababu vikaragosi vingine vilimpokea kwa bashasha”</p></blockquote>
<p>Kami aliletwa kuwasaidia watoto wengi wa Afrika Kusini wanaotaabika na janga la VVU/UKIMWI. Inaaminika kuwa Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya watu walio na VVU duniani – inakadiriwa kuwa watu <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">milioni 5.7</a> Kwa makadirio, kati ya walioathirikia, 280,000 ni watoto wa umri wa miaka chini ya 14 na kuna yatima milioni 1.4 nchini kutokana na UKIMWI. Zaidi ya madhara ya kimwili ya kuwa na VVU, vilevile kuna unyanyapaa na miiko inayotokana na kuwa na ugonjwa, ambayo husababisha ugumu kwa watu kupata matibabu stahiki na msaada. Takalani Sesame, ambayo inajumuisha lugha zote rasmi 11 za Afrika Kusini, inajaribu kuwasaidia watoto kuyatazama masuala haya kwa ujasiri kupitia Kami.</p>
<p>Hata hivyo, kulikuwa na mkanganyiko wakati Kami alipoanza kuonyeshwa, hasa hasa nchini Marekani, ambapo wengi walikasirishwa na kuwa kipindi cha watoto kinanamchezesha mhusika mwenye VVU. <em>Haven on Earth</em> <a href="http://haven-on-earth.spaces.live.com/blog/cns!C13DE188EF218F14!382.entry?sa=500695506">anafafanua</a> mjadala huo:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ilitaarifiwa kuwa ujio wa Kami kwenye kipindi cha Sesame Street nchini Afrika Kusini ulikuwa unakaribishwa.(Nina wakati mgumu kukubaliana na ukweli huu kwa sababu kiwango kikubwa cha kukataa bado kipo), kulikuwa na mkanganyiko ulio wazi hapa Marekani. Ninakumbuka kusoma kuhusu suala hili (hii ni sababu ya mimi kufurahia kukutana na kipindi kikirushwa kutokea Afrika Kusini – nisingelifikiria kukitafuta). Iliondokea kuwa kundi la wabunge wa Congress wa chama cha Republican walituma barua kwa Rais wa Shirika la Utangazaji la Umma (PBS) linalorusha kipindi cha Sesame Street. Barua ilidai kwamba mipango ya kuleta mhusika kama huyo ambaye ni mwathirika wa UKIMWI nchini Marekani haikuwa sahihi, kwa kuzingatia umri wa watazamaji. Walipendekeza kwamba hatua hiyo ingeathiri ufadhili wa umma kwa Shirika hilo (PBS).”</p></blockquote>
<p>Kami hajawahi kuonekana kwenye kipindi cha Sesame Stree cha Marekani, ingawa amedhihirisha kuwa mhusika aliyefanikiwa sana kwenye kipindi cha Takalani Sesame na zaidi. Mwaka 2003, UNICEF <a href="http://www.unicef.org/media/media_16631.html">ilimteua</a> kuwa “Shujaa wa Watoto” duniani. Katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=9eXlNn-C8BY">video</a> hii, anaungana na Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton kutoa ujumbe kuhusu VVU/UKIMWI. Jamie, anayeblogu kwenye <em>No day but Today</em>&#8230;, <a href="http://phaino.blogspot.com/2006/12/world-according-to-sesame-street.html">anajadili</a> mafanikio mengine ya Kami:</p>
<blockquote><p> “Kwa sababu watoto wengi wa Afrika Kusini wanamfahamu mtu fulani mwenye UKIMWI, mhusika huyo amekuwa shujaa wa taifa, anayependwa na watu wa nchi hiyo. Kami ameonekana kwenye Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia na alihojiwa na Katie Couric. Ameteuliwa kuwa balozi wa UNICEF wa watoto na ameonekana kwenye vipande vya onyesho la Takalami pembeni mwa Desmond Tutu na Nelson Mandela.”</p></blockquote>
<p>Pamoja na mafanikio ya Kami, wanablogu wengine bado wanaamini kuwa si mhusika sahihi kwa toleo la Kimarekani la Sesame Street. Emily Meyer, anayeblogu kwa ajili ya darasa lake la heshima, <a href="http://hons101fall09eem.blogspot.com/2009/10/kami-hiv-muppet.html">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ni muhimu kwa Wamerekani kufahamu kuhusu VVU/UKIMWI na hatari ya ugonjwa wenyewe, nadhani kuwafundisha watoto katika umri wa miaka miwili na mitatu ni kwenda mbali sana. Watoto wadogo kiasi hiki hawataweza kuelewa kuhusu VVU na hawataelewa madhara yake. Kama Kami alitakiwa aletwe Marekani kama njia kueneza elimu na kudhibiti UKIMWI, sidhani kama matokeo yaliyokusudiwa yangetokea&#8230;Watoto nchini Marekani hawalazimishwi kuhusika na masuala ya UKIMWI katika umri huo mdogo. Nadhani wakati sahihi kwa watoto nchini Marekani kujifunza kuhusu hatari ya virusi vya UKIMWI ni wanapokuwa wakubwa, kadri ya miaka kumi ama kumi na moja au wakati mwanafunzi anapoanza kujihusisha na vitendo vya mapenzi kimwili”</p></blockquote>
<p>Bado, wanablogu wengi, kama huyu hapa <a href="http://beckyluz.wordpress.com/2008/12/16/kami-the-hiv-positive-muppet/">anayeandika kwenye</a> <em>Muppets and History</em>, anamwona Kami kama mfano mwingine wa namna Sesame Street inavyosukuma mipaka. Wengine <a href="http://joburgjoblog.blogspot.com/2006/03/celebrating-aids-research.html">wanaonyesha upendo</a> wao kwa kikaragosi huyo na ujumbe anaowaletea watoto. Na wengine wanadhani anatakiwa atumike kwenye matoleo mengine ya Sesame Street. Katika blogu yake binafsi, Steisha Pintado <a href="http://steishapintado.wordpress.com/2008/12/18/final-grades-kami/">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Anawaonyesha watoto kwamba ni sawa kumkumbatia mtu mwenye virusi vya UKIMWI, na anaeleza nini cha kufanya anapokuwa na kidonda kwenye kidole chake au kama umejikata mwenyewe. Anaifundisha hadhira ya watoto wadogo kuhusu kukabiliana na kuumwa na kupotelewa&#8230;.Ingawa ngono huwa haitajwi kamwe katika kuzungumzia hali ya Kami, watu wengine wamesema kuwa kuwepo kwa mhusika mwenye virusi vya UKIMWI lisingekuwa jambo sahihi kwa hadhira ya watazamaji wadogo. Mbunge mmoja hata alidai kuwa Warsha ya Sesame ingepoteza msaada wa kifedha kutoka serikalini kama ingerusha kipindi chenye mhusika huyo kwenye nchi yetu. Inashangaza kusikia maneno haya. Wazazi wanatumia muda mfupi (na unaopungua kila siku) na watoto wao, na wanaruhusu runinga kuwaelimisha zaidi na zaidi. Ni wazi wazazi wengi hawawafundishi watoto wao namna ya kuyakabili masuala nyeti  ya uelewa na kukubalika. Wazazi tayari wamewaruhusu Warsha ya Sesame kuingiza suala la kukubalika kwa wale wenye ulemavu na kuugua, na pia kwa wale wenye rangi na dini tofauti. Je, hii ina tofauti gani? </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Azerbaijan: Baada ya Hukumu ya Wanablogu wa Video</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/azerbaijan-baada-ya-hukumu-ya-wanablogu-wa-video/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/azerbaijan-baada-ya-hukumu-ya-wanablogu-wa-video/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 10:21:01 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Azerbaijan]]></category>
		<category><![CDATA[Blogger News]]></category>
		<category><![CDATA[Central Asia & Caucasus]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=694</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naOnnik Krikorian  &#183; Imetafsiriwa na Christian Bwaya &#183;  Angalia ujumbe mama 

Siku chache baada ya hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa  sauti juu ya kifungo cha Adnan Hajizade na Emin Milli. Wanaharakati hawa wa mtandaoni watatumikia vifungo vya miaka miwili [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/onnik-krikorian/">Onnik Krikorian</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/15/more-reaction-to-blogger-trial-verdict/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/hands_off12.jpg" class="alignleft" width="177" height="187" /><br />
Siku chache baada ya <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/11/azerbaijan-bloggers-sentenced/">hukumu ya vijana wanaharakati wawili wa blogu za video</a> huko Azerbaijan, wanablogu wengine wanaanza kuongea kwa  sauti juu ya kifungo cha <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/blogger/adnan-hajizada">Adnan Hajizade </a>na <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/blogger/emin-milli">Emin Milli</a>. Wanaharakati hawa wa mtandaoni watatumikia vifungo vya miaka miwili na mwingine miaka miwili na nusu gerezani baada ya mashitaka ambayo wengi wanayaona kama yenye nguvu za kisiasa na ni katika kujaribu kuwanyamazisha wasemaji kwenye nchi hiyo.</p>
<p>Wanaungana na wengine kama <a href="http://www.se2009.eu/en/meetings_news/2009/11/12/presidency_statement_on_azerbaijan">Urais wa Jumuiya ya Ulaya</a>, <a href="https://wcd.coe.int//ViewDoc.jsp?Ref=PR839%282009%29&#038;Language=lanEnglish&#038;Ver=original&#038;BackColorInternet=F5CA75&#038;BackColorIntranet=F5CA75&#038;BackColorLogged=A9BACE">Baraza la Bunge la Ulaya</a>, <a href="http://www.osce.org/item/41288.html">Shirika la Usalama na Ushirika la Ulaya</a>, Shirika la kupingania Haki za Binadamu la <a href="http://www.hrw.org/en/news/2009/11/12/azerbaijan-young-bloggers-jailed">Human Rights Watch</a>, <a href="http://www.amnesty.org/en/library/asset/EUR55/009/2009/en/655ee814-8957-4c08-b4f3-16772a16d9c2/eur550092009en.html">Amnesty International </a>na <a href="http://www.rsf.org/spip.php?page=article&#038;id_article=34972">Waandishi wasio na mipaka </a>na wengine wengi wanaoishutumu hukumu hiyo.</p>
<p>Shirika la Amnesty International vilevile <a href="http://www.amnesty.org/en/library/asset/EUR55/009/2009/en/655ee814-8957-4c08-b4f3-16772a16d9c2/eur550092009en.html">limewatangaza vijana hao wawili kama wafungwa wa dhamira</a>. <em>Interesing times</em>, “mradi wa mtandaoni unaofuatilia jitihada  za kudhibiti na kuzuia upatikanaji huru wa mtandao duniani kote,” <a href="http://www.i-times.org/interesting_times/2009/11/azerbaijans-government-intensifies-its-war-on-free-expression.html">waliyaweka mashtaka katika muktadha</a>. </p>
<blockquote><p>matumizi ya mabavu ya hivi karibuni yaliyoonyeshwa na nguvu za dola nchini Azerbaijan hayaachi shaka yoyote kwamba wote, waandishi na wanablogu wanatumia haki yao ya kujieleza kwa uhuru ilhali wanajua hatari inayowakabili. </p>
<p> […]</p>
<p>Shukrani kwa shinikizo la kimataifa kama vile barua ya WPFC na nyingine nyingi,  serikali ya Azeri imelazimishwa kuwatoa waandishi hao gerezani.</p>
<p>Lakini kitendo hiki cha hivi karibuni cha uonevu dhidi ya wanablogu wawili hakiachi tena wasiwasi kwamba, kama wakiachwa wenyewe, maafisa wa serikali wa Azerbaijan wataendelea na njia zao za kinyanyasaji.</p></blockquote>
<p><em>Notes from Abroad</em> naye pia <a href="http://gedirem.blogspot.com/2009/11/long-prison-sentences-for-two-azeri.html">hashangazwi na hukumu  hiyo</a>:</p>
<blockquote><p>Jumanne, wanablogu wawili vijana walihukumiwa kifungo jela –mmoja kwa miaka miwili na nusu, na mwingine kwa maika miwili– kwa mashitaka ya kipuuzi ya uhuni. Suala zima ni aibu –likiendeshwa na malengo ya kisiasa, lakini haishangazi.</p>
<p>[…]</p>
<p>Kwa kuwa Azerbaijan ni utawala wenye utajiri mkubwa wa mafuta, nchi za Magharibi zimekuwa makini mno katika majibu yake kwa kitendo hiki kisichokuwa cha kidemokrasia kilichofanywa na serikali ya Azeri.</p>
<p>Serikali ya Azeri ni lazima ikemewe kwa nguvu zote na nchi zote za demokrasia duniani kwamba tabia ya aina hii hikubaliki.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu <em>The Blogar</em>, hata hivyo, <a href="http://theblogar.blogspot.com/2009/11/emin-and-adnan-in-prison.html">anakaribia kukosa maneno</a>:</p>
<blockquote><p>Kwa hiyo hukumu imetolewa.<br />
Emin na Adnan sasa ni rasmi kwamba ni ‘wahuni’.<br />
Ninakosa cha kusema hapa.<br />
Kama inavosemekana kuwa vyombo vya habari vya jamii vilihusika katika kuwatia ndani, vilihusika na kueneza habari mitaani kuhusu uvunjifu wa haki lakini havikuweza kubadili akili za mfumo wa sheria uliooza wa Azerbaijan.<br />
Usicheze na Ilham.</p>
<p> […] Mawazo yangu yako na fanilia zao pamoja na wao wenyewe.</p></blockquote>
<p>Hata hivyo, kukiwa na rufaa inayokaribia kukatwa na uwezekano wa hatua zitakazochukuliwa na Mahamakama ya Haki za Binadamu ya Ulaya, <em>L4L</em>, blogu mpya ya lugha ya Kiingereza ya Azeri, <a href="http://sympathy4thedevil.wordpress.com/2009/11/13/beginning/">inasema kwamba huu ni mwanzo tu</a>:</p>
<blockquote><p>Nini cha kufanya baada ya hapa? Awali ya yote tusikome. Tuendelee kufanya kazi kuelekea uhuru wa marafiki zetu na kuelekea kwenye uhuru wa raia wote wa Azerbaijan [&#8230;] Adnan na Emin hawakuonyesha woga na sisi hatupaswi kuwa chochote chini ya majasiri na wenye kutia moyo.</p>
<p>[…]</p>
<p>Huu hauwezi kuwa mwisho. Vyote vinaanza sasa.</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/parvana.jpg" class="aligncenter" width="440" height="294" /><br />
<em>Parvana Persiani na David Sasaki wa Jukwaa la Dunia la kublogu la Global Voices on lin, Bucharest, Romania © Onnik Krikorian / Oneworld Multimedia 2009</em></p>
<p>Wakati huo huo, kwenye pembe za Kongamano la Dunia la Kublogu mjini Bucharest, Romania, <em>Global Voices Online</em> ilifanya mahojiano yaliyoshindikana na Parvana Persiani, Mjumbe wa Heshima wa Bodi ya OL! Vuguvugu la vijana wa Azerbaijani ambalo rafiki yake wa kiume, Adnan Hajizade aliyefungwa sasa, ni mshiriki mwanzilishi.</p>
<p><object width="720" height="450"><param name="movie" value="http://dotsub.com/static/players/portalplayer.swf?plugins=dotsub&#038;uuid=4fe42f66-8f9b-42f3-85de-69e92c748374&#038;type=video&#038;lang=none"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowscriptaccess" value="always"></param><embed src="http://dotsub.com/static/players/portalplayer.swf?plugins=dotsub&#038;uuid=4fe42f66-8f9b-42f3-85de-69e92c748374&#038;type=video&#038;lang=none" type="application/x-shockwave-flash" allowscriptaccess="always" allowfullscreen="true" width="420" height="347"></embed></object></p>
<p>Habari mpya zitakuwa zilitundikwa kila zikipatikana. Wakati huo huo, habari kamili ya kukamatwa,  mashitaka na kufungwa kwa Adnan Hajizade na Emin Milli zinapatikana kwenye <a href="http://globalvoicesonline.org/-/world/central-asia-caucasus/azerbaijan/">sehemu ya Azerbaijan </a>ya <em>Global Voices Online </em>na kwenye blogu ya OL! (Kwa <a href="http://ol-en.blogspot.com/">Kiingereza</a> na <a href="http://ol-az.blogspot.com/">Kiazeri</a>). Alama ya <a href="http://twitter.com/#search?q=%23EminAdnan">#EminAdnan </a>pia inatumika kwenye Twitter.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/emin_adnan_poster.jpg" class="aligncenter" width="440" height="570" /><br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/poster.jpg" title="poster" class="aligncenter" width="440" height="525" /></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/azerbaijan-baada-ya-hukumu-ya-wanablogu-wa-video/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Philippines: Mti wa Dita Waokoa Maisha ya Watu 36 Wakati wa Mafuriko</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/philippines-mti-wa-dita-waokoa-maisha-ya-watu-36-wakati-wa-mafuriko/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/philippines-mti-wa-dita-waokoa-maisha-ya-watu-36-wakati-wa-mafuriko/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 14 Nov 2009 08:17:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Disaster]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Filipino]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Philippines]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=616</guid>
		<description><![CDATA[Mti wa aina ya Dita huko Manila mjini uligeuka kuwa "Mti wa Uzima" wakati ulipotumika kama kimbilio na wakazi ambao walitegwa kwenye nyumba zao wakati wa janga la kimbunga na mafuriko ya hivi karibuni. Somo: Usikate miti.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/mong/">Mong Palatino</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/philippines-dita-tree-saved-36-lives-during-floods/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/dita-tree-300x225.jpg" title="dita tree" class="aligncenter" width="300" height="225" /><br />
Mti wa aina ya m-dita wenye futi 40 ulikuwa kimbilio la hifadhi kwa watu 36 wa familia saba huko <a href="http://slingshot2004.blogspot.com/2009/10/ondoy-hits-brgy-bagong-silangan.html">Barangay Bagong Silangan</a> (kijiji cha New East), kwenye mji wa Quezon, Metro Manila wakati maji yalipofurika tarehe 26 Septemba. Mafuriko hayo yalisababishwa na mvua kubwa iliyovunja rekodi iliyotokana na <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/10/02/typhoon-ketsana-batters-southeast-asia/">kimbunga cha Ketsana</a> kilichoikumba nchi ya Ufilipino mwezi Septemba. Ilikuwa ni <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/09/28/philippines-flooding-documented-on-citizen-videos/">gharika mbaya zaidi</a> kutokea nchini katika miaka 40 iliyopita.</p>
<p>Kuna miti michache ya mi-dita iliyobaki kwenye maeneo ya Manila mjini. Barangay Bagong Silangan ni jamii masikini ya mjini iliyo sehemu ya kaskazini mashariki mwa mji mkuu wa nchi. Zaidi ya watu 30 walipoteza maisha yao katika jamii hii wakati wa janga la mafuriko haya.</p>
<p><em>Arkibong Bayan</em> <a href="http://www.arkibongbayan.org/2009/2009-10-Oct15-treesaved36people/bagong%20silangan.htm">anatoa undani zaidi wa tukio hili</a>:</p>
<blockquote><p>Watu 36 wa familia 7 walipanda mti huu wa m-dita wakati maji yanayofurika yalipokuwa yanaongezeka na waliokoka. Walibaki kwenye matawi ya mti huu kuanzia saa 4 asubuhi ya terehe 26 mpaka saa 9 alfajiri ya siku iliyofuata walipoteremka, na maji yakiwa usawa wa kiuno kwa sababu walipatwa na baridi kali na njaa kwa masaa 17. Kati yao mkubwa kuliko wote alikuwa na miaka 60 na mdogo zaidi alikuwa na umri wa majuma mawili tu.</p>
<p>Somo la kimaadili: Usikate miti, inaweza kuyaokoa maisha yako siku moja. (Katika suala hili, kwa maana ya moja kwa moja.)</p></blockquote>
<p>Walionusurika wanasema kwamba kulikuwa pia na majoka makubwa yaliyokuwa yakitafuta hifadhi kwenye mti huo.</p>
<p>Ukiacha mti huo wa m-dita, kulikuwa na mti mwingine ambao wakazi wengine walidai kuwa nao pia uliokoa maisha ya wanakijiji wengine.</p>
<blockquote><p>Sabi ng mga taong nakausap namin nung magpunta din kami dun, maliban sa dita tree, may isa pang puno dun na mas manipis pero mataas din. doon daw sumabit yung isang pamilyang nakasakay sa yero. Meron ding 2 month old baby na natangay ng agos sa puno kaya sinungkit din nila.</p></blockquote>
<div class="translation">Kwa mujibu wa baadhi ya wanakijiji, kuna mti mwingine (mdogo kuliko m-dita) ambao ulitumiwa na familia kama hifadhi ya muda. Kulikuwa na mtoto wa miezi miwili aliyebebwa na mafuriko ya maji karibu na mti. Mtoto aliokolewa pia.</div>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/flood-300x201.jpg" title="flood" class="aligncenter" width="300" height="201" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/flooding-300x201.jpg" title="flooding" class="aligncenter" width="300" height="201" /><br />
<em>KIKOSI MAALUM CHA KAZI: watu wa ‘children of the storm’ </em>waliweza kutembelea kijiji na kundi lingine liliweza kuuona <a href="http://tfchildrenofthestorm.wordpress.com/2009/10/19/from-ondoy-to-pepeng-more-children-reached-more-work-done/">‘Mti wa Uzima’</a></p>
<blockquote><p>Tulionyeshwa pia tunaouita sasa ‘Mti wa Uzima’, m-Dita ambako familia 7 (watu 36) walitafuta hifadhi wakati wa mafuriko na wakaokoka na mafuriko ya maji.</p>
<p>Wakazi walionusurika, waliokuwa wanakagua nyumba zao kwa ajili ya ukarabati, walizungumzia namna walivyopanda kutoka paa hadi paa kutafuta eneo lililoinuka zaidi. Walielezea namna waliovyoweza kumwokoa mtoto wa umri wa miezi miwili kwenye paa la bati lililokuwa linaelea.</p></blockquote>
<p><em>Arkibong Bayan</em> alipokea maoni kutoka kwa msomaji aliyesimulia kuhusu jinsi mti wa mwembe ulivyookoa maisha wakati wa janga mitatu iliyopita.</p>
<blockquote><p>Wakati wa Kimbunga kabambe kilichoitwa Reming Novemba 30, 2006, mwembe uliokoa maisha ya watu watano huko Padang, mjini Lagazpi (mkoa wa Bicol katika kisiwa cha Luzon). Mtu mmoja aliyenusurika alikuwa na machaguo mawili: Mwembe ama paa la nyumba. Akachagua mti; wale waliokuwa kwenye paa walisombwa na mafuriko kuelekea baharini.</p>
<p>Somo: Panda mti. Unaweza kuyaokoa maisha yako</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/ondoy-wrath-300x225.jpg" title="ondoy wrath" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/ondoy-impact-300x225.jpg" title="ondoy impact" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p>Baada ya kunusurika na mafuriko mabaya ya mwezi Septemba, wakazi wa Barangay Bagong Silangan wanakabiliwa na changamoto kubwa zaidi: kujenga upya nyumba zao na maisha yao. Jamii imekuwa<a href="http://www.arkibongbayan.org/2009/2009-10-Oct30-Survivorstelltheir%20stories/Survivors%20tell%20their%20stories.htm"> jamii iliyobadilika</a>. Nyumba zilisombwa na maji na miundo mbinu iliharibiwa vibaya.</p>
<p>Tuliambiwa kwamba kabla ya Ondoy (Kimbunga cha Ketsana) eneo hilo lilikuwa lina msongamano mkubwa wa watu kama maeneo mengine ya kimasikini mijini.</p>
<p>Sasa, nyumba bora tu ndizo zilipona. Na eneo linaonekana kuwa wazi na kuwa na nafasi zisizo na kitu –yote kwa sababu nyumba zilisombwa na gharika ya maji iliyoleta athari mbaya.</p>
<p>Picha zote kwa hisani ya <em><a href="http://www.arkibongbayan.org/">Arkibong Bayan</a></em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/philippines-mti-wa-dita-waokoa-maisha-ya-watu-36-wakati-wa-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Venezuela: Kukutana na kazi za msanii Jesus Soto</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/venezuela-kukutana-na-kazi-za-msanii-jesus-soto/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/venezuela-kukutana-na-kazi-za-msanii-jesus-soto/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 13 Nov 2009 13:14:48 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Venezuela]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=617</guid>
		<description><![CDATA[Kazi za msanii wa Kivenezuela Marehemu Jesus Soto zinapaswa kuguswa na kujizamisha ndani yake ili kuzielewa. Wachache waliwahi kutembelea kazi zake kwenye makumbusho wameandika uzoefu wao. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/laura-vidal/">Laura Vidal</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/venezuela-interacting-with-the-works-of-artist-jesus-soto/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kazi za msanii wa Kivenezuela <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jesus_Soto">Jesús Soto (1923 - 2005)</a> ni kati ya kazi maarufu zaidi zinazoonyesha sura ya sanaa ya kisasa ya Amerika ya Kati (Latin), anafahamika zaidi kwa kazi za kutumia mikono yake mwenyewe.  Soto alizaliwa huko Ciudad Bolivar, Venezuela, ambako alianza kufanya kazi kama mchoraji wa mabango ya sinema. Alipata elimu yake katika miji ya Caracas na Maracaibo, lakini ilikuwa ni huko Paris ambako kazi yake ilipata mwelekeo wenye nguvu zaidi. Kazi zake maarufu ni zile “zinazoingiliana” ambazo ni vinyago vyenye muonekano wa mistari ya miraba, mirija miembamba inayoning’inia, yenye rangi zinazong’aa zilizotengenezwa na plastiki na ambayo watu huweza kupita katikati yake. </p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha ya mtoto kwenye maonyesho ya Soto iliyopigwa na Ale na imetumiwa chini ya  leseni ya Cretive Commons" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/kids.jpg" title="kids" width="400" height="268" /><p class="wp-caption-text">Picha ya mtoto kwenye maonyesho ya Soto iliyopigwa na Ale na imetumiwa chini ya  leseni ya Cretive Commons</p></div>
<p>Kwa mujibu wa wataalamu wa sanaa, sanaa ya Sato haijitengi na mtazamaji, ambaye ni mshiriki hai wa kazi ya msanii. Mauzauza na hisia vinakamilishwa na mtazamo wa akili kama matokeo ya kuona, kugusa na kuwa sehemu ya kazi yenyewe. Wanablogu wa Venezuela na jamii ya mtandaoni kwa ujumla, wanasherehekea sanaa yake kwa kupitia makala, mapitio, na video zilizochukuliwa kwenye  makumbusho na ndani ya kazi zenyewe, wakati wakieleza maana ya kazi za Sato katika utamaduni wao, sura ya nchi na maisha yao ya kila  siku. </p>
<p>Katika blogu yake, <em><a href="http://literanova.eduardocasanova.com/index.php/2009/09/24/jesus-soto-y-el-cinetismo-conceptos-e-hi">Literanova[es]</a></em>, Eduardo Casanova anaingia ndani zaidi kidogo kuhusu maisha ya Sato na kutupa mwanga wa histroia ya mji alikozaliwa: </p>
<blockquote><p>Jesús Rafael Soto nació en Venezuela, en 1923, en una población cargada de historia: Ciudad Bolívar, donde se instituyó la prensa escrita y se fraguó la creación de la llamada Gran Colombia (…) Era una población aislada, sin museos ni actividades del arte. El mismo ha dicho que aprendió solo el arte de la pintura. Deja su ciudad natal y viaja a Maracaibo, en el occidente del país, para encargarse de la dirección de una escuela de artes plásticas. En 1950 se va a París y allí comienza su carrera de artista creador de nuevas formas.</p></blockquote>
<div class="translation">Jesus Soto alizaliwa mwaka 1923 katika mji wenye historia kubwa; Ciudad Bolivar, ambako vyombo vya habari vilitoa taarifa rasmi kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi na ndipo  wazo la kuundwa kwa kwa Colombia Kuu lilipoanzishwa. Ilikuwa ni eneo la watu waliotengwa, wasio na makumbusho ya kihistoria wala shughuli za kisanii. Alizoea kusema kwamba alijifunza namna ya kuchora yeye mwenyewe. Aliondoka kwenye mji huo alikozaliwa na kwenda Maracaibo, magharibi ya nchi kuwa Mkurugenzi wa shule ya sanaa. Mwaka 1950, Soto alienda Paris na huko ndiko alikoanza ubunifu wa mtindo mpya (wa sanaa).</div>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha ya tufe la Soto katika Cracas ya Gillermo Ramos Flamerich chini ya leseni huru ya GNU. " src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/sotosphere.jpg" title="sotosphere" width="400" height="379" /><p class="wp-caption-text">Picha ya tufe la Soto katika Cracas ya Gillermo Ramos Flamerich chini ya leseni huru ya GNU. </p></div>
<p>Chaneli ya YouTube ya  <a href="http://www.youtube.com/watch?v=kqetiW8MClE&#038;feature=fvw">VenezuelaTuya</a> inatoa mfano wa uzoefu wa kutembea kwenye mchoro wa maonyesho kwenye Makumbusho ya  Jesús Soto, mjini Ciudad Bolívar:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/kqetiW8MClE&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/kqetiW8MClE&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Blogu ya <em><a href="http://talentovenezolano.blogspot.com/2007/01/jess-soto-venezolano-universal.html">Talento Venezolano [es]</a></em> pia inatoa nafasi maalumu kwa ajili ya kuzungumzia yanayohusu wasaniii na ubunifu wao maarufu: </p>
<blockquote><p>En 1967 creó la primera obra de la serie Penetrables, la cual consiste en instalaciones de tubos de plástico a través de los cuales el espectador se siente en un espacio mágico. Ambas obras que pudieron admirarse en el Museo de Arte Moderno, en el Grand Palais y el Centro Pompidou de París.</p></blockquote>
<div class="translation">
Mwaka 1967 (Soto) alitengeneza moja ya kazi zake za kwanza “zinazoingiliana” ambazo ni mirija ya plastiki ambapo mtazamaji anaweza kujisikia kwenye eneo  la kimazingaombwe. Kazi zote zilizonyeshwa kwenye Makumbusho ya sanaa ya Kisasa, huko Paris kwenye Grand Palais na Kituo cha Pompidou. </div>
<p>You Tube vilevile imekuwa njia ya watu kuonyesha mawasiliano na hisia zao wakati wanashiriki kazi za Soto kwa vitendo. Hasa watoto, wamekuwa na muelekeo maalum wa uzoefu ndani ya kazi za msanii, ambao umeonyeshwa na kushirikishwa kwenye viideo hizi: </p>
<p>Mtumiaji wa YouTube elizaul1:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/kWZd2DQ1ASc&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/kWZd2DQ1ASc&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Na mtumiaji wa YouTube skaracas:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/OlacQOCh0H4&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/OlacQOCh0H4&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kwenye <a href="http://www.jr-soto.com/fset_menuprincipal_fr.html">tovuti</a> ya msanii kuna kurasa za picha na habari zaidi.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/venezuela-kukutana-na-kazi-za-msanii-jesus-soto/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Cameroon: Wezi “wakarimu” na Malipo kwa Kutumia Salio la Simu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cameroon-wezi-%e2%80%9cwakarimu%e2%80%9d-na-malipo-kwa-kutumia-salio-la-simu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cameroon-wezi-%e2%80%9cwakarimu%e2%80%9d-na-malipo-kwa-kutumia-salio-la-simu/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 13 Nov 2009 12:56:57 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Business]]></category>
		<category><![CDATA[Cameroon]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Humor]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=618</guid>
		<description><![CDATA[Karibu wakazi milioni 20 wa Cameroon wanakabiliwa na kiwango kinachoongezeka cha unyang’anyi. Majambazi wameweza hata kuyavamia makao makuu ya taifa ya polisi na Wizara ya Mambo ya Nje katika mji mkuu wa Yaounde. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/george-esunge-fominyen/">George Esunge Fominyen</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/10/cameroon-from-kind-thieves-to-mobile-credit-as-legal-tender/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Karibu wakazi milioni 20 wa Cameroon wanakabiliwa na kiwango kinachoongezeka cha unyang’anyi. Majambazi wameweza hata kuyavamia makao makuu ya taifa ya polisi na Wizara ya Mambo ya Nje katika mji mkuu wa Yaounde. </p>
<p>Mwanablogu wa <a href="http://patiencentemgwa.blogspot.com/2009/11/mokolo-organised-petty-crime.html">PNT Attitude</a> alitoa uzoefu wake kuhusu jinai katika makala ya hivi karibuni akielezea jinsi mkoba wake ulivyoibwa kutoka kwenye gari yake:</p>
<blockquote><p>…niliegesha pembeni (gari) ili kununua maembe. Maembe yaliponunuliwa,, nikafungua mlango wa gari ili kuweka maembe kwenye kiti cha nyuma. Hapo hapo ndipo nilipomwona jamaa huyu akishangaa shangaa kwenye upande mwingine wa gari. </p>
<p>Sikumjali. Ghafla alifungua mlango wa abiria, akaupokonya mkoba wangu uliokuwa kwenye kiti cha mbele, na akakimbilia sokoni. Mwanzoni nilifikiri anataka kuteka gari, au alitaka kunifanya nijisikie wasiwasi kwa kuingia kwenye gari? Inawezekana alikuwa na matatizo ya akili? Nilipiga kelele ‘mwizi’ na kumkimbiza nikiwa na maembe, ambayo nilimrushia kabla hajakata kona, na hivyo kunipotea machoni. Ndio, unaweza kudhani sikuwa makini kwa kuacha mkoba wangu pale, kwa taarifa yako, ulikuwa umefichwa chini ya kiti kile kile mpaka nilipofikiri kuwa nimemaliza manunuzi!’</p></blockquote>
<p>Lakini jambo zuri kwenye habari yake ni kwamba wezi wengine mjini Yaounde wanaweza kuwa ‘wakarimu’. Hata polisi wanajua kwamba kama mtu ana bahati wanaweza kumrudishia vitu vyake binafsi kwa kutembelea sehemu ambayo aliibiwa (kwapuliwa). Kwa hiyo akaendesha mpaka pale:</p>
<blockquote><p>Niliambiwa kwamba jamaa mwenye mkoba mwekundu alikuja dakika kadhaa baada ya mimi kuondoka na kuuliza “yuko wapi mwanamke ambaye mkoba wake ulikwapuliwa”. Kwa sababu hawakuniona, waliuchukua. </p>
<p>Mimi na rafiki yangu tulimtafuta maeneo ya njia aliyotorokea kwa muda mchache na mtu mwingine akashauri tujaribu kituo jirani cha redio. Tulienda na wahudumu wa mapokezi wakasema: “ndio tulipokea mkoba huu asubuhi ya leo na vitu vilivyomo kwa jina la&#8230;Ntemgwa&#8230;!” na hvyo ndivyo ilivyokuwa, nilijisikia AHUENI kwamba nimeupata mkoba wangu, akauleta, nikapekua vilivyomo na nikasema kila kitu kilikuwa kama kilivyokuwa timamu, isipokuwa bila shaka fedha na hawala ya kununulia mafuta. Akaongeza “frs 10.000, gharama ya kuutoa”. Nilijaribu kubembeleza punguzo na baadae nikafahamu kuwa kilichokuwa kwenye mkoba kilikuwa  na thamani kuliko gharama hiyo iliyoombwa. Hata hivyo niliomba punguzo mpaka frs 5.000 na nikaupata mkoba, nikarudi nyumbani, kwa furaha.”</p></blockquote>
<p>Baada ya tukio hilo hapa kuna mafunzo aliyojifunza PNT:</p>
<blockquote><p>-Si wezi wote wana nia mbaya, wengine ni wabahatishaji wenye njaa tu;</p>
<p>-Kuna mtandao ulijpanga wa ujambazi (uchwara) kwenye soko la Mokolo, uwe makini na chochote unachofanya kila mara unapojikuta pale, (mtandao) uliojipanga kwa sababu wanachohitaji zaidi ni fedha zako, na kila mmoja aliye kwenye maeneo hayo anajua wapi unaweza kuupata mkoba wako baada ya tukio, nani ajuye kama kuna zaidi kwenye mpango mzima kuliko kinachoonekana?</p>
<p>-Ni kawaida kushambuliwa kwenye masoko kama haya yenye msongamano wa watu, polisi hawakuutilia maanani mchezo mzima, wakishangaa kwa nini nilikuwa najisikia vibaya, ndio hakuna huduma za kuhudumia waliotharika katika vituo vya polisi kwa sababu ni ‘kawaida’ kuathirika kwa namna hiyo&#8230; haggle<br />
-Ninayakumbuka kwa hamu yale maembe na sina lolote dhidi yake;”</p></blockquote>
<p>Akizungumzia ununuzi wa matunda mjini Yaounde, mfanyakazi wa kujitolea wa shirika la kujitolea la Marekani  (U.S. Peace Corps ) anayeblogu kwenye <a href="http://adventuresofaubrey.blogspot.com/2009/11/oh-cameroon.html">Adventures of Aubrey</a> inaelekea amekuwa akibishana kidogo juu ya bei ya matofaa. Mazungumzo na wauza matofaa kwa hakika yanaibua mengi kuhusu mitizamo inayoambatana na rangi ya mtu ambayo ina mkanganyiko: </p>
<blockquote><p>Wakati wa safari yangu ya Yaounde juma hili nilienda kununua matofaa mara mbili. Mara ya kwanza nilikuwa nikitembea mtaani na kumwona mtu mwenye mkokoteni wenye matunda. Nikamwuliza bei na nikamwambia hiyo ilikuwa ni bei kwa mzungu na kwamba matunda hayo yalipaswa kugharimu kiasi hiki na kwamba nilitaka kununua matunda mawili kwa kiasi hiki. Akacheka na kushusha bei lakini si sana. Tukazungumza kwa kuvutana dakika chache na mwishowe akataka CFA50 zaidi (kama senti 10) na sikuweza kulipa na ndipo nikachukua mfuko wangu na kupakia matunda yangu na kuacha hela kwenye mkokoteni wake wakati sote tukicheka na kuondoka huku nikisema asante na kwamba ningerudi wakati mwingine (hii ni namna iliyozoeleka ya kumaliza mazungumzo nchini Cameroon –kusema asante, wakati mwingine).”</p></blockquote>
<blockquote><p>…Nilimuona mtu mwingine akiwa na mkokoteni wa matofaa nje ya duka la mzungu kwenye mtaa mwingine mjini Yaounde (hilo lilikuwa kosa la kwanza, kujaribu nje ya duka la mzungu). Nikamuuliza matunda hayo yalikuwa yanauzwa bei gani, tukaingia dukani pamoja na rafiki yangu na mama yake, tukarudi na nikaamua ninayahitaji matunda hayo na kuanza kuomba kupunguziwa bei. Akawa na hasira na akaanza kunipigia kelele kwamba kwa nini nilifikiri bei ingepungua –aliniambia bei na alitegemea ningetakiwa kuikubali na blah blah blah. Basi nikacheka nikimwambia, hii ni Cameroon unaomba punguzo kwa kila bei na nikajaribu kuomba anipunguzie. Akakasirika  tena. Ndipo, na mimi nikawa mkali. Nikamwambia alikuwa si muungwana na kwamba sijali matunda yake yalikuwa ni bei gani sasa sikuwa na mpango wa kununua kwake tena. Akanikemea kwamba nilikuwa si muungwana kujaribu kuomba kupunguziwa bei wakati nilikuwa tajiri (yaani mzungu). Nikarudia kwamba alikuwa si muungwana na kwamba asingeipata fedha yangu leo na hata siku nyingine na kuondoka. Mwaka mmoja uliopita hali hiyo ingenikasirisha sana lakini sasa ninakimbia kwa urahisi kwenda kukutana na rafiki yangu na mama yake na kusimulia tukio hilo huku nikicheka na kusema kwamba kwamba nilidhani haikuwa siku yangu ya matofaa.” </p></blockquote>
<p>Badala ya kukimbilia kwenye matatizo ya kupatana bei, labda Aubrey (au yeyote anayepanga kukaa Cameroon) anapaswa kutumia huduma ya simu za mkononi ya kununua vocha za kulipia-kadri-ya-matumizi za simu ya mkononi kama malipo halali. Inaelekea  kuwa ni njia rahisi zaidi ya kununua vitu bila fedha taslimu kama mtu atafuata maneno ya <a href="http://patiencentemgwa.blogspot.com/2009/09/i-discovered-form-of-legal-tender.html">PNT Attitude</a>: </p>
<blockquote><p>Nilikuwa karibu ya kumaliza kununua bidhaa kwenye orodha yangu nilipoamua kwenda kwenye duka la nguo za ndani kutafuta bidhaa iliyokuwa kwenye orodha yangu ya manunuzi kwa muda mrefu: sidiria isiyokiwa na pindo wala waya.</p>
<p>Nilikuwa na bahati sana kuikuta kwenye duka hilo, na kama nilivyokuwa nimeandikiwa, ilikuwa ni ya mwisho iliyobaki na sikuwa nimeiona kwenye duka lingine lolote. Muuzaji akasema iligharimu CFA 4,500. Tazama nilikuwa na CFA 3,500 tu mfukoni! Nilijaribu kuomba kupunguziwa mpaka bei niliyokuwa nayo, bila mafanikio. Nikafikiri kutembea mwendo unaotisha kuelekea kwenye gari na pia  uwezekano wa kuwalipa kidogo kidogo kwa kutumia huduma ya kuhamisha salio kwa simu. Chaguo la pili lilionekana kuwa linawezekana zaidi. </p>
<p>Kwa hiyo nikamuuliza kama alikuwa na simu ya MTN ili niweze kumalizia malipo kwa kupitia huduma ya kuhamisha salio kwa simu. Akasema hapana, alikuwa na Simu ya mtandao wa Orange. Hata hivyo akaongeza, “nina rafiki mwenye mtandao wa MTN unaweza kutuma kiasi kilichobaki kwake (CFA 1000). Tatizo limetatuliwa, nikaondoka na sidiria niliyokuwa nimeitafuta sana, nikitabasamu wakati nikiondoka”</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/cameroon-wezi-%e2%80%9cwakarimu%e2%80%9d-na-malipo-kwa-kutumia-salio-la-simu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ujauzito na Magereza: Afya na Haki za Wanawake Magerezani</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 05 Nov 2009 13:24:11 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[Ecuador]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Laos]]></category>
		<category><![CDATA[Peru]]></category>
		<category><![CDATA[Photography]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Spain]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=493</guid>
		<description><![CDATA[Mapambano bado yanaendelea kuhakikisha haki za binadamu kwa wanawake wajawazito duniani pote, ni inaelekea kwamba katika mchakato huo, wanawake waliopo magerezani wanasahauliwa. Je ni hatua zipi zilizochukuliwa kuhakikisha kuwa nao wanaangaliwa kwa utu, kwa kuzingatia uhai wanaoubeba.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/24/pregnancy-and-prisons-womens-health-and-rights-behind-bars/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/2044749780_4ade9e2e3f-300x225.jpg" title="2044749780_4ade9e2e3f" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><strong>Je, wanawake wote wajawazito wanastahili haki sawa za binadamu, au wanawake wajawazito walio jela huziacha haki hizo? </strong></p>
<p>Kuna maswali machache yanayokuja akilini kuhusu haki ya mwanamke mjamzito kuishi na kumlea mwanae anapokuwa kapatikana na hatia kwa kosa la jinai la namna fulani:<br />
•	Inakuwaje kwao wanapokuwa wajawazito na kupata mtoto wakiwa gerezani?<br />
•	Je, wanapaswa kuwa kipaumbele wakati kuna wanawake wengine nje ya vyuo vya mafunzo bila msaada wa kitabibu?<br />
•	Je, ujauzito unapaswa kuwa juu ya hali nyinginezo za kisheria kumhakikishia mwanamke mjamzito haki zake za kibinadamu? </p>
<p><strong>Marekani: wanawake walio kwenye uchungu wa kuzaa hawatafungwa tena minyororo.  </strong></p>
<p>Je unaweza kufikira mwanamke akijifungua huku mikono yake ikiwa kwenye pingu na miguu yake ikiwa imefungwa na minyororo kwenye kitanda? <a href="http://www.rhrealitycheck.org/user/malika-sadaa-saar">Malika Saada Saar</a>, mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa <a href="http://www.rebeccaproject.org/">Mradi wa Rabecca kwa Haki za Binadamu</a>, <a href="http://www.rhrealitycheck.org/blog/2009/10/06/in-labor-and-in-chains">anatuelezea</a> kuhusu kitendo hiki ambacho bado kinatokea nchini Marekani, ambapo wanawake wajazito wanaotumikia kifungo wamekuwa wakifungwa minyororo wakati wa uchungu na kujifungua na kuwa hiki ni kitendo kilichozoeleka katika baadhi ya magereza (ya kurekebishia tabia), ingawa ni hatari kwa afya ya mama na mtoto. Ifuatayo ni video ya mahojiano yaliyoambatanishwa kwenye makala iliyoandikwa kwa ajili ya mradi wa <em>RH Reality Check</em>, jamii ya mtandaoni kuhusu afya na haki ya uzazi na jinsia inatupa taarifa na uchambuzi kwa afya ya uzazi:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
<strong><br />
Kitu gani hutokea kwa mtoto mchanga wa wa mfungwa baada ya kuzaliwa?</strong></p>
<p>Nchi mbalimbali zina kanuni tofauti kuhusiana na watoto magerezani. Kwa mfano, nchini Argentina, kwa mujibu wa <em>Ajintem</em>, chombo cha mawasiliano cha taarifa za uhamamiaji,  <a href="http://portal.ajintem.com/archivo/80-argentina-prision-domiciliaria-para-embarazadas-y-madres.html">sheria ilipitishwa</a> mwaka uliopita ikifafanua kwamba wanawake wajawazito, wanawake wenye watoto wadogo chini ya miaka mitano na wale wenye watoto walemavu wangenufaika na mpango wa kutumikia kifungo chao makwao chini ya ulinzi wa nyumbani. Sheria hii ingewanufaisha si tu akina mama, ambao kwa kuwa gerezani wasingepata huduma za afya wakati wa ujauzito, lakini pia (ingemnufaisha) mtoto, ambaye angelelewa ama katika mazingira yasiyo salama yanayokosa uhuru na upungufu wa udhibiti wa afya na chakula, au wangelelewa mbali na mama, na hivyo kusababisha mlolongo wa matatizo mengine. Hata hivyo, ujumbe ni kwa ajili ya mahakimu kufuatilia kiini cha sheria na kutoa ruhusa hii kwa wanawake wale ambao hawahusishwi na mashitaka ya jinai ya matumizi ya nguvu, kuhakikisha kwamba idadi kubwa ya raia iliyobaki haiuchukulii ujauzito kama kadi ya kumtoa mtu jela bure.</p>
<p>Katika visiwa vya Canary, kwa mujibu wa blogu ya <em>Prisiones y penas</em>, ambayo huandika kuhusu habari zinazohusu jela na magereza, wanawake wanaruhusiwa <a href="http://prisionesypenas.blogspot.com/2009/09/detenidas-con-hijos-en-carceles.html">kuishi na watoto wao hadi umri wa miaka mitatu</a> ndani ya selo zao, lakini wakiwa pamoja na wafungwa wenzao, kitu ambacho sio mazingira mazuri sana kwako. Kwa hiyo, wanawake wajawazito au wanawake wenye watoto wenye umri wa chini ya miaka 3 huambiwa kuhusiana na kuingia kwenye magereza kuwa si vizuri kwa mtoto kukualia gerezani, na hupewa uchaguzi wa kumpeleka mtoto kwa wanafamilia wengine. Hali ni hii hii huko <a href="http://www.reuters.com/article/worldNews/idUSTRE5085ZV20090109">Peru</a> na <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">Urusi</a>. Nchini Marekani, kuna magereza mawili tu yenye kuruhusu jambo hili, huko New York na Nebraska, <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/e_moms.html">kama ilivyoonyeshwa na mpiga picha maarufu Jane Evelyn Atwood</a> kwenye insha ya picha zake tatu kwa ajili ya <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/"><em>Shirika la kimataifa la Amnesty International</em>, inayoitwa <em>Too Much Time</em></a>, ambapo alitembelea dazani nyingi za magereza kote duniani kurekodi na kuweka kumbukumbu za maisha ya wafungwa.</p>
<p>Kwa nini mfumo wa magereza nchini Marekani hauruhusu, kwa ujumla, wanawake wenye watoto kubaki nao? Atwood anaeleza kwamba kwa sababu ya mazingira ufungwa, hairuhusiwi. Kwenye <a href="http://prisonphotography.wordpress.com/2009/10/07/women-behind-bars-jane-evelyn-atwoods-too-much-time/"><em>blogu ya Prison Photography</em> wanaelezea madai haya</a>: </p>
<blockquote><p>Watoto hawahusishwi kwenye magereza yote isipokuwa mawili tu nchini Marekani. Tishio la usalama linatajwa kama sababu: mtoto ndani ya gereza ni dhaifu na atakuwa shabaha ya malengo maovu siku zote. Madai yanaonekana kuwa hayana maana kwa kiasi fulani kwa unapofananisha na mifumo ya adhabu kwa nchi nyinginezo.</p></blockquote>
<p>Insha ya Atwood kwenye wavuti ya <em>Amnesty International</em> inaonyesha mambo mawili, sehemu inayohusu taratibu za kujifungua huku umefungwa minyororo kama yalivyoelezwa kwenye <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/f_vanbab.html">Mtoto wa Vanessa</a> na pia inaonyesha jambo jingine kuhusu mfumo wa magereza na umama, kwa kutumia picha za wanawake wakati mpigapicha akisoma insha kuhusu uzoefu wake wa kutembelea magereza huku akipiga picha. </p>
<p><strong>Ujauzito kama zana ya mapatano? </strong></p>
<p>Kwa nini haki za wanawake wajawazito gerezani zinatatanisha? Katika  <em>Russia Today</em>, idhaa ya matangazo ya Kirusi, <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">mada hii inatajwa</a> panapojadiliwa suala la watoto kuzaliwa na kulelewa katika mfumo wa magereza wa Kirusi:</p>
<blockquote><p>Wenye kutilia mashaka (suala hili) wanadhani akina mama wengine hupata ujauzito kwa makusudi ili tu kurahisisha maisha huko gerezani. Ruhusa ya kwenda hospitali, halafu kuwa na ratiba iliyojaa muda mwingi na mwanao –ni afadhali kuliko kukaa kwenye seli ya magereza, wanadai. </p></blockquote>
<p>Na kuna wanawake ambao wanaona kwamba kuwa na mimba ni njia pekee ya kukwepa hukumu, kama ilivyotokea mwezi Juni, pale mwanamama wa Kiingereza aliwekwa ndani na kuhukumiwa kifo huko Laos kwa sababu ya kusafirisha madawa ya kulevya akapata ujauzito gerezani na akanusurika kunyongwa, kwa sababu serikali ya Laos isingemnyonga mwanamama mjamzito. <a href="http://www.dailyexpress.co.uk/posts/view/105278/No-firing-squad-for-girl-who-fell-pregnant-in-jail">Madai yaliyotolewa </a>kwa mujibu wa jarida la Kiingereza la <em>Daily Express</em>, ni kwamba alipata ujauzito kwa kupandikiziwa mbegu za kiume ‘ili kupata hukumu nyepesi zaidi” </p>
<p><strong>Kwa maneno yao: Wanawake wanaeleza kuhusu watoto wao na maisha ya gerezani</strong></p>
<p>Geraldin Rodríguez, Mwajentina aliye kwenye jela za Ecuador kwa sababu ya biashara ya madawa ya kulevya anamueleza <a href="http://marcosbrugiati.blogspot.com/2009/07/carcel-de-mujeres.html">Marcos Brugiati</a>, mwandishi mshiriki katika chapisho la mtandaoni linalohusiana na masuala ya sanaa liitwalo <em><a href="http://www.indexarte.com.ar/noticias/562/las-rejas-de-la-carcel-el-arte-de-la-espera.htm">Plastica-Argentina</a></em>, masimulizi kuhusu kuigiza na kufanya maonyesho ndani ya jela, kupata ujauzito gerezani na kumpata mwanae. Aliruhusiwa kuwa na mwanae, lakini akaamua kwamba mwanae anahitaji kukua akiwa mtu huru:</p>
<blockquote><p> “Decidí que salga para vivir, tenía miedo que sufra de grande los traumas que hoy tengo. Se lo llevó al año mi hermano quien se hice cargo con su esposa”.</p></blockquote>
<div class="translation">Niliamua aondoke ili aishi, nilikuwa na wasiwasi angeteswa na msongo wa mawazo nilionao leo. Baada ya mwaka kaka yangu alimchukua na anamtunza kwa kushirikiana wa mke wake. </div>
<p>Juvinete yuko kwenye <a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">gereza la Kihispania</a>, na alikuwa mjamzito wakati alipofungwa kwa kusafirisha madawa ya kulevya. Anasimulia habari zake kwenye gazeti la kanda huko Uhispania linaloitwa <em><a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">NorteCastilla</a></em>. Miaka mitatu baada ya kujifungua mwanae akiwa gerezani, mwanae ilibidi aondoke, na alipelekwa kwa familia ya kufikia. Juvinete humuona mwanae huyo wa kike kila baada ya siku 15 na kila miezi miwili hupata ruhusa ya wiki mbili kukaa na mwanae. Hata hivyo, mambo hayaonekani kuwa mazuri sana: kuna uwezekano kwamba Juvinete atapelekwa Brazil alikozaliwa, na anahofia matokeo ya mabadiliko haya kwa mwanae. Anao ushauri kwa mwanamke yeyote anayeamua kupata ujauzito akiwa jela:</p>
<blockquote><p>-Intento convencerlas para que no se queden en estado dentro porque ver a un niño privado de libertad es muy duro, es irresponsable. Ellos no tienen que pagar nuestros errores.</p></blockquote>
<div class="translation">
Ninajaribu kuwashawishi wasipate ujauzito wakiwa bado ndani kwa sababu kumuona mtoto akikosa uhuru wake ni vigumu sana, ni kutokuwajibika. (Watoto wanaozaliwa jela) wasilipie gharama ya makosa yetu</div>
<p>.  </p>
<p>Kwenye wavuti ya <em><a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">Woman and Prison</a></em>, iliyojikita katika kuyatazama maisha ya wanawake wakiwa kwenye mifumo ya magereza , <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">mfungwa Kebby Warner anaongelea ujauzito wake</a> mwenyewe alipokuwa akitumikia kifungo kwenye gereza la Kimarekani, na jinsi alivyotendewa wakati wa ujauzito wake, utungu na baadae, wakati alipokuja kunyang’anywa mwanae. Hapa ni muhtasari anapoandika kuhusu hatua za kujifungua: </p>
<blockquote><p>Wakati wa utungu, hakuna mtu anaruhusiwa kuwa kwenye chumba cha kujifungulia. Familia yangu wala haikujua kwamba nilikuwa ninajifungua au nimempata (mwanagu) mpaka nilipokuwa nimetoka hospitali. Wakati huo wa siku tatu baadhi ya walinzi walikuwa ndani ya chumba, lakini muda mwingi, wakati wauguzi walipowaomba kukaa nje ya mlango, walitii. Nimesikia simulizi za kutisha za wanawake wakifungwa kwa mnyororo kwenye kitanda cha uzazi. Ninashukuru kwa kutokukumbana na hali hiyo. Wauguzi wengi walinitendea kama binadamu badala ya mfungwa.</p></blockquote>
<p>Unaweza kusoma shuhuda zaidi kuhusu kukua na mzazi gerezani na madhara mbalimbali ambayo kufunga wanawake kunaweza kuyawasababisha kwa watoto wao <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/index.html">kwenye Wanawake na Magereza</a>.</p>
<p>Kwa hiyo unafikiriaje? Kwa wanawake wajawazito duniani kote kutokupata huduma za afya za namna yoyote, je jitihada zaidi zinahitajika kuwanufaisha wanawake walio gerezani? Je, kuna tofauti kati ya wanawake wanaotumikia kifungo kwenye magereza (ya mafunzo) na wale wanaoishi nje? Je, ni lazima kuwatendea tofauti?<br />
<em><br />
Picha iliyotumika kwenye makala hii ni “17 de noviembre” ya <a href="http://www.flickr.com/photos/daquellamanera/2044749780/">daquella manera</a>.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Saudia Arabia: Ambako Kuiga Kazi Kinyume cha Haki Miliki ni Kosa la Jinai</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 03 Nov 2009 12:06:46 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Saudi Arabia]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=458</guid>
		<description><![CDATA[Wanablogu wa Kisaudia wanaungana ili kumuunga mkono mwanablogu mwenzao anayelituhumu gazeti moja kuwa limetumia picha na kuzinakili kutoka mwenye blogu yake bila ruhusa. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/amira-al-hussaini/">Amira Al Hussaini</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/20/saudi-arabia-where-plagiarism-is-a-crime/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wanablogu wa Kisaudia wanaungana ili kumuunga mkono mwanablogu mwenzao anayelituhumu gazeti moja kuwa limetumia picha na kuzinakili kutoka mwenye blogu yake bila ruhusa. </p>
<p><em><a href="http://saudijeans.org/2009/10/14/alyaum-steals-kaust-blogger/">Saudi Jeans</a></em>‘ Ahmed Al Omran anazo sifa kiduchu mno kwa gazeti hilo linalotuhumiwa kwa kitendo cha kutumia kazi za wengine kinyume cha haki miliki: </p>
<blockquote><p>Ingawa gazeti la al – Yaum, kwa muda mrefu limefurahia nafasi kubwa katika Jimbo la Mashariki, (EP) linabaki kuwa kati ya machapicho duni zaidi nchini. Nilizaliwa na kukuzwa katika Jimbo la Mashariki, na nilizoea kusoma magazeti ya Ashraq al-Awsat, al-Hayat na al-Watan lakini sio al-Yaum. </p></blockquote>
<p>Kutofurahishwa kwa Al Omran kulichochewa zaidi baada ya <em><a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/i-should-be-getting-paid-for-this.html">Saudi Aggie</a></em>, mwanafunzi mwenye jina la Nathan wa <em>Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mfalme Abdulla</em> (KAUST) <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/09/26/saudi-arabia-kaust-to-inspire-scientific-achievement-and-more/">kilichofunguliwa hivi karibuni</a> alipoleta malalamiko kwamba gazeti hilo limetumia picha zake pamoja na uchambuzi wake kuhusu uchaguzi wa wanafunzi hivi majuzi. Ameweka nakala ya habari hizo kutoka gazetini na kuwauliza wasomaji wake:</p>
<blockquote><p>Siwezi kuamini hili! Angalia makala hii iliyochapishwa hivi majuzi kwenye gazeti maarufu la Saudi Arabia, Al Yaum. Je, picha hizi zinaonekana kana kwamba zinafahamika? Vipi kuhusu maneno? Kama huwezi kusoma Kiarabu, hii ilichukuliwa karibu neno kwa neno kutoka kwenye makala ya blogu yangu niliyoipa jina la ‘<a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/elections.html">uchaguzi</a>’ na kuichapa Oktoba 5, 2009. Hii haiwezi kuwa sahihi kisheria, hata hapa Saudi Arabia!</p></blockquote>
<p>Mwanafuzi huyo wa Kimarekani anaongeza: </p>
<blockquote><p>
Kama ningekuwa Marekani ningefungua kesi ya haki miliki ya utaaluma dhidi ya Al Yaum. Kama lingekuwa ni Gazeti la New York Times limetumia kazi yangu bila ruhusa, ningekuwa tajiri sasa hivi. Hivi haki miliki za utaaluma kwa mawazo na picha zilizochapishwa zina thamani yoyote hapa?</p></blockquote>
<p>Al Omran anazingatia: </p>
<blockquote><p>Nathan anafikiria kuwashitaki, jambo ambalo nadhani litakuwa zuri sana, lakini labda wameshajitia aibu vilivyo wao wenyewe.  </p></blockquote>
<p>Watoa maoni kwenye blogu ya Nathan wanaguswa na yaliyompata mwanablogu: </p>
<p><em>Mazoo</em> anaandika: </p>
<blockquote><p>Ninasikitika kuona hili linatokea kwako&#8230;<br />
Lakini, hili ni jambo lililozoeleka hapa Saudi Arabia&#8230;</p>
<p>Nimesikia kesi nyingi ambazo kazi za marafiki zangu (maandiko ya blogu, picha na mawazo) yameibwa na waandishi habari wavivu. Walilalamikia hali hii na wengine waliaandikia wahariri wakuu –wengine wao huandika taarifa za kuomba msamaha na wengine wao humfukuza kazi mtu aliyeiba maudhui</p></blockquote>
<p><em>Al Hanouf</em>, anayejielezea mwenyewe kuwa ni mwanafunzi wa sheria, anataka haki itendeke: </p>
<blockquote><p>Kama kitendo hiki kikiangaliwa chini ya makosa ya jinai yanayohusiana na kompyuta, basi huyu – mwana habari – inatakiwa awe jela kwa zaidi ya miezi sita na kukulipa si chini ya fedha ya Riyali za Saudia 250,000.<br />
Unapaswa uende kwa mwanasheria, na tafadhali usilimalize hili kwa kuliandikia gazeti barua pepe! Kuna sheria, na (gazeti) halitaweza kurekebisha makosa yake kama tutalimaliza suala hili kwa njia zatu za kizembe!</p></blockquote>
<p>Na Chiara anashauri: </p>
<blockquote><p>Nami ninashiriki katika kuchefuka na uvunjifu huu wa sheria ya haki miliki, na njia iliyozoeleka ya kutafsiri na ‘kuiba’ kazi za wengine si nafuu. Unaweza kuweka blogu yako nzima chini ya haki miliki kama ambavyo wanablogu wengine wamefanya, na kufanya namna ambayo jina lako litaonekana kwenye picha. </p></blockquote>
<p>Kwenye makala fuatilizi, Nathan anaandika:  </p>
<blockquote><p>Nchini Saudi Arabia, umbea huenea kama vile ugonjwa wa mlipuko. Blogu hii imepokea makumi elfu ya watembeleaji wapya katika juma moja tu </p>
<p>[…] </p>
<p>Nilikuja Saudia kujenga madaraja (ushirikiano), sio kutengeneza maadui. Nilikuja kusoma na kutafiti katika Chuo kikuu ambacho kinajitahidi kwa nguvu zote kuwa moja wapo ya vyuo vikuu bora vya utafiti duniani, na sio kupata fedha kutoka kwa watu ama mashirika. </p>
<p>Ninataka uwajibikaji. Ilichokifanya <em>Al Yaum</em> kilikuwa ni makosa, lakini mwenendo wa mjadala pia una makosa. </p></blockquote>
<p>Na maneno yake ya mwisho kwa wasomaji wake ni: </p>
<blockquote><p>Kama unataka kuazima kitu kutoka kwenye blogu yangu, tafadhali omba kwanza. Hakuna mtu, nikijijumuisha na mimi, anayependa kutokuelewana. </p></blockquote>
<p>Kwa kutumia kifaa cha kutafsiri, <a href="http://saudiaggie.blogspot.com/2009/10/i-should-be-getting-paid-for-this.html?showComment=1255467311093#c5285446355482995533">mwandishi husika</a> anamwandikia Nathan akilielezea vyema suala lake.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/saudia-arabia-ambako-kuiga-kazi-kinyume-cha-haki-miliki-ni-kosa-la-jinai/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Malayasia: Serikali ya Jimbo Yaja na Sera ya ‘Msala Mmoja’</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/malayasia-serikali-ya-jimbo-yaja-na-sera-ya-%e2%80%98msala-mmoja%e2%80%99/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/malayasia-serikali-ya-jimbo-yaja-na-sera-ya-%e2%80%98msala-mmoja%e2%80%99/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 27 Oct 2009 11:47:16 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Malaysia]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=457</guid>
		<description><![CDATA[Kwa kuiga chapa ya Malaysia1, serikali ya Jimbo la Terengganu hivi majuzi ilikuja na sera ya ‘msala 1’ kama hatua kwa walimu na wanafunzi (wa jinsia moja) kuchangia misala (vyoo) ili kukuza hisia za umoja. Kumekuwepo na maoni mchanganyiko katika ulimwengu wa blogu kuhusiana na sera hii.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/syafique-shuib/">Syafique Shuib</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/21/malaysia-state-government-introduces-1toilet-policy/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Waziri Mkuu wa Malaysia Najib Tun Razak ameanzisha wazo la Malaysia Moja, maarufu kama <a href="http://www.1malaysia.com.my/">Malaysia1</a>, alipoingia madarakani. Ikiwa ni nchi ya watu wa rangi tofauti, lengo kubwa la Malaysia1 ni kuukuza umoja wa kitaifa na kuimarisha ushirikiano baina ya makundi mbali mbali yenye rangi tofauti. </p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 258px"><img alt="Sera ya Msala1 imeiga dhana ya Malaysia1" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/1_malaysia-248x300.jpg" title="The 1Malaysia Logo" width="248" height="300" /><p class="wp-caption-text">Sera ya Msala1 imeiga dhana ya Malaysia1</p></div>
<p>Kwa kuiga chapa ya Malaysia1, serikali ya Jimbo la Terengganu <a href="http://thestar.com.my/news/story.asp?file=/2009/10/15/nation/4906693&#038;sec=nation#">hivi majuzi ilikuja na sera ya ‘msala 1’ </a>kama hatua kwa walimu na wanafunzi (wa jinsia moja) kuchangia misala (vyoo) ili kukuza hisia za umoja. </p>
<p>“Pale wanafunzi wanapochangia msala na mwalimu, wataamini (wanafunzi) kwamba wako sawa na wanataaluma na hii moja kwa moja huamsha hisia za kujichukulia kuwa na umuhimu katika taasisi, ambako, kwa mukhtadha huu, ni shule,” anasema mwenyekiti wa Kamati ya Elimu, Elimu ya Juu, Rasilimali watu, Sayansi na Teknolojia wa Jimbo hilo, Ahmad Razif Abd Rahman katika gazeti la mahali hapo la <a href="http://www.thestar.com.my/">The Star</a>. </p>
<p>Sera pia itapanuliwa zaidi ya suala la choo ambapo walimu pia wanashauriwa kula katika mikahawa ya shule pamoja na wanafunzi. Ni njia ya makundi hayo mawili (walimu na wanafunzi) kujichanganya wakati wa mapumziko. </p>
<p>Kumekuwa na maoni tofauti kutoka kwenye ulimwengu wa blogu kuhusiana na mada hii. Wengine waliichukulia kama utani, wakati wengine walifikiri ilikuwa ni ubunifu chanya. </p>
<p><a href="http://asiancorrespondent.com/jeff001/2009/10/littleuse_chameleon.php">Jeff Ooi</a>, ambaye ni mwanablogu mkubwa na sasa ni Mbunge anasema: </p>
<blockquote><p>Wakati huu, matunda ya kupanuka kwa Malaysia1 yako mahali pa kujisaidia. </p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa <em><a href="http://liangseng.blogspot.com/2009/10/liang-seng-and-one1.html">Life And Ti(m)es Of Liang Seng</a></em> hakuweza kuamini kwamba Serikali ya Jimbo hilo inakuja na wazo la ‘Msala mmoja’: </p>
<blockquote><p>Ningeelewa sehemu ya kuchangia mkahawa. Lakini hivi kweli kuchangia msala ni kukuza hisia za ushirikiano na kujenga mafanikio ya kitaaluma? Tuwe wakweli. Tunaweza kufanya vyema zaidi. </p></blockquote>
<p>Mwandishi wa habari, mwanablogu na mwandishi wa Global Voices <a href="http://www.nikicheong.com/blog/1thing-to-many.html">Niki Cheong</a> anaandika kwenye blogu yake binafsi: </p>
<blockquote><p>Kichaa yupi alikuja na wazo hili zuri [&#8230;] Nadhani kuchangia msala na mwalimu hakutamsadia mwanafunzi kufanikiwa katika masomo yake, ufundishaji mzuri unaweza! </p>
<p>Ni  nini kinachoendelea? Je, tunaenda kuanza kula ‘chakula kimoja’ baada ya hapa? Au kuanza kusikiliza ‘1 Buck Short’? Au tutaanza kuwataka watu kuandikisha majina kama ‘Sharina1’ kwenye vyeti vya kuzaliwa? </p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa <em><a href="http://siamooi.blogspot.com/2009/10/1toilet-1malaysia.html">Thots Here And There</a></em> anaamini kwamba viongozi ni lazima watende wayasemayo kabla ya kutekeleza sera zozote: </p>
<blockquote><p>Kwa nini tusianze na makundi ya tabaka la juu kwanza kabla kwenda kwa walio wengi? Shuleni kwangu, Kundi la tabaka juu hupata ufunguo maalumu kwa choo chao maalumu [&#8230;] Najua kwenye makampuni fulani ya sekta binafsi kuna upendeleo wa namna hiyo pia. Nakumbuka rafiki yangu alipofurahi sana kwa sababu alikuwa amefikia kiwango cha upendeleo wa kuwa na ufunguo wake mwenyewe wa sehemu hiyo malum! Sasa, kama tunataka kutekeleza kitu kama hiki cha msala mmoja shuleni –fikiria wanafunzi watakavyopanga foleni kutumia msala –hebu na tuanze na kundi la juu la watumishi kwanza. Viongozi wanazungumza kuhusu Malaysia1 &#8230;tuwe wakweli, fanya usemacho. Tuonyesheni, enyi viongozi wa Malaysia kwamba sisi tu kitu kimoja kwa namna zote zinazoshirikisha matumizi ya msala!!!!</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa <em><a href="http://joesimple.wordpress.com/2009/10/16/from-1malaysia-to-1toilet">Voices Inside My Head</a></em> anaeleza upande chanya wa sera ya msala1: </p>
<blockquote><p>Wakati nilipokuwa shuleni nilijiuliza jambo hili hili, inakuwaje walimu wajisaidie kwenye vyoo tofauti. Hivi wanajisaidia kwa namna tofauti? Hivi wana kitu kinginecho tusichokuwanacho sisi? Nadhani inatakiwa kufanyika pote, hata kwenye maeneo ya kazi ya utawala wa juu watumie vyoo hivyo hivyo! Labda hata mawaziri washirikiane vyoo na wafanyakazi wengine wa serikali na hapo ndipo nitakaposema wanasiasa wetu wanatenda wasemacho!</p></blockquote>
<p>Mwandishi huyu, kupitia kwenye <a href="http://www.syafiqueshuib.com/syafique/?p=1068">blogu yake binafsi</a>, anasema: </p>
<blockquote><p>Walimu pia wanapaswa kuongoza kwa mifano na kupata matokeo mazuri kwa wanafunzi wao. Kama mwanafunzi tayari ana tatizo la kujisikia duni awapo darasani, atawezaje kuibuka na hisia za kujiona wa maana kwa sera ya Msala1? </p></blockquote>
<p>Hivi tunatakiwa kuchangia msala ili kuwa na hisia za umoja baina ya wanafunzi na walimu? Je, ushirikiano huu wapaswa kuanzia darasani kwenyewe?</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/malayasia-serikali-ya-jimbo-yaja-na-sera-ya-%e2%80%98msala-mmoja%e2%80%99/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
