Mghosya · Oktoba, 2012

makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Oktoba, 2012

Ghana: Vikwazo Vinavyowakabili Wanawake Kimaendeleo

  16 Oktoba 2012

Betty Mould Iddrisu, Jaji na Waziri wa Sheria wa Ghana, anaandika [fr] kwenye blogu ya pambazuka.org: Kufikia ngazi za juu kabisa za utawala si rahisi, na hata unapopanda mpaka juu kabisa, bado unajikuta unakabiliwa na hisia za watu zenye uadui na watu wanakuwa na mashaka na uwezo wako, kwa sababu...

Venezuela: Tathmini za Baada ya Uchaguzi

  15 Oktoba 2012

Msisimko ulikuwa mkubwa sana usiku wa siku ya Jumapili baada ya matokeo rasmi ya uchaguzi wa Rais wa Venezuela kutangazwa. Sehemu ya nchi ilisherehekea kuendelezwa kwa 'Mapinduzi ya Venezuela' chini ya Rais Hugo Chávez, wakati upande mwingine ulilalamika kwa kushindwa tena kwenye uchaguzi huo.

Zambia: Filamu yaYouTube Kuhusu Athari za Machimbo ya Madini

Filamu ya Uchunguzi yenye jina "Zambia: Shaba Nzuri, Shaba Mbaya" inayohusu machimbo ya shaba nchini Zambia na athari zake kwa jamii imewekwa kwenye mtandao wa YouTube na mpaka sasa imevuta watazamaji zaidi ya 6,000. Baada ya kuitazama filamu hiyo, mtumiaji mmoja wa mtandao wa YouTube aliandika, "Jililie eeh nchi yangu nzuriKwa nini tubaki masikini katikati ya utajiri huu wa madini yanayochimbwa kwa gharama ya afya za wenyeji?"

China: Hatua za Kubana Uhuru wa Habari Majimboni

  15 Oktoba 2012

Jing Gao kutoka blogu ya Tofu anaeleza namna serikali ya Fuji ilivyo na mikakati michafu dhidi ya Yunnan na jinsi inavyochukua hatua za kuzuia uchapishaji wa habari zinazoweka wazi kashfa za ufisadi zinazomkabili afisa mmoja wa serikali.

Venezuela: Ni Chávez Tena kwa Miaka Sita Zaidi

  11 Oktoba 2012

Baada ya chaguzi zilizokuwa na changamoto na ushindani mkubwa katika muongo uliopita, Venezuela itaongeza miaka mingine sita kwa utawala wa Hugo Chávez Frías ulioanza mwaka 1999. Idadi ya watu waliokuwa mtandaoni hasa kwenye mitandao ya kijamii, hasusani twita, ilikuwa kubwa sana hasa kabla matokeo rasmi hayajatangazwa.

Uganda Yaadhimisha Miaka 50 ya Uhuru

Terehe 9 Oktoba, 1962, Uganda ilijipatia uhuru wake kutoka kwa Mwingereza. Wakati nchi hiyo iliposherehekea Kumbukumbu yake ya Dhahabu hivi karibuni, wa-Ganda wanaotumia mtandao wamekuwa wakitumia zana za kijamii kama Twita na Facebook kusema maoni yao kuhusu sherehe hizo za kutimiza miaka 50!

Je, Una Swali Lolote kwa Jimmy Carter?

  10 Oktoba 2012

Rais wa zamani wa Marekani Jimmy Carter anapokea maswali kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twita (#CarterQA) kama sehemu ya kuadhimisha miaka 30 ya Kituo cha Carter (Carter Center) kinachojishughulisha na “kupigania masuala ya amani na kupambana na magonjwa duniani kote”. Rais Carter atakuwa anayajibu maswali hayo kwa njia...