makala mpya zaidi zilizoandikwa na Mghosya kutoka Disemba, 2011
Dondoo za Video: Maandamano, Chaguzi, Utamaduni na GV
Baadhi ya habari za kuvutia za Global Voices na video za hivi karibuni kutoka Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, Mashariki na Ulaya Kati, Karibeani pamoja na Marekani ya Kusini, zimeletwa na Juliana Rincón Parra.
Global Voices: Changia Leo
2011 umekuwa mwaka usio wa kawaida katika maudhui ya mtandaoni. Global Voices imekuwepo pale wakati mapinduzi yalipotokea, wakati tawala za kidikteta zikianguka, na matokeo ya matumizi ya mtandao yaliposambaa katika miji na mitaa ya wachangiaji wetu wanaoripoti kutoka duniani kote.
Rwanda: Watumiaji wa Twita Wajadili Mpango wa Rais Kagame wa Kugombea Awamu ya Tatu
Wakati mjadala wa ikiwa katiba ya Rwanda ibadilishwe kuruhusu muhula wa tatu uanzidi kupamba moto, Rais wa Rwanda Paul Kagame asema raia wanao uhuru wa kusema kwamba wanamhitaji. Mwandishi wa Kiingereza Ian Birell alijibu kwenye twita akisema, “Hawako huru, na kwa kweli ndivyo ilivyo, kusema aondoke…
Korea Kusini: Dikteta Kim Jong Il wa Korea ya Kaskazini afariki dunia
Kim Jong Il, dikteta wa Korea Kaskazini amefariki. Japokuwa kifo cha dikteta huyo mwenye sifa mbaya duniani ni jambo ambalo watu wanapaswa kulipokea vyema, watu wengi wa Korea Kusini wameonyesha wasiwasi juu ya hali tete katika bahari ya Korea itakayotokana na kifo chake cha ghafla.
Syria: Mwanablogu Razan Ghazzawi Ameachiwa HURU!
Habari zinasambaa mtandaoni kwamba mwanablogu wa Syria aliyekuwa gerezani anaweza kuachiwa huru wakati wowote kuanzia sasa. Ghazzawi, anayeblogu akiwa Syria kwa kutumia jina lake halisi, aliwekwa kizuizini akiwa njiani kuhudhuria warsha ya uhuru wa Vyombo vya habari iliyokuwa ikifanyika mjini Amman. Kuwekwa kwake kizuizini kulikosolewa na watumiaji wa mtandao, ambao sasa wanasubiri kwa hamu kuachiwa kwake. Amekuwa ndani kwa siku 15 sasa.
Zimbambwe: Hasira wakati Mzee Mugabe Anapowania Uchaguzi wa 2012
Chama cha ZANU –PF (Zimbabwe African National Union - Patriotic Front) kimempitisha Robert Mugabe kuwa mgombea wake kwa ajili ya uchaguzi wa rais unaotazamiwa kufanyika mwaka ujao. Kama uchaguzi utafanyika mwakani, Mugabe atakuwa na umri wa miaka 88 na atakuwa Mwafrika wa pili mzee zaidi kugombea katika uchaguzi wa rais. Kupitia Twita na Facebook wa-Zimbabwe wameonyesha hasira na kutokuamini kilichotokea.
Zambia: Magari Mapya ya Kifahari ya Mtoto wa Rais Yasababisha Minong’ono
Taarifa zilizotangazwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi ya Kiraia ya Committee of Citizens, Gregory Chifire, kwamba mtoto wa kiume wa rais wa Zambia, Mulenga Sata, hivi karibuni alijipatia magari mawili ya kifahari, zimevutia hisia mchanganyiko kutoka kwa wa-Zambia watumiao mtandao
Kongo (DRC): Wakongo Waishio Nje ya Nchi Walipuka Kumpinga Kabila
Wakati Kongo (DRC) ikingoja matokeo ya mwisho ya kura za Urais na wabunge, wa-Kongo waishio nje ya nchi hiyo, ingawa hawakuruhusiwa kupiga kura, wameonyesha kujitolea kwako kwa kuzifanya sauti zao zisikike. Julie Owono anataarifu.
Tanzania: Zinavyosema Blogu na Twita Katika Sherehe za Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania
Desemba 9, 2011, ni siku maalumu kwa Watanzania wakati Tanganyika, ambayo ni sehemu ya Muungano wa Tanzania ikitimiza miaka 50 ya uhuru. Katika mtandao, wanablogu na watumiaji wa twita wanasherehekea na kutafakari kwa kina mustakabali wa Tanzania.
Madagaska: Wajadili Uhalali wa Uwekezaji wa Kigeni wa Moja kwa Moja
Wakati Madagaska ikijaribu kutafuta suluhisho la matatizo ya muda mrefu ya kiasa, Wanablogu wa ki-Malagasi wanajadili thamani ya Uwekezaji unaofanywa Moja kwa Moja na raia wa Kigeni. Wa-Malagarasi wanaamini kwamba Madagaska, kama nchi nyingine za Kiafrika inao utajiri mkubwa wa rasili mali lakini tatizo likiwa ardhi yenyewe kupokonywa kwa sababu ya utawala mbovu na biashara zisizoangalia maslahi ya wananchi.