GlobalVoices katika

Christian Bwaya

Wasifu wa mwandishi · 199 jumbe · alijiunga 18 Mei 2009

Kiungo cha RSS kwa Christian Bwaya Kiungo cha RSS kwa Christian Bwaya

A science educator by certification, a lover of language by practice. Blogger, volunteer, translator and, well, a young husband.

Anwani ya Barua Pepe Christian Bwaya

makala mpya zaidi ya Christian Bwaya

11 Mei 2013

Uchaguzi Tume ya Uchaguzi Msumbiji: Mwanaharakati Ajitoa Kugombea

Kutokuwepo uwazi na weledi katika mchakato wa kumchagua mgombea, mbali na kufahamika nani hasa watachukua nafasi zinazogombewa kabla hata ya uchaguzi katika taasisi hiyo. Hizo zilikuwa baadhi ya sababu zilizotolewa na mwanaharakati wa haki za binadamu, Benilde Nhalivilo, wakati akijitoa rasmi kugombea nafasi kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Msumbiji[pt], chombo kinachohusika na kuandaa na kusimamia chaguzi nchini humo. Taarifa zaidi zinapatikana kwenye gazeti la A Verdade [pt].

7 Mei 2013

Mfululizo wa Tamthilia ya Runinga ya Nchini Tanzania

The Team Tanzania (Timu Tanzania) ni mfululizo wa Tamthilia ya Runinga yenye kuzungumzia:

[...] Bi. Wito, mwalimu mahiri wa somo la uraia, anaigeuza kabisa mitazamo ya vijana makinda watatu anapowauliza maswali mazito mfano “Wewe ni nani”? vijana wale wenye umri wa miaka 16, waliofahamiana vyema tangu wakikua. Katika kuingia katika umri wa utu uzima, vijana hao wanatafuta kujitambua huku wakikabiliwa na misongo mingi ya kifamilia na kiutamaduni.

Michoro ya Dar: Sanaa kwa Maendeleo Endelevu

Dar Sketches (Michoro ya Dar) ni sehemu ya mradi unaoanzia ngazi ya Mtaa jijini Dar Es Salaam, Tanzania ulioanzishwa na msanii na mchoraji Sarah Markes:

Ni katika kuenzi urithi wa kitamaduni na wa sanaa ya ubunifu wa majengo kwa jiji la Dar Es Salaam sambamba na juhudi za kukuza uelewa kwa wananchi juu ua tishio la urithi huu linalotokana na kasi kubwa ya kupanuka holela kwa jiji hilo.

6 Mei 2013

TEDXSão Tomé: Mkutano Wanukia São Tomé na Príncipe

TEDXSão Tomé

TEDXSão Tomé

Uandikishaji wa awali kwa ajili ya mkutano wa TEDXSão Tomé umezinduliwa rasmi. Mkutano huo una kaulimbiu inayosema “Visiwa Vimeunganishwa : São Tomé + Príncipe = Áfrika Vimeunganishwa na Ulimwengu” na utafanyika tarehe 20 Juni. Wasemaji katika mkutano huo waliothibitishwa ni pamoja: Dynka Amorim, Ismael Sequeira, Profesa Robert Drewes na Aoaní d'Alva. Tiketi linapatikana kwa Euro 20. Zaidi kuhusu mkutano huo tembelea ukurasa wa Facebook na tovuti [viungo vyote katika lugha ya Kireno].

China Yadhibiti Habari za Maandamano Yakupinga Kujenga Kiwanda cha Kemikali

Soma makala hii.

Wakazi wa jiji la kusini magharibi mwa China liitwalo Kunming waliingia mtaani mnamo Mei 4, 2013 kupinga mpango wa kuzalisha kemikali zenye sumu karibu na makazi yao. Vyombo vya Habari vya serikali havikutangaza habari za maandamano hayo, na katika hali ya kushangaza wafuatiliaji wa mtandaoni wamefuta habari na picha zinazohusiana na maandamano hayo kwenye mtandao maarufu wa kijamii uitwao Sina Weibo tangu Mei 4, 2013.

5 Mei 2013

Wagombea wa Urais katika Uchaguzi wa Madagaska

Habari Mpya:  Hapa ni orodha kamili ya wagombea 49 [fr] wanaowania nafasi ya Urais katika uchauzi ujao. Orodha hiyo haina jina la rais wa sasa wa mpito.

Siku ya mwisho ya kurudisha fomu kwa ajili ya kugombea Urais katika uchaguzi ujao ilikuwa tarehe 28 Aprili, na inavyoonekana ni wagombea wachache sana wasiotarajiwa wamejitokea kuwania kiti hicho. Wakati wagombea wa awali walikuwa wapya kabisa wasiofahamika sana, wanasiasa wachache machachari wanaofahamika wanatarajiwa kugombea akiwemo rais wa zamani Didier Ratsiraka, rais wa sasa wa mpito Andry Rajoelina [fr] na mke wa rais wa zamani Ravalomanana, anayeitwa Lalao Ravalomanana.

4 Mei 2013

Photos jumbe Video jumbe
Maelfu ya Wafanyakazi Waandamana Barani Asia

Soma makala hii.

Global Voices inayapitia kwa haraka maandamano ya Siku ya Wafanyakazi Mei Mosi kwenye nchi za Cambodia, Filipino, Indonesia na Singapore. Mikutano, ambayo iliandaliwa kudai haki za wafanyakazi na makundi mengine ya utetezi, yalifanyika kwa amani katika bara lote la Asia ya Kusini Mshariki.

Ethiopia: Mwanablogu Ahukumiwa Miaka 18 Jela kwa “Kuvunja Katiba”

Soma makala hii. GV Advocacy

Mnamo Mei 1, Mahakama Kuu ya Ethiopia ilitoa hukumu kali kwa mwandishi aliyeshinda tuzo Eskinder Nega, ambaye sasa atatumikia kifungo cha miaka 18 jela. Mohamed Keita wa Kamati ya Kuwalinda Waandishi anasema, “Kushitakiwa na hatimaye kutiwa hatiani kwa Eskinder na waandishi wengine ni dalili za utawala unaoogopa maoni ya raia wake.”

24 Aprili 2013

Jaribio la Mapinduzi katika Visiwa vya Comoro

Jeshi la Pilisi nchini Comoro limesema linawashikilia watu wanaosemekana kuwa wahaini raia wa Kongo na Chadi kwa tuhuma za jaribio la kuiangusha serikali lililofanyika mwisho wa wiki. Linfo.re anaongeza kwamba [fr]:

Makamanda wa Jeshi hawakutaka kupambana waziwazi na wahaini hao. Waliamini kwamba ” Kujeruhi raia wa Comoro kwa lengo la kuwalinda wakubwa inaleta picha ya usaliti kwa nchi hiyo ya Comoro”.

Washindi wa Tuzo za Kwanza za Uandishi wa Kiraia Nchini Ghana

Soma makala hii.

Tumepata matokeo ya Tuzo za kwanza kabisa za Uandishi wa Kiraia nchini Ghana.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha